St. Francis Mbeya kuna siri gani?

St. Francis Mbeya kuna siri gani?

Let's assume wanafunzi 2000 wameenda kwa interview ya kujiunga form one pale st Francis girls alafu wanafanya wrritten na oral interview baada ya hapo wanachagua wanafunzi timamu 120 pekee walopata kuanzia wastan wa 95 iv na kila wanavoingia kidato kingne wanachuja na kufukuza wasiofika viwango vya wastan wao unafikir hawawez kupata one ya7?? Inawezekana tena hata bila kuiba hata Mzumbe Kibaha kilakala iliboru tabora boys zingefanya ivo zingekuwa top kuzid hata hz za private⛷🏇🚴‍♂️
Hiyo shule haina habari za mchujo. Angalia matokeo yao ya form 2. Wanafunzi 91 wote wana div 1 za 7. Na miaka yote idadi yao ni hiyo. Wanacheza 90.
 
Hiyo shule haijaanza kufaulisha leo, ndani ya shule kuna sehemu wanaubao ambao unaonyesha nafasi waliyoshika kila mwaka kitaifa kuanzia mwaka 1997 kama sijakosea. Nimepeleka dogo hapo anasoma, shida huwa kupita kwenye interview tu na masister wako very strict.
Imeanza 98 na walikuwa wa 9.... Kuna mwaka fulani walitaka waitie kibano kwa kuiba matokea ila Rais yule aliingilia kati wakayamaliza
 
Imeanza 98 na walikua wa 9....kuna mwaka fulani walitaka waitie kibano kwa kiiba matokea ila Rais yule aliingilia kati wakayamaliza
Asante kwa marekebisho. Kuhusu kuiba mitihani sina uhakika, maana huyu dogo tangu primary alikuwa smart na huwa anasoma sana so hata anavyofaulu sishangai, na ndio ameingia form four huu mwaka.
Nakumbuka wakati wa interview kulikuwa na wanafunzi wengi sana lakini walichukuliwa 96 tu, na madarasa yao mnapitishwa kuyaona.
 
Hiyo shule haijaanza kufaulisha leo, ndani ya shule kuna sehemu wanaubao ambao unaonyesha nafasi waliyoshika kila mwaka kitaifa kuanzia mwaka 1997 kama sijakosea. Nimepeleka dogo hapo anasoma, shida huwa kupita kwenye interview tu na masister wako very strict.
Ada imefika ngapi? Na ni maswali yapi wanauliza kwenye interview?
 
Mimi binafsi nakataaa hayo matokeo aisee ,hata kama Wana akili huo ufaulu wa kiasi hicho Kuna kitu cha ziada ...hio shule ichunguzwe vzuri kuanzia miezi mitatu kabla ya kufanya mtihani na siku za mitihani
Kwa taarifa yako huwa inachunguzwa sana tu. Siri ya kufaulu kwao ni 1.Walimu wanalipwa vizuri sana, kwahiyo wanafundisha bila stress 2.Walimu wanafundisha sana 3.Motisha kwa Walimu ni nyingi Matharani kila A Ina kiwango chake Cha pesa ambayo Mwalimu analipwa akifaulisha. 4.Watoto wale wakiwa mazingira ya shule ni kuongea kingereza muda wote. 5.Mazingira mazuri na tulivu ya Wanafunzi kujisomea. 6.Screening aka mchujo wa Wanafunzi ni mkubwa Sana. 7.Commitment ya Walimu na Wanafunzi.
 
Hio shule inanunua mitihani na kufanya mwezi mmoja kabla ya mitihani ya taifa ,na huwa maswali yanarudiwa kwa msisitizo mkubwa Sana ......

Hao watoto wanaomaliza huko hawana uwezo kabisa wa kufaulu hivo ,never ever ,....

Hapa bongo ukishakiwa na pesa hakuna kinachoshinfikana ,pepar za necta zinanunuliwa na watoto Wana solve mapema kabisa ...

Hio shule ada yake tu unaweza kula mwaka mzima ,kununua pepar wizaran kupitia kwa mamuruki ni kitu rahisi Sana .....mbaya zaidi wafanyakazi wengi wa serikali dawa yao ni pesa ,kwa million 20 anakuletea pepar la necta lotee mwezi mmoja kabla .....


Niamaini Mimi haya nayoyasema
Leta ushahidi.
 
Mkuu hakuna ufaulu wa namna hio ,kwa hio ratio ....

Hapo ni wazi kabisa wamenunua mtihani na kusolve ...

Hakuna kitu kama hicho ,watoto wa kitanzania Mimi nawajua ,kuapata div 1.7 kaa watoto wote sio kwa uwezo wao ,japo wenye uwezo wapo lakin sio kwa hio idadi kabisa ...


Mimi nakataa kabisa 🤣
Kwa hiyo kila mwaka wao wananunua?

Feza schools nao kila mwaka wananunua?
 
Sie Waswahili tumewekeza sana kwny ufaulu na si ueleawa

Hizi division one kalikali zinapoteleaga wapi hadi hazionekani tena?

Tanzania one wa form four walio graduate sambamba na Samia Suluhu miaka hiyo sijui sasa hivi yupo pori gani wakati mwenzie sasa ni Rais?
Ufaulu hauna mahusiano kabisa na mafanikio kisiasa, kiuchumi na kufahamika. Ukute Wana kazi kubwa na za maana lakini kwasababu kazi zao sio za kuwapa umaarufu ndio maana huwezi kujua.
 
Tuache wivu usio na maana,
Tusiongee tusiyo yajuwa,

Tembelea ile shule uone walivyo makini.

Kuanzia kutunza muda, kazi za ziada pamoja na masomo.

Ni kweli kabla ya kuingia pale lazima mwanafunzi afanye mtihani wao, ambapo waliofaulu vizuri ndio huchaguliwa, hakuna rushwa.

Hivyo siri ya kwanza ni uchaguzi wa wanafunzi.

Siri ya pili ni walimu bora na wanao jituma.

Siri ya tatu ni motisha kwa walimu na wafanyakazi kutoka kwa mwajiri.

Siri ya nne ni nidhamu kali ikiambatana na sheria zao

Siri nyingine ni kumcha Mungu, wana ratiba nzuri ya kumcha Mungu

Siri nyingine ni nidhamu ya ratiba na muda, kwa waliopeleka watoto wao pale waulize hutokea nini wakichelewa hata dakika 5.

Hakika wanastahili pongezi.

Hivyo badala ya kubeza, yafaa kujifunza utaratibu wao wa ulezi na ufundishaji.

Ada yao 2021 ilikuwa around milioni mbili na laki tano kwa mwaka, shule nyingi pia zinatoza hivyo.

Dhana ya kwamba A level hawafaulu sana ni kwa sababu ya ufundishaji tu wa shule waendazo.

Hata huko vyuoni, sababu ni hizo hizo, na uhuru ambao hawajauzoea na hupelekea kujisahau kisha kuharibikiwa, wababa na vijana wengi huwaharibu watoto wa vyuo iwe kwa tamaa au ushawishi. Lakini pia bado wahadhiri wengine wana ile tabia ya kukomoana, ama kutofundisha ipasavyo...

#Kutokufaulu siyo chaguo!

Hongera sana kwa St. Francis Girls.


Wanastahili kwa kweli.

View attachment 2083779
 
Asante kwa marekebisho. Kuhusu kuiba mitihani sina uhakika, maana huyu dogo tangu primary alikuwa smart na huwa anasoma sana so hata anavyofaulu sishangai, na ndio ameingia form four huu mwaka.
Nakumbuka wakati wa interview kulikuwa na wanafunzi wengi sana lakini walichukuliwa 96 tu, na madarasa yao mnapitishwa kuyaona.
Wako vizuri sana. Mtihani wa form wameongoza kitaifa. Wapili Kemebos. Sasa baada ya miaka miwili tutazishutumu wizi.
 
Hivi pale St Francis Girls Mbeya, pana siri gani wazee? Mwaka huu licha ya kwamba imekua ya pili kitaifa lakini ufaulu wake ni wa ajabu na kuogofya sana.

Picha linaanza darasa lina watahiniwa 92 ambao wote wamepata div 1, hii si ajabu sana ajabu ni hili hapa kati ya hizo 1- 92, div 1.7 ambazo ndo ufaulu wa juu kabisa nchi hii kwa upande wa olevel zipo 79 yani 1.7 pale St Francis Girls zipo 79 kama utapata shida kuelewa na maanisha hivi wanafunzi waliopta A saba kwenye jumla la masomo yao wapo 79.

Mwanafunzi wa mwisho pale yani mwenye ufaulu dhaifu au unaweza kuuita goigoi ama kilaza, mmoja ana div 1.14 na mwingine ana div 1.13 na wapo wawili pekee.


Mabinti wamejua kukung'uta aisee div 1.10 ipo moja, 1.9 zipo 6 na 1.8 zipo 4


Kama unadhani maajabu yao mwaka huu ni hayo tu basi Pole mabinti hawa wameendeleza maajabu mpaka kwenye Wanafunzi bora ambapo kumi bora imepambwa na wao.Hatari sana hii mwanafunzi 1-5 kwenye kumi bora anatoka kwao afu wanajichomeka others kwenye 6,kisha namba 7 wanarudi wao afu 8,9 wanajikongoja fedha na ilboru kisha kumi kitabe kabisa wanamaliza wao.Kifupi 10 bora wanafunzi 7 wote wametoka St FRANCIS.

1. Consolata Prosper Luguva - St. Francis Mbeya🔴

2. Butoi Ernest Kangaza - St. Francis🔴

3. Wllhemia Steven - St. Francis 🔴

4. Cronel John - St Francis🔴

5. Merry George Ngoso - St Francis🔴

6. Holly Beda Lyimo - Bright Future
Girls🔴

7. Brandina - St. Francis🔴

8. Imamu Suleiman - Feza Boys

9. Mfalme Hamis Madili - Ilboru

10. Clara Straton - St. Francis🔴


Huu ufauru si wa kitoto sasa nauliza siri yao hasa ni ipi maana tangu miaka hiyo hawa mabinti wamekua moto ina maana shule zingine wameshindwa kabisa kujifunza?

View attachment 2082037

View attachment 2082038
Baraza la mitihani lijitadhini upya. Waepuke mitihani ya multiple choice haraka iwezekanavyo.
 
Mimi nimesoma chuo na watoto wanaotoka hizo shule mkuu ...

Siku ya mtihani wanakutana na maswali waliyokuwa wanasolve mwezi mmoja kabla ya necta ...

Sio kwamba siku ya mtihani wanasoviwa hapa ,ila pepar linasoviwa week kadhaa kbala ya necta na hayo maswali ndio yanatoka necta ,mbaya zaidi walimu wanawasisitiza ,.

Usiwe mjinga kuelewa mambo yanayoendelea huko ...

Wananunua mtihani ,pamoja na kuwa na mazingira mazuri ya kusomea ,walimu wazuri ,malazi ,na ufundishaji mzuri ....wananunua mtihani mkuu ....
Chuo wapi wewe? Hata sisi tumesoma na hao pia wanafunzi unamdanganya nani humu? Au kisa hakuna kujuana names humu
 
Back
Top Bottom