Spika Ndugai awaapisha Humphrey Polepole na Riziki Lulida. Asema Bunge linawatambua Wabunge 19 wa Viti Maalum waliofutiwa uanachama CHADEMA

Spika Ndugai awaapisha Humphrey Polepole na Riziki Lulida. Asema Bunge linawatambua Wabunge 19 wa Viti Maalum waliofutiwa uanachama CHADEMA

Mi ningekuwa ndo Ndugai, hawa ningewaapishia kwenye Car Wash kabisa ili ma-CCM wenzangu yaseme "...Si mnaona tuliwaambia hakuna kifungu kilichovunjwa pale... eti Mbowe alikuwa anahoji akina Mdee kuapishwa garage, si mnaona akina Polepole hao wameapishiwa kwenye carwash!

Amini usiamini... kuwa mwana-CCM raha sana! Yaani huumizi kichwa!!!
e "daily order ya Mlale JKT"Huumizi kichwa,kila asubuhi mambo yamepangwa wewe ni kutekeleza pamoja na dagaa waliooza alkini tulinenepa
 
Nafasi kumi alizopewa Rais na Katiba ya JMT ni kama katika wabunge waliopo hakuna mtu ana sifa anazotaka lakini sio mbunge ndio anateua sasa huyu wetu anateua watu wa ovyoovyo ili kujaza makasuku kule mjengoni shida
siyo kweli, Naona ameangalia makatibu wa uenezi waliopita, kama hawakuwa wabunge, then maslahi yao baada ya kuondoka kwenye utumishi huo si ya kuridhisha kulingana na utumishi wao katika chama.

Kwa hiyo ukiwapa ubunge watapata mafao ya kibunge, Ujue kuwa si lazima mwenyekiti afuatae aendelee kuwa na polepole kama katibu mwenezi
 
Huyu mama aliekuwa m'bunge wa KAFU ameunga mkono juhudi za meko au ni meko kujipendekeza.
Aliunga juhudi mara tu Bunge lililopita lilipo maliza muda wake. Na wakati anaomba kurudi nyumbani, aliwachamba sawasawa wabunge wa Chadema.

Amandla...
 
Kwa msimamo huo, hata wakina Halima wakiamua ku resign ubunge wao hawatakubaliwa.

Amandla...
 
MKuu kwa kejeli hizi huwasaidii Chadema bali unawapoteza. Ulitakiwa, ninavyodhani, uwape maelekezo wafungue kesi ya kikatiba ama ya aina yoyote ile na inyofaa kuhoji na kupinga utekelezaji wa shughuli za bunge chini ya Mheshimiwa Spika Ndungai. Ni hayo tu!
NInao uzi wa aina hiyo waiting to be reviewed and posted lakini sio kwa ajili ya ku-counterattack viroja vya Ndugai ambavyo kimsingi vyenyewe ni matokeo tu ya uongozi wa juu ulioamua kwa makusudi kumpa Ndugai mamlaka ya kufanya mambo ya hovyo!!!

Sheria zipo wazi, kwahiyo sidhani kama kuna mgogoro wowote wa kikatiba au kisheria zaidi ya uhuni tu!!

Lakini ndugu yangu TUJITEGEMEE unanionea unaposema eti nakejeli!! Mimi huwa naandika kutegemeana na maoni ya wachangiaji wa kambi husika!! Kufuatia sakata hili, nimeona posts kadhaa za wana-CCM wakielezea jinsi Halima Mdee alivyo Msomi, NGULI la Sheria, Mzalendo anayweka mbele maslahi ya taifa badala ya chama, jinsi Mbowe alivyomuonea Mdee na wenzake na kadhalika na kadhalika na kadhalika!!

Lakini uonevu huu wa Mbowe uliotajwa ulikuja baada ya hao hao hapo kabla wengine kusema there's no way Mbowe angeacha kupeleka majina wakati anafahamu hayo majina ndo posho yenyewe!

Sasa ndugu huoni watu walivyo na raha manake wanaongea lolote lile linalopita kichwani!!!! Wana-CCM wangapi wamejiuliza imetokea tokea vipi vipi kwa mfano mtu kama Nasrati Hanje kuweza kuapishwa wakati alikuwa lupango kwa zaidi ya miezi 3 na mamlaka ziligoma kumpa dhamana?!

Ni wangapi wamejiuliza inakuaje NEC waseme walipokea majina November 09 wakati NEC hao hao hapo kabla walikanusha kupokea majina wakati huo?!

Ni wana-CCM wangapi wanajiuliza ikiwa Mnyka na Mbowe wamesema hawajapeleka hayo majina, sasa kapeleka nani?!

Sasa hivi huoni ikiwa kuna kundi halina hata time time kwa kujiuliza hata mambo ya wazi kama hayo basi ni kwa sababu hawataki kuumiza kichwa?! Ni raha ilioje huyo ndugu yangu!!!
 
Kama kawa wamewaapishia chooni. Ofcourse tulitegemea mtu mfupi lazima ayambue covid 19
 

Spika wa Bunge Job Ndugai leo November 30,2020 atawaapisha Wabunge wawili walioteuliwa na Rais Magufuli, Wabunge hao ni Humphrey Polepole ambaye ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM na Riziki Said aliyekuwa Mbunge Viti Maalum katika Bunge la 11 kupitia CUF...
 
Umma wa watanzania utatulia kungoja ushahidi. Ulitulia kwa Yule aliyerudishwa, kwa silinde na wengine kwasababu Bunge lilikuwa linavunjwa. Sidhani kwa miaka mitano watu wataangalia tu katiba ikisginwa kwa makusudi utafikiri nchi haina wasomi wa sheria. Sidhani
Sidhani kama Mungu kanichukia kiasiki kuendelea kuona matendo yanayonikera na kuniumiza robo bila Kulipa msaada wa kuyaondoa na kutoa adhabu kali kwao
 
Huyo amewasababisha hata ile akili kidogo mliodhaniwa kuwa nayo kuvurujika.
Sasa hivi sii mahaka,, bunge, taasisi yeyote iliyo huru.
Zote zinaulilia uhuru maana wako chini ya kitisho na hofu
Hata wewe ni mtumwa ndani ya nchi yako ila uwezo wa kutambua hilo huna.
Teteh,
Kutoka wabunge 50+ hadi mbunge 1 wa jimbo lazima akili iwaruke tu
 
Kwani mimi niko chadema!?

Mimi ni mwanaume na niko ccm, hizo nafasi za akina Halima ni za nyie wanawake wa huko chadema ndio maana mnapigana vikumbo.
Amekutuna mkuu, Una bahati hujaelewa! Ana maanisha Bulaya ni ‘mke’ wa Mdee, ndo nafasi anayokuambia ukachukue!!
 
Nimecheka kwa nguvu, eti wastaafu waachwe wapumzike maana mambo yanabadilika, kwani katiba imebadilika? Yaani huyo Ndugai sio kuwatambua tu hao wabunge, awape na nyumba za kuishi kabisa kuzunguka hilo bunge, lakini Chadema wamashawavua uanachama fullstop.
 
Hatuwezi kuwaita Mheshimiwa wale jina lao ni Covid-19 tu
 
Kiapo mwendokasi! Waambie wafagizi wapambe kwenye mango kuu, nitakuja muapisha Fastafasta hapo ili watu waone kuwa hiyo ni sehemu rasmi yakuapishia.
 
Nafasi kumi alizopewa Rais na Katiba ya JMT ni kama katika wabunge waliopo hakuna mtu ana sifa anazotaka lakini sio mbunge ndio anateua sasa huyu wetu anateua watu wa ovyoovyo ili kujaza makasuku kule mjengoni shida
Mbowe hawezi kuteuliwa hata mkilialia imetoka hiyo.
 
Cha kushangaza ni Ndugai huyohuyo ndio alimfungia Halima Mdee mwaka mzima kutokukanyaga bungeni. Leo eti ana mahaba naye! Kama kuna motoni kweli basi huyu atakuwa kuni.
Leo ndugai anamwonea huruma Mdee aliyevunjwa mkono na askari magereza, dah, Shetani yupo na anaishi.
 
Back
Top Bottom