MKuu kwa kejeli hizi huwasaidii Chadema bali unawapoteza. Ulitakiwa, ninavyodhani, uwape maelekezo wafungue kesi ya kikatiba ama ya aina yoyote ile na inyofaa kuhoji na kupinga utekelezaji wa shughuli za bunge chini ya Mheshimiwa Spika Ndungai. Ni hayo tu!
NInao uzi wa aina hiyo waiting to be reviewed and posted lakini sio kwa ajili ya ku-counterattack viroja vya Ndugai ambavyo kimsingi vyenyewe ni matokeo tu ya uongozi wa juu ulioamua kwa makusudi kumpa Ndugai mamlaka ya kufanya mambo ya hovyo!!!
Sheria zipo wazi, kwahiyo sidhani kama kuna mgogoro wowote wa kikatiba au kisheria zaidi ya uhuni tu!!
Lakini ndugu yangu TUJITEGEMEE unanionea unaposema eti nakejeli!! Mimi huwa naandika kutegemeana na maoni ya wachangiaji wa kambi husika!! Kufuatia sakata hili, nimeona posts kadhaa za wana-CCM wakielezea jinsi Halima Mdee alivyo Msomi, NGULI la Sheria, Mzalendo anayweka mbele maslahi ya taifa badala ya chama, jinsi Mbowe alivyomuonea Mdee na wenzake na kadhalika na kadhalika na kadhalika!!
Lakini uonevu huu wa Mbowe uliotajwa ulikuja baada ya hao hao hapo kabla wengine kusema there's no way Mbowe angeacha kupeleka majina wakati anafahamu hayo majina ndo posho yenyewe!
Sasa ndugu huoni watu walivyo na raha manake wanaongea lolote lile linalopita kichwani!!!! Wana-CCM wangapi wamejiuliza imetokea tokea vipi vipi kwa mfano mtu kama Nasrati Hanje kuweza kuapishwa wakati alikuwa lupango kwa zaidi ya miezi 3 na mamlaka ziligoma kumpa dhamana?!
Ni wangapi wamejiuliza inakuaje NEC waseme walipokea majina November 09 wakati NEC hao hao hapo kabla walikanusha kupokea majina wakati huo?!
Ni wana-CCM wangapi wanajiuliza ikiwa Mnyka na Mbowe wamesema hawajapeleka hayo majina, sasa kapeleka nani?!
Sasa hivi huoni ikiwa kuna kundi halina hata time time kwa kujiuliza hata mambo ya wazi kama hayo basi ni kwa sababu hawataki kuumiza kichwa?! Ni raha ilioje huyo ndugu yangu!!!