LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Na imagine anavyofura kwa hasira akiona kinachoendela huko,huenda kila mara anachungulia kilipo kitufe cha Nyuklia code. Kwakweli wampe tu japo ukweli unajulikana Mtu mzima kavuliwa nguo mchana kweupe 🀣
πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
 
Nenda pale ikulu wakupe tausi watatu nitalipa mimi ndugu.Kuna kauli inayosema ,ukisikiliza vyombo vya habari una habarishwa uongo na usiposikiliza unakosa habari.
 
Rais wa Ukraine kulalamika kila siku ni mbinu mojawapo ya kivita. NATO na USA wako nae bega kwa bega.

Wanachokifanyika NATO na USA ni kuitumia Ukraine kama chambo ya kuiangusha Russia kiuchumi ambapo matokeo yake haitatawalika na nguvu zake kijeshi zitapungua sana kwa siku zijazo.

Ukraine itapata hasara ya miundombinu ila NATO na USA watasaidia kuijenga upya.

Shughuli itakua kwa Russia maana itapata hasara kubwa kiuchumi kwa miaka mingi ijayo.
 
Hata Katuni pia tunakoelekea Watoto hawatoziona.Inaelekea Putin alishapaniwa siku nyingi sana ajichanganye tu wamkomeshe,kila kunapokucha hali inazidi kuwa mbaya upande wa vikwazo na hivi vinawagusa wananchi wa kawaida kabisa moja kwa moja 😟
Putin kazua songombingo Sana.
 
Ona sasa shida imekuja mpaka kwa Team yngu pendwa 😑
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ila team haijaguswa huyo kaongeza chunvi tu...

Aliyepigwa kikwazo ni Abrahmovic mwenyewe so Club...

Apa sasa ndo utarejea kule nilikokua nakusema.... Taarifa ukizibeba bila kuzichunguza unabak na taarifa sehem kweli sehem uongo kwasabab waleta taarifa wana mahaba na pande walizonazo.
 
Roman Abromovich sanctioned

Chelsea hairuhusiwi kuuza mchezaji, kuuza jezi, kununua mchezaji, kuongeza mkataba,

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii ni fake news!! Hakuna maamuzi kama hayo yamefanyika. Mimi ni mfuatiliaji mzuri wa mgogoro wa Ukraine na Urusi, pia ni mpenzi wa Chelsea. Weka ushahidi wa madai yako!! Mmiliki was Chelsea aliamua kujiweka pembeni mwenyewe na baadaye akaamua kuiuza Chelsea.
 
Mwaka juzi kulikuwa na uzi nadhani ni wa North Korea nikadokeza somewhere kwamba Uturuki inaweza ipiga Iran watu wakaja juu kweli kwamba nawakosea Iran. Ila Uturuki ni taifa lingine kwenye silaha na ni superpower kwenye drone tangu kabla ya hii vita ianze. Silaha nyingine za Uturuki kama meli za kivita, helicopters, jet trainers, IFVs na APCs, missiles na precision guided munitions tuziache kwanza. Bado nasema hivi Iran hawezi kumpiga Uturuki na ambavyo dynasties za Persians zina historia ya kupigana na Ottomans mara nyingi. Hawa wote wapiganie mipakani ila sio deep in territories hiki tunachokiona kwa Ukrainians kiko kwenye damu ya Wairan sio kwamba unaanza kuwahamasisha.

Yale mapinduzi ya 2016 yaliyofeli Uturuki maelfu ya raia waliingia barabarani kutengeneza human chain kuzuia vifaru vya wanamapinduzi visipite, kuna clip nadhani YouTube bado zipo raia wamezuia njia crew ya kifaru ikafungua hatch kuongea nao raia wakawashusha na kuwachapa makofi. Nikiunganishi na jinsi Ottomans walivyopigana kwenye Gallipoli campaign kuzuia zile staits ambazo unapitisha meli za kivita ndio uende Urusi. The way kina Winston Churchill kipindi hicho ni kamanda walivyoshindwana na Waturuki mpaka kila upande ukapoteza wanajeshi 56,000 kwa vifo naamini Uturuki ukiwachokoza ujipange sana. Kuna jamii zina spirit ya tangu kale ya kupigana

Uturuki anaizidi China na Urusi kwenye unmanned aerial vehicles ila anazidiwa mbali na Israel na Marekani. Hizi ndege za Russia kina Su-25 na Mig-34 zinazopigwa kwenye anga la Ukraine hazina ulazima sana wa kutumika kama Russia ingekuwa na effective attack drones. Uzuri ni kwamba ukiwa na drone huogopi kupoteza rubani na unakuwa na confidence, rubani akiwa na Su-25 anakuwa na hofu, anaenda haraka na coordinates anaweza kosea kwa kiwewe maana kila siku ndege zinadondoshwa na mwishowe anakosea target. Operator wa drone anatulia maana haoni kingine zaidi angani, hata ikipigwa hatokufa, drone si gharama sana na zimetengenezwa kwa materials ambazo ni ngumu kuziona kwa radar
 
View attachment 2144767

Askari wa Russia wakiiba Kuku πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Hawa mwezi wa nne wataanza kufa kwa njaae
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚Dah inaonyesha Wana njaa Sana!Ila kumtumikia kichaa Putin yataka Moyo!anakupeleka vitani na njaa na kifaru anakuwekea mafuta nusu tank!kazi kwelikweli
 
Roman Abromovich sanctioned

Chelsea hairuhusiwi kuuza mchezaji, kuuza jezi, kununua mchezaji, kuongeza mkataba,

Sent using Jmapp
Uingereza haiwezi kufanya maamuzi yatakayoiathiri timu ya nchi yao. Mmiliki wenyewe alishaamua kuiuza
 
Upande wa Chelsea ni uongo ila upande wa Abrahmovic ni sahihi....

Source Al Jazeera
 
Tatizo hawezi kumtoa,Wananchi wake wanampenda comedian wao yeye Putin atafute sehemu nyingine ya kumuweka huyo kibaraka wake mwingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…