Stendi mpya ya mabasi Nyegezi yaanza kazi, ni zaidi ya Airport

Stendi mpya ya mabasi Nyegezi yaanza kazi, ni zaidi ya Airport

Stendi mpya ya mabasi ya Nyegezi jijini Mwanza imeanza kazi rasmi leo tarehe 5/6/2023 huku uzuri wake ukiwaacha hoi wananchi na kusema iko vizuri zaidi ya viwanja vingi vya ndege.

Ikumbukwe jiwe la msingi la ujenzi wa stendi hii liliwekwa na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Magufuli, hivyo wananchi wamemlilia tena kwenye uzinduzi wa stendi hii na kusema bila Magufuli kuwa Rais huenda ingewachukua miaka 50 kwa jiji la Mwanza kujengewa stendi nzuri kiasi hiki.


Uliposema ni zaid ya airport, mara raia wameshangaa uzuri wake! Sitii neno maana nawajua ndugu zang akina ng'wizukulu mayunga 🤣🤣🤣🤣
 
Ni vigumu sana kumsahau jpm naamini tungekuwa nae tungekuwa mbali sana[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]View attachment 2646930
images.jpeg
 
Stendi mpya ya mabasi ya Nyegezi jijini Mwanza imeanza kazi rasmi leo tarehe 5/6/2023 huku uzuri wake ukiwaacha hoi wananchi na kusema iko vizuri zaidi ya viwanja vingi vya ndege.

Ikumbukwe jiwe la msingi la ujenzi wa stendi hii liliwekwa na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati Magufuli, hivyo wananchi wamemlilia tena kwenye uzinduzi wa stendi hii na kusema bila Magufuli kuwa Rais huenda ingewachukua miaka 50 kwa jiji la Mwanza kujengewa stendi nzuri kiasi hiki.


Stendi itabaki kuwa stendi tu siku zote.... Usilinganishe stand na airport....

Hata wangewekewa maghorofa na mandhari kama ya dubai....

Tabia za watu wa stendi hazijawahi staarabika.....na hazitawahi staarabika kamwe!
 
Stendi mpya ya mabasi ya Nyegezi jijini Mwanza imeanza kazi rasmi leo tarehe 5/6/2023 huku uzuri wake ukiwaacha hoi wananchi na kusema iko vizuri zaidi ya viwanja vingi vya ndege.
Wiki mbili tu zijazo vyoo havitakuwa vinatazamika, waswahili bado sana
 
Magufuli terminal vyoo vichafu vimeharibiwa hakuna matengenezo
Msamvu Morogoro vyoo vipo hoi vimebomoka uchafu kila sehemu
Dodoma stand kuu vyoo havifanyiwi matengenezo hakuna anayayejali
Hata hivyo vya Nyegezi vitaishia kuwa vya hovyo kama hakuna mikakati ya matunzo
 
Dodoma ni alama ya mwisho kabisa ya mazuri ya Hayati yatakayokumbukwa milele, tuache masihara Magufuli City ni mji wa mambele huku. Apumzike kwa amani Rais wetu kipenzi, aliipenda Tanzania kwa moyo wake wote.
Hata Mimi nilikua na mponda siku hizi ndo namuelewa Kama alivyosema tutamkumbuka mwamba wa Africa
 
Back
Top Bottom