Stendi mpya ya mabasi ya Magufuli haikuwa tayari kuanza kutumika

Stendi mpya ya mabasi ya Magufuli haikuwa tayari kuanza kutumika

jogoo_dume

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
2,204
Reaction score
1,939
Habari za muda huu na ni matumaini mko wazima wa afya.

Straight to the matter, hiki kituo kipya cha mabasi ya mikoani hapa Dar es Salaam yaani Magufuli Bus terminal hakikuwa tayari kuanza kutumika. Ilitakiwa kipewe muda kidogo ili kiwe sawa.

Leo nimefika toka Morogoro muda huu kwa mara ya kwanza ktk hicho kituo na kuna changamoto nyingi. Nafikiri kina Jafo walifanya maamuzi kumridhisha tu bwana mkubwa.

Baadhi ya vitu niliyoviona;
1. Mabasi hayana sehemu maalum ya kupandia au kushushia, yaani anayewahi eneo ndio kwa muda huo anatumia hilo eneo hivyo ni ngumu kwa abiria kujua eneo sahihi la kupandia au kushushia kwa kampuni fulani ya basi.

2. Nimetafuta sehemu ya kula ndani hamna zaidi ya wamama lishe waliozagaa zagaa kwa kupanga meza zao maeneo hayo hayo ya karibu na yanaposhushia mabasi abiria.

3. Nimeenda msalani kuna changamoto ya maji.

4. Eneo sehemu kubwa ni giza na kibaya zaidi ukitoka tu nje ya kituo hamna taa, kuelekea kituo cha daladala yaani ni giza na unapishana na vijana kwa muonekano wanaweza kuwa vibaka na wakatumia faida ya hilo giza kuibia watu.

5. Barabara ya kuingia na kutoka mabasi haiko sawa bado, ya vumbi.

6. Ukifika stendi ya daladala ya Mbezi kuna taa zimewekwa ila zimezimwa sijui mbovu houo eneo ni giza mpaka zimewashwa taa 'vibatari'.

7. Mwendokasi hamna.

8. nk

Nilitegemea wangekua wameshafanya research na kujua walau basic issues ambazo ilitakiwa ziwe tayari kabla ya kuanza kutumika kwa kituo.

viongozi waache kukurupuka maana wanaopata tabu kutokana na mikurupuko yao ni raia watumiaji wa hiyo miundo mbinu.
 
Binafsi nashangazwa Sana kutumika wakati ni just tu nilipelekakifusi Cha kambodia pale kumwaga hata week mbili haijaisha na ilikuwaa bado Sana mchina ananiambia kuwaa ni mpk labda mwakani ndio ingekuwa taayar sasa sasahv wanalipua tu ilimradi wamridhishe raisi Magufuli.
 
Upo sahihi, wamekurupuka kutokana na woga kwa Mfalme.

Changamoto nyingine kubwa zaidi itakayofuata ni UCHAFU, utashangaa siku si nyingi kuta zimeloa mikojo na chini kuna vichupa vya mikojo kila pahala.

Wabongo wengi wachafu, si wastaarabu na zaidi sio watunzaji wa vitu vizuri.
 
INASIKITISHA SANA.
Mbona ni jambo dogo sana, kiongozi kama waziri nk kama unaona kitu flani hakijakidhi matumizi na boss wako anataka kitumike mapema, mwambie ukweli na ukiona vipi tembea kafanye mambo mengine ili uingie kwenye rekodi.

Siyo kuharibu kodi ya mtanzania kwa upuuzi wowote.
 
INASIKITISHA SANA.
Mbona ni jambo dogo sana, kiongozi kama waziri nk kama unaona kitu flani hakijakidhi matumizi na boss wako anataka kitumike mapema, mwambie ukweli na ukiona vipi tembea kafanye mambo mengine ili uingie kwenye rekodi.

Siyo kuharibu kodi ya mtanzania kwa upuuzi wowote.
Hakuna waziri mwenye ubavu huo
 
Nibora tutumie hiyo kuliko ya ubungo!! Kn nivibaka ubungo ndo ilikuwa makao makuu yao, km nimikojo ilikuwa kila sehem hapo ubungo!

Hongera magufuri.
 
Hata lile daraja halijakamilika bado. Sina uhakika kama kwa umati kama ule wa ubungo terminal ukija pale zebra cross lazima izidiwe tu.
 
Back
Top Bottom