Spika Ndugai haya uliyosema kuhusu Wabunge wa CHADEMA waliofukuzwa mbona mwaka 2017 hukuyasema wabunge wa CUF walipotimuliwa?

Spika Ndugai haya uliyosema kuhusu Wabunge wa CHADEMA waliofukuzwa mbona mwaka 2017 hukuyasema wabunge wa CUF walipotimuliwa?

  1. Chadema walisusa matokeo ya uchaguzi 2020, walikaza hata walioshinda wasiende kuapishwa na kushiriki bunge
  2. Akina Halima mmeshawafukuza kwenye chama chenu tayari hivyo wametumia mbinu zao binafsi na akina Ndugai kuendelea kuhudhuria bunge pamoja na kufukuzwa kwenye chama chao.
  3. Sasa hoja ya Chadema na Bawacha kutaka Ndugai awafukuze bungeni akina Halima ni nini?. Nini kinawawasha akina Halima kubaki bungeni wakati wao wameyasusa matokeo wenyewe?
  4. Au wanataka sasa kuyakubali matokeo ya uchaguzi ule ili wachague watu wao badala ya akina Halima kwenda bungeni?.
  5. Kwani hela wanazokipwa akina Mdee kwa kwenda bungeni ni za chadema?.

  6. Nijuavyo mimi akina Halima waliona ni upuizi kuachia nafasi 19 zote ziende bure kama viongozi wa chadema walivyotaka iwe. Kwa njia zao na mipango yao wenyewe nje ya chama wakazitumia hizo nafasi badala ya zingebaki tupu au kuchukuliwa na CCM.
  7. Je, kama Ndugai angeamua kuwapa CCM hizo nafasi 19 za ubunge zilizosuswa na chadema viongozi wa chadema wangesema nini? Bado wangedai?.
  8. Chadema mlishasusa kupeleka majina 18 ya wabunge wa viti maalumu kwenda kula kiapo, pia mlitaka hata yule mbunge mmoja aliyechaguliwa jimboni asiende bungeni, hivyo wenyewe kwa njia zao wako bungeni na nyie mmeshawafukuza kwenye chama, hivyo mwacheni Spika Ndugai ahangaike nao yeye mwenyewe kwa kutumia njia zake nyie endeleeni kutoyatambua matokeo hivyohivyo.
  9. Au mnataka kuwapeleka wake zetu bungeni badala ya akina Halima? Kama ni hivyo anzeni kwanza kwa kuyakubali matokeo ya uchaguzi kabla ya kudai akina Halima watoke bungeni.
Mkuu kavulata, kwanza asante kwa bandiko hili, naunga mkono hoja.
  1. Kwanza ni kweli Chadema walisusa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga tuu. Chedema ilikuwa inafanya ujinga. Very fortunately sio wana Chadema wote ni wajinga, hivyo Halima na kundi lake la wabunge 19, waliukataa ujinga huo wa Chadema. Hawa ni mashujaa.
  2. Ni kweli Kina Halima wamefukuzwa kwa vivu tuu na ujinga, ila pia kufukuzwa kwao ni batili kwasababu Chedema haikufuata sheria, taratibu na kanuni zao wenyewe walizo jiwekea. Chadema walizoea Mmezoea vya kunyonga hamviwezi vya kuchinja. Hongera sana Halima Mdee na Makamanda wote kwa kugomea wito wa kienyejienyeji
  3. Chadema inasumbuliwa na wivu tuu wa inda!. Kitu wewe hukitaki, akikipata mwingine, unakasirika!
  4. Hili la kuyakubali matokeo ndio mpango mzima, hata mimi niliwashauri CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao
  5. Huu pia ni kuwaonea wivu tuu.
  6. Hizo njia kina Halima walizotumia ndio issue. Kwa vile nafasi za wabunge wa viti maalum, zinatolewa kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, kama kuna mbinu zozote zilizokwenda kinyume cha sheria, taratibu na kanuni katika kuwapata, then huu ni ubatili. Tusikubali Bunge letu liendeshwe kwa ubatili.
  7. Nafasi hizo ni za Chadema kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, haziwezi kugaiwa CCM, zingebaki wazi.
  8. Kwa vile kutoyatambua matokeo ni ujinga, uliosababishwa na kuchanganyikiwa na matokeo. Sasa akili zimeanza kuwakaa sawa and doing the right thing kwa kuyatambua matokeo.
  9. Huu sasa ndio mpango mzima, ila ni kama kawaida yao, sio tuu watapeleka wake zao, kwasababu kumpeleka mke bungeni ni heshima, ila watapeleka sio wake tuu, hadi vimada na vidumu!.
P
 
Chadema walisusa matokeo ya uchaguzi 2020, walikaza hata walioshinda wasiende kuapishwa na kushiriki bunge, sasa kinachowauma chadema kutaka akina Halima wasishiriki vikao vya bunge ni nini?

Akina Halima mmeshawafukuza kwenye chama chenu tayari hivyo wametumia mbinu zao binafsi na akina Ndugai kuendelea kuhudhuria bunge pamoja na kufukuzwa kwenye chama chao. Sasa hoja ya Chadema na Bawacha kutaka Ndugai awafukuze bungeni akina Halima ni nini?. Nini kinawawasha akina Halima kubaki bungeni wakati wao wameyasusa matokeo wenyewe?

Au wanataka sasa kuyakubali matokeo ya uchaguzi ule ili wachague watu wao badala ya akina Halima kwenda bungeni?

Kwani hela wanazokipwa akina Mdee kwa kwenda bungeni ni za chadema?

Nijuavyo mimi akina Halima waliona ni upuizi kuachia nafasi 19 zote ziende bure kama vionhozi wa chadema walivyotaka iwe. Kwa njia zao na mipango yao wenyewe nje ya chama wakazitumia hizo nafasi badala ya zingebaki tupu au kuchukuliwa na CCM.

Je, kama Ndugai angeamua kuwapa CCM hizo nafasi 19 za ubunge zilizosuswa na chadema viongozi wa chadema wangesema nini? Bado wangedai?

Chadema mlishasusa kupeleka majina 18 ya wabunge wa viti maalumu kwenda kula kiapo, pia mlitaka hata yule mbunge mmoja aliyechaguliwa jimboni asiende bungeni, hivyo wenyewe kwa njia zao wako bungeni na nyie mmeshawafukuza kwenye chama, hivyo mwacheni Spika Ndugai ahangaike nao yeye mwenyewe kwa kutumia njia zake nyie endeleeni kutoyatambua matokeo hivyohivyo.

Au mnataka kuwapeleka wake zetu bungeni badala ya akina Halima? Kama ni hivyo anzeni kwanza kwa kuyakubali matokeo ya uchaguzi kabla ya kudai akina Halima watoke bungeni.
Nafikiri wakati mwingine tunatakiwa kuwa wakweli pale ambapo kila kitu kiko wazi. Tusingoje kuabishwa. Pamoja na mimi kutopenda kususia uachaguzi, lakini hiyo ni hiari ya chama cha siasa. Kususia uchaguzi kunakuja na faida au hasara zote za kususia. Tokeo kubwa la kususia ni kupoteza nafasi zote ambazo zingipatikana na huo uchaguzi. Kwa maana hiyo unaposusia huwezi susia nusu nusu. Kwa kifupiwaliposusia walipoteza haki ya ubunge wa vitu maalum.

Hata kama CHADEMA wangeamuwa kususia nusu nusu, ni lazima taratibu za kujaza hizo nafasi zifuatwe. Mimi nasikitika chombe kikubwa kama bunge kwa ushauri mbovu wa Ndugai wanaweza kukubali wabunge toka CHADEMA, ambao CHADEMA ilisema haikuwateua. Kama hawakuteuliwa, hiyo inatosha kuwaondoa buneni, kwa sababu hawana kigezo chochote cha kuwaruhusu kuwa wabunge, kwa sababu sponsor wao CHADEMA amewakana.

Tatizo lingine, ni pale mwanachama anapokuwa amefukuzwa chama. Ukifukuzwa kwenye chama, huwezi kuendelea kuwa mbunge unaotegemea uteuzi wa chama husika. Hawa tayari si wanachama, kwa hiyo hawawezi kuendelea kuwa wabunge kwa sababu tayari wamekosa sifa baada ya kufukuzwa.

Mimi mara nyingi namuona Ndugai anaendesha chombo muhimu kihuni. Bunge siyo sehemu tunayotegemea kutakuwa na uvunjaji wa katiba. Bunge linatakiwa kuilinda katiba. Kuilinda katiba ni pamoja na kuhakikisha wabune wote walioapishwa au watakaoapishwa wako bungeni kisheria kwa kuwa na sifa zote za kuwa wabunge. Kama ndugai hana hakika ni juu yake kutafuta ushauri wa kisheria kuhusu hilo.

Mwisho, namuomba Ndugai aheshimu bunge na kiti chake. Aache uzandika na matani ambayo hayana tija. Matani na uzandiki na ishara tosha kuwa huyu Bwana kiti cha Uspika kimempwaya, ndiyo maana anafanya maamuzi ya ovyo na inaonekana hana msimamo. Ndugai alikuwa ni kati ya wabunge ambao walikuwa wanampigia Magufuli, lakini leo hii utamuona anajaribu na yeye kujionyesha ana mawazo yake, ndiyo maana akachomekea ishu ya bandari ya Bagamoyo, huku huko nyuma alikuwa nyuma ya ishu. Nafikiri huyu ni mtu wa kujipendekeza, na hakuna mtu wa hatari kama mtu wa kujipendekeza.
 
Kuna mambo mengine ni bora ujifunze kukaa kimiya kuliko kujidhalilisha
 
Chadema walisusa matokeo ya uchaguzi 2020, walikaza hata walioshinda wasiende kuapishwa na kushiriki bunge, sasa kinachowauma chadema kutaka akina Halima wasishiriki vikao vya bunge ni nini?

Akina Halima mmeshawafukuza kwenye chama chenu tayari hivyo wametumia mbinu zao binafsi na akina Ndugai kuendelea kuhudhuria bunge pamoja na kufukuzwa kwenye chama chao. Sasa hoja ya Chadema na Bawacha kutaka Ndugai awafukuze bungeni akina Halima ni nini?. Nini kinawawasha akina Halima kubaki bungeni wakati wao wameyasusa matokeo wenyewe?

Au wanataka sasa kuyakubali matokeo ya uchaguzi ule ili wachague watu wao badala ya akina Halima kwenda bungeni?

Kwani hela wanazokipwa akina Mdee kwa kwenda bungeni ni za chadema?

Nijuavyo mimi akina Halima waliona ni upuizi kuachia nafasi 19 zote ziende bure kama vionhozi wa chadema walivyotaka iwe. Kwa njia zao na mipango yao wenyewe nje ya chama wakazitumia hizo nafasi badala ya zingebaki tupu au kuchukuliwa na CCM.

Je, kama Ndugai angeamua kuwapa CCM hizo nafasi 19 za ubunge zilizosuswa na chadema viongozi wa chadema wangesema nini? Bado wangedai?

Chadema mlishasusa kupeleka majina 18 ya wabunge wa viti maalumu kwenda kula kiapo, pia mlitaka hata yule mbunge mmoja aliyechaguliwa jimboni asiende bungeni, hivyo wenyewe kwa njia zao wako bungeni na nyie mmeshawafukuza kwenye chama, hivyo mwacheni Spika Ndugai ahangaike nao yeye mwenyewe kwa kutumia njia zake nyie endeleeni kutoyatambua matokeo hivyohivyo.

Au mnataka kuwapeleka wake zetu bungeni badala ya akina Halima? Kama ni hivyo anzeni kwanza kwa kuyakubali matokeo ya uchaguzi kabla ya kudai akina Halima watoke bungeni.


Wewe umeshiba kweli au??!!-----Hao kina Halima ni Wanachama wa chama kipi cha siasa??, je inaruhusiwa na sheria mtu kuwa mbunge bila Chama??.

Chadema imewafutia uanachama hao akina Halima, moja kwamoja na ubunge wao unakoma.

Yeye Spika mambo ya ndani ya Chadema yanamuhusu nini??, mambo ya ndani ya Chadema ni kati ya hao waliofukuzwa uanachama na uongozi wa chama na suala hilo laweza pia kupelekwa Mahakamani, kamwe Spika hawezi kuwa hakimu wa mgogoro huo wa kisiasa.
 
Chadema walisusa matokeo ya uchaguzi 2020, walikaza hata walioshinda wasiende kuapishwa na kushiriki bunge, sasa kinachowauma chadema kutaka akina Halima wasishiriki vikao vya bunge ni nini?

Akina Halima mmeshawafukuza kwenye chama chenu tayari hivyo wametumia mbinu zao binafsi na akina Ndugai kuendelea kuhudhuria bunge pamoja na kufukuzwa kwenye chama chao. Sasa hoja ya Chadema na Bawacha kutaka Ndugai awafukuze bungeni akina Halima ni nini?. Nini kinawawasha akina Halima kubaki bungeni wakati wao wameyasusa matokeo wenyewe?

Au wanataka sasa kuyakubali matokeo ya uchaguzi ule ili wachague watu wao badala ya akina Halima kwenda bungeni?

Kwani hela wanazokipwa akina Mdee kwa kwenda bungeni ni za chadema?

Nijuavyo mimi akina Halima waliona ni upuizi kuachia nafasi 19 zote ziende bure kama vionhozi wa chadema walivyotaka iwe. Kwa njia zao na mipango yao wenyewe nje ya chama wakazitumia hizo nafasi badala ya zingebaki tupu au kuchukuliwa na CCM.

Je, kama Ndugai angeamua kuwapa CCM hizo nafasi 19 za ubunge zilizosuswa na chadema viongozi wa chadema wangesema nini? Bado wangedai?

Chadema mlishasusa kupeleka majina 18 ya wabunge wa viti maalumu kwenda kula kiapo, pia mlitaka hata yule mbunge mmoja aliyechaguliwa jimboni asiende bungeni, hivyo wenyewe kwa njia zao wako bungeni na nyie mmeshawafukuza kwenye chama, hivyo mwacheni Spika Ndugai ahangaike nao yeye mwenyewe kwa kutumia njia zake nyie endeleeni kutoyatambua matokeo hivyohivyo.

Au mnataka kuwapeleka wake zetu bungeni badala ya akina Halima? Kama ni hivyo anzeni kwanza kwa kuyakubali matokeo ya uchaguzi kabla ya kudai akina Halima watoke bungeni.
Ndiyo uhiru wenyewe huu wa kutoa maoni yako, ingawaje ni vyema ujipime mwenyewe kwanza kwa kile ambacho kipo ndani ya mada ili uweze kupata uhalisia juu yake.
 
Chadema walisusa matokeo ya uchaguzi 2020, walikaza hata walioshinda wasiende kuapishwa na kushiriki bunge, sasa kinachowauma chadema kutaka akina Halima wasishiriki vikao vya bunge ni nini?

Akina Halima mmeshawafukuza kwenye chama chenu tayari hivyo wametumia mbinu zao binafsi na akina Ndugai kuendelea kuhudhuria bunge pamoja na kufukuzwa kwenye chama chao. Sasa hoja ya Chadema na Bawacha kutaka Ndugai awafukuze bungeni akina Halima ni nini?. Nini kinawawasha akina Halima kubaki bungeni wakati wao wameyasusa matokeo wenyewe?

Au wanataka sasa kuyakubali matokeo ya uchaguzi ule ili wachague watu wao badala ya akina Halima kwenda bungeni?

Kwani hela wanazokipwa akina Mdee kwa kwenda bungeni ni za chadema?

Nijuavyo mimi akina Halima waliona ni upuizi kuachia nafasi 19 zote ziende bure kama vionhozi wa chadema walivyotaka iwe. Kwa njia zao na mipango yao wenyewe nje ya chama wakazitumia hizo nafasi badala ya zingebaki tupu au kuchukuliwa na CCM.

Je, kama Ndugai angeamua kuwapa CCM hizo nafasi 19 za ubunge zilizosuswa na chadema viongozi wa chadema wangesema nini? Bado wangedai?

Chadema mlishasusa kupeleka majina 18 ya wabunge wa viti maalumu kwenda kula kiapo, pia mlitaka hata yule mbunge mmoja aliyechaguliwa jimboni asiende bungeni, hivyo wenyewe kwa njia zao wako bungeni na nyie mmeshawafukuza kwenye chama, hivyo mwacheni Spika Ndugai ahangaike nao yeye mwenyewe kwa kutumia njia zake nyie endeleeni kutoyatambua matokeo hivyohivyo.

Au mnataka kuwapeleka wake zetu bungeni badala ya akina Halima? Kama ni hivyo anzeni kwanza kwa kuyakubali matokeo ya uchaguzi kabla ya kudai akina Halima watoke bungeni.
 
Kutokana na shinikizo la kutaka wabunge hawa waondolewe Bungeni, na pia ili kumpa Spika amani na zaidi ili kulinda hadhi ya Bunge isiendelee kuporomoka, wenye mamlaka watawataka wabunge hawa wajiuzu ila watahakikisha wanalindwa hata wakiwa nje ya Bunge.
Endelea kusubiri meli airport
Hiyo ni mpaka 2025
 
Kwa mfano CHADEMA kuna loopholes zipi ?
Sina details kama wamefanya ama la, ila naziona hizi

1. Ile barua ya Halima na wenzie ni forged. Je, imefunguliwa kesi ya jinai Mahakamani kuikana ile? Kama bado, kwanini na tunangojea nini?

2. Kwanini Baraza Kuu haliitishwi kama Kamati Kuu ilikutana kujadiri jambo lilelile kwa dharura?

3. Ni kweli kwamba barua ilikwenda kwa Ndugai bila hizo attachments? Kama ni kweli, je, hatujui utaratibu?

4. Kwanini tuliukubali “ushindi” wa Aidah na tukawa happy aingie Bungeni ila tunang’aka na hatutaki kupeleka Wabunge wa Viti maalumu ambao na wao ni zao la uchaguzi uleule haramu uliotupatia Aidah

5. Hivi Chama kilishaandika barua Tume kuikana ile barua ya kuwatambulisha Halima na wenzie? Vipi kuhusu barua kwa Tume (sio Bunge) kuijulisha kwamba wale watu walishafukuzwa uanachama?
 
Sina details kama wamefanya ama la, ila naziona hizi

1. Ile barua ya Halima na wenzie ni forged. Je, imefunguliwa kesi ya jinai Mahakamani kuikana ile? Kama bado, kwanini na tunangojea nini?

2. Kwanini Baraza Kuu haliitishwi kama Kamati Kuu ilikutana kujadiri jambo lilelile kwa dharura?

3. Ni kweli kwamba barua ilikwenda kwa Ndugai bila hizo attachments? Kama ni kweli, je, hatujui utaratibu?

4. Kwanini tuliukubali “ushindi” wa Aidah na tukawa happy aingie Bungeni ila tunang’aka na hatutaki kupeleka Wabunge wa Viti maalumu ambao na wao ni zao la uchaguzi uleule haramu uliotupatia Aidah

5. Hivi Chama kilishaandika barua Tume kuikana ile barua ya kuwatambulisha Halima na wenzie? Vipi kuhusu barua kwa Tume (sio Bunge) kuijulisha kwamba wale watu walishafukuzwa uanachama?
1. Haijalishi waliteuliwa kihalali au siyo kihalali wakishafutwa uanachama wanapoteza sifa ya ubunge na hili limekuwa likifanyika mara kwa mara kuna wabunge nane wa CUF walifukuzwa na Lipumba na kesi ikiwepo Mahakamani Ndugai aliwaondoa bungeni akiwa South Africa.

2. Speaker anapaswa kupewa taarifa na siyo minutes za vikao hata sheria ya uchaguzi iko wazi juu ya hilo.

Ni kuulize hivi Spika anatumia sheria ipi kuomba mihutasari ya vikao vya CHADEMA ?

Kamati kuu ina mamlaka ya kuwafukuza uanachama mwanachama yeyote hata Mbowe hilo Baraza kuu wewe unalitaka la nini ?

CHADEMA wameshaandika barua ya kuwa wao hawakufanya mchakato wa uteuzi wa hao wabunge na kwa taarifa yako katika hao 19 wawili walikuwa ni wajumbe wa kamati kuu ya chama hivyo vikao vya kuwateua vilifanyika wapi ?
 
Ndugu zangu, nawasalimu kila mmoja kwa salamu ya dini na kabila lake.

Hebu kwa muda kidogo mahaba yetu kwa vyama au mtu fulani tuweke pembeni, alichokisema Spika Ndugai, juu ya kinachotakiwa kufuatwa ili na yeye hatimaye afanye maamuzi juu ya wabunge 19 wa CHADEMA ni sahihi na mimi binafsi kama mtanzania wa kawaida nawashauri CDM wafanye hayo aliyoyashauri halafu tuone kama atakataa kuheshimu maamuzi halali, yenye hoja na sababu zenye mashiko, kutoka kwenye chama halali baada ya kufanya vikao halali, vilivyohudhuriwa na wajumbe halali, ndani ya muda halali kama unavyoelekezwa na katiba halali ya chama husika.

Tukumbuke kuwa kuna Mbunge Aida Kenani ambaye kwa mujibu wa maelezo ya siku za nyuma kutoka Chadema mara tu baada ya wabunge kuapa na yeye kwenda kuapa wakasema ameenda kinyume na maazimio ya chama hivyo baada ya kumalizana na hawa wabunge 19, watarudi kumalizana naye, sasa sijui kama kuna chochote kilichoendelea au huu mkwamo kwa wabunge 19 ndio imekua ahueni kwake kuepuka msukosuko wa kuadhibiwa.

Kwa muktadha huo huo ina maana kama Chadema wangefanikiwa kumalizana na hawa 19 kama walivyotaka, Je! Aida, naye wangemwadhibu kwa sababu amekubali kutii na kukubali wito kutoka kwa wananchi wa kuwa mwakilishi wao? Hii nayo imekaaje? Hapa binafsi ndio nauona umuhimu wa spika kuwa na msimamo na issue kama hizi nashauri pia zitungiwe sheria ili pale mbunge atakapofukuzwa kiholela holela basi alindwe kisheria hadi amalize kipindi chake na tusiwe tunalazimishwa kurudi ktk uchaguzi na kutumia gharama kubwa kwa mambo yasiyo ya msingi.

Kuna wanaosema Spika afanye kama alivyofanya kwa Sofia Simba na wabunge wa CUF, tujiulize hivi kama kipindi kile alikosea ndio na sasa arudie makosa yale, yale? Ndio Spirit tunayotaka kuihamasisha ktk kutekeleza majukumu yetu si kuna msemo unasema " kufanya kosa si kosa, bari kurudia kosa ndio kosa" sio sahihi na sio busara kama kuna mambo yalifanyika kimakosa siku za nyuma basi yarudiwe tena, hilo hapana.

Chadema, pelekeni barua, muambatanishe na muhtasari, na katiba yenu na kila kitu ambacho Spika ametaka maana yeye ndiye mwenye mamlaka ya kutekeleza hayo mnayotaka kwa mujibu wa sheria na taratibu pia mkumbuke hiki kinachoendelea ndio CCM wanachokitaka na kukifurahia na mlishuhudia makofi yaliyokuwa yanapigwa wakati Spika akitoa hotuba yake.

Mwisho kabla ya mwafaka wa kitaifa, basi tafuteni mwafaka huko ndani ili kazi iendelee, mbona wamama wale bado tunawasikia wanatoa hoja nzito na zenye maslahi kwa watanzania! Wale bado ni hazina kwa chama lakini pia sio wote wakifungiwa akaunti zao maisha yanaendelea kuwa mepesi kama ya Mwamba, hapana wengine hizo ndio fursa za kuendesha maisha yao pia.

Ushauri alioutoa Spika ni muhimu ukazingatiwa.
 
Sina details kama wamefanya ama la, ila naziona hizi

1. Ile barua ya Halima na wenzie ni forged. Je, imefunguliwa kesi ya jinai Mahakamani kuikana ile? Kama bado, kwanini na tunangojea nini?...
CHADEMA wameandika barua mbili na wameshaitisha press conference zaidi ya mbili kuongelea jambo lile lile kuwa hawakufanya uteuzi wa wagombea na wagombea hawateuliwi na BAWACHA wanateuliwa na kamati kuu
 
CHADEMA wameandika barua mbili na wameshaitisha press conference zaidi ya mbili kuongelea jambo lile lile kuwa hawakufanya uteuzi wa wagombea na wagombea hawateuliwi na BAWACHA wanateuliwa na kamati kuu
Barua imeandikwa kwa nani sasa? But forgery ni kosa kisheria na hatuwezi kuandika barua tu, tukatulia as if nothing ever happened na kuliacha kama lilivyo. He who alleges must prove.

Kwanini wasiteuliwe wengine 19 kwa kuwa wale wa kwanza Chama hakiwatambui?
 
Bila aibu wala kuona soni unadiriki kusema kuwa ili uamini kuwa hao akina Mdee na wenzake 18 lazima upewe muhtasari wa kikao kilichowafukuza? Mbaya zaidi unaongea bila aibu kuwa ili wewe upate uthibitisho kuwa hao akina Mdee walifukuzwa unataka uthibitisho kuwa natural justice ilizingatiwa. Hivi una mshipa wa aibu kweli?...
Kwan Pascal mayala anasemaje juu ya hili? Ngoja aje atupe facts 🤣🤣
 
Mkuu kavulata, kwanza asante kwa bandiko hili, naunga mkono hoja.
  1. Kwanza ni kweli Chadema walisusa, kwa maoni yangu, huu ni ujinga tuu. Chedema ilikuwa inafanya ujinga. Very fortunately sio wana Chadema wote ni wajinga, hivyo Halima na kundi lake la wabunge 19, waliukataa ujinga huo wa Chadema. Hawa ni mashujaa..
Sawa kada mtiifu
 
Bila aibu wala kuona soni unadiriki kusema kuwa ili uamini kuwa hao akina Mdee na wenzake 18 lazima upewe muhtasari wa kikao kilichowafukuza? Mbaya zaidi unaongea bila aibu kuwa ili wewe upate uthibitisho kuwa hao akina Mdee walifukuzwa unataka uthibitisho kuwa natural justice ilizingatiwa. Hivi una mshipa wa aibu kweli?

Kama natural justice haukuzingatiwa mbona walikata rufaa? Kama kulikuwa hakuna kikao halali mbona walikata rufaa?

Mwaka 2017 mwezi julai ulipokea barua toka kwa Lipumba juu ya wabunge wa CuF waliofukuzwa. Na wewe bila mashariti yoyote unayotoa sasa hivi uliridhia kuwafukuza. Iweje kwa hawa akina mama 19 ndio uwe na masharti?

Tumia akili na utambue kuwa katiba ni sheria mama.

 
Back
Top Bottom