LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
Ndo nafungua Tv hapa baada ya majukumu, Naona kwenye heading hapa Tajiri wa chelsea Roman naye alikuwepo kwenye mazungumzo na Eukraine.. naona kuna tukio la UN-GA

Nini kingine? Kuna matumaini ya kumaliza vita?
 
SmartSelect_20220228-192018_Chrome.jpg
 
Unaujua mwenendo wa kivita wewe. Alafu unaujua umbali kutoka huko donbass mpaka Kiev wewe? Au unafikiria msafara wakati wa kivita kunakuwaga safari ya Moja kwa Moja, Unaijua ambush wewe. Au unafikiria hao waukrein Ni Adf nalu?.
Watu wana tembe umbali Fulani alafu msafara unasimama inafanyika swip reconnaissance Kisha unaenda Tena mbele kwa umbali ulio weka buffer zone.
Sema huwezi nielewa ungepita Jkt/mgqmbo labda ungenielewa kidogo. Ila nakuhakikishia huyo rais wa Ukraine asipo afikiana ndio atajua hajui maana hivyo vikwazo vya Eu,Uk,na baby wao USA. Sio vya kawaida vinamaanisha. Sasa Putin anaenda kufanya kitu haijawahi kufanya. Tatizo jingine jifunze kuujua mwenendo wa Vita.
Mpe somo huyo hajapitia hata mgambo
 
Wanajeshi wote huwa na vitambulisho na pia dog tags zenye service number, kwamba hata akiuawa achomwe hadi kuwa majivu, hizo dog tag number zinasomeka.
Kimsingi ni kuingia kwenye tovuti uone picha ya maiti ya ndugu yako na namba yake ya usajiri jeshini kisha umwombe Putin amrejeshe mwanao/ndugu yako umzike mwenyewe, kauawa huko alikopelekwa akapigane vita vya kuonyesha ubabe wa Putin.
Kenya hamnaga ubongo
 
Kwanza kbs napenda kutanguliza salam kwa wana JF wenzangu hapa jukwaani, pili naomba mods msiuunganishe huu uzi na uzi wowote unaohusiana na mambo ya Ukraine maana kila mtu ana uwasilishaji wake wa taarifa hapa jukwaani, so kuuchukua uzi wa mtu ambae kila siku anatumia data zake, muda wake, fikra zake na energy yake kuchangia comment mbali mbali au kuandika thread mbali mbali afu kwenda kuunganisha na uzi wa mtu mungine bila taarifa au sababu za msingi ni kuingilia uhuru wa watu kutoa maoni yao hapa jukwaani. Kwahiyo mwisho wa siku mtajenga hofu na uoga kwa wateja wenu, maana mtu atajua akileta uzi hapa kwa ajili ya kuhabarisha umma kuhusu yanayojiri huko duniani mods watauchukua huo uzi wake na kuupeleka sehem wanayojua wao bila idhini yake ili kupoteza maana ya kile alichoandika hapa jukwaani. So nina imani mods mtazingatia ushauri wang huu niliowapa. Tuje kwenye mada husika. Ndugu zangu kitendo cha raisi wa Russia kuomba poo ya mazungumzo ya kumaliza mapigano kati ya jeshi lake linalosifika kuwa na nguvu zaidi duniani baada ya lile la Marekani, kimewashangaza wengi waliokuwa wakimuunga mkono mbabe huyo na jeshi lake. Wakati akijiandaa na uvamizi, wengi wa wapambe wake walitegemea uvamizi wake ungechukua usiku mmoja tu kumaliza kile alichoita safisha safisha ya viongozi vibaraka wa magharibi. Sasa anashangaa pamoja na ukubwa wa jeshi lake, wingi wa silaha zake, na ukubwa wa nchi yake ameshindwa kutwaa hata miji mitatu tu mikubwa, badala yake yeye ndo amekuwa akirudishwa nyuma na kunyang'anywa mji wa pili kwa ukubwa ambapo hapo awali jeshi lake ndo lilikuwa linaumiliki. Bila shaka Putin ashasoma alama za nyakati baada ya kunusa ule mtego wa Marekani ambao waliutega kwa lengo la kupata sababu ya kuingia kijeshi kuiadhibu Russia kupitia katika ardhi ya Ukraine. Ikumbukwe Marekani na genge lake la NATO walisema hawawezi kuingia vitani kuisadia Ukraine kwani sio mwanachama wao kamili wa NATO. Ila nyuma ya pazia Marekani alikuwa anapanga mpango wa kurushwa kombora moja tu la Russia nchini Poland ambae ni mwanachama wa NATO ili watemi hao wa dunia waweze sasa kuingia kazini live bila kujificha kwa kisingizio kuwa Russia ndio ilianza uchokozi wa kumshambulia mwanachama mwenzao wa NATO (Poland) Silaha kubwa kubwa zimekuwa zikitumwa Ukraine usiku na mchana kwa kisingizio cha kuipa msaada wa silaha Ukraine, kumbe wakubwa hawa wanaziandaa kwa ajili ya kwenda kuzitumia wenyewe hapo baadae baada ya mipango kukamilika. Mimi na wewe hatujui hilo kombora lingerushwaje rushwaje ili mission yao ikamilike kuingia mzigoni. Wangesubiri kombora la Russia likosee njia na kuangukia kwa mwanachama wao? au wale wale askari wa Ukraine wangetafuta njia ya kupata kombora la Russia na kulivugumiza nchi yoyote mwanachama kinyemela ili msala umuangukie Putin? Pongeza kwa Putin kwa kuliona hili mapema na kuwahi kuomba poo before mambo hayajaharibika, maana Mmarekani na genge lake sio watu wazuri hata kidogo. Kweli unaweza kujikakamua kupambana nao lkn mwisho wa siku wewe ndo utaanguka miguu juu. Mungu aepushe mbali vitaa hii, ili dunia iwe sehemu salama ya kuishi kwa amani.
 
Kim Jong-un atoa Tamko
Seoul, South Korea:
North Korea has accused the United States of being the "root cause of the Ukraine crisis" while defending Russia, in Pyongyang's first official response to Moscow's invasion of Ukraine.

Russia ordered troops into neighbouring Ukraine this week, prompting global outcry and punishing sanctions from the West, some directed against Russian President Vladimir Putin himself.

But North Korea, in a muted response issued in the form of a commentary posted on the Foreign Ministry's website, said the United States was to blame for the unfolding disaster.

Washington has pursued "military supremacy in disregard of the legitimate demand of Russia for its security" according to the commentary, attributed to Ri Ji Song, a researcher at the North's Society for International Politics Study.

"The root cause of the Ukrainian crisis also lies in the high-handedness and arbitrariness of the US," said the post uploaded on the North's foreign ministry website on Saturday.

Ri slammed the US for holding a "double standard" -- saying it meddled in the internal affairs of other countries in the name of "peace and stability" but "but it denounces for no good reason self-defensive measures taken by other countries to ensure their own national security."

"Gone are the days when the U.S. used to reign supreme," the post said.

The response is a "low-key" official reaction as it was published under an individual name, said Park Won-gon, a professor of North Korean Studies at Ewha Womans University.

"The conclusion is that it's all because of the US. The main point is that you will suffer if you don't have power," he told AFP.

Along with Beijing, Russia is one of the North's few international friends and has previously come to the regime's aid.

Moscow has long held the line against increasing pressure on nuclear-armed North Korea, even asking for relief from international sanctions for humanitarian reasons.

China, North Korea's most important ally, has also blamed the United States and its Western allies in recent weeks for "hyping up" the Ukraine crisis.
 
Waziri wa Ulinzi wa Russia amemuambia Rais Putin nuclear triad is on 'standby alert duty' na ameshatoa maelekezo ya kufanya kwa wa husika, hivyo tutegemee lolote kuanzia muda huu...[emoji24]
Hiyo jeuri ya kupress Nuke code haipo na wala hawezi thubutu,huna haja ya kuwa na wasiwasi Mkuu.
 
Hata kama huyo bwana anahatarisha Maisha yako, familia yako na mtoto uliyempata na x wako

Ila marekani akiwachagulia watu namna ya kuishi mnaita demokrasia

Ukraini Hadi aombe poo na kuachana na penzi la bwana ake mpya
sentensi ya mwisho dah 🤣
 
Mimi nina mashaka sana na Russia kuhusu ukweli wa Silaha zake. Ninaona kama Fix hivi. Hii vita ikiendelea halafu NATO waingie unawezakuta hizo silaha alizoaminisha dunia huenda sio za kihiiiivyo. Hata nuclear unawezakuta zipo lakini low grade. Na akicheza hao NATO/USA wanaweza kum surprise wakazipiga hapohapo Russia.

Kuna uwezekano NATO wameshajua uwezo halisi wa RUSSIA na kugundua mbona ANAPIGIKA KIRAHISI TU.
Russia hawez lolote , kinachokufanya uonekane mbabe ,ni huge backup under fire , kitu ambacho Russia Hana ,na pia kuna different opinion among public , moja ya kitu kibaya mno kwenye vita , ametuaminisha ni mbabe yes tumekubal , but in reality huwez kurun show against European giants +US combined together , hao mnaosema washirika wake hawana chochote new cha kutoa hata wakijoin naye , kwanza hawana hela ,aiseee vita bila hela hamkna kitu , unaweza kujitutumua Kwa mwaka mmoja after that inakuwa ni disaster ...!!! Atakuwa ameishiwa kila kitu huku ukiwa umebanwa na vikwazo
 
Back
Top Bottom