LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

LIVE Special Thread: Yanayojiri Mgogoro wa Ukraine na Urusi. Nini chanzo na hatma ya mzozo?

Live coverage on JamiiForums
The delegation of Ukraine arrived at the third round of negotiations with Russia in Belovezhskaya Pushcha by helicopter.

SmartSelect_20220301-220358_Gallery.jpg
 
FIFA may postpone the play-off between Russia and Poland to June

About this writes the publication Interia. It is reported that the International Football Federation is trying to find a way out so as not to exclude the national team from the qualification of the world championship.

One of the options is to postpone the meeting with Poland until June.

At the same time, the opponent's press officer Jakub Kwiatkowski stressed that FIFA has not yet informed PZPN about the fate of the joint.
IMG_20220307_164232_413.jpg
 
Sidhani kama ataweza kuitawala maana raia hawawataki.
Ila malengo yao kwa kiasi kikubwa yata kuwa yametimia maana Ukraine haita weza tena kujiunga na Nato na wenda ikaishia kusambaratika kama iliyo kuwa Yugoslavia.

Sent from my TECNO BB4 using JamiiForums mobile app
Hapo malengo yatakuwa hayajafanikiwa kama ni hivyo.Hakukuwa na maana ya kwenda kupigana kama unajua mwisho wa siku huwezi kuwacontrol hao uliokuwa unapigana nao baada ya kuwashinda.Watarudi pale pale na malengo yao watayaendeleza.Nilimwelewa member mmoja alicomment hapa,kwa nini Putin hakutumia indirect way ya kuwafitinisha Ukraine wakagombana wao kwa wao ili apenyeze agenda yake kati kati ya mgogoro badala ya hii direct confrotation ambayo kawapa mwanya rahisi mahasimu wake wa kumwadhibu kwa vikwazo.
 
A number of EU countries, including Germany and the Netherlands, oppose granting Ukraine candidate status for membership this week - Bloomberg.
SmartSelect_20220301-220358_Gallery.jpg
 
Zelenskiy alitangaza wanajeshi wake waliyo kisiwa cha Zminyi(sina uhakika kama nimepatia jina lake) wakakipa jina la uongo Snake Island wale waliyoambiwa wasalimu wakatoa tusi la kejeli kwa Russia kuwa wamekufa na akawapa shahada ya ushujaa.

Taarifa rasmi ni kuwa hawakufa bali walijisalimisha. Ushahidi wa video upo ukihitaji tembelea RT utawaona na wanaonyeshwa taarifa iliyotolewa na rais wao kuwa wamekufa.
View attachment 2141927

Ukraine walitangaza wamemuua kamanda wa jeshi la Chechen lakini juzi kati kaonekana video clip iliyorushwa wakiwa wameteka moja ya kambi za Ukraine na silaha walizozikamata.

Ukraine walisema kuna ghost of Kieve. Ukweli ni hakuna! Ile kipande cha meme kutoka kwenye game. Imethibitishwa kuwa ni kweli.

Ukraine wameweka vipande vya video clip wakionyesha Russia wanachoma na kuteketeza makazi ya raia. Imekuja kuthibitika ni kipande cha movie ya nchini Serbia.

Ukraine walionyesha rais wao yupo mstari wa mbele naye kaingia vitani. Picha zote walizosisambaza zikimuonyesha na magwanda ni za mwaka 2016 kama sijakosea na uthibitisho upo! Wakati huo alienda kutembelea mazoezi ya kijeshi.

View attachment 2141919
Hii juu ni taarifa iliyotolewa na Zelenskiy

View attachment 2141920
US wakaona propaganda hii ni chungu. Taarifa ni ya uongo wakaamua kuipotezea kwa kuwataarifu mabalozi wasi re tweet hiyo habari.

View attachment 2141922
Ni hii hapa ikiendelea kukanushwa taarifa ya Zelenskiy.


View attachment 2141924
Polish wakikanusha kuwa hiyo taarifa ni ya uongo.
Huyo jamaa wa chini anawajibu Polish baada ya tweet yao kuwa inabidi azungumze na rafiki yao US kuhusu hilo kwa sababu matangazo anayoyatoa yanatofautiana na wao.
View attachment 2141925

Kwenye hii vita kuna propaganda nyingi sana zinafanyika. Nilizokuwekea ni chache. Kuwa makini mahali unapozipata taarifa.
Acha kutujazia server na mapicha picha yako ya kijinga asee kama vip wewe toa taarifa zako za ukweli!!
 
Russia operation yao walishaitangaza mapema kabla ya kuingia Ukraine: Mpango wao ni kulidhoofisha jeshi la Ukraine. Ndiyo maana wanashambulia kambi, viwanda na maghala ya kuhifadhia silaha za kivita.

Ukiitizama hali ya Ukraine kuna mengi utang'amua na mojawapo ni kuwa Russia inaonekana anaihitaji Ukraine. Hivyo hawezi akaharibu miundombinu, majengo pamoja na rasilimali watu.

Ukiangalia kwa sasa hivi kuna maeneo tofauti ya Ukraine yanapatiwa msaada wa vyakula na Russia. Hakuna shughuli ya kiuchumi ambayo inaendelea Ukraine. Kuna kitu Russia anajaribu kukiwekeza kwa raia wa Ukraine.

Kuhusu ushindi/Mshindi: Nafikiri ni busara tukawasikiliza wenye ubobezi kwenye hii tasnia ya masuala ya kivita. Na wanayoyasema wakiwemo majenerali wa US ni kuwa; Russia hajatumia hata 20% ya nguvu yake ya jeshi.

Nafikiri tutosheke na hili. Ijapokuwa swali muhimu ni kujiuliza kwa nini ametumia chini ya 20% ya nguvu yake ya kijeshi(?)
Acha propaganda twambie Russia ameachieve nini cha maana mpaka sasa katika hii vita ukiniuliza mimi nitakwambia mpaka sasa Ukrai ndo mshindi maana kaweza kuilinda kwa nguzu zote mipaka ya Ardhi vip kwa Russia mvamizi yeye kagain kipi cha maana kwenye hii vita mpaka sasa
 
News: Saudi Arabia imekataa ombi la United States ya kuongeza usambazaji wa mafuta kukabiliana na mfumuko wa bei( Saudi Arabia Refused to boost output of oil).

Nahisi ule umoja wao wa uzalishaji wa mafuta kuna makubaliano wamewekeana akiwemo na Urusi. Maana hadi mtangazaji anashangaa leo inakuwaje Saudi Arabia anamgomea USA kwenye ishu hii ya mafuta.
OPEC+ huwa wanapenda bei ya mafuta ipande. Ukiongeza uzalishaji soko linakuwa saturated bei inashuka, ukipunguza uzalishaji bei inapanda. Wao wanapata hela zaidi wakizalisha mafuta kidogo kuliko wakizalisha mafuta mengi. Mwaka 1973 Waarabu walipovamia Israel nayo ikapewa silaha nyingi kutoka Marekani, Waarabu wa OPEC wakaweka mgomo wa kuiuziamafuta Marekani na yakapanda bei duniani. Marekani iliteseka mwaka huo na ndio chanzo cha kupotea sokoni kwa ndege zenye injini nne na mashirika giants kama PanAm Air (hili lilikuwa CocaCola ya hewani, kama hulijui basi hujui shirika lolote) yakafirisika, kampuni kama Boeing ikazidi kuuza maana ilikuwa na ndege nyingi za injini mbili ambazo hazili sana mafuta. Marekani kuanzia hapo ikajikaribisha na Middle East kuhakikisha usalama wa nishati yake.

After that Marekani ikawa na vibaraka kwenye OPEC (ambayo inasimamiwa na Saudi Arabia ndio maana Russia na wengine hazikuwepo ila zilikuja baadae kama OPEC+ ambayo Russia huwa ni mbishi mara nyingi). Mafuta yaliongezeke kuzalishwa, yakawa mengi sokoni na yakashuka bei miaka ya 80s, Soviet Union ikapungua mapato ikazidisha uchungu kwenye mgogoro wake mpaka kuanguka. Saudi Arabia hasa Royal family haina kauli sana mbele ya Marekani wakikaa mazungumzo wanaweza tatua shida zao, OPEC ni Saudi Arabia, OPEC+ ni independent wakileta ubishi wote dunia ufurahia maana kila mtu huzalisha kadri awezavyo hapo Iran anaweza pump hata mapipa milioni 2 kwa siku.

Ubishi wao huwa haudumu Marekani ina fracking technology ambayo ni expensive ila mkipandisha sana mafuta mnafanya wazalishaji wa Marekani wa-activate mitambo yao wakishaona watapata breakeven. Na wakifanya hivyo, OPEC+ inashusha uzalishaji ghafla kuwakomoa wale hasara. Ni mwendo wa kutegeana
 
Acha propaganda twambie Russia ameachieve nini cha maana mpaka sasa katika hii vita ukiniuliza mimi nitakwambia mpaka sasa Ukrai ndo mshindi maana kaweza kuilinda kwa nguzu zote mipaka ya Ardhi vip kwa Russia mvamizi yeye kagain kipi cha maana kwenye hii vita mpaka sasa
Mipaka gani iyo unaongelea ndugu maana sehemu kubw za mipani zipo chini ya warusi
 
Back
Top Bottom