Uchaguzi 2020 Spika Ndugai: Wabunge wa CHADEMA (Viti Maalum) wasipohudhuria mikutano mitatu wamejifukuzisha

This is one of the usual uselesses we should get used to hearing in the coming years.
 
Mkuu tuwe watulivu muda ni Mwalimu mzuri Sana, kama iliwezekana kwa Lowassa sitashangaa lolote kutokea....hii ni November mpaka April tutaona mengi.
Njaa inayokukabili wewe hadi kukudhalilisha haihusu watu wengine , Chadema haijapeleka majina ya wabunge wa viti maalum Tume , hii maana yake ni kwamba hawapo , kwa kiswahili fasaha ni kwamba wabunge hao hawapo , sasa hata kama ungekuwa bwege kiasi gani unadhani Ndugai atafukuza wabunge gani ?
 
Ana juaje yeye atakuwa hai hadi vikao vitatu viishe??
 

Afadhali umekuja huku uwafahamishe hao wabishi kipi ni kipi.
 
Halafu jisemee wewe binafsi usimsemee mtu, maana kila mmoja ana maamuzi yake...wangapi waliominiwa kuwa ni makamanda halisi lakini mwisho wa siku waliokigeuka chama mchana kweupe.

Wanasiasa wetu wengi kama sio wote ni wanafiki wanajali matumbo yao kwanza..

Kuna watu ndani ya CHADEMA humo hawalali wanaziota hizo nafasi, subiri muda utaongea.
 
Kichwa kibovu hicho, umekulupuka. Vitu viwili tafauti
 

Vipi wa CUF na ACT wamehudhuria Bunge ?
 
Samahani ndugu zangu, hili swali limeulizwa sana. Nami nauliza tena, Hivi hao wabunge anaowaongelea Ndungai ni akina nani? Kuna anayewajua kwa majina atutajie hapa. Maana simjui hata mmoja.

Sijafuatilia hilo bunge hata siku moja.
Tumia akili muamama, kishelia chaga dema wanatakiwa wapeleke hao wachumia tumbo wa vitu spesheli na wasipokuwepo mpska aplili n fyuuuuu, fyekelea kuleeeeeeeeee
 
Abunuasi
 
Hana lolote huyo. Kwa tunaosoma katikati ya Mistari hapo kuna mambo mawili tu:

1. Kufanya Propaganda ili ionekane kuna Wabunge wa Viti Maalumu wa Chadema ili baadaye waje watangaze kuwa wamewafukuza. Kufanya hivyo ni kufikiria wanaichongea Chadema kwetu Wananchi. Hizi ni Siasa za kitoto sana kufanywa na Chama kilicho ndani ya Koti la Vyombo vya Dola.

2. Ni kuwatisha hao Wabunge wanaowatongoza wakubali Offer ya kuwa Wabunge ili waharakishe kuchangamkia hiyo. Hii ni Mbinu ya kitoto na ya Kishamba sana!
 
Mkuu tuwe watulivu muda ni Mwalimu mzuri Sana, kama iliwezekana kwa Lowassa sitashangaa lolote kutokea....hii ni November mpaka April tutaona mengi.
Unanishangaza kidogo mkuu wangu 'idawa' kwa mfano wako huo wa Lowassa!

Lowassa alikuwa na 'commitment' gani na CHADEMA, mbali ya kutimiza ndoto zake alizokosa kuzitimiza akiwa CCM?

'In fact', chukua tahadhari sana unapotoa mifano ya aina hii, kwa sababu ina-'reflect' uamini ulionao mwenyewe.

Ngoja nikwambie, ni bora zaidi ungetaja mfano mwingine, kama huo unaotumia kwa 'Avatar' yako, ungeeleweka zaidi kuliko huo wa Lowassa. Lakini najua hukupenda kufanya hivyo kwa maksudi mazima.

Mkuu 'idawa' siasa na mwelekeo wa nchi yetu ulivyo sasa usizichukulie siasa hizi kimchezomchezo tena kama hivi tunavyofanya hapa JF.
Tuko kwenye siasa za kuumizana na kutesana ili mradi matakwa aliyojipangia mwenye vyombo kandamizi yanatimizwa.

Lowassa, na hao wengine na hata kipenzi chako ni kielelezo tosha cha mzaha wa siasa zilizoingizwa na huyu mwenye maguvu.
 
Hio viti maalumu wapewe polisi maana nao ni chama cha siasa wamefanya kazi nzuri Sana ya kuiweka ccm madarakani wapewe hata viti 10
Mtachukua tu hizo nafasi, aliyekuwa anazuia kesha lala mbele,
Mbowe anataka pesa kisha azire kwa lipi?
Mwenzake keshaenda kula maisha bila kazi, na mbweadanganyike aone cha mtema kuni.
Hata akina mdee kukaa nje ya bunge ndo kwa heri hiyo.

Nyie washabai humu JF ndo mmesaidia kuangusha chama baada ya kulazimisha Tundu Lisu kupeperusha bendera.
 
Huyu naye akifa utawasikia "tutamkumbuka kwa mengi, amefanya makubwa kwa taifa"[emoji3]
 
Mimi CHADEMA nasema kama Mkuu wetu Mbowe amekosa bora wakose wote. Hakuna mkubwa zaidi ya Mbowe ndani ya chama chetu.
 
Mbunge wa viti maalum hajiteui , kama Kamati Kuu haikuteua majina ni yupi anayeweza kuleta hayo majina na kwa mamlaka ipi ? Mahera alijaribu kutaka kufanya hiki kituko lakini amechemsha , hii ni kwa sababu hiyo hiyo katiba yao mbovu inakataza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…