Spika Ndugai ataka Walimu waongezewe kazi wafundishe masomo kuanzia matatu ili kupunguza uhaba wa Walimu

Spika Ndugai ataka Walimu waongezewe kazi wafundishe masomo kuanzia matatu ili kupunguza uhaba wa Walimu

Haina shida,ndugai yuko sahihi. Maana walimu wa shule za msingi wanafundisha masomo yote ndo maana hakuna uhaba wa walimu katika shule za msingi.Ndugai ni akili kubwa ,kumuelewa hadi uwe na PhD,na nionavyo Mimi kwa Tanzania ya sasa hatuhitaji madaktari wa meno,sijui figo,moyo nk. Ni upotevu wa pesa haiwezekani daktari yeye kazi yake ni kutibu meno tu au macho,ni matumizi mabaya ya raslimali watu,daktari wa meno inapidi pia asomee ubongo,figo nk.ili kuwa na matumizi sahihi ya raslimali watu.

Safi sana,kuna wakati viongozi wetu huwa wanatoa maoni /kauli hadi unashindwa kujua hii kauli ilitolewa na huyu kiongozi akiwa katika khali gani.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
Nashukuru Nina uvumilivu wa kusoma kitu mpaka mwisho. Tofauti na hapo ningekutukana. Nisamehe maana nilianza kukutafutia laana ya kukupa.
 
Akili kichwani mwako na future ya mtoto wako. Mwalimu hata ukimpa masomo 13 atafundisha hadi bible ila matokeo yake sasa...
Wao hawana shida na hilo kwasababu hata matokeo siku hizi wanapika kama wali.
 
Kama vipi hayo masomo matano amrundikie yule mwalimu wa kemia na hesabu, maana yeye anajua mambo kibao ikiwemo namna hukumu zinavyotakiwa kuandikwa na majaji...
 
Hakuna cha walimu wa kujitolea, serikali iajiri walimu fullstop... Tunalipa kodi ili zilete hizo huduma za jamii, moja ya huduma za jamii ni elimu, elimu sio kuwa na madarasa na madawati, uwepo wa vitendea kazi na walimu Pia ni muhimu mno.... Watumie kodi zetu kuajiri walimu, sio kununua midege inayoleta hasara tu.
Nafikili kila shule ipate walim wa kujitolea sie mazazi tuwachangie ili kupata ufanisi mzuri , kuliko kulazimisha kuongeza , masomo
 
Na nyie ndio ambao mmepitisha utawala huu wa hovyohovyo
Muheshimiwa speaker mbona unakosa ya kushauri Serikali? Hujui kama kadri mtu anavyokuwa na masomo mengi anapunguza ufanisi? Umeshinda kushauri Wizara na Serikali kulipa mdeni na kupandisha madaraja, unataka Mwalimu mmoja afundishe masomo matatu shule.
Ama kweli, ulishapata wewe. Huoni shida tunazopata walimu, unachoona ni kuwa hakuna kazi tunazofanya.
Kwani hujui kwa kawaida Mwalimu mmoja anatakiwa kuwa na watoto wangapi anaoweza kiwamudu? Inakuwa kama mtu asiyeona? KWA hiyo unataka kusema walimu wanatosha sana tatizo wanafundisha masomo machache!

Hongera sana Job Ndungai, lisimamie hilo, ikiwezekana Mwalimu mmoja afundishe masomo saba (7) hapo tutakuwa tumetatua tatizo.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpatie! Walimu tuna maumivu..... Hilo mnalijua..
 
Wagogo wanaomba kujengewa maghorofa makubwa makubwa Dodoma!

Yaani kila kitu wanaomba hawajuwagi kujiongeza.

Taratibu wanaondolewa mjini kisayansi watabakia pembezoni tu Kibaigwa, Bahi na Mtera.

Warangi nawakubali sana akina Kimbisa ni watu wa kujiongeza sana!
For the third time nakubaliana na wewe ...Kuna saa MATAGA wewe unanyoosha maelezo
 
Nawakumbusha tu kwamba spika Ndugai alitumia zaidi ya $10 million kwa matibabu India.
 
Labda sijamwelewa vizuri. Hivi anamaanisha hata kupunguza uhaba wa madaktari. Daktari moja atibu sikio, jicho, figo, ini siyo?
Sasa maswali hayo sijui anamwuliza nani,maana yeye yupo huko bungeni zinakotungwa na kurekebisha Sheria zaidi ya miaka 20 hakulitambua hilo.

Kutokana na Mazingira ya kada ya ualimu iilivyo hakuna mzazi eti mwanae kafaulu PCM, PCB, PGM atameleka ualimu.
 
Akikazia mawazo ya wabunge kama kawaida yake nimemsikia Spika ameitaka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuwaongezea masomo ya kufundisha walimu kwa maana ya kuwafundisha kuyafundisha tangu wakiwa vyuoni hasa vyuo vikuu ili kupunguza uhaba wa walimu na kuongeza tija kwa Wanafunzi....
Bora mbunge mmoja angewakilisha majimbo hata 30.

Ili fedha itumike kuwapa akira walimu wengine.

Walimu wanaumuhimu katika kuendelea nchi kuliko Hawa wabunge
 
Baada ya walimu kukamilisha zoezi la usimamizi wa uchaguzi kwa ufanisi Sana hatimae Ndugai amewalipa walimu stahiki zao kea kuwataka waongezewe masomo ya kufundisha.

Hongera mh Nddugai.
 
Ngazi ya shule ya msingi mwalimu anaweza akafundisha masomo kadhaa. Lakini kuanzia sekondari una-speacialise somo moja tu. Mengine utababaisha tu. Kwa mfano mwalimu wa Fizikia anaweza kushikilia nafasi ya mwalimu wa Hisabati wakati kuna dharura.

Lakini topics nyingi hawezi kuzimudu kwa kiwango anachozimudu mwalimu wa Hisabati. La sivyo tutakuwa tunawadanganya wanafunzi kwamba wamesoma Hisabati wakati wamebabaisha tu. Nasema haya kutokana na uzoefu wangu wa kufundisha wa miaka 35.
 
Back
Top Bottom