Stori: Uko wapi rafiki? Kuna cha kujifunza hapa?

Stori: Uko wapi rafiki? Kuna cha kujifunza hapa?

Misada ya huruma mingine kama hiyo ya watu unawakuta wemegongewa barabarani usiku inahitaji moyo kuwa saidia😕
 
Mkuu, mimi sijam-criticise jamaa ila nimesema hivyo alipoandika na kukatisha utamu ili tuanze kumsubiria, kila mara tuchungulie kama jamaa kesha-post mwendelezo! Hii strategy wanatumia sana manguli wa hadithi hapa JF ili kuvuta attention za followers wao! By the way, nakuomba mkuu ubaki njia kuu, michepuko siyo dili! (just joking with your ID)!
mbona unamcriticise wakati hakuna dalili yoyote ya uongo hapo?
 
....umewezaje kujua majina yake, anapokaa, umri wake? km si mpenzi wako?......YAHAYA unaishi wapiii...
 
Tulipoishia jana:

Polisi wetu wakasisitiza tuzungumze kwa ufupi ili safari yetu ianze kwenda eneo la tukio! Wakati naanza kuwasimulia wale wana ndugu kuhusu tukio lililompeleka ndugu yao Muhimbili, kulikuwa na maswali yanachomekewa na wale wadada, hapa na pale!

Ilifika zamu ya Yule mtu wa kiume kuuliza swali! Swali lake la kwenza lilikuwa la ajabu, ni swali lililochanganyika na majibu, naomba nimnukuu Yule mtu wako rafiki: "wewe ni mwanaume, unawezaje kumsaidia mtoto wa kike, usie na uhusiano nae?

Nyie mtakuwa mmetoka guest, kwa haraka zenu mwenzio akagongwa na gari! Wewe unamjua huyu binti acha ujanja bwana mdogo!" wakati najaribu kujitetea, jamaa akanikunja kwa ile style ya kunisimamisha kutoka pale chini nilipokaa! Ghafla Polisi wetu wakashtuka!

Tukutane baada ya ftari!

Leo tena:

Polisi wale wakaingilia kati purukushani ile, wakanitoa mikononi mwa mbabe-mp***vu Yule! Polisi wakajipa jukumu la kumuelimisha Yule mbabe – mpu**avu, hapa ndio sehemu nyingine nilipowapendea Polisi wale!

Yupo mmoja wa polisi wale alinifurahisha kwa namna alivompiga maswali mkorofi wangu:


  1. Hata kama jamaa anakumegea demu wako, bado lazima umpe hongera kwa kuwa amemjali wakati alikuwa na fursa ya kumtelekeza!
  2. Dsm hatuna watu wa hivi, huyu bwana mdogo hana nia ovu hapa, ndio maana amejitolea muda wake na pesa kumsaidia huyu binti!
  3. "Utakuwa huna akili wewe," alisema mwanausalama mwingine! Unajua gharama ya hela ambayo huyu bwana ametumia mpaka mtu wenu anapata matibabu hapa, eeeeeeh!
  4. Alifoka Mwanausalama yule, akaendelea! Kijana pole, hongera kwa kumsaidia Yule binti, lakini pole kwa kuwa umeanza kulipwa maumivu hapa hapa! Afande tumchukue huyu mpum**vu…..!

Mazungumzo yangu ya nini kilitokea kwa wale jamaa wa manusra wangu, yalifika kikomo kwa kuwa kulikuwa na mada mpya imeingia - kuwasihi wanausalama wale wasiondoke na Yule "mbabe – mpu**avu!"

Aibu na fedheha aliyosababisha Yule bwana ilitukwaza wote pale, hasa mimi ambaye sikuwa nimefikiria kitu kama kile.

Rafiki yangu, Yule dada ako mkubwa ni muungwana sana, aliwaomba wale polisi wanipe fursa, nitaje gharama nilizotumia ili anirudishie. Nilikataa. Dadako alinibembeleza sana, kutaja kiasi ambacho nimegharamia mpaka kufika muda ule. Nilikataa.

Yupo nesi mmoja, alikuwa akishuudia zile vurumai, aliingilia kati mazungumzo yetu na akaanza kumorodheshea dada yako pesa ambazo nilitumia pale hospitali mpaka wewe - manusra wangu ulipopatiwa kitanda!

Alitaja gharama zote tena kwa kiasi kile kile nilichotoa pesa, na kamwambia dada kuwa "sijui kwa huko nyuma walipotoka, ila kwa hapa ametumia pesa hizo kwa ndugu yenu".

Dadako alitoa kiasi cha pesa ambazo sikuweza kujua ni kiasi gani kwa kuwa zilikuwa zimekunjwa ktk muundo wa "msokoto", bado nilikataa! Nilisisitiza hakukuwa na sababu ya kulipana, cha msingi tuweke nguvu ktk afya ya Mgonjwa wetu!

Nakumbuka gharama halisi za pesa nilizotumia kwako, kwa usiku ule hazikufika hata elfu 30, ila ni zaidi ya elfu 20. Pesa ambazo dadako alitaka kunipa zilikuwa ni zaidi ya hata elfu hamsini (nilihisi kwa macho ya usiku ule na namna zile noti zilivosokotwa).

Baada ya kuzikataa pesa, dada aliniomba namba yangu ya simu, bahati mbaya sikuwa na simu (ndio kwanza nilikuwa nimetoka kumaliza A – level, na kipato changu kilitokana na kufundisha tuition wanafunzi wa secondary, maeneo ya mwenge, DSM, nyuma ya NAKIETE PHARMACY, tutiton yetu ilikuwa maarufu kama MAPAMBANO, ama kwa MUSSA au P.Diddy).

Dadako alichoka kabisa, kwake aliniona mimi ni mtu ambae anaitaji kuwa na mawasiliano naye mara kwa mara kuanzia siku ile! Kufika hapo, dadako mkubwa akawa hana namna ya kuwasiliana na mimi.

Akaniuliza ninapoishi nikamjibu – BUGURUNI, akazidi kuchoka kwa kuwa alijua siwezi kumtajia jina la mtaa, na pia namba ya nyumba. Huku kwetu namba za nyumba ni muhimu zaidi kwa serikali, tena serikali ya mtaa kuliko hata sisi wakazi wa nyumba hiyo!

Kwanza hata kichwani haikuwepo, japo najua nyumba ninayokaa, pale juu ya mlango wa nje kuna namba! Kwetu majina ya mitaa ni ya wazee maarufu ama mti mkubwa! Kufupisha mazungumzo yale, dada akanisihi mapema asubuhi kesho yake nifike pale hospitali, bila kukosa, ombi lake lilikuwa ndani ya uwezo wangu!

Kitu kimoja ambacho nilifanya kabla ya kuondoka na wanausalama wale, niliwatajia jamaa zako amana zote ulizokuwa nazo mpaka unapatwa na masaibu yale.

Niliwaambia kuwa, ulikuwa na mkoba (handbag), ulikuwa na saa ya mkononi, ulivaa viatu – mchuchumio, ulikuwa na simu, ulikuwa na herein za dhahabu, ulikuwa na handkerchief.

Tulivikabidhi hivi vitu kwa mama mmoja, msamariamwema aliekuwa anauza duka la dawa pembeni ya Mandela rd, ni mama huyu ambae alipekuwa mkoba wako (kujiridhisha) na kukuta pamoja na vitu vingine, ulikuwa na pesa.

Niliwatajia jamaa zako hizi data, na kuwaomba waende wakaonane na mama huyu, wajitambulishe, wapewe amana zako zote! Na kama kutakuwa na tofauti kati ya vile nilivoeleza na vile watakavyopewa na mama Yule, nilimuahidi dada kuwa, nitakuwa tayari kutoa ushirikiano!

Mpaka kufika saa 8 usiku ule, tayari tulikuwa eneo la tukio, Ubungo, maeneo ya kituo cha dala dala BAKWATA. Wale ndugu wa manusra wangu waliondoka kivyao, hususani baada ya Yule "shemeji" kutibua hali ya hewa!

Hapa maofisa wa polisi hawakuwa na maswali mengi. Walihoji na kutaka kujua vitu vichache sana kama:

  • Hilo gari uliliona kwa macho yako?
  • Lilikuwa la aina gani?
  • Gari lilikuwa linatokea wapi?
  • Huyu manusra wako alikuwa anatoka upande gani na anavuka kwenda upande gani?
  • Wewe na wenzio mlikuwa mmekaa wapi?

Ni maswali ambayo yalikuwa yanajibika. Niliwajibu vizuri, huku nikijua nipo mbali na hatari dhidi ya wanausalama hawa, na kuwa hii ndio ng'we ya mwisho, na mimi nirudi nyumbani, nikajipumzishe.

Walinishukuru wanausalama wale, wakaniomba wanipe lift mpaka Buguruni, baada ya mimi kuwaambia naishi Buguruni. Wakanisihi nisikose kwenda kumjulia hali mgonjwa wangu ifikapo kesho asubuhi, kitu ambacho hata wasingesema, nilishaweka nia!

Niliamka salama, japo na uchovu wa kutolala kwa kutosha. Safari ya Muhimbili ikanihusu. Nilibahatika kuwahi Muhimbili.

Ngojeni kwanza, baadae nitarudi, kuna kionjo cha Mkude Simba hapa e.fm nakiskiliza!


 
....umewezaje kujua majina yake, anapokaa, umri wake? km si mpenzi wako?......YAHAYA unaishi wapiii...

mimi sikujua kwa nini wanihisi ni mpenzi wangu, na sio dada yangu?
 
Uliposema - ".....aya kwa hiyo unasubiria fadhila yakupewa penzi au ni nini?" Nakuomba usubiri, mwezi huu uishe, hizi lugha ni ngumu kipindi hiki kuzijibu!

Aya ika jibu unalo kichwani
 
Back
Top Bottom