St. Francis Mbeya kuna siri gani?

St. Francis Mbeya kuna siri gani?

Mitihani ya siku hizi hamna kitu 1. Rais wa kwanza wa Tanzania ni nyerer......... 2. Binadamu ana macho mawi.......
Sawa mitihani ya siku hizi hamna kitu. Hebu niambie, wale wa kule Pemba na Mtwara ambao shule zao zinakuwa za mwisho kitaifa, WANAFANYA MITIHANI IPI!? Ni hiyo wanayofanya hawa wa Mbeya au mingine.!?? Kwamba ni migumu zaidi ya wanayofanya wenzao.!????
 
ina maana sisi tulosoma kipindi kile hatukuwa na akili kweli?
Unaweza ukawa uko vyema ila kwa hawa wadada achana nano hata mimi nilijitahidi nilipata point kumi na mbili O level ila kawaida tu
 
Watanzania tuko kinyume sana na mafanikio ya wengine......mioyo yetu na akili zetu muda wote zinatarajia habari mbaya na maanguko ya watu baada ya mafanikio......

Taarifa za mafanikio ya mtu au kikundi cha watu tunazipokea kwa mshituko wa chuki na hasira ili kufurahisha mioyo yetu hasi tunatafuta namna ya kuyatia doa mafanikio hayo.......

Wengi wetu hatutambui na kuthamini juhudi za watu wengine juu ya mafanikio yao badala yake tunawapachika majina mabaya......

Ili uishi Tanzania unatakiwa kuwaelewa watanzania na hawa ndio waTanzania kwa wingi wao......

Hongereni ST FRANCIS MBEYA juhudi zenu zimeonekana na kuwaangaza kwa watu wanaoshangilia na kufurahia mafanikio ya watu.....
Yaani umeandika uhalisia. Badala ya kupongeza waliofaulu, tunawalaumu kwanini wanafaulu
 
Hizi shule zina mbinu mbadala sio bure one ya saba wanafunzi wote kwa hiyo wanalingana akili wote ila hongera zao kwa sasa elimu ni biashara,huyo wa ilboru amepiga kazi sana.
Kuna shule ya kata ya kichangachui hapa kgm kuna one za saba kama 7 hawa ndio wanajeshi wa kweli hakuna biashara ni kichwa madogo wameongoza kwa somo la physics kimkoa kitaifa wamekuwa wa 36 kwa somo la physics tena shule ya kata kubaabeki hawa ndio majemedari.
 
Tuache wivu usio na maana,
Tusiongee tusiyo yajuwa,

Tembelea ile shule uone walivyo makini.

Kuanzia kutunza muda, kazi za ziada pamoja na masomo.

Ni kweli kabla ya kuingia pale lazima mwanafunzi afanye mtihani wao, ambapo waliofaulu vizuri ndio huchaguliwa, hakuna rushwa.

Hivyo siri ya kwanza ni uchaguzi wa wanafunzi.

Siri ya pili ni walimu bora na wanao jituma.

Siri ya tatu ni motisha kwa walimu na wafanyakazi kutoka kwa mwajiri.

Siri ya nne ni nidhamu kali ikiambatana na sheria zao

Siri nyingine ni kumcha Mungu, wana ratiba nzuri ya kumcha Mungu

Siri nyingine ni nidhamu ya ratiba na muda, kwa waliopeleka watoto wao pale waulize hutokea nini wakichelewa hata dakika 5.

Hakika wanastahili pongezi.

Hivyo badala ya kubeza, yafaa kujifunza utaratibu wao wa ulezi na ufundishaji.

Ada yao 2021 ilikuwa around milioni mbili na laki tano kwa mwaka, shule nyingi pia zinatoza hivyo.

Dhana ya kwamba A level hawafaulu sana ni kwa sababu ya ufundishaji tu wa shule waendazo.

Hata huko vyuoni, sababu ni hizo hizo, na uhuru ambao hawajauzoea na hupelekea kujisahau kisha kuharibikiwa, wababa na vijana wengi huwaharibu watoto wa vyuo iwe kwa tamaa au ushawishi. Lakini pia bado wahadhiri wengine wana ile tabia ya kukomoana, ama kutofundisha ipasavyo...

#Kutokufaulu siyo chaguo!

Hongera sana kwa St. Francis Girls.
Yaani kiongozi wewe ndiye umemaliza kila kitu. Comments nyingine baada ya hii ni za kunogosha tu mazungumzo sebuleni.
 
Sawa mitihani ya siku hizi hamna kitu. Hebu niambie, wale wa kule Pemba na Mtwara ambao shule zao zinakuwa za mwisho kitaifa, WANAFANYA MITIHANI IPI!? Ni hiyo wanayofanya hawa wa Mbeya au mingine.!?? Kwamba ni migumu zaidi ya wanayofanya wenzao.!????
Fidel castro pemba
IMG-20220115-WA0007.jpg
 
Wakiingia chuo makarai, masup, macarry-over na madisco ya kufa mtu.
 
Hio shule inanunua mitihani na kufanya mwezi mmoja kabla ya mitihani ya taifa ,na huwa maswali yanarudiwa kwa msisitizo mkubwa Sana ......

Hao watoto wanaomaliza huko hawana uwezo kabisa wa kufaulu hivo ,never ever ,....

Hapa bongo ukishakiwa na pesa hakuna kinachoshinfikana ,pepar za necta zinanunuliwa na watoto Wana solve mapema kabisa ...

Hio shule ada yake tu unaweza kula mwaka mzima ,kununua pepar wizaran kupitia kwa mamuruki ni kitu rahisi Sana .....mbaya zaidi wafanyakazi wengi wa serikali dawa yao ni pesa ,kwa million 20 anakuletea pepar la necta lotee mwezi mmoja kabla .....


Niamaini Mimi haya nayoyasema
So wanaweza kununua miaka yote hiyo, mbona zingine hazinunui na zinalipa ada kubwa lakin matokeo sisimizi
 
Mkuu hakuna ufaulu wa namna hio ,kwa hio ratio ....

Hapo ni wazi kabisa wamenunua mtihani na kusolve ...

Hakuna kitu kama hicho ,watoto wa kitanzania Mimi nawajua ,kuapata div 1.7 kaa watoto wote sio kwa uwezo wao ,japo wenye uwezo wapo lakin sio kwa hio idadi kabisa ...


Mimi nakataa kabisa [emoji1787]
Unazungumziaje ilboru yenye 1.7 kama 39 hivi?
 
Mimi binafsi nakataaa hayo matokeo aisee ,hata kama Wana akili huo ufaulu wa kiasi hicho Kuna kitu cha ziada ...hio shule ichunguzwe vzuri kuanzia miezi mitatu kabla ya kufanya mtihani na siku za mitihani
Uliza kwanza kabla hujaandika. Wanafanya mitihani watoto wangapi wa la saba kabla hawajachukua hao 92? Wanafika mpaka 3000 na zaidi. Sasa imagine out of 3000 wanachukua 92. Cream tupu
 
So wanaweza kununua miaka yote hiyo, mbona zingine hazinunui na zinalipa ada kubwa lakin matokeo sisimizi
Sikia nikwambie mkuu maisha ya shule Mimi nayajua Tena zaidi ya unavodhani ...

Shule kubwa kama hizo ,zinawalimu wakubwa Sana wenye uzoefu wa hali ya juu ,na wanakuwa na connection na walimu wengine zaidi ..

Wanaotunga mitihani ni walimu kutoka kanda mbalimbali ,na wabobevu ,hutoa maswali na mwisho wa siku mtihani kitungwa ...

Utake usitake ,upende usipende hizi shule zinamazingira Safi ,walimu Safi ,lakini wananunua mitihani week kadhaa kabla ya pepar ,.....

Fuatilia mitihani wanayofuanya week mbili kabla ya mtihan pre -necta ,ready for necta ,hio ndio mitihan inayotolewa imejaa maswali yanayotoka necta ...

Sio kwamba wanasoviwa siku ya mtihan hapana ,wanafanya maswali yatakayotoka necta week kabla na walimu wanasisitiza kuyakalili ,....

Kama Kuna swali gumu ambalo linasahaulika ,basi mwalimu ataliimba darasana kila siku na mwisho wa siku wanalikuta necta ....

A inaanzia 81-100 ,bro mtihan wa physics , mathematics , biology , chemistry kwa watoto wote 97 wapate A ,???????? Hawa wa kibongo kabisa ? Woteeeee ? ....

Aiseee ,Mimi nakataa hayo matokeo ...hao watoto uwezo wao wa kawaida tu ,sio wa kupata huo ufaulu wote ,kwa kusema sijui walimu Bora ,mazingira Bora ,...
 
Sikia nikwambie mkuu maisha ya shule Mimi nayajua Tena zaidi ya unavodhani ...

Shule kubwa kama hizo ,zinawalimu wakubwa Sana wenye uzoefu wa hali ya juu ,na wanakuwa na connection na walimu wengine zaidi ..

Wanaotunga mitihani ni walimu kutoka kanda mbalimbali ,na wabobevu ,hutoa maswali na mwisho wa siku mtihani kitungwa ...

Utake usitake ,upende usipende hizi shule zinamazingira Safi ,walimu Safi ,lakini wananunua mitihani week kadhaa kabla ya pepar ,.....

Fuatilia mitihani wanayofuanya week mbili kabla ya mtihan pre -necta ,ready for necta ,hio ndio mitihan inayotolewa imejaa maswali yanayotoka necta ...

Sio kwamba wanasoviwa siku ya mtihan hapana ,wanafanya maswali yatakayotoka necta week kabla na walimu wanasisitiza kuyakalili ,....

Kama Kuna swali gumu ambalo linasahaulika ,basi mwalimu ataliimba darasana kila siku na mwisho wa siku wanalikuta necta ....

A inaanzia 81-100 ,bro mtihan wa physics , mathematics , biology , chemistry kwa watoto wote 97 wapate A ,???????? Hawa wa kibongo kabisa ? Woteeeee ? ....

Aiseee ,Mimi nakataa hayo matokeo ...hao watoto uwezo wao wa kawaida tu ,sio wa kupata huo ufaulu wote ,kwa kusema sijui walimu Bora ,mazingira Bora ,...
Kwa uwongo huu unapaswa utunukiwe PHD katika sector hiyo😂
😂
 
Back
Top Bottom