Spika Ndugai: Rais Samia naomba unisamehe kwa sintofahamu iliyotokana na kauli yangu🙏

Spika Ndugai: Rais Samia naomba unisamehe kwa sintofahamu iliyotokana na kauli yangu🙏

RWANDES

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2019
Posts
1,788
Reaction score
4,401
Baada ya matamko kutoka viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi na serikali dhidi ya kauli ya Spika Job Ndugai kuhusu mikopo, leo Jumatatu saa 5:00 asubuhi, Ndugai anazungumza na waandishi wa habari, jijini Dodoma.



radhi-pic-data.jpg

NDUGAI: NIMEUMIA KUOENEKANA NAPINGA MKOPO WA SERIKALI WA TSH. TRILIONI 1.3

Spika Job Ndugai amesema kauli yake aliyoitoa Desemba 26, 2021 alipoalikwa kwenye tukio la makumbusho ya wagogo kuwa imechukuliwa vibaya na kuleta mkanganyiko

Amesema alikuwa anazungumza kuhusu sababu iliyoifanya bunge kukubali na kuipitisha tozo na sio kuwa alikuwa akizungumzia taasisi nyingine yoyote

Ndugai amesema video iliyosambaa ilikatwa bila kuleta ujumbe kamili aliokuwa amekusudia. Ameumia kuonekana anapinga mkopo wa serikali

NDUGAI: TUTENGENEZE MAKUMBUSHO YA BUNGE

Spika wa Bunge Job Ndugai, amesema ni muhimu kwa Bunge kuwa na makumbusho yake ili wanaotembelea ofisi hizo wajue historia ya bunge kwa namna ilivyokuwa

Jambo hilo amesema ni muhimu hata kwa taasisi nyingine kuwa na makumbusho yake ili watu waweze kujua kuhusu historia ya taasisi husika

Amesema hayo alipokuwa anaongea na waandishi wa habari ofisi za Bunge Dodoma

NDUGAI: NAMUOMBA RADHI RAIS NA WANANCHI WOTE

Spika wa Bunge Job Ndugai amemuomba radhi Rais Samia Suluhu na wananchi wote kwa sintofahamu iliyotokana na kauli yake

Amesema yeye ni CCM ambao lengo lao ni moja hawawezi kutofautiana. Kuna watu wanaojaribu kuwafarakanisha lakini hawatafanikiwa

Ndugai amesema Rais anafanya vizuri lakini peke yake hawezi kwa hiyo ni jukumu la watu wote kumsaidia


Pia soma;
Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni
 
Yaani unaweza andika hiyo habari hata bila kuhudhuria huo mkutano au kumsikiliza ... inajulikana atakachosema, kwa Mwandishi kuhudhuria ni kupoteza tu muda ... pia atakazia kupiga watu mkwara kuheshimu bunge
 
Baada ya matamko kutoka viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi na serikali dhidi ya kauli ya Spika Job Ndugai kuhusu mikopo, leo Jumatatu saa 5:00 asubuhi, Ndugai anazungumza na waandishi wa habari, jijini Dodoma.

Baada ya matamko kutoka viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi na serikali dhidi ya kauli ya Spika Job Ndugai kuhusu mikopo, leo Jumatatu saa 5:00 asubuhi, Ndugai anazungumza na waandishi wa habari, jijini Dodoma.

Asije kuyakana Meneno yake tu na kusema wamnukuu vibaya.
 
Police wanasemaje, kuhusu intelejinsia? Uendelee au la!
Kosa kubwa kama atasema amenukuliwa vibaya, kwa nafasi yake apaswi kuomba radhi ni kujiuzulu tu, kwa kuwa mawazo yake yanatofauti kubwa na mihimili mkuu.
lakini mawazo yake kuna baadhi wanayaunga mkono, mwisho kwa nafasi yake kukoromewa na mwenezi wakata, wawilaya na bado aendelee kutumika nafasi hiyo si sawa!
 
Naachia Ngazi by Edward Lowassa 2008!
Kama siyo Uspika huyu kichaa angekuwa ameshafukiwa kabulini siku nyingi tu.

Hana jeuri hiyo, hata kuropoka kwake ni sababu ya kunyimwa mgao na mama.

Alivyopewa dollar laki moja alikuwa akimsifu mama, leo za Covid hajapewa mgao ndio hasira zake.

Kinachonikera mimi ni Magufuli kutumia pesa za umma kumnunulia mashine ya dayalisis mtu mmoja tena ipo nyumbani kwake, hii ndio siri ya Ndugai kuwa house boy wa Meko.
 
Back
Top Bottom