Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Akili zake zimeanza kumrudia taratibu
USHAHIDI PLEASE? AU NI HISIA ZA KINYUMBUMbona bosi wake amepoka madaraka ya bunge na mahakama na hasemi chochote, aache unafiki kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake.
Unajua sana budget zinapitishwa Magogoni(uwanja wa ndege, hospitali ya rufaa, ofisi za TRA Mkoa Chattle, n.k)USHAHIDI PLEASE? AU NI HISIA ZA KINYUMBU
Kabisa mkuuHana jipya huyo
CCM KUNA KANUNI ZINARUHUSU KUSEMA KWELI DAIMA, SASA SIJUI KAMA VYAMA VINGINE KUNA HILO JAMBO. Maana sijawahi wasikia nyumba ya jirani wakiongea mapungufu yao hadharani, hila utasikia tu huyu jamaa ni msaliti ,ha ha hapopoma ,
Mkuu
Binafsi, hadi nimeogopa maana , isijekuwa ametokewa na vya kutokewa hadi akili zimemrudia kiasi hiki.
Tangia, awe madarakani hizi ndiyo points mbili (2) ameongea.
Eeeh, mola rejesha akili za wengine pia.
Ee,eeee!!??Kumbe zimo
CCM KUNA KANUNI ZINARUHUSU KUSEMA KWELI DAIMA, SASA SIJUI KAMA VYAMA VINGINE KUNA HILO JAMBO. Maana sijawahi wasikia nyumba ya jirani wakiongea mapungufu yao hadharani, hila utasikia tu huyu jamaa ni msaliti ,ha ha ha
Mkuu umeona mbali.Ndio maaana hawaaminiki.shida halmashauri ikipewa madaraka inapanga kwa rushwa... za ngono na hela
Dodoma. Spika wa Bunge, Job Ndugai amepinga mpango wa Serikali wa kuwapangia vituo vya kazi moja kwa moja walimu wanaoajiriwa, akihoji ni kwanini inapoka madaraka ya Halmashauri.
Ndugai ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Desemba 23, 2017 ikiwa ni siku moja baada Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Selemani Jafo kutangaza majina ya walimu 3,033 waliopangiwa vituo vya kazi.
Katika kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa wa Dodoma leo, Spika Ndugai amehoji TAMISEMI ni nani hata aweze kujua ikama ya walimu shuleni. Amesema wamekuwa wakijaza walimu maeneo yasiyo na mahitaji.
"Hili jambo linakera, yaani kila mahali sasa ni TAMISEMI hadi napata shaka sasa, hivi hii zana ya D by D (ugatuaji wa madaraka) ina maana haijatafsiriwa vyema au ndiyo kupoka madaraka kwa wengine," alihoji Ndugai.
Spika ametoa mfano wa Shule ya Banyibanyi wilayani Kongwa ambayo amesema ina wanafunzi wanaoingia kidato cha tatu lakini hawajawahi kusoma masomo ya sayansi hata siku moja.
"Lakini juzi hapa mmepanga walimu na nilipita tena hapo hakuna hata mwalimu. Hawajasoma hesabu, fizikia, baiolojia, kemia na jiografia; nauliza tena wanasema Tamisemi, hivi hao walisoma wapi na ninyi mmesoma shule zipi," alihoji.
Ndugai amewatupia mzigo wabunge wa Mkoa wa Dodoma amesema wanatakiwa kuupinga mpango huo bungeni wakati yeye akiongoza vikao vya Bunge.
Pia, amepinga mpango wa utoaji fedha kwa vikundi amesema umepitwa na wakati kwa kuwa zinaliwa bure.
Amesema hakuna umuhimu wa kusema watu waunde vikundi ndipo wapewe fedha au uwezeshwaji, badala yake waangaliwe mtu mmoja mmoja ambao wanakuwa na uwezo wa kuzalisha na kisha wafuatiliwe.
Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde na Meya wa Manispaa ya Dodoma, Profesa Davis Mwamfupe kwa nyakati tofauti waliunga mkono hoja ya kutopeleka fedha kwa vikundi.
Lusinde amesema kumekuwa na utitiri wa vikundi baada ya kusikia kuna fedha wakati uwezo wa uzalishaji haupo.
"Namuunga mkono Spika katika hili, tunaunganisha watu hata wasiokuwa na mbinu za uzalishaji, naomba tuachane na vikundi havina tija kwa kuwa wanagawana fedha tu," amesema Lusinde.
Profesa Mwamfupe amesema Serikali inagawa vibaya rasilimali fedha kwa kauli ya kasungura kadogo tugawane lakini zinaishia kutoleta tija.
Akijibu hoja hizo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge amewaagiza wakurugenzi wa wilaya kuangalia ikama ya walimu na kuwatawanya mara moja.
Kuhusu fedha za vikundi kwa vijana na akina mama amesema jambo hilo liko kisheria. Amesema hakuna ubaya kuwasaidia watu mmoja mmoja ambao wanajiweza katika uzalishaji.
Unaishi Tanzania ipi kushindwa kujua kuwa hayo yapo?Je unao ushahidi? Usiongee kwa mambo usiokuwa na ushahidi, ukipigwa pingu hapo utaanza kulalama.
shida halmashauri ikipewa madaraka inapanga kwa rushwa... za ngono na hela
ameambiwaje kwani? press reease iko wapi mkuu. mimii naongea vitu vinavyoonekana wala am not basing on hypothesis .baruti 1
Mkuu,
You're making "makosa ya kimkakati" jiangalie sana uandikavyo...
Nape ameambiwaje baada ya kukosoa sana serikali yake ya CCM!?