Spika Job Ndugai, amejiuzulu Uspika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Hatimaye Job Ndugai abwaga manyanga

View attachment 2070772
Kwani katibu wa Bunge anapokea nakala au ndiye mhusika mkuu? CHECHEMEA party
 
Ameomba kwa chama chake kwanza , kama chama kikiridhia basi atakubaliwa na atapewa barua ya chama na hatua zingine kuendelea
 
Kama mnampenda sana Ndugai, mwambieni arudishe kadi ya CCM, na kwenye kikao kijacho cha Bunge, agombee tena u-spika kama Private Candidate na sio kama mwakilishi wa chama... haya mambo simple sana!!!
 
Hakuna utaratibu wa kikatiba wa namna ya spika kujiuzulu. Kwanza katiba yenyewe haitaji kama spika anaweza kupoteza nafasi yake kwa kujiuzulu, Soma Katiba kifungu cha 84 kuanzia kifungu kidogo cha 7(a) Nakinukuu kwa manufaa yetu sote:

(7) Spika atakoma kuwa Spika na ataacha kiti cha Spika

litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo -

(a) iwapo mtu huyo alichaguliwa kutoka miongoni mwa

Wabunge, basi ikiwa atakoma kuwa Mbunge kwa

sababu yoyote ambayo haihusiki na kuvunjwa Bunge;

au

(b) ikiwa kutatokea jambo lolote ambalo, kama

asingekuwa Spika, lingemfanya mtu huyo asiwe na

sifa za uchaguzi au apoteze sifa za uchaguzi wa

Spika; au

(c) Bunge litakapokutana kwa mara ya kwanza baada ya

Uchaguzi Mkuu uliofanywa baada ya Bunge kuvunjwa,

lakini masharti ya aya hii yatatumika bila ya kuathiri

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

masharti ya ibara ndogo ya (4) ya ibara ya 90 ya

Katiba hii; au

(d) ikiwa mtu huyo ataondolewa kwenye madaraka ya

Spika kwa azimio la Bunge lililoungwa mkono na

Wabunge amabo idadi yao haipungui theluthi mbili ya

Wabunge wote; au


(e) ikiwa mtu huyo atashindwa kuwasilisha kwa Rais

tamko rasmi kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo

(5) ya ibara hii; au

(f) ikiwa mtu huyo atapatikana na hatia kwa kosa la kutoa

habari za uongo, kwa kiapo kinyume cha sheria ya

Kanuni ya jinai, kuhusu tamko rasmi lolote lililotolewa

kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya (3) ya ibara

hii; au

(g) ikiwa mtu huyo atashindwa kuwasilisha kwa Rais

taarifa ya mali kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo

ya (5) ya ibara hii kabla ya kumalizika muda uliowekwa

kwa ajili hiyo kwa mujibu wa sheria iliotungwa na

Bunge;

(h) ikiwa itathibitika kuwa mtu huyo amevunja masharti ya

Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
 
Binafsi sioni kosa la Spika Job Ndugai, ni mbunge kazi yake ni kushauri, kukosoa, kusimamia , kutunga Sheria, kupitisha Bajeti na mikopo zikiwemo sio kupokea maagizo ya Serikali, kusifia au kuwa praise team wa Serikali
 
Ndugai alikuwa kinara wa kumshughulikia CAG Prof Asaad kwa kusema kuwa Bunge ni dhaifu lakini mwisho wa siku yeye mwenyewe Ndugai kadhihirisha maneno ya Assad baada ya kujisubmit kwa Rais na kuomba msamaha kwa kauli ambayo haikuwa na tatizo lolote. Matokeo yake ni kilichompata sasa
 
Hili sijambo lakawaida kwakuwa ni jipya nadhani ipo haja ya kuliangalia kwa mapana yake kunani TZ.
 
Mazuzu yameungana kushangilia sasa hao uliowataja watakemea vipi?
 
Tena kama machadema ndio bure kabisa!
.
Huwezi amini kama Lema leo hii anashangilia bunge kubanangwa namna hii
 
Uandishi wako ni mbovu sana!!
 
Hili sijambo lakawaida kwakuwa ni jipya nadhani ipo haja ya kuliangalia kwa mapana yake kunani TZ.
Kama kwenu Tanzania halijatokea huko nchi nyengine je huwezi kujifunza? au unaishi dunia ipi wewe

Kuwajibika ni jambo la kawaida sana ukifanya uzembe na ujinga kwenye wajibu wako., ni kutunza heshima yako isimalize kabisa kabisa, unataka mtu akae madarakani ata akifanya nini wakati kuna mamilioni ya watu wanamatumaini yao mbali mbali kwa nchi yao
 
Lile soko pale Idodomya bado linasomeka kwa jina lake?
Nashauri lile jina pale lifutwe haraka sana lisije nalo kuporomoka tukaingia hasara wajameni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…