Spika Ndugai alikuwa na hoja ya msingi, tatizo sio kukopa bali kukopa wakati kuna tozo za miamala ambazo mlidai zanajenga madarasa na vituo vya afya

Bunge la JMT lilipitisha tozo ambazo ama kwa hakika zilizua tafrani na kuzua kilio kwa wananchi, bila hata aibu Mwigulu Nchemba akainuka na kudai kuwa ambae hataki kulipa tozo basi ahamie Burundi...
Udikteta. Hawataki kukosolewa.
 
Mkuu Rais kasema tozo zinatekeleza ila kwa kazi ndogo sana.

Kumbuka January 17 shule zinafunguliwa na ktk demand ya madarasa 10,000 tozo imejenga madarasa 560 pekee hivyo kulikua bado na uhitaji wa madarasa 9440...
Acheni ujinga nyinyi..
Kila muama serikali inakusanya kiasi gani kwamwenzi?
Zile za escrow tulisema zinatosha kufanya nini nchi nzima na zilikuwa bil300.
 
Na siku anazinadi tozo aliinanga mikopo kuwa haifai au sio yeye
vichwa panzi mnawahi kusahau mbona.
 
Achaneni na akili mfu kama hizo..
Haina maana hii sentensi
Hivi kwa rasilimali na utajiri wa taifa letu ni wa kwenda kuminya tozo kweny miamala?
Rasilimali zako zipi ambazo hazina alternatives nchi nyingine? Taja tatu tu ambazo bei ikiwa juu hazina mbadala.
Mtu wa kawaida ukizidisha matumizi unafiliska Mwanasiasa akizidisha matumizi
anaongeza kodi.
Takwimu za matumizi ya wanasiasa wa Jamhuri unazo?
Aweke sera nzuri za biashara watu wengi walipe kodi.
Nakubaliana na wewe.
 
Haina maana hii sentensi

Rasilimali zako zipi ambazo hazina alternatives nchi nyingine? Taja tatu tu.

Takwimu za matumizi ya wanasiasa wa Jamhuri unazo?

Nakubaliana na wewe.
Achaneni na akili mfu nyiny huwezi justify tozo kisa madarasa..
Aliyekuwa anainanga mikopo siku anazinadi tozo sio yeye?
VIchwa panzi samahani kukuita ivo..
 
Nakuuliza tena, kama tozo zimeshindwa kumaliza tatizo sasa za nini? Maana tatizo linawezwa kunalizwa na mkopo at once.
 
Hivyo mtoa mada ni kwamba tozo zimejenga vyumba vya madarasa 560 pekee wakati uhitaji ni madarasa 10,000.

Hivyo mkopo umeweza kuharakisha utekelezaji na kuziba gap kwa wakati mfupi.

NB ; Mkopo wa uviko-19 hauna riba kwa miaka 20.
Hayo madarasa 10,000 yakikamilika kwa hiyo hela ya mkopo na tozo,

Tozo itastop?
 
Bunge la JMT lilipitisha tozo ambazo ama kwa hakika zilizua tafrani na kuzua kilio kwa wananchi, bila hata aibu Mwigulu Nchemba akainuka na kudai kuwa ambae hataki kulipa tozo basi ahamie Burundi...
Ndugai ana hoja ya msingi na itabaki hivyo na wananchi ni waelewa sana na hata sisi baadhi yetu wana CCM tunaelewa tunawaacha Utopolo wajibambe na wajikweze
 
Hayo madarasa 10,000 yakikamilika kwa hiyo hela ya mkopo na tozo,

Tozo itastop?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Tozo imepitishwa na bunge sheikh
 
Shida ni alivyoiwasilisha ndio tatizo.
 
Wewe umefanya nini kuhakikisha hizo rasilimali zinaleta tija au unaongea tuu?
 
Huko vijijini unakotolea mfano ujue kwamba kulikuwa na harambee za ujenzi wa madarasa na miundo mbinu kama hiyo; zile jitihada za kujenga zingeendelea kwa hamasa zaidi, na tozo zifanye finishing.
Je wananchi waendelee kuamini kuwa serikali inaweza kila kitu, wao wazaliane tu? Kama siyo, je on nini ni mchango wao wa maana kwenye miundombinu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…