Stendi ya Mbagala Rangi Tatu kuhamishiwa Kijichi, sababu ni nini?

Stendi ya Mbagala Rangi Tatu kuhamishiwa Kijichi, sababu ni nini?

Satoh Hirosh

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2021
Posts
6,432
Reaction score
25,646
Leo asubuhi nimepishana na mabasi mengi sana ya mikoa ya Kusini pamoja na basi ndogo za Mkuranga na Kibiti yakielekea stendi ya Kijichi. Nikamuuliza mtu mmoja imekuwaje leo haya magari yanaenda Kijichi badala ya Mbagala rangi 3? akajibu magari yote ya mikoani yanayoanzia Mbagala Sasa hivi stendi yao ni Kijichi.

Kwa hiyo hata Ester ya Arusha na Tashirifu ya Tanga zitaanzia Kijichi, hapo Mbagala panabomolewa.

Majibu yalikuwa mengi maana kila mtu akawa anasema yake, mara mtu kanunua lile eneo la Rangi Tatu, mara halikuwa eneo la serikali, mara serikali inataka kuliendeleza eneo. Sikutoka na jibu moja la uhakika.

Ila serikali imeruhusu vipi kuhamishia stendi Kijichi au ni dharura?

Nimefika njia ya ng'ombe nimekutana na tashirifu ya ya Tanga inastrugle kukata Kona, gari linaenda mbele taratibu Kisha linarudi nyuma ili likae vizuri kwenye lane yake kisha iendelee na safari. Barabara nyembamba na gari ni refi, nina uhakika hata njia panda ya Neruka Kuna kitu Kama hiko kinatokea.

Zile barababra za mtaani kule Kijichi, kuanzia Neruka hadi kufika stendi ilipo ni nyembamba nazo, ukipishana tu na roli za mchanga mwenye gari ndogo lazima asimame kwanza Kisha roli lipite maana linajaa Barabara yote.

Kama stendi imehamia Kijichi moja kwa moja sijui itakuwaje na ile mibasi ya mkoani kwenye zile Barabara nyembamba!

Alafu Kijichi naona Kama imekaa kushoto kwa abiria wa sehemu zingine maana ipo ndani. Ni kama uitoe stendi ya Magufuli pale Mbezi Kisha uihamishie Goba kwa ndani, lazima kutatokea usumbufu sana.

Mpaka Sasa hivi sijui kwanini stendi imehamishwa rangi tatu. Mtu mmoja nilimsikia anasema ni heri wangejenga stendi mpya Kongowe au Mwandege karibu na kiwanda cha bahresa kuna eneo kubwa.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Weka picha ya stand ya kijicho ili tuseme neno...

Bado pia tuna taka kuwa sogeza nje ya mji huko karibu na viwanda vya bakhresa vikindu

Mjini hapo tufanye uwekezaji swafi na mwendo kasi upige kazi vyema bila shida kama ilivyo kuwa ubungo na sasa imepelekwa mbezi
 
Lile eneo linalotumika kama stendi pale mbagala la mtu. Kuna kampuni inamiliki lile eneo. Hii stendi ya rangi tatu miaka ya 2000 haikuwaga pale,kuna sehem ilihamishwa. Inawezekana yote yakatokea.
Pia hii barabara kubwa ya kijichi sio ya mbagala kuu. Barabara kuu haijaisha mpaka leo inapita kichemchem mpka Jeshi la wokovu. Ile ndo barabara kuu sasa
 
Weka picha ya stand ya kijicho ili tuseme neno...

Bado pia tuna taka kuwa sogeza nje ya mji huko karibu na viwanda vya bakhresa vikindu

Mjini hapo tufanye uwekezaji swafi na mwendo kasi upige kazi vyema bila shida kama ilivyo kuwa ubungo na sasa imepelekwa mbezi
Kuna siku nitawashauri nini cha kufanya.
 
Kuna Engineer mmoja aliwahi niambia lile eneo ni lao na kakaake ndiye mtu anayekusanya ushuru pale kila Siku.
Let's assume ni kweli, je kwa nini serikali isiwalipe fidia na kuchukua hilo eneo liwe for public use? Hii nchi ngumu sana, hapo kuna mwenyekiti wa mtaa, kuna diwani, kuna mbunge nk but jambo linafanyika bila kutaarifu umma kwamba serikali ina mpango wa kuhamisha stend from A to Z kwa sababu Y and W... Yaani ni full dharau kwa wananchi wao.
 
Let's assume ni kweli, je kwa nini serikali isiwalipe fidia na kuchukua hilo eneo liwe for public use? Hii nchi ngumu sana, hapo kuna mwenyekiti wa mtaa, kuna diwani, kuna mbunge nk but jambo linafanyika bila kutaarifu umma kwamba serikali ina mpango wa kuhamisha stend from A to Z kwa sababu Y and W. Yaani ni full dharau kwa wananchi wao.
Dharau kweli, ww jifikirie ni stendi ngapi zilizohamishwa huku wananchi wakiteseka. Ubungo to Mawasiliano, Mwenge to Makumbusho etc.
 
Hivi unajua ardhi ya Tanzania, ni mali ya serikali, na mwananchi ni mpangaji, hivyo ardhi ikihitajila kwa matumizi ya umma serikali huichukua, sema kikwazo kingine ila siyo swala la pale ni kwa mtu.
 
Barabara za kijichi zile mbona mtihani upo. Kona za karibu karibu sana alafu barabara ni nyembamba, pia nyumba zipo karibu sana na barabara sidhani hata kama mita tano inafika. Kuna siku basi litapitiliza hadi chumbani.

Ngoja tuone
Kuna sehemu nyingine basi zinakata Kona na kurudi nyuma vinginevyo zinapitiliza kwenye maduka ya watu,mfano njia ya ng'ombe
 
Back
Top Bottom