Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

Nimependa sana .mulichofanya startimes, kitendo cha kuja humu haraka na kujibu malalamiko ya mteja.

Jitahidini kufanya hivyo kwa kila mteja.
Mulifanya kosa kubwa kutokutoa majibu/taarifa ya haraka kipindi cha tatizo la itv na eatv...

Tafakari...
 
Nimelipia kifurushi cha mambo yapata week sasa lakini channel zinazo onyesha vizuri ni tatu tu nyingine zina katakata sana na zingine hazionyeshi kabisaa yani pesa yangu imekwenda bure najuta hata kwanini nimekilipia bora ningebaki naangalia free channel hizo mlizo tuachia kama nibomba nimeshazungusha sana nimelipandisha na kulishusha lakini hakuna mabadiliko


habari yako tunaomba ututajie unaishi maeneo gani! tutamtuma fundi wetu aje aku saidie upate huduma zetu vizuri!
 
habari yako

tafadhari tujulishe uko Arusha sehemu gani, huduma yetu arusha inapatikana vizuri wala haina matatizo. kuscratch kwa decoder kunasababishwa na upokeaji hafifu wa mawimbi ambao unaatokana na matatizo katika antena yako

Natumia antenna ya nje. Mwanzo ilikuwa poa lakini sasa ni shida. Naishi along old Moshi road karibu na chuo cha Nelson Mandela
View attachment 226589
 
habri yako

kwa maeneo ya Tukuyu mbeya tunakushauri utumie huduma yetu ya SATELITE DISH, ambayo inaonekana vizuri huko, hii huduma ni ving'amuzi vya startimes vinavyotumia DISH

Ahsante, je ntakipata king'amzi kwa bei gani ? Napenda startimes
 
habari...mimi niko kibaha mwendapole, namba ya akaunti ya king'amuzi changu cha startimes ni 02035111864 nina malalamiko yafuatayo🙁1) hii ni wiki ya 3 sasa steshen za tv zifuatazo hazipo kabisa kwenye menu list.....itv,eatv,mlimani tv,star tv,e star tv,nimekuwa nikikosa mambo mengi ya kielimu,kiuchumi,kijamii,burudani na kiutamaduni kwa muda mrefu sasa.(2)sielewi hiki kifurushi kipya nakipataje? karibu wiki 3 sasa tangu nimelipa tshs 4000/ sikukipata na hela yangu haukurudishwa,sasa mbona hatuwaelewi startimes?(3)tafadhalini naomba utatuzi wa masuala hayo yanayonitatiza ili niendelee kufurahia king'amuzi chetu cha startimez.asanteni kazi njema.
 
Habari,kwa singida ile ofa yenu ya king"amuzi vyemu vya ofa,yaani tsh 34,000,kifurushi cha nyota na king"amuzi kwa miezi saba na nusu inapatikana wapi?
 
Big up star times kwa kunijibu kwa haraka. Leo nitabadilisha na kuweka kifushi cha nyota then nitalipia tena 4000 ili nione.
Asante sana kwa majibu
 
kwanini usifunge free TV channel zilizopo Amos5@17e mbona kuna channel kibao za Bure bila malipo za ndani na nnje ya nchi.

Hii makitu inapatikana wapi aiseee niiwahi fasta nishaibiwa sana na hivi vishumbushi mtu chanel za bure tunalipishwa yaani wanatuibia mchana kweupee.
 
Habari yako

ndugu mteja, sio kweli kuwa kifurushi cha NYOTA kina matatizo kama unavyofikiri, kama unataka kuhama kifurushi kutoka kifurushi ulichokuwa unalipia awali, ni lazima ubadilishe kifurushi chako, kama awali ulikuwa unatumia kifurushi cha mambo 10000@mwezi alafu ukalipia 4000 bila kubadilisha kufurushi basi fedha yako 4000 itatumika katika kifurushi cha mambo, yaani utaangalia kwa muda wasiku 12 chanel za mambo.

hivyo basi kama awali ulikuwa unatumia kifurushi cha mambo, utakapolipia kifurushi cha NYOTA 4000 ni lazima ubadilishe kifurushi. unaweza kubadilisha kifurushi kwa kupiga namba yetu ya huduma kwa wateja, au kwa kutembelea ofisi zetu au kwa kutumia simu yako ya mkononi kwa kupiga *150*63# kisha ufuate maelekezo utayopewa

ahsante

Si kweli mimi nina ving`amuzi viwili baada ya hili tangazo la Nyota kimoja nimekilipia shs 4000 hakuna channel yoyote ya mambo iliyofunguliwa acheni wizi au ndio mnataka kuwaiga Voda?
 
mimi naitwa lupakisyo mwaisumo, nimefanya miamala mitatu, kulipia kifurushi cha dstv lakini kwa bahati mbaya namba niliyokuwa nalipia ilikosewa, badala ya 42793676695, nilikuwa naweka 4279367669 , yaani namba 5 ya mwiso sikuiweka, hivyo tarehe 1/1/2015 mnamo saa 1:07 nilipoteza sh. 7,000/=, tarehe 2/1/2015 saa 11:55 asubuhi nikaipoteza tena sh 10,000/=. Nimekuja kugundua tena nilipofanya muamala tarehe 2/2/2015 wa sh. 17,500/= saa 2:09 usiku. Nimewapigia watu wa tigo pesa kunirudishia hizo fedha zangu, wakanielekeza kuwanapaswa kuongea na nyie watu wa startimes. Hivyo naomba kusaidiwa katika tatizo hili. Namba niliyoitumia kulipia king'amuzi hiki ni 0713874005, na smartcard inamilikiwa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya kilolo, mkoani iringa.

umeengia choo cha wanawake
 
Nahitaji kununua Startimes ni sh: ngapi decoder pamoja na dish 2 je kuna free chanel ngapi na nizipi na zipi? 3 malipo kwa chanel zingine ni Tsh:ngapi kwa mwezi? ni hayo tu. Chacha wa marwa niko Tarime Mara.
 
Week ya 2 sasa.. li ng'amuz lenu halionyeshi star tv. Ndo nn sasa??
 
Mimi nimenunua king'amuzi cha tshs 59000 kama siku sita zilizopita. nimeunganisha kila kitu sawa na maelezo yaliyopo katika "user's guide" lakini hakuna kinachoonekana. Nikienda ktk signal status inasoma zero. Nifanyeje au tatizo ni nini? Naishi Tandika.
 
kuna watu wana moyo wa chuma,yaani hawa startimes ni bure,yan nna miezi 6 ckitumii,yan nmeachana nacho.yan za bure pia nlipie tena za bongo,km kuna mtu anataka ata bure ntampa,uchafu tuh.bora nlipie dstv.nienjoy movies.
 
mbona sijibiwi?
Kama sistahili kujibiwa mniambie nikadai pesa yangu ninunue king'amuzi kingine.
 
Huduma zenu bado zinahitaji kuboreshwa huwez ukalinganisha na huduma za vingamuz vingine kama azam nk.
 
Napenda kujua vifurushi mbali mbali na gharama zake na jinsi ya kuvipata vifurushi hivyo Bila kuja ofisini kwenu
 
nimekuwa nikinunua kifurushi cha nyota bila mafanikio. ujumbe naoupata ni huu "smart kadi hiyo 02035..... imefanikiwa kupata4. subiri kwa dakika15 kisha kuhakikisha chaneli zako". lakini baada ya muda huo kupita hakuna mabadiliko yoyote. baada ya shida hiyo ndani ya siku tatu nikajaribu kulipia kupia menu ya m-pesa, napo hadi leo ni siku ya pili hakuna chochote! ujumbe wa kuthibitisha malipo nimeupata toka selcom. nipo dom
 
Habari zenu wanaJamiiForums

Je una tatizo lolote unapotumia huduma zetu? Unaushauri wowote ili kuboresha huduma zetu?

Tafadhali tunaomba utumie thread hii, ili tukusaidie? Tafadhali tunaomba unapokuwa na tatizo ili tukusaidie kirahisi

1. Utaje tatizo lako
2. Taja sehemu unayoishi?
3. Pia kama unaweza tunaomba ututumie na namba yako ya smartcard!

STARTIMES tutajibu maoni, malalamiko na ushauri ule tu ambao utakuwa umejitosheleza na wenye nia ya kutusaidia kuboresha huduma zetu.

Ahsanteni sana na karibuni nyote

nimekuwa nikinunua kifurushi cha nyota bila mafanikio. ujumbe naoupata ni huu "smart kadi hiyo 02035..... imefanikiwa kupata4. subiri kwa dakika15 kisha kuhakikisha chaneli zako". lakini baada ya muda huo kupita hakuna mabadiliko yoyote. baada ya shida hiyo ndani ya siku tatu nikajaribu kulipia kupia menu ya m-pesa, napo hadi leo ni siku ya pili hakuna chochote! ujumbe wa kuthibitisha malipo nimeupata toka selcom. nipo dom
 
Back
Top Bottom