Spika Ndugai: Vyuo vikuu vianze kufundisha Ujasiriamali kama vile vya Kenya vijana wasisubiri ajira ambazo hazipo!

Spika Ndugai: Vyuo vikuu vianze kufundisha Ujasiriamali kama vile vya Kenya vijana wasisubiri ajira ambazo hazipo!

Kuna rafiki zangu kama wawili hivi wamefunga biashara zao wanasema hakuna mauzo, watu hawana pesa mtaani.
Unawezaje kuanzisha huduma bila kufanya utafiti wa kile unachotaka kuuza au huduma unayotaka kutoa, washindani wako, changamoto zinazoweza kujitokeza hapo mbeleni na jinsi ya kukabiliana nazo?
Ndio maana Job kasema wafundishwe ujasiliamali HALISI sio huu wa kujibia mitihani, mfano...hakuna kumpa graduate cheti kama hajaonyesha kwa vitendo mradi wake alioubuni kabla hajamaliza masomo yake, mfano kijana anayemaliza kozi ya Ufamasia lazima aonyeshe "kijiwe" chake hata kama ni cha kuuza supu ya kongoro na chapati( naona mnacheka eti famasi na supu ya kongoro wapi na wapi) ndio, hivi unafahamu kiwanda cha kutengeneza kalamu cha BIC sasa hivi wanatengeneza nini? ( Kwa wazee wenzangu enzi zetu hapakuwepo na kalamu ya wino tofauti na Bic Afrika mashariki nzima na kalamu ya wino tulikuwa tunaiita Bic kama wengine vituo vya kuuza mafuta wanavyoviita Shell!
 
Spika Ndugai amesema ni wakati sasa vijana wetu wakaachana na mawazo ya kuajiriwa na badala yake wajikite kwenye shughuli za ujasiamali na kilimo.

Ndugai amesema vijana waliomaliza darasa la saba ni mfano mzuri wa kuigwa kwa sababu wao hawachagui kazi tofauti na wale wanaojiita wasomi ambao wanazeeka wakiwa bado wanatafuta ajira ambazo hazipo.

Amevitaka vyuo vikuu viwaige wenzao wa Kenya.

Source TBC 2

Maendeleo hayana vyama!
Pia ashauri vyuo vikuu vipunguze ada.
 
Unawezaje kuanzisha huduma bila kufanya utafiti wa kile unachotaka kuuza au huduma unayotaka kutoa, washindani wako, changamoto zinazoweza kujitokeza hapo mbeleni na jinsi ya kukabiliana nazo?
Ndio maana Job kasema wafundishwe ujasiliamali HALISI sio huu wa kujibia mitihani, mfano...hakuna kumpa graduate cheti kama hajaonyesha kwa vitendo mradi wake alioubuni kabla hajamaliza masomo yake, mfano kijana anayemaliza kozi ya Ufamasia lazima aonyeshe "kijiwe" chake hata kama ni cha kuuza supu ya kongoro na chapati( naona mnacheka eti famasi na supu ya kongoro wapi na wapi) ndio, hivi unafahamu kiwanda cha kutengeneza kalamu cha BIC sasa hivi wanatengeneza nini? ( Kwa wazee wenzangu enzi zetu hapakuwepo na kalamu ya wino tofauti na Bic Afrika mashariki nzima na kalamu ya wino tulikuwa tunaiita Bic kama wengine vituo vya kuuza mafuta wanavyoviita Shell!
Kwa bahati mbaya sana umekutana na mimi ambaye sio mtu wa siasa za kujibizana na kupindishiana maneno. Good Bye.
 
Mlimani wanafundisha ujasiriamali
Mbona ujasiriamali unafundishwa sana vyuoni, labda Mh. Spika hana taarifa sahihi na alipaswa kuuliza kwa wakuu wa vyuo kabla ya kutoa tamko hili.

"Entrepreneurial Spirit" nayo ni kipaji kama soccer. Sio kila mtu anaweza kuwa mfanyabiashara.

Ndio maana kuna wafanyabiashara wazuri ukiwapeleka katika soccer nao wanashindwa.

Tatizo mtaani hakuna pesa, hata ukilima mauzo yatakuwa ni madogo sana.
 
Spika Ndugai amesema ni wakati sasa vijana wetu wakaachana na mawazo ya kuajiriwa na badala yake wajikite kwenye shughuli za ujasiamali na kilimo.

Ndugai amesema vijana waliomaliza darasa la saba ni mfano mzuri wa kuigwa kwa sababu wao hawachagui kazi tofauti na wale wanaojiita wasomi ambao wanazeeka wakiwa bado wanatafuta ajira ambazo hazipo.

Amevitaka vyuo vikuu viwaige wenzao wa Kenya.

Source TBC 2

Maendeleo hayana vyama!

TBC1 iko wapi hapa? Unge upload video au audio na kuitupia pamoja na maelezo yako. Sasa wewe unatuambia source ni TBC1 wakati wengine huo kwetu ni msamiati tusiotaka kujua hata maana yake...

Huyu hapa Spika Ndugai. Lakini kwa upande mwingine hawa viongozi wetu ni wabinafsi sana. Na tunaweza kusema ni maboya sana na pengine hawaelewi dhamana waliyo nayo kwa wananchi na nchi hii nzuri ya Tanzania...

Sasa Spika Ndugai anapolamika wakati yeye ndiye kiongozi wa chombo cha wananchi chenye mamlaka kuu ktk nchi hii kinachoweza kuielekeza serikali nini cha kufanya kutatua jambo fulani, anakuwa haeleweki kidogo...

Tatizo hili ni kubwa mno na hii ni ishara moja tu ndogo ya kushindwa kwa SERA na MIPANGO ya chama kilichotawala nchi tangu Uhuru mwaka 1961...

Bahati mbaya zaidi ni kuwa awamu hii ya tano imepata viongozi ambao mtu anaweza kusema ni AFADHALI YA JANA....

Hawana kitu vichwani mwao kuanzia kwa Farao hadi kwa Vifarao vya chini huku. Na kama wana chochote kwenye vichwa vyao, basi ni kwa kiwango kidogo sana...

Wanatumia nguvu nyingi zaidi kuongoza kuliko BUSARA, HEKIMA, MAARIFA na UFAHAMU....


Busara (WISDOM), maarifa (KNOWLEDGE) na ufahamu/uelewa (UNDERSTANDING) ndivyo ambavyo Mfalme Sulemani aliomba kwa Mungu alipotawazwa kuwa Mfalme wa Israel enzi hizo...

Nini kilitokea baada ya kuomba hayo na kupewa na Mungu, Bwana?

Mengine yote yalifuata; ustawi Wa jamii yake yote, Amani na utulivu, Uchumi imara, upendo na furaha ya maisha katika taifa lote alilokuwa analiongoza...

Viongozi/wafalme wa mataifa ya leo, wametanguliza kujipenda wenyewe (ubinafsi), kupenda kukwezwa na kunyenyekewa, kupenda pesa na ufahari kwa kuwanyonya wananchi wanaowaongoza na wakijua kabisa kuwa wanaogolea kwenye taabu na umasikini wa kutupwa na hawana mipango ya kuwatoa huko...

OLE WAO HAWA KINA NDUGAI NA WENZAKE...
 
mimi siyo msomi lakini naamini taifa lina vijana wasomi kwalifaidi kwenye fildi tofauti tofauti
tatizo ni mfumo mbovu
mimi naona sirikali haijaweka mkakati maalumu wa kuangalia vijana hawa tunawatumia vp kupigania taifa hasa wakati huu wansomi wanapoongezeka
taifa linahitaji nguvu kazi hii mapema kwa manufaa ya sasa na baadae hasa baada ya hao wanaojidai kuchonga michongo kauli daily
 
Mtu anazaliwa automatically anakuwa na akili,mbinu za ujasiriamali
Mfano tu mtoto kutoka rombo analetwa mjini kuuza duka baada ya muda naye ana duka lake.

Biashara ukatayo fundishwa chuoni usitege kama utai apply huku mtaani
Maisha ni ujanjajanja

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom