Hatimae imekuwa , Yule joka mkuu ameanguka. Babeli imeanguka na waliokuwamo ndani yake hawatapona asilani, aliyeumiza wengine ,aliyedharau maumivu ya wengine,aliyewavua ubunge watu waliojeruhiwa kwa risasi wakiwa I.C.U aliyewapiga bakora waliopingana nae,hatimae nae ameanguka kwa kishindo kikuu.
Asante CCM kwa Sasa mtaelewa umuhimu wa wapinzani bungeni, bunge hili lilinoga Sana wakati ule wa miamba akina John Heche, Joseph Mbilinyi, Freeman Mbowe nk .
Job Ndugai alijua ana nguvu kuliko Serikali ,alijua yeye ni mwamuzi wa mwisho, ameumiza watu wengi na kudhulumu haki za wengi, kinachomuondoa Ndugai ni Mungu mwenyewe
Asante Mungu kwa kuwa kila aliyebeba kusudi baya katika nchi yetu umemuondoa kwa njia unazoweza wewe
Asante Mungu kwa kuipenda nchi yetu, tupe Spika atakaesimamia mapenzi yako juu ya nchi yetu ona Sasa mtego wa panya umekunasa na kuondoa kabisa heshima yako
Asante Mungu