Stori: Uko wapi rafiki? Kuna cha kujifunza hapa?

Stori: Uko wapi rafiki? Kuna cha kujifunza hapa?

Dah! afadhali imeunganishwa,
Btw Hicho kionjo cha mkude hakijaisha tu mkuu.?
 
Rudiii wewe lete story la sivyo ntawapigia wale wanausalama wakutie ndani mpaka mgonjwa atapopona
 
mbona nimesharudi na Part 3!

Uwe unanishtua basi...ujue hii stori yako na mimi nawasimulia washikaji hapa kijiweni

Btw mbona hii part III inaonekana kama hujaiedit vizuri, maana naona ni kama simulizi linalofanywa na mtu kwa mtu mwingine na sio simulizi la slim5 kwa wanaJF?
 
Last edited by a moderator:
duh.. yaan utamu unakolea umekatisha. ukirudi tena inabidi nianza kuvuta hisia upya.GUD GUD STORY
 
Uwe unanishtua basi...ujue hii stori yako na mimi nawasimulia washikaji hapa kijiweni

Btw mbona hii part III inaonekana kama hujaiedit vizuri, maana naona ni kama simulizi linalofanywa na mtu kwa mtu mwingine na sio simulizi la slim5 kwa wanaJF?

Watu8 bado mimi mwenyewe slim5 ndiye ninaesimuli, hajatokea mwingine wa ku-hack!
 
hahahaaaa... no need of comments... we all know demu alipona, mkawa wapenzi then akakulima kibuti coz huna hela... ryt now upo in great pain....

umejitahidi kukurupuka!
 
Walinishukuru wanausalama wale, wakaniomba wanipe lift mpaka Buguruni, baada ya mimi kuwaambia naishi Buguruni. Wakanisihi nisikose kwenda kumjulia hali mgonjwa wangu ifikapo kesho asubuhi, kitu ambacho hata wasingesema, nilishaweka nia!

Niliamka salama, japo na uchovu wa kutolala kwa kutosha. Safari ya Muhimbili ikanihusu. Nilibahatika kuwahi Muhimbili.

Bado nakumbuka rafiki yangu. Nilikuwa wa kwanza kufika pale MNH. Na kwa kuwa ulikuwa ni muda wa kuona wagonjwa, nilipitiliza moja kwa moja hadi wodini. Ilikuwa rahisi kukumbuka. Niliukumbuka mtindo wako wa nywele uliokuwa nao tangu jana yake, siku ya ajali.

Pia nilikukumbuka kwa urahisi, hasa baada ya kuona mguu wako umevishwa POP, lile vijana wa mtaani wanaita ogo (sina uhakika kama sio hogo!). nilifika mpaka kitandani kwako.

Nikakusalimia. Ukaitikia. Ndani ya nafsi ukawa katikati ya hisia kwamba huyu ndiye Msamariamwema aliekuokota ama ni mtu mwingine.
Wakati nikiendelea kukusikiliza, ukielezea namna ulivolala usiku ule wa kwanza ndani ya MNH, ukifafanua na maumivu ulioyaskia usiku ule!

Ghafla kikundi cha wwatu, zaidi ya watano, ukawaona wanaingia. Nilikuona ukitabasamu. Kwa sauti ya chini, sijui ulikuwa ukininong'oneza ama kunielekeza, ukasema: "jamani, dada Yule!" Nilipogeuka na mimi, niliwakumbuka watu wawili. Nilimkumbuka dada yako mkubwa. Nilimkumbuka na Yule rafiki yangu, mwenye makeke mengi. Nakumbuka vizuri, Yule jamaa hakuweza hata kunisalimia, alishindwa.

Rafiki yangu, unakumbuka namna dada yako mkubwa alivonikumbatia kwa furaha, kwa mashamsham tele, na alilitaja jina langu kwa ufasaha (sio slim5) kama vile ni watu tunaofahamiana vzr kwa muda mrefu.

Na mimi nilionyesha kumfurahia dada yako. Alionyesha kushangaa sana kuona nimemudu kuwahi MNH. Pia aliniuliza kuhusu jana, nini kiliendelea kule Ubungo, eneo la tukio, baada ya mimi kuondoka na wale wanausalama. Niliwasimulia yote. Ulionyesha kuguswa sana na simulizi yangu kwa lile jopo la wanafamilia yako na Yule mpenzi wako.

Mungu wangu.
Kumbe rafiki yangu hukuwa na kumbukumbu nzuri ya nini kilikupata usiku wa jana. Dada yako mkubwa alinisaidia kazi hii. Alisimulia vizuri sana namna mfululizo wa matokio ulivokuwa unakufuata usiku wa jana, huku mimi nikitumika kujalizia maelezo. Muda wote huu, Yule mtu wako hakuwa na kauli hata moja. Alikuwa bubu ghafla.

Nakumbuka rafiki yangu, ulivoanza kutoa mfululizo wa maneno, mengi sana, yaani mengi mno, yote yalilenga kuelezea namna unavonishukuru, nilikuona namna ulivoishiwa maneno yenye kumaanisha unanishukuru. Nilikuomba usiendelee sana na shukrani zako, lakini bado ulisisitiza kunishukuru. Nilielewa nini ulimaanisha. Na mimi nilikushukuru sana.

Dada ako nae alitumia muda kidogo kunipamba na sifa mbali mbali, mstaarabu, muungwana, mwenye huruma, mjasiri, mwenye kujitolea, una moyo wa ajabu! Sifa zilikuwa nyingi sana. Nakumbuka. Nilikuwa nampiga kijicho jamaa yako muda wote ambao nilikuwa nasifiwa, nilikosa maelezo ya namna sura yake ilivokuwa ikibadilika badilika.

Alikuja nesi, akatoa maelezo ya pamoja kuhusu hali yako na maendeleo yako. Tulimshukuru sana nesi Yule. Nakumbuka dada yako alimpa na hela ya chai. Nesi Yule nae hakuwa mchoyo, aliwaomba wale wanafamilia yako, warudishe shukrani kwangu, akidai nimefanya kazi kubwa sana. Na mimi nilimrushia mpira yeye mwenyewe nesi kuwa, ndiye anaestahili kupewa sifa zote!

Muda wa kuona wagonjwa ukawa umeisha! Tukakuaga. Ukamuomba dada yako, ahakikishe anakuwa na mawasiliano mazuri na mimi, ikibidi apajue nyumbani ninapoishi (dadako alikujibu, kuwa sina simu). Ulisisitiza kuwa nisijeacha kukuona pale MNH. Nikakuahidi nitaendelea kufuatilia siha yako mpaka utakapotolewa pale hospitali. Ulifurahi. Ukatabasamu rafiki yangu.

Rafiki yangu kuna kosa ukalifanya.
Hukujua kama ni kosa. Baadae nikaja jua lilikuwa kosa kubwa. Wakati tumeshaagana na wewe, tunaondoka kama kikundi cha wanafamilia moja, mimi na wale jamaa zako, ukaniita kwa jina langu (ambalo ulilijua muda mfupi tu, tangu tufike pale kitandani kwako, jina langu halisi lina herufi 4 tu, na ni moja ya majina common sana kwa watanzania wengi, sijui kwa nini)

Kosa la pili. Bila kujijua.
Na mimi nikaitikia wito wako. Nikarudi peke yangu. Huku wale wengine kwenye ile convoy wakiwa wamebutwaa, wanaangalia nini kimetokea. Hawakwenda. Hawakurudi. Walisimama. Wakaona ulivokuwa unaniomba nikuinamie pale kitandani. Na mimi nikatii.

Kosa la tatu. Mara, ukaonekana unaninong'oneza sikioni, huku mkono wako mmoja umeupitisha sehemu ya nyuma ya shingo yangu.

Muda wa ftar.
 
Back
Top Bottom