DALALI MKUU
JF-Expert Member
- May 7, 2022
- 2,011
- 4,705
Ni jambo la kusikitisha sana Stand ya daladala Mbezi luis kugeuzwa soko, hasa nyakati za Jioni kuanzia saa 12 Jion na kuendelea.
Ukipita stand ya Mbezi luis kuanzia barabara ya kwenda Kinyerezi kunakuwa na foleni kubwa sana daldala haziingii ndani ya stand zinapaki na kushusha abiria njiani kwa sababu Wfanyabiashara wadogo wa Vyakula, matunda,nguo,viatu n.k hupanga bidhaa zako katiaka maeneo ambayo magari hutakiwa kusimama na kwenye vibanda vya kupumzikia abiria.
Watu hawana hata wasiwasi wanawasha Jiko la mkaa na kuni wanapikia kule stand, wakati kuna vyombo vya Moto vinavyotumia Petrol hii ni hatari mno.
Hili ni Jambo la ajabu na kushangaza sana kwa Viongozi wa Manispaa, LATRA NA TANROAD wanashindwa vipi kusimamia au kuwaondoa kabisa wale wafanyabiashara kule ndani ya stand, au wapangwe vizuri watengewe maeneo maalum kule stand lakini sio kule katikati Ile ni hatari sana.
Wale wafanyabiashara hawafanyi usafi ukipita asubuhi kule stand ni kuchafu, vyakula vimemwagwa, uchafu wa matunda na wale wamama wenye watoto wanajisaidia kule kule ndani lakini hakuna kiongozi anayejali.
Hii ni kero Kubwa kwetu wakazi wa Mbezi Luis tunaiomba Serikali ifanye jambo kuinusuru stand ya mbezi luis ambayo kwa sasa imegeuzwa kuwa soko.
Ukipita stand ya Mbezi luis kuanzia barabara ya kwenda Kinyerezi kunakuwa na foleni kubwa sana daldala haziingii ndani ya stand zinapaki na kushusha abiria njiani kwa sababu Wfanyabiashara wadogo wa Vyakula, matunda,nguo,viatu n.k hupanga bidhaa zako katiaka maeneo ambayo magari hutakiwa kusimama na kwenye vibanda vya kupumzikia abiria.
Watu hawana hata wasiwasi wanawasha Jiko la mkaa na kuni wanapikia kule stand, wakati kuna vyombo vya Moto vinavyotumia Petrol hii ni hatari mno.
Hili ni Jambo la ajabu na kushangaza sana kwa Viongozi wa Manispaa, LATRA NA TANROAD wanashindwa vipi kusimamia au kuwaondoa kabisa wale wafanyabiashara kule ndani ya stand, au wapangwe vizuri watengewe maeneo maalum kule stand lakini sio kule katikati Ile ni hatari sana.
Wale wafanyabiashara hawafanyi usafi ukipita asubuhi kule stand ni kuchafu, vyakula vimemwagwa, uchafu wa matunda na wale wamama wenye watoto wanajisaidia kule kule ndani lakini hakuna kiongozi anayejali.
Hii ni kero Kubwa kwetu wakazi wa Mbezi Luis tunaiomba Serikali ifanye jambo kuinusuru stand ya mbezi luis ambayo kwa sasa imegeuzwa kuwa soko.