Spika Ndugai: Uingereza kuna Mbunge aliapishiwa hospitali akiwa amelazwa na "bahati" mbaya alifariki bila kwenda Bungeni

Spika Ndugai: Uingereza kuna Mbunge aliapishiwa hospitali akiwa amelazwa na "bahati" mbaya alifariki bila kwenda Bungeni

Kama suala ni kuiga Uingereza mbona hawaigi kuwa na mfalume na Serikali kuongozwa na waziri mkuu kisha Bunge kuwa na nguvu ya maamuzi sahihi Spika anayeheshimu taratibu na Sheria siyo kama Tanzania Spika anatumia mawazo yake binafsi na ushauri wa mkewe kuongoza Bunge.
Fafanuzi za kisheria huenda na mifano mbalimbali bwashee!
 
No. Maendeleo yana chama. Kwa miaka kadhaa Uturuki ilikuwa ikichukuliwa kama 'mtu mgonjwa wa Ulaya' kutokana na ubovu wa uchumi wake. Vyama kadhaa vimekuja vikaondoka lakini havikuweza kuuguza gonjwa gumu la kufanya uchumi wa Uturuki angalau ufanane hata na ule wa nchi maskini zaidi Ulaya (kabla ya Umoja wa Ulaya) Ureno...
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]tatizo tukikiondoa tunaweka kipi?
 
Ndugai hao wenzetu Waingereza Katiba yao haisemi take oath before the parliament. Tatizo wewe umetunga kanuni inayokinzana na sheria mama ( katiba). Chutama.
Ndungai hutumia mifano ya kuhadithiwa tu bila takwimu wala uhakika wa hizo story, alishagundua hakuna cha kuwafanya hakuna wa kuthubutu kuwahoji chochote ndiyo maana huamua chochote kadri anavyojisikia ipo siku atamwapisha hata house girl wake na kuushangaza ulimwengu
 
Mwaka 1972 Senator Joe Biden (Rais mteule wa USA) aliapishwa akiwa hospitalini akiwauguza watoto wake wawili walionusurika kwenye ajali mbaya ya gari iliyochukua maisha ya mke wake na binti yake mdogo! Suala la wapi mtu anaapishwa linategemea na mazingira kulingana na kanuni zilizopo.
Lakini mazingira ya hawa 19 hayakua na udharula kama hao waliokua hospitalized....... Hawa walikua kwenye mazingira ya uhuru wa ku organise uapishwaji katika taratibu za kawaida. Tena wako 19, angekua ni mmoja tungesema labda kulikua na mazingira ambayo hayawezi kuwekwa wazi.
 
Lakini mazingira ya hawa 19 hayakua na udharula kama hao waliokua hospitalized....... Hawa walikua kwenye mazingira ya uhuru wa ku organise uapishwaji katika taratibu za kawaida. Tena wako 19, angekua ni mmoja tungesema labda kulikua na mazingira ambayo hayawezi kuwekwa wazi.
Tatizo la Ndungai na ccm kwa ujumla ni dharau kubwa waliowafanyia watanzania, wanawadharau wananchi kwa kiwango cha kutisha sana,
 
Lakini mazingira ya hawa 19 hayakua na udharula kama hao waliokua hospitalized....... Hawa walikua kwenye mazingira ya uhuru wa ku organise uapishwaji katika taratibu za kawaida. Tena wako 19, angekua ni mmoja tungesema labda kulikua na mazingira ambayo hayawezi kuwekwa wazi.
Amesema wanatakiwa kuingia kwenye kamati za bunge na kuanza kazi!
 
We Mzee Ndugai, kila Halima na kundi lake washakubali kuwa wamefukuzwa uanachama na sasa wanafanya utaratibu wa kukata rufaa kwenye kikao cha juu cha chama chao.

Sasa we Mzee mbona unawangangania wawe wabunge? Kwa nini unapenda sana kuingiza nchi kwenye vikwazo vya kikatiba?
 
Amesema wanatakiwa kuingia kwenye kamati za bunge na kuanza kazi!
Na hilo ndilo lengo kuu la sarakasi zao toka mwanzo. Kama umefuatilia threads na comments nyingi kwenye hili sakata, utakua umeona watu wakiliweka katika picha hiyo. Baada ya CCM kuharibu uchaguzi na kujikuta wako wenyewe Bungeni, wakakumbuka kwamba kuna kamati za fedha Bungeni ambazo zinatakiwa kuongozwa na wabunge wa upinzani, ndipo sarakasi hizi zikaanza hasa baada ya msimamo wa CDM kuonyesha hawako tayari kupeleka wabunge wa viti maalumu. Tena CCM waligeuka na kufurahi baada ya kuona kuna angalau hiyo fursa ya hao 19 wa viti maalumu wa CDM.

Hata hivyo mbinu iliyotumika kufikia kuwapata hao wa kuwapa hizo kamati ni chafu, hilo nina uhakika umeshalijua. Halima kwenye maelezo yake ya press, haelezei mchakato wa kuwapata hao 19, anakwepa kujibu hilo swali kutokana na alivyoelekezwa nini aongee na kipi asikiongelee.

Mwisho wa yote, kama speaker aliapa kulinda na kuifuata katiba ya JMT, hastahili kuwapokea hawa wabunge wasio na chama, full stop.
 
2c14dc58-6d07-44e5-baef-35110b8a10a2.jpg
 
No. Maendeleo yana chama. Kwa miaka kadhaa Uturuki ilikuwa ikichukuliwa kama 'mtu mgonjwa wa Ulaya' kutokana na ubovu wa uchumi wake. Vyama kadhaa vimekuja vikaondoka lakini havikuweza kuuguza gonjwa gumu la kufanya uchumi wa Uturuki angalau ufanane hata na ule wa nchi maskini zaidi Ulaya (kabla ya Umoja wa Ulaya) Ureno.

Fast Forward, kimekuja chama cha Adala (Justice) cha Prime Minister Rajab Orduwan....hivi sasa Uturuki ndiyo yenye uchumi imara zaidi Ulaya, kiasi Wazungu (kama kawaida yao) wanaanza kuiweka mizengwe na kuipiga vita.

Uturuki ndiyo yenye fleet kubwa zaidi ya ndege duniani, ina uwanja mkuu zaidi wa ndege duniani, inazalisha vitu viwandani zaidi kuliko nchi zote za Ulaya ukitoa Ujerumani! Nani anasema maendeleo hayana chama? Kitoeni hicho chama chenu kizee muone kama nchi haitapaa!
itapaa kwa wachumia tumbo kama Aikael na genge lake?
 
Back
Top Bottom