Spika Ndugai: Nyani wanashangilia kifo cha mkulima wa mahindi wanasahau mwakani hawana pa kula

Spika Ndugai: Nyani wanashangilia kifo cha mkulima wa mahindi wanasahau mwakani hawana pa kula

Hii kauli ya Spika wa bunge mh Ndugai inafikirisha sana.

Hao nyani wanaofurahia kifo cha hayati Magufuli ni akina nani?

Je, ni Ufipa?

Na kwanini mwakani watakosa chakula?

Hata hivyo Ndugai amesema wanaoshangilia wanajidanganya Tanzania haitarejea kuwa shamba la bibi kamwe.

Maendeleo hayana vyama!

========================

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, amewashukia watu wanaofurahia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Magufuli (61), kilichotokea Jumatano ya tarehe 17 Machi 2021.

Kiongozi huyo wa mhimili wa bunge, amewashukia watu hao leo Jumatatu tarehe 22 Machi 2021, wakati mwili wa Hayati Rais Magufuli ukiagwa na wabunge kwenye viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Hayati Magufuli amefariki dunia katika Hospitali ya Mzena, mkoani Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu ya matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo.

Akizungumzia kifo hicho, Spika Ndugai amewafananisha watu hao na nyani waliofurahia kifo cha mwenye shamba la mahindi, ambaye alikuwa anawazuia kula mahindi yake.

“Sasa iko hadithi ya wale nyani walioshambulia shamba la mkulima kwenye mahindi, wakifurahi sana mahindi yanapokuwa yanaiva wanavuna wanakula, walipopata habari mwenye shamba amefariki wale nyani walifurahi sana.”

“Naamini katika nchi yetu manyani wa namna hii hawakosekani, lakini wakasahau mwaka uliofika wakati mahindi kuiva wakarudi shambani kula mahindi wakasahau mwenye shamba alifariki mwaka jana wakawa wanasikitika,” amesimulia Spika Ndugai.

Spika Ndugai ameshauri Watanzania, wasiwe kama ngedere hao kwa kutofanya mambo mabaya ambayo hayati Rais Magufuli aliyakataza.
Nyani atakuwa Tundu Lissu na genge lake la wapigaji
 
Kauli kama hizi hazijengi, wala hazitakiwi kutoka kwenye kinywa cha mtu kama Spika wa Bunge. Binafsi sipendi watanzania wengi ambavyo wameonesha hisia chanya juu ya msiba wa Raisi Magufuli, japo ukitazama kwa undani utafahamu kweli wengi waliumizwa sana (Japo kiuungwana hili halihalalishi watu kushangilia).

Katika mtazamo wa uhalisia, ndani ya miaka mitano iliyopita watu walinyamazishwa kwa nguvu ya dola, sasa huu ndiyo wakati muafaka wanatumia kuyatoa ya moyoni (Venting out anger and frustrations). Hivyo ni heri uwaache waongee wee mwishoni yataisha na watanyamaza na kujirudi. Ukitaka kuwazuia watu wasiseme huku mwenyewe Spika ulikuwa ni sehemu ya tatizo nadhani mtajenga chuki kubwa sana na kumponza hata Raisi mpya.

Tanzania ni yetu sote, hili nalo japo linaumiza lakini litapita na mambo yatakaa sana.
Tuache propaganda za kipumbavu zinazoligawa taifa na tusonge mbele.
 
Most of you miss the point kwanini wanyonge mnaowasemea ndio msiba umewagusa sana.

If you know anything about Maslow hierarchy of needs Magufuli alichowapa watu maskini kwanza ni sense of belonging ndani ya nchi yao.

Kuwatoa unyonge kama ilivyozoeleka hawana sauti, haki zao kupata shida na awasikilizwi.

Magufuli kawarudishia hiyo hadhi wana haki kama mtu yeyote ndani ya taifa lao na jukumu la viongozi kuwasikiliza na kuja na majibu.

Huko kwenye uchumi ni swala la muda hizi investment zipo Kwenye incubation period kuna faida tayari but full impact ni miaka 5–10 baada ya kukamilika na ndipo hapo ajira zitakuja.

Swala la wages ni serikali sasa sio mimi but then inabidi uone na faida zenyewe, ideal mfanyabiashara anaelipa kodi bora aongeze mishahara ili expenses zake ziongeke kuliko hiyo hela alipe kodi.

So kabla ya kulaumu watu onyesha faida zao then demand minimum wages.
Bahati mbaya hayo yaliweza fanya kazi, under 1 man show, tuulizane ametuachia mfumo dhabiti wa kuendeleza haya??

Miaka 5-10 ijayo, hii generation hapa inakuwa imedhulumika, wengi wamesoma kwa mikopo ambayo HESLB haijali wana vipato au hawana inawapiga penalty.
Unahalalishaje hawa kupoteza gap la maisha, in the meantime ndugu, rafiki, watoto wa vigogo hawajawahi kukosa kazi!

Nazidi kusema ku-terrorize the mass, kuwa demoralize kama hawa graduates wasio na ajira wala vipato huku wakiambiwa wajiajiri na vigogo walio kwenye maviete kama wabunge wanaojilipa milumbesa, na kuhakikisha wamatumbi they remain poor, na waaamini wao ni wanyonge ili kazi ya kuwatawala na siyo kuwaongoza iwe rahisi.
Ndiyo maana nasema wale waliozaliwa kwenye asali na maziwa hawawezi kuelewa kilio chetu wanyonge wa kweli siyo wale waliokuwa wanasimama kwenye majukwaa. Wakati wa ziara na kupewa mil5 wakilalamika nyungo zao zimebebwa na mgambo wa jiji.

Demoralize, terrorize and make sure they are poor enough to believe u their savior not their ruler.
Psychological!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Huyu jamaa akili yake ina walakini sana.....

Moja, je leo ni siku muafaka ya kuanza kuzebezana na kuvutana na kuleta kebehi ?

Mbili, Yaani Nchi na Taasisi zote zinamtegemea mtu mmoja, kwamba yeye akiondoka kila kitu kinasimama ? (kama ndivyo wote watoke huko pamoja na yeye tutafute mtu mmoja / mkulima sababu inaonyesha hao wengine wote waliopo hawawezi kazi...

Haya ya watu wengine kufurahia ni kazi nzuri / mbaya iliyofanywa na Awamu ya Tano ya Kuwatenga watu badala ya kuwaunganisha (hakuna sababu ya kuendelea kuonyesha utofauti hususan wakati huu ambapo nchi imeingia kwenye tafrani ambayo haijawahi kuingia) Huyu mtu asiye na busara anaendelea kuongeza ufa wa mshikamano... (Bure Kabisa...)
 
Waislam wengi ni watu waungwana sana (though mimi sio Muslim). Kwenye hotuba ya Speaker wa baraza la wawakilishi na yule mbunge (mwislam) aliyeenda kusoma dua wamemeombea Hayati Magufuli msamaha kwa kuwa wanatambua kuwa Magufuli alikuwa binadamu hivyo kuna watu aliwakosea. Hawa wa kwetu wameanza kuita wenzao manyani. Inasikitisha sana.
Ni imani tu mkuu. Wakristo wana amini kuwa kila nafsi ni huru, ndiyo maana wanabatiza ili unapofanya dhambi, wakiamini kuwa kila nafsi ina dhambi, unatubu mwenyewe. Na unatubu ukiwa hai. Kwa hiyo hayati rais alitakiwa awe ameshatubu dhambi zake alipokuwa hai wakristo wengine wanamuombea tu raha ya milele.
 
Bahati mbaya hayo yaliweza fanya kazi, under 1 man show, tuulizane ametuachia mfumo dhabiti wa kuendeleza haya??

Miaka 5-10 ijayo, hii generation hapa inakuwa imedhulumika, wengi wamesoma kwa mikopo ambayo HESLB haijali wana vipato au hawana inawapiga penalty.
Unahalalishaje hawa kupoteza gap la maisha, in the meantime ndugu, rafiki, watoto wa vigogo hawajawahi kukosa kazi!

Nazidi kusema ku-terrorize the mass, kuwa demoralize kama hawa graduates wasio na ajira wala vipato huku wakiambiwa wajiajiri na vigogo walio kwenye maviete kama wabunge wanaojilipa milumbesa, na kuhakikisha wamatumbi they remain poor, na waaamini wao ni wanyonge ili kazi ya kuwatawala na siyo kuwaongoza iwe rahisi.
Ndiyo maana nasema wale waliozaliwa kwenye asali na maziwa hawawezi kuelewa kilio chetu wanyonge wa kweli siyo wale waliokuwa wanasimama kwenye majukwaa. Wakati wa ziara na kupewa mil5 wakilalamika nyungo zao zimebebwa na mgambo wa jiji.

Demoralize, terrorize and make sure they are poor enough to believe u their savior not their ruler.
Psychological!

Everyday is Saturday............................... 😎
Kwenye kuendeleza kusimamia haki mwenye macho aambiwi tazama, viongozi wote wameona vilio vya wananchi wanyonge nani atawatetea tena.

Kwenye uchumi nadhani umeshakutana na msemo ‘Rome wasn’t built in a day’.

Sometimes sacrifices za leo ni lazima kwa faida ya kizazi kijacho. Watu waliojenga canals nchi za wenzetu, njia za train za juu na underground; na infrastructure zingine engineers walioshiriki kwenye main designing kwa umri wao wengi waliona mwanzo tu wa projects zenyewe.

Hii miradi ya leo ndio itamfanya mtu alie Arusha miaka ijayo badala kufikiria uwekezaji ni kwenye sector ya utalii tu; kuna opportunity ya kuleta alizeti kutoka Shinyanga mpaka Arusha na train na kukamua mafuta huku aki target soko la kaskazini na nchi jirani.

Watu wanafikiria kutokana na fursa zilizopo, uwezi kufikiria kujenga kiwanda cha kuongeza thamani ya maharage (tin packaging) Tanga wakati hujui utayotoa vipi kutoka mbeya. Lakini ukishawawekea wanatanga access ya barabara au train wanaweza kufikiria hizo possibilities ndio uchumi unavyokua.

Serikali aiwezi kusema iache kutoa elimu kisa inazalisha wasomi kushinda uwezo wa soko kuajiri, hiyo itakuwa ni kuwanyima raia wengine haki zao za msingi. Kwa sasa ni jukumu la wahitimu kuwa wabunifu.

Kupata kwao ajira baada ya kumaliza masomo sio jukumu la serikali, kazi ya serikali ni kuweka mazingira ya kuvutia uwekezaji zaidi ili ajira zizalishwe ndio alichokuwa anajaribu kuwafanyia Magufuli.

Umeshawai kuisikia hii hadithi ya ‘Walt Disney’, alifariki miezi michache kabla ya theme park yake ya kwanza kufunguliwa.

Siku ya uzinduzi mdogo wake akaulizwa “it’s a shame, Walt isn’t here to witness the opening” jibu lake lilikuwa lifuatalo “not at all, he saw all of this first in his head before any of us”. Ndio baadae mtakavyokuja kumuelewa Magufuli investment zikianza kuleta faida.
 
Hii kauli ya Spika wa bunge mh Ndugai inafikirisha sana.

Hao nyani wanaofurahia kifo cha hayati Magufuli ni akina nani?

Je, ni Ufipa?

Na kwanini mwakani watakosa chakula?

Hata hivyo Ndugai amesema wanaoshangilia wanajidanganya Tanzania haitarejea kuwa shamba la bibi kamwe.

Maendeleo hayana vyama!

========================

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, amewashukia watu wanaofurahia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Magufuli (61), kilichotokea Jumatano ya tarehe 17 Machi 2021.

Kiongozi huyo wa mhimili wa bunge, amewashukia watu hao leo Jumatatu tarehe 22 Machi 2021, wakati mwili wa Hayati Rais Magufuli ukiagwa na wabunge kwenye viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Hayati Magufuli amefariki dunia katika Hospitali ya Mzena, mkoani Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu ya matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo.

Akizungumzia kifo hicho, Spika Ndugai amewafananisha watu hao na nyani waliofurahia kifo cha mwenye shamba la mahindi, ambaye alikuwa anawazuia kula mahindi yake.

“Sasa iko hadithi ya wale nyani walioshambulia shamba la mkulima kwenye mahindi, wakifurahi sana mahindi yanapokuwa yanaiva wanavuna wanakula, walipopata habari mwenye shamba amefariki wale nyani walifurahi sana.”

“Naamini katika nchi yetu manyani wa namna hii hawakosekani, lakini wakasahau mwaka uliofika wakati mahindi kuiva wakarudi shambani kula mahindi wakasahau mwenye shamba alifariki mwaka jana wakawa wanasikitika,” amesimulia Spika Ndugai.

Spika Ndugai ameshauri Watanzania, wasiwe kama ngedere hao kwa kutofanya mambo mabaya ambayo hayati Rais Magufuli aliyakataza.
..
Hii kauli ya Spika wa bunge mh Ndugai inafikirisha sana.

Hao nyani wanaofurahia kifo cha hayati Magufuli ni akina nani?

Je, ni Ufipa?

Na kwanini mwakani watakosa chakula?

Hata hivyo Ndugai amesema wanaoshangilia wanajidanganya Tanzania haitarejea kuwa shamba la bibi kamwe.

Maendeleo hayana vyama!

========================

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, amewashukia watu wanaofurahia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Magufuli (61), kilichotokea Jumatano ya tarehe 17 Machi 2021.

Kiongozi huyo wa mhimili wa bunge, amewashukia watu hao leo Jumatatu tarehe 22 Machi 2021, wakati mwili wa Hayati Rais Magufuli ukiagwa na wabunge kwenye viwanja vya bunge jijini Dodoma.

Hayati Magufuli amefariki dunia katika Hospitali ya Mzena, mkoani Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu ya matatizo ya mfumo wa umeme wa moyo.

Akizungumzia kifo hicho, Spika Ndugai amewafananisha watu hao na nyani waliofurahia kifo cha mwenye shamba la mahindi, ambaye alikuwa anawazuia kula mahindi yake.

“Sasa iko hadithi ya wale nyani walioshambulia shamba la mkulima kwenye mahindi, wakifurahi sana mahindi yanapokuwa yanaiva wanavuna wanakula, walipopata habari mwenye shamba amefariki wale nyani walifurahi sana.”

“Naamini katika nchi yetu manyani wa namna hii hawakosekani, lakini wakasahau mwaka uliofika wakati mahindi kuiva wakarudi shambani kula mahindi wakasahau mwenye shamba alifariki mwaka jana wakawa wanasikitika,” amesimulia Spika Ndugai.

Spika Ndugai ameshauri Watanzania, wasiwe kama ngedere hao kwa kutofanya mambo mabaya ambayo hayati Rais Magufuli aliyakataza.
..shamba siyo la mtu, ni la "manyani wote" mwakani hakuna shaka ya chakula kwani haliko wazi hadi sasa. Yupo nyani mteule na tayari kaanza kutia mbegu shambani.
 
Back
Top Bottom