Sri Lanka: Wakazi zaidi ya milioni 22 waishio nchini humo wamelala gizani, na yote sababu ya Tumbili

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Sasa hii nayo imetokea usiku wa kuamkia Februari 10, 2025 huko Sri Lanka ambapo wakazi zaidi ya milioni 22 waishio nchini humo wamelala gizani, na yote sababu ya Tumbili mmoja tu. Unaambiwa Tumbili huyo aliyeruka na kuingia kwenye mfumo wa gridi ya umeme alisababisha umeme kukatika karibu eneo lote la nchi hiyo.

Waziri wa Nishati, Kumara Jayakody tayari ameshatolea ufafanuzi juu ya tatizo hilo la umeme huku akitaja sababu kubwa kuwa ni Tumbili.

Je, Mtaani kwenu, tumbili alishawahi kufanya kisanga gani hadi wote mkamchukia?”
 
Huko Sgr tumbili walininginia kwenye waya treni likasimama kwa muda!
 
ni kitendo cha kuingia darasani na kutafuta cha kula, kakosa akaishia kuchanachana madaftari ya wanafunzi waliyoyatelekeza darasani
 
Tuko shambani tumekula tukashiba tukabakisha ugali wetu na mboga dagaa, alikuja tumbili akala chakula chote kisha akabondabonda sufuria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…