Stara Thomas afunguka kuhusu mahusiano yake na the late Adam Kuambiana

Stara Thomas afunguka kuhusu mahusiano yake na the late Adam Kuambiana

warumi

R I P
Joined
May 6, 2013
Posts
16,218
Reaction score
18,440
Msanii Stara Thomas amefunguka kuhusiana na mahusino yake na aliyekuwa msanii wa bongo movie Adam Kuambiana aliyefariki wikiendi iliyopita na kuzikwa jana kwenye makaburi ya Kinondoni. Stara amesema ni kweli aliwahi kuwa na mahusiano na Kuambiana lakini hata hivyo walitengena kutokana na kupishana baadhi ya tabia.

Anasema mahusiano yao yalianza walipokutana uwanja wa Taifa kwenye moja ya mechi iliyozikutanisha Bongo movie na Bongo flava na katika mahusinao yao hakuwahi kumwambia kama ana mke Zaidi ya kumwambia kuwa amewahi kuoa na ameachana na mke wake kwa talaka. "Ni kweli nimewahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Adam,uhusiano ambao ulifika mbali kiasi cha kutambuliwa nyumbani kwao kwa baadhi ya ndugu wakiwemo dada zake na hata babu yake mkubwa lakini hatukuweza kufikia kufunga ndoa kama tulivyokuwa tunafikiria, nakumbuka nilimuuliza kama ana mke akaniambia aliwahi kuoa na ameachana na mke wake" alisema Stara.

Amesema moja ya mambo makubwa ambayo walitofautiana ni pamoja na hasira kali kiasi cha kupelekea ugomvi mara kwa mara ,uvutaji wa sigara kupita kiasi wa Kuambiana ambaye hata alipokuwa akimueleza hakuwa akimuelewa, lakini pia kuna hitilafu ziliwahi kutokea kati yao walipokuwa safarini Zanzibar na Morogoro na mwisho akaona hawawezi kuishi kama mke na mume na kuamua kusitisha mahusiano. "Unajua Adam alikuwa na kisukari sasa kwa kiasi kikubwa alikuwa anavuta sigara anapokuwa na stress zake na pia alikuwa mtu wa hasira sana,lakini kikubwa ni kutofautiana kwa baadhi ya tabia ambazo nikaona hatuwezi kuendelea na mahusiano yetu nikasitisha rasmi japo yeye mwenyewe aliomba kuwa atajirekebisha lakini ni vitu ambavyo vilikuwa vinajirudia nikaona hapana" Stara alisema.

Hata hivyo Stara amesema mbali ya kuwa na tofauti lakini Kuambiana hakuwa muhuni wa kubadili wanawake alikuwa ni mwenye kujiheshimu kwa kiasi kikubwa.
 
Sipati picha kuambiana alivyokua anaruka sarakasi kwa Stara maana ni bongeeee
Ila ana jichoo huyoo
 
Mngoni Kuambiana mzee wa Gambe na Tantalila...alikua ana "Likomo" kweli la wanaume wa Kingoni, jeuri ya kufa mtu..RIP Adam mutoto ya Kawe!
 
Sipati picha kuambiana alivyokua anaruka sarakasi kwa Stara maana ni bongeeee
Ila ana jichoo huyoo

Mi mwenyewe nilichoka duh, ila sasa ivi kapungua vizur kweli na yupo smart , ila aliniacha hoi tu eti alikuwa ananga'ang'ania msiba wa adam uwekwe kwake, sijui alikuwa anataka umaarufu au ndo mahaba niue, yeye si ana mume?? Asubir wake ndo ang'ang'anie zile zilikuwa mali official za watu, ye alikuwa mchepuko tu, halafu huyu atakuwa anavuta bangi yani utembee na mume wa mtu halafu unajigamba hadharan au ndo anasafisha nyota kupitia marehem, maana naona mwingine kaibuka anadai mareh alikuwa buz lake na alikuwa anakaa kwake yaan vifo ivi vina mambo binamu
 
Mngoni Kuambiana mzee wa Gambe na Tantalila...alikua ana "Likomo" kweli la wanaume wa Kingoni, jeuri ya kufa mtu..RIP Adam mutoto ya Kawe!

Kawe??, mh mi nilisikia eti marehemu alikuwa ule wimbo maarufu wa lady jaydee, maana kuna kipindi alisema anakaa mikocheni, mara kunduchi akaja tena kusema kajenga tabata, alivyokufa msiba ulikuwa bunju , marehemu alikuwa ana nyumba nyingi kwli apa mjini..
 
kuna mambo nadhani yanatokea Tanzania tu, sisi hizi hadithi zake stara zinatuhusu nini? nilikuwa namuheshimu kumbe bure kabisa.

imagine wewe ndio umemuoa na unaishi naye halafu mtu anamshobokea marehemu kiasi hiki? gime a break.
 
Kawe??, mh mi nilisikia eti marehemu alikuwa ule wimbo maarufu wa lady jaydee, maana kuna kipindi alisema anakaa mikocheni, mara kunduchi akaja tena kusema kajenga tabata, alivyokufa msiba ulikuwa bunju , marehemu alikuwa ana nyumba nyingi kwli apa mjini..

Ha ha marehem alianzia kusoma kawe, kisha Tambaza, SA na Uingereza hayo ya Uyahaya mi siyajui mkwe!
 
Kawe??, mh mi nilisikia eti marehemu alikuwa ule wimbo maarufu wa lady jaydee, maana kuna kipindi alisema anakaa mikocheni, mara kunduchi akaja tena kusema kajenga tabata, alivyokufa msiba ulikuwa bunju , marehemu alikuwa ana nyumba nyingi kwli apa mjini..

Hahhhhaaahhhhhaa lolll kumbee ndio hivyooi a.k.a Yahaya jamanii nimechekaa mnooo
 
kuna mambo nadhani yanatokea Tanzania tu, sisi hizi hadithi zake stara zinatuhusu nini? nilikuwa namuheshimu kumbe bure kabisa.

imagine wewe ndio umemuoa na unaishi naye halafu mtu anamshobokea marehemu kiasi hiki? gime a break.

Mimi nimeshangaa tu anavyojitapa aliwahi kutoka na marehemu, sasa anatangaza ili iweje?, si angefanya iwe siri au tetesi tu, huyu mama atakuwa anavuta bangi, unajitapa kutoka na mume wa mtu, halafu mlokole aka mwimba kwaya
 
Mi mwenyewe nilichoka duh, ila sasa ivi kapungua vizur kweli na yupo smart , ila aliniacha hoi tu eti alikuwa ananga'ang'ania msiba wa adam uwekwe kwake, sijui alikuwa anataka umaarufu au ndo mahaba niue, yeye si ana mume?? Asubir wake ndo ang'ang'anie zile zilikuwa mali official za watu, ye alikuwa mchepuko tu, halafu huyu atakuwa anavuta bangi yani utembee na mume wa mtu halafu unajigamba hadharan au ndo anasafisha nyota kupitia marehem, maana naona mwingine kaibuka anadai mareh alikuwa buz lake na alikuwa anakaa kwake yaan vifo ivi vina mambo binamu

Yaan anajisema katembea na marehemu huku ana mme huyo hafaii kama ni wangu talaka siku hiyo hiyoooo
 
kuna mambo nadhani yanatokea Tanzania tu, sisi hizi hadithi zake stara zinatuhusu nini? nilikuwa namuheshimu kumbe bure kabisa.

imagine wewe ndio umemuoa na unaishi naye halafu mtu anamshobokea marehemu kiasi hiki? gime a break.

Mi nilidhan kasema hivyo hana mme kumbe ana mme hata kama ana mpenzi unatakiwa kupiga kimyaaa tu
 
Ha ha marehem alianzia kusoma kawe, kisha Tambaza, SA na Uingereza hayo ya Uyahaya mi siyajui mkwe!

Ndo hivyo nasikia marehemu makazi yake yalikuwa mahotelin na ma lodge ,yaani wakiwa kambini kutengeneza movie, yeye ndo yanakuwa makazi yake, nilikukwa namuonaga sana baa za sinza na brazil kule tegeta, dah ukistaajabu ya kifo cha kanumba utayaona ya adam kuambiana, aya tusubir mwingine tena tujue mengi zaidi
 
Jamani, kwa ukweli nilikua mamuheshimu sana Stara Thomas, kumbe naye ni walewale tu. Kujiheshimu ni pamoja na kuficha mambo yako ya faragha watu wasiyajue au wayajue lakini wasiamini. Ila sipati picha lile titi akiwa naked huwa anatokelezeaje!
 
Ndo hivyo nasikia marehemu makazi yake yalikuwa mahotelin na ma lodge ,yaani wakiwa kambini kutengeneza movie, yeye ndo yanakuwa makazi yake, nilikukwa namuonaga sana baa za sinza na brazil kule tegeta, dah ukistaajabu ya kifo cha kanumba utayaona ya adam kuambiana, aya tusubir mwingine tena tujue mengi zaidi

Brazil pako so local..hata umauti wake unamkuta usiku wake alikua pale Igo Lounge alikua akikung'uta mma kama mgonjwa wazimu..hata mm nimewah skia hivyo jamaa "kambi popote"
 
Ndo hivyo nasikia marehemu makazi yake yalikuwa mahotelin na ma lodge ,yaani wakiwa kambini kutengeneza movie, yeye ndo yanakuwa makazi yake, nilikukwa namuonaga sana baa za sinza na brazil kule tegeta, dah ukistaajabu ya kifo cha kanumba utayaona ya adam kuambiana, aya tusubir mwingine tena tujue mengi zaidi

Hapa sicheki yamejitoa. At nini?
 
Back
Top Bottom