Steve Nyerere: Mchungaji Peter Msigwa nimemchukulia mwanamke ndio maana anaendekeza ugomvi na wasanii kutangaza utalii nchini

Steve Nyerere: Mchungaji Peter Msigwa nimemchukulia mwanamke ndio maana anaendekeza ugomvi na wasanii kutangaza utalii nchini

Wasanii ni vikaragosi vya CCM, kwanini walipwe kwa hela zetu wakati hawaajiriwa kihalali.
Hivi huyu Steve amepata wapi Ujasiri wa kumsema hadharani Mchungaji, Baba, Mume na Mbunge wa Wananchi Kwa kasfa mzito kama hii. Msigwa ni Waziri Kivuli utaliii alikuwa anatia Mawazo yake Bungeni.
 
Mwelezeni Huyo msanii steve mangele (sio sahihi kutumia jina Nyerere kwa huyu kwani ni kulidhalilisha) kuwa Mchungaji Msigwa Peter anayo kinga ya kibunge kwa kila anachoongea akiwa ndani ya Bunge, hivyo achunge kauli zake zisijesababisha akachukuliwa hatua na Mchungaji Msigwa kwa haya anayoropoka mitaani
 
Katika kuelekea mwishoni wa mwaka jana kulikua na harakati za kutangaza utalii wa nchi yetu kutumia "celebrities" wetu wa Kitanzania. Katika kampeni wasanii wa filamu pamoja na wa Bongo fleva walihusika kwa kushirikiana na kiongozi wa Wizara husika. Mimi ni mdau wa utalii na ninajua utalii wa Tanzania kwa kiasi changu. Kwa kufanya analysis ya kampeni ile naweza kusema malengo ya kutangaza utalii kwa namna ile yanatija ndogo sana kwa utalii. Kwa sababu zifuatazo..

1. Watanzania tunafahamu hifadhi zetu
Ukiangalia ile kampeni ilikua kana kwamba watanzania hatujui vivutio vyetu kitu ambacho si kweli. Kwa maana hiyo kumtumia Ayo, Naseeb na wengineo ambao 99% ya followers ni Watanzania haina mashiko sana (poor allocation of resources) sababu tatizo la sisi si kutokujua uwepo wa Serengeti, Ngorongoro au Ruaha ila tatizo ni uwezo wa kwenda kutembelea hivyo vivutio.

2. Utalii wa hifadhini ni ghali
Ukichukulia hifadhi zetu za taifa kitu pekee ambacho Mtanzania wa kawaida kwake ni nafuu ni Kiingilio tu cha hifadhini lakini vyote vilivyobaki si rafiki. Kuanzia gharama za malazi hadi usafiri ndani ya hifadhi.

Nini Kifanyike?

Kwa utalii wa Mbugani ili mtanzania wa kawaida aweze kufanya kuna haja ya kutatua tatizo la usafiri ndani ya hifadhi. Ambapo hifadhi inaweza kua na magari yao kama ilivyo kwa hifadhi ya Mkomazi ili kuweza watembeza watu ndani ya hifadhi. Pili kuboresha public campsites ndani ya hifadhi kwa kuweka miundo mbinu rafiki zaidi kwa watanzania kutembelea hifadhi zetu kwa gharama nafuu na usalama wa kutosha.

Baada ya kufanya hayo sasa hata Wizara ikiwatumia wasanii kutangaza utalii wa ndani na kuweza kuwajulisha upatikanaji wa huduma husika kwa gharama nafuu utalii wa ndani utakua.

****************
Zile hoteli za kitalii ndani ya hifadhi zinazotoa huduma za malazi kwa wasanii bure si kwamba wao hawakufanikiwa katika kutangaza hoteli zao, ni wamefanikiwa sana sababu target yao si wewe bali ni ile 1% ya watanzania ambayo wanaweza fanya utalii ukweli wa kuufanya. Hivyo kwa kumuona mbongo fleva/bongo movie ndani ya hoteli husika yule Mtanzania anayeweza nunua atahamasika.
Labda hukumuelewa mchungaji msigwa au hukubahatika kuona huo mchango wake. Alichokuwa anashauri ndugu msigwa ni kwa waziri badala ya kuhangaika na wasanii wa ndani tu atumie na wasanii wa nje (celebrities) kama wanavyofanya Rwanda ili kutangaza utalii kwa mataifa ya nje ambayo ndiyo kazi yake ili kuongeza idadi ya watalii wa nje.
 
Nimeangalia hoja za Steve kuhusu kauli alizotoa Mh Msigwa bungeni jamaa amekuja na kashfa na sio hoja kwa nini anastahili nafasi aliyopewa na Mh Kigwangala.

Hivi ina maana anaamini kuwa anaweza kuleta watalii Tanzania ni Mara 10000 Bongozozo anaweza fanya hiyo kazi ila si yeye. Ni kweli yeye, wenzie na Mh Kigwangala walikua na nia nzuri ya kukuza utalii ila hawakua watu sahihi kwa kazi ile




!
!
kwa speech hii tu anaonekana hafai kuwa balozi wa utalii huyu
 
Hivi ni sahihi kwa mtu wa nje ya Bunge kumporomoshea kashfa mbunge kwa aliyoyaongea ndani ya Bunge? Nina imani kama Msigwa angekua Mbunge wa Chama tawala na Steve angemkashifu namna ile basi angeitwa na ile kamati ya nini sijui ile

Ni kweli Mh Msigwa alimtaja Steve kwa njia ambayo yeye anadhani ilimvunjia heshima na kwamba yeye hana fursa ya kujibu tuhuma au kashfa hizo, lakini nadhani kuna utaratibu wa kuandika Barua wamuite yeye kwenye hiyo kamati pamoja na Mbunge husika kama alivyowahi kufanya marehemu Reginald Mengi ili aitwe na kupewa nafasi ya kujitetea ndani ya kamati ya hadhi na maadili na ikiwezekana kuomba Bunge limchukulie hatua Msigwa
Hapo kanuni inatakiwa ifanye kazi mbunge analindwa na kanuni Kwa yote anayosema ndani ya Bunge.
 
Labda hukumuelewa mchungaji msigwa au hukubahatika kuona huo mchango wake. Alichokuwa anashauri ndugu msigwa ni kwa waziri badala ya kuhangaika na wasanii wa ndani tu atumie na wasanii wa nje (celebrities) kama wanavyofanya Rwanda ili kutangaza utalii kwa mataifa ya nje ambayo ndiyo kazi yake ili kuongeza idadi ya watalii wa nje.
Msigwa alikua sahihi, Steve Nyerere hata aposti mara 700 kuleta mtalii hataweza..
 
Ila kwakweli tumefika pabaya sana.yani kila mtu anaongea tu kumtukana mwenzake? Sasa kosa la msigwa lilikuwa nn pale? Si alishauri tu jamani?
Nahuyu Steve anamtukana mbungwe kwann

Sent using Jamii Forums mobile app
Wabunge wa Upinzani Awamu hii wameondolewa Heshima na hakuna wa kuwatetea. Yeyote Tu anaweza kuwatukana hadharani akijinadi anaisapoti Serikali. Si haki Mbunge ana title Mheshimiwa tena aliopewa na Wananchi Nobody Anatolka kuwakashifu for Fame. Mhe Msigwa pole Sana.
 
Nimeangalia hoja za Steve kuhusu kauli alizotoa Mh Msigwa bungeni jamaa amekuja na kashfa na sio hoja kwa nini anastahili nafasi aliyopewa na Mh Kigwangala.

Hivi ina maana anaamini kuwa anaweza kuleta watalii Tanzania ni Mara 10000 Bongozozo anaweza fanya hiyo kazi ila si yeye. Ni kweli yeye, wenzie na Mh Kigwangala walikua na nia nzuri ya kukuza utalii ila hawakua watu sahihi kwa kazi ile



Huyu na ni mpuuzi tu.
Aende bungeni bungeni akapinge hiyo hoja.

NB:
Kutokana na tabia yake iwe kweli au kazuga, hili la kugombea wanawake linamuondolea heshima yeye na wasanii wengine. \inaonesha wasanii ni wahuni na wanaenndekeza mambo ya ngono/uzinzi na ukahaba
 
Nimeangalia hoja za Steve kuhusu kauli alizotoa Mh Msigwa bungeni jamaa amekuja na kashfa na sio hoja kwa nini anastahili nafasi aliyopewa na Mh Kigwangala.

Hivi ina maana anaamini kuwa anaweza kuleta watalii Tanzania ni Mara 10000 Bongozozo anaweza fanya hiyo kazi ila si yeye. Ni kweli yeye, wenzie na Mh Kigwangala walikua na nia nzuri ya kukuza utalii ila hawakua watu sahihi kwa kazi ile



katika hili Msigwa hoja yake ilikuwa inasimama katika utaratibu na kama ilivyokuwa huko nyuma, kabla ya awamu ya 5, na alikuwa yuko sahihi; kitu ambacho si lazima kifanyike hivyo hata kwenye awamu hii. Kwa kipindi hiki cha JPM, ukiamua kutumia utaratibu wa zamani kwamba wewe ni Waziri unasimamia Sera, hivyo ukawa unakaa ofisini hufanyi hata ziara wakati Tandahimba watu wanalalamika hawana maji, anakutumbua within seconds.

Mawaziri kutatua kero za wanachi LIVE haimaanishi kuwa wameacha kusimamia sera, au kwamba wanafanya kazi kwa operation. Kwani mimi kama ni Waziri, kutatua kero za wananchi nikiwa niko kwenye ziara ya kukagua miradi ya maendeleo, KUNANIZUIAJE KUSIMAMIA SERA? Je, sera inasimamiwa tu kwa kukaa kwenye dawati nikiwa ofisini? Aache kuwachangaya mawaziri na mimi ninachelea kusema kuwa atakayefuata ushauri wa Msigwa anaweza akapoteza nafasi yake kirahisi tu kwa sababu kwa kipindi hiki cha JPM, utendaji kazi wa aina hiyo ni kama hauwezekani, ilikuwa huko nyuma! Sera naweza hata nikasimamia hata nikiwa nimekaa ofisini mwaka mzima, isipokuwa sasa MATOKEO ya utekelezaji wake ndiyo utakuwa mgogoro. Ndiyo maana tulikuwa tunapata matatizo huko nyuma ambayo tumeshaanza kuyaondoa sasa, kwa sababu tulikuwa tunastick na kanuni za kwenye maandishi ambazo katika uhalisia, zilikuwa hazitunufaishi na chochote. Huko ndiko Msigwa anataka turudi?
 
Huyu jamaa aliwahi kuwa msanii wa kitu gani?
 
Kuwe na affordable hotels kwa watu wa kipato cha kawaida. Wazungu wengi wanaofanya utalii wanategemea credit cards. Akishapata kazi mortgage , gari na starehe inayofuata ni kuzunguka dunia. Sehemu kama Egypt unaweza kupata holiday ya $2,000 hiyo ni package pamoja na nauli ya ndege, hotel na usafiri kwa siku saba.

Ukipata watalii 50,000 wanaotumia $2,000 kwa mwaka kuna faida. Wahudumu wa hoteli watakua na uhakika wa kusomesha watoto wao.
Wazo lako limekaa vema ila tatizo nchi yetu kila kitu kinafanyiwa siasa tu, ifike muda tuache siache uchwara tufanye kazi....yan mpaka Wakenya jirani zetu wana tupiku....
 
Nimeangalia hoja za Steve kuhusu kauli alizotoa Mh Msigwa bungeni jamaa amekuja na kashfa na sio hoja kwa nini anastahili nafasi aliyopewa na Mh Kigwangala.

Hivi ina maana anaamini kuwa anaweza kuleta watalii Tanzania ni Mara 10000 Bongozozo anaweza fanya hiyo kazi ila si yeye. Ni kweli yeye, wenzie na Mh Kigwangala walikua na nia nzuri ya kukuza utalii ila hawakua watu sahihi kwa kazi ile


Sijawahi kumchukulia serious Stivie Nyerere aka MZEE WA FUTUHI.
 
Yaani wote mnamuatack Steve nyerere.
Msameheni yule ni mgonjwa Wa akili anafahamika,mnachofanya ni unyanyapaa
 
so ametukana wanawake wote ....arudishe pesa za msiba wa mtoto wa muna na kayumba
 
Back
Top Bottom