Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 15,692
- 23,038
Mkuu, umeeezea uzuri sana na yaeleweka khasa.Mtazamo wangu kuhusu huu uvamizi wa Kursk:
1) Inawezekana wapanga mikakati wa Ukraine waliamua kuuvamia huu mji ili Urusi apunguze wanajeshi kule upande wa Mashariki ambako ameelekeza nguvu kubwa kule na ndiyo kiini cha mgogoro upo kule.Hapa Putin kagoma kula chambo.
Walitumia hii theory ya Sun Tzu:
"You can be sure of succeeding in your attacks if you only attack places which are undefended".
2) Ukraine waliamua kuuvamia huu mji ili wapate nguvu kwenye mazungumzo ya kumaliza vita.Huu mji una kinu kikubwa cha nyuklia.
Urusi amekikamata kinu cha nyuklia cha Ukraine kwa muda sasa na Ukraine ametulia na hana cha kufanya!.
Kama wakifanikiwa kukikamata hiki kinu basi Urusi hatakuwa na namna zaidi ya kutulia! Hapa unaweza kusema Putin kakubali kumeza chambo!
Hapa walitumia hii theory ya Sun Tzu:
"You can ensure the safety of your defense if you only hold positions that cannot be attacked".
Majibu ya Urusi kuhusu uvamizi wa Kursk:
Wao wenyewe bado wanaendelea na kusonga mbele huko Mashariki mwa Ukraine, kwenye huu mji wamepelekwa askari wasiokuwa na mafunzo makubwa na wasio na uzoefu.
Vyanzo (vya kimagharibi) vinasema Putin katoa amri mpaka mwezi wa kumi Ukraine wawe wameondolewa hapo Kursk. Hapa utaona wanataka wamalize mchezo hapo Mashariki kisha waje nyumbani!
Maamuzi magumu ni haya: Mfumo wa upiganaji wa kirusi ni kuharibu kila kitu halafu tuanze upya! Atafanya hivi nyumbani kwake?? Muda utaamua!
Mpaka sasa Putin kaamua kutumia hii theory ya Sun Tzu:
" Do not swallow bait offered by the enemy".
Ni mtazamo wangu!