Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
Leo spika Job Ndugai amewaapisha wabunge walioteuliwa jana na Rais Samia Suluhu na kuahirisha Bunge kwa ajili ya hafla ya kuwaapisha mawaziri jioni ya leo.
Pamoja na mambo mengine, Spika Ndugai amewaambia mawaziri na mawaziri watarajiwa kwamba Bungeni ndio nyumbani na uwaziri ni matembezi ambayo muda wowote yanaweza kumalizaka na kurudi nyumbani(Bungeni) hivyo wasisahauliane.
Kisha akawaongelea wafanyabiashara na kuwakumbusha mawaziri wanahitaji nini kujua eneo la biashara ni kipaumbele namba moja!
"Mimi nasikia kila siku habari za wafanyabiashara wa nchi hii wakilalamika, kila siku. Hivi waziri wa uwekezaji, viwanda na biashara, fedha na waoendana na hiyo kada ya biashara, mnahitaji kengele gani igongwe kusema kwamba hili eneo ni kipaumbele namba moja" Alihoji spika Ndugai
Pia Spika Ndugai ameziongelea shida za wizara za TAMISEMI, tatizo la dawa MSD na tatizo la upimaji ardhi.
Pamoja na mambo mengine, Spika Ndugai amewaambia mawaziri na mawaziri watarajiwa kwamba Bungeni ndio nyumbani na uwaziri ni matembezi ambayo muda wowote yanaweza kumalizaka na kurudi nyumbani(Bungeni) hivyo wasisahauliane.
Kisha akawaongelea wafanyabiashara na kuwakumbusha mawaziri wanahitaji nini kujua eneo la biashara ni kipaumbele namba moja!
"Mimi nasikia kila siku habari za wafanyabiashara wa nchi hii wakilalamika, kila siku. Hivi waziri wa uwekezaji, viwanda na biashara, fedha na waoendana na hiyo kada ya biashara, mnahitaji kengele gani igongwe kusema kwamba hili eneo ni kipaumbele namba moja" Alihoji spika Ndugai
Pia Spika Ndugai ameziongelea shida za wizara za TAMISEMI, tatizo la dawa MSD na tatizo la upimaji ardhi.