St. Francis Mbeya kuna siri gani?

St. Francis Mbeya kuna siri gani?

Kama una mtoto ni average pale hana nafasi,hakuna blah blah,mtoto Kipanga atapeta,akiwa slow learner wewe tafuta kwingine,St.Francis wala usiifikirie kichwani mwako,nyingine ni Cannosa na Marian,hizo usisogelee pia.
😂😂😂Hafu wanafunzi wao wote unakuta primary kasoma shule ya private ambayo ni nzuri sana, hupati Binti wa kayumba mle
 
Siri ya kwanza ni ubora wao ila pia
Kuna kaujanja ujanja fulani kwa idhini ya refa......

Ngoja niishie hapo.....

Pongezi kwa vijana wote na wale waliokosa wasijione sio kitu maisha hayahitaji kukata tamaa
Kwa idhini ya refa hembu funguka mzee wangu?
 
Hio shule inanunua mitihani na kufanya mwezi mmoja kabla ya mitihani ya taifa ,na huwa maswali yanarudiwa kwa msisitizo mkubwa Sana ......

Hao watoto wanaomaliza huko hawana uwezo kabisa wa kufaulu hivo ,never ever ,....

Hapa bongo ukishakiwa na pesa hakuna kinachoshinfikana ,pepar za necta zinanunuliwa na watoto Wana solve mapema kabisa ...

Hio shule ada yake tu unaweza kula mwaka mzima ,kununua pepar wizaran kupitia kwa mamuruki ni kitu rahisi Sana .....mbaya zaidi wafanyakazi wengi wa serikali dawa yao ni pesa ,kwa million 20 anakuletea pepar la necta lotee mwezi mmoja kabla .....


Niamaini Mimi haya nayoyasema
Muongo
 
St. Francis ni sawa na vipaji maalum kwa shule za binafsi, kwasababu wanaopita interview karibia wote wamechaguliwa vipaji maalum. Ukiwafundisha kwa spoon feed wanakua moto zaidi.

Hawa watu wako vizuri sana, kinachowafelisha mbeleni ni ujifunzaji mpya. Nakumbuka niko form 4 nafanya mitihani ya jumamosi ya kitaa akaja dogo wa Maua Seminary wa form 3 akawa anafanya mitihani ya form 4. Alitukimbiza mpaka likizo inaisha.
Walau kuna watu mnaukubali uhalisia.Hawa wanaobisha,si wapeleke kwanza watoto wao tuone kama hata watapata hiyo nafasi ya kuingia pale
 
Let's assume wanafunzi 2000 wameenda kwa interview ya kujiunga form one pale st Francis girls alafu wanafanya wrritten na oral interview baada ya hapo wanachagua wanafunzi timamu 120 pekee walopata kuanzia wastan wa 95 iv na kila wanavoingia kidato kingne wanachuja na kufukuza wasiofika viwango vya wastan wao unafikir hawawez kupata one ya7?? Inawezekana tena hata bila kuiba hata Mzumbe Kibaha kilakala iliboru tabora boys zingefanya ivo zingekuwa top kuzid hata hz za private[emoji961][emoji470][emoji2187]
Shule za vipaji maalumu za serikali nazo zinachuja wanafunzi.
 
Sie Waswahili tumewekeza sana kwny ufaulu na si ueleawa

Hizi division one kalikali zinapoteleaga wapi hadi hazionekani tena?

Tanzania one wa form four walio graduate sambamba na Samia Suluhu miaka hiyo sijui sasa hivi yupo pori gani wakati mwenzie sasa ni Rais?
Kuwa na high IQ co lazima uwe presidaa jomba, co lazima uwe ktk position inayoonekana.

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Kipindi cha magufuli kipi twende ya mwaka 2020 tu hapo. Mbona ilikua na 1 tupu na zote single digit na ilikua ya kwanza kitaifa
Let's kuanzia 2016- 2020 tuone. Sema nimeshagundua hizi shule zinachuja Sana wanafunzi wanachukua Ile cream.
Kuwa huyu mwanafunzi anayeenda hapa pia unakuta akachaguliwa shule zile zenye ufaulu mkubwa aka vipaji.
So alifika huko mwalimu anakuwa na bidii kutaka kumzidi mwanafunzi.ujue Kuna shule ambazo mwalimu Ana bidii kuliko dent.
So ukichanganya kuwa hizi shule both dent and ticha have got bidii na ushirikiano wa Hali juu. Wako committed lazima watoboe.
Mana kwa serikali ni bidii zetu kukomaa.
Binafsi advance physics na maths nimekomaa na washkaji wakanielekeza hata sidhani kuwa nilitegemea walimu kufaulu.
Olevo kidogo baadhi ya subjects yaani unaenda class tayari umeshasoma
 
Binti yangu alisomea pale na kupata div. one na ushindi huo ulimpa msingi mzuri sana wa A level na kufanikiwa kupata pointi 6 A level. St. Francis ni shule nzuri sana.
Asante sana kwa huu ushuhuda,nina Nieces wawili pia,wamepita pale na UDSM,huyo aliemaliza kwa sasa yupo TPDC na mwingine yuko mwaka wa pili ,tunasubiri akimaliza tuone atapata GPA ipi.
 
Unalosema ni kweli, angalia A zao ni za yale masomo ambayo wakipiga past paper za kutosha lazima wapate A. Waangalie katika physics Wana C na B za kutosha. Mwanafunzi akifundishwa vizuri mitihani ya kidato cha 4 ni rahisi sana kwa masomo ya sanaa.
Ndo ivo mkuu sasa nashangaa hawa watu wanaosema eti wananunua mitihani wakati ni ishu ya mipango tu.

Mi mwenyewe kuna dogo apa alikua anasoma kwa bidii somo la computer akijua wazi kua hesabu anaweza kufeli, na kweli hesabu kagonga F lakini hiyo comp ana A. Na hiyo imembeba mpaka ana diviaion 1 kabisa.

Ni mipango tu sio ishu ya kushangaza.
 
Pia aina ya watoto wanaokwenda pale ni top cream kuanzia walikotoka,halafu mtu anatuletea hapa hadithi za Shule kununua mitihani😂
Yani ni vichekesho mkuu, mpaka unashangaa inakuaje mtu ashangae huo ufaulu mpaka unapata shaka yeye alipata ngapi mpaka aone haiwezekani kupata one hizo.

Mtu kama huyu ataona ni sawa mwanae akipata hata 4 au 0 kabisa coz yeye mtihani kwake ni kitu kigumu kichizi.
 
Wanafunzi wanandaliwa vyema sana na zaid Walimu wanapewa motisha sana wanafanya kazi kwa moyo

Mwl kupewa gari kawaida sana nyumba kawaida
Bado mashahara mnono



Sent from my TECNO CX Air using JamiiForums mobile app
 
Yani ni vichekesho mkuu, mpaka unashangaa inakuaje mtu ashangae huo ufaulu mpaka unapata shaka yeye alipata ngapi mpaka aone haiwezekani kupata one hizo.

Mtu kama huyu ataona ni sawa mwanae akipata hata 4 au 0 kabisa coz yeye mtihani kwake ni kitu kigumu kichizi.
Nasoma comment nabaki kucheka tu,kama wanajua ni rahisi hivyo,si wapeleke watoto wao wakajaribu mchujo wa pale kama wataweza.
 
Sio kwamba hawafundishi ila naomba kujua data kama tatu:-

Wote walioingia walikuwa na Passmark kiasi gani (creme de la cream)
Michujo ilifanyika kiasi gani (yaani potential failures wote kuondolewa)
Ufundishaji mzuri na kulenga mitihani (sijajua uelewa wa hawa vijana wala thinking capacity yao ila Mitihani hii ilivyo unaweza ulenga mitihani kwa kukariri hata kama thinking capacity yako ni ndogo)

Kwahio binafsi ubora wa shule naupima kwa mtu kumtoa point A kwenda B; bila mchujo wala kuchagua wanaojiweza pekee..., kama mtu amekuja hajui kitu na after four years akapata hata three huenda shule hio imefanya kazi kuliko kuchukua the best na katika hao best wale wote ambao ni better kuwabakisha madarasa (hio haijengi sababu hata Div 1 mpaka Three kwa form four bado ni ufaulu na kuna a long way forward na kuna a room for improvement
Na hiki ndicho inachofanya shule kama Tusiime ile shule naipa big up sana inajua kulea wanafunzi mwanafunzi anakuja hajui kitu ila anatoka na matokeo ya kuridhisha

Siyo shule kama Marian ambazo wanachukua watoto wenye ufaulu mkubwa ili wasihangaike nao kuwalea kutoka kuwa vilaza hadi vipanga ili walinde reputation ya shule yao

Mfano Marian form five mara nyingi huwa wanachukua waliopata division one za single digits tu kwenye matokeo ya form four yaani 1.7 hadi 1.9 tu chini ya hapo hawaenroll
 
😂😂😂Hafu wanafunzi wao wote unakuta primary kasoma shule ya private ambayo ni nzuri sana, hupati Binti wa kayumba mle
Sijui wanadhani hizo Div 1 zinatokea tu kwa bahati mbaya,mtoto kapita Canossa Primary School au Liberman anakwenda St.Francis,uje ushangae kapataje division One😂
😂😂
 
Hivi pale St Francis Girls Mbeya, pana siri gani wazee? Mwaka huu licha ya kwamba imekua ya pili kitaifa lakini ufaulu wake ni wa ajabu na kuogofya sana.

Picha linaanza darasa lina watahiniwa 92 ambao wote wamepata div 1, hii si ajabu sana ajabu ni hili hapa kati ya hizo 1- 92, div 1.7 ambazo ndo ufaulu wa juu kabisa nchi hii kwa upande wa olevel zipo 79 yani 1.7 pale St Francis Girls zipo 79 kama utapata shida kuelewa na maanisha hivi wanafunzi waliopta A saba kwenye jumla la masomo yao wapo 79.

Mwanafunzi wa mwisho pale yani mwenye ufaulu dhaifu au unaweza kuuita goigoi ama kilaza, mmoja ana div 1.14 na mwingine ana div 1.13 na wapo wawili pekee.


Mabinti wamejua kukung'uta aisee div 1.10 ipo moja, 1.9 zipo 6 na 1.8 zipo 4


Kama unadhani maajabu yao mwaka huu ni hayo tu basi Pole mabinti hawa wameendeleza maajabu mpaka kwenye Wanafunzi bora ambapo kumi bora imepambwa na wao.Hatari sana hii mwanafunzi 1-5 kwenye kumi bora anatoka kwao afu wanajichomeka others kwenye 6,kisha namba 7 wanarudi wao afu 8,9 wanajikongoja fedha na ilboru kisha kumi kitabe kabisa wanamaliza wao.Kifupi 10 bora wanafunzi 7 wote wametoka St FRANCIS.

1. Consolata Prosper Luguva - St. Francis Mbeya🔴

2. Butoi Ernest Kangaza - St. Francis🔴

3. Wllhemia Steven - St. Francis 🔴

4. Cronel John - St Francis🔴

5. Merry George Ngoso - St Francis🔴

6. Holly Beda Lyimo - Bright Future
Girls🔴

7. Brandina - St. Francis🔴

8. Imamu Suleiman - Feza Boys

9. Mfalme Hamis Madili - Ilboru

10. Clara Straton - St. Francis🔴


Huu ufauru si wa kitoto sasa nauliza siri yao hasa ni ipi maana tangu miaka hiyo hawa mabinti wamekua moto ina maana shule zingine wameshindwa kabisa kujifunza?

View attachment 2082037

View attachment 2082038
Mkuu hao huwa wanaselect wenye vipaji tuu.Mchujo wao siyo wa kitoto,ni heavy duty.Mtoto wako akichaguliwa st.Francis maana yake yuko vizuri sana kichwani.Halafu wanakutana na mazingira wezeshi sana ya shule.Mimi nawaheshimu sana hao wanaopata point 7 toka government school.huyu angekuwa pale angepata A zote za mia mia
 
Na hiki ndicho inachofanya shule kama Tusiime ile shule naipa big up sana inajua kulea wanafunzi mwanafunzi anakuja hajui kitu ila anatoka na matokeo ya kuridhisha

Siyo shule kama Marian ambazo wanachukua watoto wenye ufaulu mkubwa ili wasihangaike nao kuwalea kutoka kuwa vilaza hadi vipanga ili walinde reputation ya shule yao

Mfano Marian form five mara nyingi huwa wanachukua waliopata division one za single digits tu kwenye matokeo ya form four yaani 1.7 hadi 1.9 tu chini ya hapo hawaenroll
Wameset standard yao hivyo,kwanini uwalaumu?
 
Back
Top Bottom