Stori: Usife haraka mpenzi wangu

Stori: Usife haraka mpenzi wangu

usife kwanza mpenzi wangu....episode.36




Deo ameamua kutua mzigo mzito moyoni mwake, amemwambia Cleopatra kwa uwazi kabisa kwamba hawezi kumuoa tena kwa kuhofia kumuudhi Levina ambaye alimsaidia sana hadi kupata elimu na baadaye kazi, jambo hilo linaungwa mkono na mama yake Cleopatra. Deo anaondoka zake.

Akiwa ndiyo kwanza anaingia nyumbani kwake, Deo anapokea ujumbe mfupi kutoka kwa Levina ambaye anamshukuru kwa kusikia sauti yake. Kwa Deo inakuwa maajabu, maana hakumweleza chochote kuhusu uamuzi wake. Jambo hilo linamchanganya sana Deo.
SASA ENDELEA…

ALIRUDIA kusoma ule ujumbe mara mbili zaidi, lakini maneno yaliendelea kuwa yale yale, kutoka kwa mtu yule yule, yakiwa ndani ya simu yake yeye mwenyewe! Deo akapigwa na butwaa.

“Amejuaje haya?” Akajiuliza, lakini hakupata majibu.
Akajivuta hadi mlangoni, akafungua mlango na kuingia ndani, akaenda kujitupa kwenye sofa kubwa akihema kwa kasi. Hapo akaanza kumkumbuka kwa upya kabisa Levina. Kuna kitu kilianza kumwingia akilini mwake.

Hakuwaza tena juu ya meseji ile iliyoingia kwenye simu yake kimaajabu, alimuwaza Levina, mwanamke ambaye alimpenda kwa mapenzi yake yote, pasipo shinikizo kutoka kwa mtu yeyote. Pasipo matarajio ya kupata kitu chochote! Alimpenda yeye tu!
Mapenzi tu!

Penzi la dhati!
“Kuna kitu natakiwa kufanya,” akawaza akiangalia simu yake.
Wazo la kumpigia Levina likamwingia akilini mwake.

Ilikuwa lazima azungumze naye. Wakati huo hakuwaza tena kuhusu kazi, suala la kazi halikuwa na maana sana kwake. Kwa kutumia vyeti vyake alikuwa na uhakika mkubwa sana wa kupata kazi sehemu nyingine, kuliko kuendelea kukaa na mateso moyoni kwa kuishi na mwanamke ambaye mapenzi yake yalikuwa ya wasiwasi.
Akabonyeza namba za Levina na kumpigia, kiasi cha sekunde nane tu, Levina alikuwa hewani akizungumza na Deo…

“Haloo Levina!”
“Yes Deo, mambo vipi?”
“Poa, lakini sipo sawa sana!”
“Nini tatizo?”
“Kuna kitu nahisi kinaniumiza sana moyoni mwangu, Levina naomba unisamehe kwa yote yaliyotokea, tafadhali sana, nakuomba kwa moyo wangu wote. Mimi ni binadamu na nilipitiwa, siku zote kwenye maisha ni vyema kukosea ili kupata nafasi pia ya kujifunza.

“Waswahili wanasema, watu wanajifunza kutokana na kukosea. Nakuomba unisamahe ili niweze kuishi kwa amani moyoni mwangu!” Deo akasema kwa sauti ya chini sana akionekana kujutia sana yaliyotokea.
“Deo!” Levina akaita.

“Nakusikia mama…”
“Ni kweli unaomba msamaha kwa moyo wako wote?”
“Kweli kabisa, naweza kuapa kwa namna yoyote unayotaka!”
“Hakuna sababu ya kuapa, ni wewe mwenyewe na nafsi yako, kama ni kweli unajua umekosea ni vizuri na ni rahisi kusamehewa.”

“Kweli Levina najuta kukukosea, nimetambua kosa langu, nisamehe tafadhali!”
“Nilishakusamehe Deo, lakini ukweli ni kwamba sijakusamehe kikamilifu!”
“Unamaanisha nini?”

“Namaanisha kwamba nilishakusamehe tangu siku nyingi, lakini si kwa moyo wangu!”
“Sawa, naomba basi kuanzia leo uwe umenisamehe kwa moyo wako Levina!”
“Inawezekana Deo, lakini kuna masharti mawili!”
“Masharti?” Deo akauliza kwa mshangao mkubwa.
“Ndiyo kuna masharti mawili, kama ukiweza kuyatimiza, basi nitakusamehe moja kwa moja na nyongo iliyokuwa ndani ya moyo wangu itaondoka.”

“Ni masharti gani hayo? Niambie tafadhali!”
“Si kwa haraka kiasi hicho, lakini nitakuambia.”
“Lini?”
“Nipe muda, lazima nikutane na wewe, nahitaji kuzungumza na wewe, tena uso kwa uso.”
“Itakuwa lini?”
“Nitakujulisha, kwa sasa pumzika kwanza.”
“Sawa Levina, lakini nina ombi moja kwako!”
“Nakusikia!”

“Isiwe muda mrefu sana, siwezi kukaa na hili jambo muda mrefu, nahisi moyo wangu unaungua!”
“Usijali najua ni kiasi unateseka, najua pia ni kiasi gani unataka kuishi huru. Yote hayo nayajua na nitayachukulia kwa uzito mkubwa, muda ukifika nitambia!”

“Nimekuelewa vizuri, lakini nilikuwa na lingine!”
“Nini tena?”
“Nimepata meseji yako muda si mrefu!”
“Ndiyo!”
“Umejuaje hayo?”

“Siku zote kama kitu unakipenda, ni rahisi kujua kinavyoendea hata kama hutapewa taarifa. Nimejua kwa sababu nakupenda Deo!”
“Lakini haraka sana!”
“Ni kwa sababu nakupenda sana!”
“Haya bwana.”
“Siku njema Deo!”
“Kwako pia.”

Deo hakutoa simu haraka sikioni pamoja na kwamba alikuwa ameshaagana na Levina ambaye alishakata simu. Ni kama alikuwa amepigwa bumbuwazi au hajui kinachoendelea. Moyo uliendelea kuteswa na mapenzi, alimtaka sana Levina kwa wakati huu.

Aligundua kwamba penzi lake kwa Levina lilikuwa zito na lenye thamani zaidi ya Cleopatra ambaye alijilazimisha kutokana na mali zake.
“Nitampata Levina wangu, lazima arudi tena kwangu, lazima...” akawaza akisimama na kujivuta chumbani mwake.
***
Mama Cleopatra baada ya kutoka chumbani na kuwaacha Deo na Cleopatra aliifuata simu yake chumbani kwake na kumpigia Levina ili kutafuta ukweli.

“Hujambo mwanangu?”
“Sijambo mama shikamoo...” Levina akasalimia.
“Marhaba...haya mbona mwenzio anafanya mambo ya ajabu unashindwa kuniambia binti yangu?”
“Nani mama? Patra?”
“Ndiyo!”
“Amefanya nini tena?”
“Unamjua Deo?”
“Ndiyo!”
“Unamjuaje?”

“Mama Deo alikuwa mpenzi wangu, lakini Patra kwa sababu ya pesa zake ak....” Levina alishindwa kumalizia sentesi yake na kuanza kulia
 
USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.37

Mama Cleopatra baada ya kutoka chumbani na kuwaacha Deo na Cleopatra aliifuata simu yake chumbani kwake na kumpigia Levina ili kutafuta ukweli.
“Hujambo mwanangu?”

“Sijambo mama shikamoo...” Levina akasalimia.
“Marhaba...haya mbona mwenzio anafanya mambo ya ajabu unashindwa kuniambia binti yangu?”
“Nani mama? Patra?”
“Ndiyo!”

“Amefanya nini tena?”
“Unamjua Deo?”
“Ndiyo!”
“Unamjuaje?”

“Mama Deo alikuwa mpenzi wangu, lakini Patra kwa sababu ya fedha zake ak....” Levina alishindwa kumalizia sentesi yake na kuanza kulia.
SASA ENDELEA...

YALIKUWA maumivu makali sana kwa Levina ambaye alianza kukumbuka tangu siku ya kwanza alipokutana na Deo sokoni na kuvutiwa naye. Akakumbuka jinsi alivyofanya mbinu na kuhakikisha anaingia nyumbani kwao kama mfanyakazi wa ndani lakini ndani ya moyo wake akiwa na kitu tofauti kabisa na hicho.

Ni Levina huyo huyo ndiye aliyejitolea kumsomesha Deo hadi kufikia mafanikio na kupata kazi. Kunyang’anywa na rafiki yake mpenzi, waliokua na kusoma pamoja kulimuuma sana ndani ya nafsi yake. Alishindwa kuzuia hisia zake na kujikuta akianza kulia kwenye simu.

Alianza kwa sauti ndogo, lakini jinsi kumbukumbu zile mbaya zilivyozidi kumsumbua, ndivyo alivyozidisha kilio chake.
Mama Cleopatra akapata kazi ya kumbembeleza Levina.

“Pole sana mwanangu, naomba usilie, nimeshajua kila kitu na huyu kijana mwenyewe ameamua kuachana na Patra na kwa jinsi anavyoonekana, anajutia sana kitendo alichokifanya. Nahisi bado anakupenda na ni mapenzi hayo ndiyo yanayomsukuma kusema ukweli leo hii na kuamua kuachana naye.

“Kuna uwezekano mkubwa sana akarudi kwako na kukuomba msamaha, tafadhali naomba umsamehe na nitakuwa tayari kuwasaidia kwa namna yoyote. Najua thamani ya mapenzi mwanangu, najua maumivu ya kunyang’anywa mpenzi. Tafadhali mwanangu rudisha moyo wako, naomba umkubalie huyo kijana!” Mama Levina akasema kwa sauti ya utulivu sana.

“Kweli mama?”
“Ndiyo mwanangu!”
“Lakini unadhani Deo ana mapenzi ya kweli mama? Si ni aina ya wanaume ambao wanaweza kuyumbishwa ovyo?”
“Ni tamaa tu, halafu ukumbuke kwamba alikuwa na hofu ya kufukuzwa kazi.”

“Mama, sasa ni kwanini asiwe na hofu na mimi ambaye ndiye niliyemtafutia hiyo kazi, akawa na wasiwasi wa kupoteza tu hiyo kazi bila kumkumbuka aliyemfanya akaipata?”

“Umeongea jambo la msingi sana mama, lakini ujue kwamba, shetani naye ana mambo yake. Naweza kusema kwamba alipitiwa, lakini kiukweli mwanangu mpatie nafasi nyingine, utaona mabadiliko yake. Atakuwa amejifunza.”
“Sawa mama, nitajitahidi!”

“Siyo kujitahidi, naomba iwe hivyo!”
“Sawa mama.”
“Niahidi Levina!”
“I promise you mom!” (Nakuahidi mama)
“Thank you my daughter!” (Nashukuru binti yangu)

Kila mmoja alikuwa na lake kichwani mwake, mama Cleopatra alikuwa na nia ya dhati ya kumsaidia Levina ambaye alikuwa sawa na mwanaye kwa namna walivyokuwa marafiki wakubwa. Bado aliona thamani yake kama mwanaye.

Hakufikiria juu ya aibu ya watu wengi walioalikwa kwa ajili ya sherehe hiyo, kwake yeye sherehe hiyo isingekuwa na maana kama ingefungwa ndoa huku Levina akilalamika.

Levina alifurahishwa sana na maelezo ya mama yake Cleopatra, alimuona mzazi bora ambaye anaangalia usawa na kuonesha mapenzi yake kwa watoto wake wote. Bado alikuwa akifikiri vizuri suala la kurudiana na Deo.
Moyoni mwake Deo alikuwepo!
Amejaa tele!

***
Mawimbi yalikuwa yanapiga kwa kasi sana ufukweni mwa Bahari ya Hindi eneo la Coco. Watu walikuwa wengi sana Jumamosi hiyo walipunga upepo baharini. Ilikuwa jioni, mishale ya saa 11:30, jua likianza kung’ang’ania kupotea na giza kusita kuchukua anga!

Ni kama vitu hivi viwili vilikuwa vikishindana, mashindano hayo yalifanya ufukwe kuwa na rangi kama ya dhahabu, mwanga kuwa hafifu kiasi na kupendezesha mandhari ya Ufukwe wa Coco.

Pembeni kabisa, juu ya jiwe kubwa, walikuwa wamekaa Deo na Levina, mikononi mwao kila mmoja alikuwa ameshika box lenye maji ya matunda wakinya taratibu kwa mrija. Levina ndiye aliyemwalika Deo kwa mtoko huo akitaka kuzungumza naye na kumpa masharti yake aliyosema anataka kumpa.

Deo alikuwa kimya akisubiri kusikia masharti ya Levina ambaye alikuwa amependeza sana jioni hiyo. Tayari Deo alikuwa ameshapona kabisa, afya yake ikianza kunawiri na makunyanzi usoni yakianza kupotea.

“Kwanza kabisa, naomba unisamehe kwa kukukosesha kazi. Najua kama siyo mimi, ungekuwa unaendelea na kazi yako. Kwa hilo naomba sana unisamehe Deo!” Levina alianza kwa kutamka maneno hayo.

“Hapana Levina usiseme hivyo, mimi ndiye mkosaji. Halafu hiyo kazi haina maana yoyote kwangu kama wewe hutakuwa na amani na mimi. Hutakuwa na furaha na mimi. Haitakuwa na maana yoyote kabisa. Napenda kuona unafurahi!”

“Deo lazima utambue kwamba nakupenda sana, nilikupenda kwa moyo wangu wote na nimeshindwa kukutoa moyoni mwangu!”
“Najua!”

“Nitakupa masharti mawili, najua ni magumu sana, lakini ukiyaweza nitakusamehe milele.”
“Nipo tayari Levina niambie tu mama!”
“Labda nisisitize tena kwamba, nakupenda sana, siwezi kuacha kukupenda katika maisha yangu yote, sharti la kwanza ili nikusamehe Deo, unatakiwa ukubali kufunga ndoa na mimi!” Levina akasema akimwangalia Deo usoni.

“Kwa hilo nipo tayari, sijui kuhusu wazazi wako!”
“Mambo ya wazazi niachie mimi, kama umekubali basi vizuri, sharti la pili ni gumu kidogo, lakini nalo ukikubaliana nalo nitakusamehe!”
“Sema mpenzi, nipo tayari kwa chochote!”

“Deo naomba unisamehe kwa nitakalokuambia, najua litakuumiza na hutanielewa kirahisi, lakini ndiyo ukweli wenyewe. Naomba unielewe kwamba sikuwa na nia mbaya, nia yangu ilikuwa nzuri kabisa, lakini lazima unisamehe Deo!”
“Ni nini? Hebu niambie basi Levina...” akasema Deo akimkazia macho Levina.

“MIMI NDIYE NILIYEKODI WATU WAKUPIGE RISASI KWENYE LIFTI!” Levina akasema akilia.
“Unasemaje?” Deo akauliza kwa sauti ya ukali sana.
 
USIFE KWANZA MPENZI WANGU.....EPISODE.37

Mama Cleopatra baada ya kutoka chumbani na kuwaacha Deo na Cleopatra aliifuata simu yake chumbani kwake na kumpigia Levina ili kutafuta ukweli.
“Hujambo mwanangu?”

“Sijambo mama shikamoo...” Levina akasalimia.
“Marhaba...haya mbona mwenzio anafanya mambo ya ajabu unashindwa kuniambia binti yangu?”
“Nani mama? Patra?”
“Ndiyo!”

“Amefanya nini tena?”
“Unamjua Deo?”
“Ndiyo!”
“Unamjuaje?”

“Mama Deo alikuwa mpenzi wangu, lakini Patra kwa sababu ya fedha zake ak....” Levina alishindwa kumalizia sentesi yake na kuanza kulia.
SASA ENDELEA...

YALIKUWA maumivu makali sana kwa Levina ambaye alianza kukumbuka tangu siku ya kwanza alipokutana na Deo sokoni na kuvutiwa naye. Akakumbuka jinsi alivyofanya mbinu na kuhakikisha anaingia nyumbani kwao kama mfanyakazi wa ndani lakini ndani ya moyo wake akiwa na kitu tofauti kabisa na hicho.

Ni Levina huyo huyo ndiye aliyejitolea kumsomesha Deo hadi kufikia mafanikio na kupata kazi. Kunyang’anywa na rafiki yake mpenzi, waliokua na kusoma pamoja kulimuuma sana ndani ya nafsi yake. Alishindwa kuzuia hisia zake na kujikuta akianza kulia kwenye simu.

Alianza kwa sauti ndogo, lakini jinsi kumbukumbu zile mbaya zilivyozidi kumsumbua, ndivyo alivyozidisha kilio chake.
Mama Cleopatra akapata kazi ya kumbembeleza Levina.

“Pole sana mwanangu, naomba usilie, nimeshajua kila kitu na huyu kijana mwenyewe ameamua kuachana na Patra na kwa jinsi anavyoonekana, anajutia sana kitendo alichokifanya. Nahisi bado anakupenda na ni mapenzi hayo ndiyo yanayomsukuma kusema ukweli leo hii na kuamua kuachana naye.

“Kuna uwezekano mkubwa sana akarudi kwako na kukuomba msamaha, tafadhali naomba umsamehe na nitakuwa tayari kuwasaidia kwa namna yoyote. Najua thamani ya mapenzi mwanangu, najua maumivu ya kunyang’anywa mpenzi. Tafadhali mwanangu rudisha moyo wako, naomba umkubalie huyo kijana!” Mama Levina akasema kwa sauti ya utulivu sana.

“Kweli mama?”
“Ndiyo mwanangu!”
“Lakini unadhani Deo ana mapenzi ya kweli mama? Si ni aina ya wanaume ambao wanaweza kuyumbishwa ovyo?”
“Ni tamaa tu, halafu ukumbuke kwamba alikuwa na hofu ya kufukuzwa kazi.”

“Mama, sasa ni kwanini asiwe na hofu na mimi ambaye ndiye niliyemtafutia hiyo kazi, akawa na wasiwasi wa kupoteza tu hiyo kazi bila kumkumbuka aliyemfanya akaipata?”

“Umeongea jambo la msingi sana mama, lakini ujue kwamba, shetani naye ana mambo yake. Naweza kusema kwamba alipitiwa, lakini kiukweli mwanangu mpatie nafasi nyingine, utaona mabadiliko yake. Atakuwa amejifunza.”
“Sawa mama, nitajitahidi!”

“Siyo kujitahidi, naomba iwe hivyo!”
“Sawa mama.”
“Niahidi Levina!”
“I promise you mom!” (Nakuahidi mama)
“Thank you my daughter!” (Nashukuru binti yangu)

Kila mmoja alikuwa na lake kichwani mwake, mama Cleopatra alikuwa na nia ya dhati ya kumsaidia Levina ambaye alikuwa sawa na mwanaye kwa namna walivyokuwa marafiki wakubwa. Bado aliona thamani yake kama mwanaye.

Hakufikiria juu ya aibu ya watu wengi walioalikwa kwa ajili ya sherehe hiyo, kwake yeye sherehe hiyo isingekuwa na maana kama ingefungwa ndoa huku Levina akilalamika.

Levina alifurahishwa sana na maelezo ya mama yake Cleopatra, alimuona mzazi bora ambaye anaangalia usawa na kuonesha mapenzi yake kwa watoto wake wote. Bado alikuwa akifikiri vizuri suala la kurudiana na Deo.
Moyoni mwake Deo alikuwepo!
Amejaa tele!

***
Mawimbi yalikuwa yanapiga kwa kasi sana ufukweni mwa Bahari ya Hindi eneo la Coco. Watu walikuwa wengi sana Jumamosi hiyo walipunga upepo baharini. Ilikuwa jioni, mishale ya saa 11:30, jua likianza kung’ang’ania kupotea na giza kusita kuchukua anga!

Ni kama vitu hivi viwili vilikuwa vikishindana, mashindano hayo yalifanya ufukwe kuwa na rangi kama ya dhahabu, mwanga kuwa hafifu kiasi na kupendezesha mandhari ya Ufukwe wa Coco.

Pembeni kabisa, juu ya jiwe kubwa, walikuwa wamekaa Deo na Levina, mikononi mwao kila mmoja alikuwa ameshika box lenye maji ya matunda wakinya taratibu kwa mrija. Levina ndiye aliyemwalika Deo kwa mtoko huo akitaka kuzungumza naye na kumpa masharti yake aliyosema anataka kumpa.

Deo alikuwa kimya akisubiri kusikia masharti ya Levina ambaye alikuwa amependeza sana jioni hiyo. Tayari Deo alikuwa ameshapona kabisa, afya yake ikianza kunawiri na makunyanzi usoni yakianza kupotea.

“Kwanza kabisa, naomba unisamehe kwa kukukosesha kazi. Najua kama siyo mimi, ungekuwa unaendelea na kazi yako. Kwa hilo naomba sana unisamehe Deo!” Levina alianza kwa kutamka maneno hayo.

“Hapana Levina usiseme hivyo, mimi ndiye mkosaji. Halafu hiyo kazi haina maana yoyote kwangu kama wewe hutakuwa na amani na mimi. Hutakuwa na furaha na mimi. Haitakuwa na maana yoyote kabisa. Napenda kuona unafurahi!”

“Deo lazima utambue kwamba nakupenda sana, nilikupenda kwa moyo wangu wote na nimeshindwa kukutoa moyoni mwangu!”
“Najua!”

“Nitakupa masharti mawili, najua ni magumu sana, lakini ukiyaweza nitakusamehe milele.”
“Nipo tayari Levina niambie tu mama!”
“Labda nisisitize tena kwamba, nakupenda sana, siwezi kuacha kukupenda katika maisha yangu yote, sharti la kwanza ili nikusamehe Deo, unatakiwa ukubali kufunga ndoa na mimi!” Levina akasema akimwangalia Deo usoni.

“Kwa hilo nipo tayari, sijui kuhusu wazazi wako!”
“Mambo ya wazazi niachie mimi, kama umekubali basi vizuri, sharti la pili ni gumu kidogo, lakini nalo ukikubaliana nalo nitakusamehe!”
“Sema mpenzi, nipo tayari kwa chochote!”

“Deo naomba unisamehe kwa nitakalokuambia, najua litakuumiza na hutanielewa kirahisi, lakini ndiyo ukweli wenyewe. Naomba unielewe kwamba sikuwa na nia mbaya, nia yangu ilikuwa nzuri kabisa, lakini lazima unisamehe Deo!”
“Ni nini? Hebu niambie basi Levina...” akasema Deo akimkazia macho Levina.

“MIMI NDIYE NILIYEKODI WATU WAKUPIGE RISASI KWENYE LIFTI!” Levina akasema akilia.
“Unasemaje?” Deo akauliza kwa sauti ya ukali sana.
Mmmmmhhh mbona makubwa tena haya..kweli haya mapenzi yaache yabaki kama yalivyo...ni hatari sana kwa kweli
 
ni kweli lakini si kwa kuQuote jamvi lote mnakera sana
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji6] [emoji6] [emoji6] [emoji6] [emoji6] [emoji6]

Ngoja Shunie Aje Hapo kwa jinsi Nimjuavyo Lazima Atatia Neno Hapo
 
[emoji39] [emoji39] story tamuuuu sanaaaa mkuu ila ukiishia sema kuwa itaendelea lini ili tusiwe na arosto kama mateja wa jiji la bashite[emoji3]
 
Story mbaya. Haivutii. Haina msisimko.
Maneno mengi yamejazwa ili ionekane ndefu.

Mbaya zaidi episode YA kwanza ghorofa ya tatu imerudiwa mara mbili.
 
USIFE KWANZA MPENZI WANGU......EPISODE.38


“Deo naomba unisamehe kwa nitakalokuambia, najua litakuumiza na hutanielewa kirahisi, lakini ndiyo ukweli wenyewe. Naomba unielewe kwamba sikuwa na nia mbaya, nia yangu ilikuwa nzuri kabisa, lakini lazima unisamehe Deo!”

“Ni nini? Hebu niambie basi Levina...” akasema Deo akimkazia macho Levina.
“MIMI NDIYE NILIYEKODI WATU WAKUPIGE RISASI KWENYE LIFTI!” Levina akasema akilia.
“Unasemaje?” Deo akauliza kwa sauti ya ukali sana.
SASA ENDELEA...

HAIKUWA rahisi kwa Deo kuamini kwamba Levina ndiye aliyefanya jaribio la kutaka kumuua, moyo wake ulibadilisha mapigo na hasira yake kuwa kubwa. Aliyatoa macho yake akimwangalia Levina, akiwa haamini kabisa kwamba angeweza kufanya kitendo kile.

“Levina ulitaka kuniua?” Deo akauliza kwa hasira.
“Siyo hivyo mpenzi wangu!”
“Siyo hivyo vipi na umekiri kwamba ulituma watu wanipige risasi.
“Deo kabla sijakuambia lazima nikupe masharti ili nikusamehe. Ni kweli nilifanya kosa, lakini kosa lenyewe ni katika kulinda penzi langu!”
“Ulitaka kuniua au kunilinda?”

“Kwani uliuawa?”
“Hapana.”
“Kuna kitu uliibiwa?”
“Hapana!”

“Basi ndiyo unatakiwa kufahamu kwamba nilifanya hivyo kwa ajili ya kukupata. Deo sikuwa na njia nyingine, vinginevyo wewe ungefunga ndoa na Cleopatra. Sikiliza nikuambie Deo, mimi nakupenda sana, moyo wangu una mzigo mzito wa mapenzi ambayo siwezi kufananisha na kitu chochote.”
“Sijui kama ni rahisi kukuelewa!”

“Lakini unataka kuelewa?”
“Ndiyo!”
“Ngoja nikusimulie...” Levina akasema akikaa sawa sawa kwa ajili ya kumweleza kisa kizima kilivyokuwa.

***
Alikuwa amekaa mwenyewe kwenye meza ya peke yake, macho yake yakiangaza kila upande, ni kama alikuwa anawasubiri watu wafike katika baa ile. Ilikuwa ni usiku wa saa mbili na dakika zake, Levina ametulia kwenye kona akinywa soda yake taratibu kabisa.

Akiwa anaendelea kuangaza macho yake, simu yake ikaita. Haraka akapokea akiangalia kwenye mlango mkubwa wa kuingilia pale baa.
“Yes...” akatamka Levina akisubiri sauti ya upande wa pili.
“Ni wewe uliyekaa hapo kwenye kona peke yako?”
“Ndiyo!”

“Ok! Tunakuja, nimeshakuona!” Sauti nzito ya kiume ilisikika kwenye spika za simu ya Levina.
Dakika moja baadaye, wanaume watatu walikuwa wamekaa kwenye viti kuizunguka meza aliyokuwa amekaa yeye. Walisalimiana kisha wote wakakaa kimya.

“Karibuni sana, mimi ndiye Levina niliyemuagiza Asnath awatafute, nimefurahi kukutana nanyi!” Akasema Levina.
“Hata sisi pia.”
“Kama Asnath alivyowaambia, sina haja ya kumuua huyo jamaa, hakikisheni mnampiga risasi ya bega, nataka alazwe, mambo mengine nitamaliza mwenyewe!”

“Unataka hiyo kazi ikamilike baada ya muda gani?” Mmoja wao akauliza.
“Ndani ya wiki moja kutoka sasa, unajua amebakiza siku chache sana kabla ya kufunga ndoa, ni hiyo ndiyo ambayo sitaki ifungwe!”
“Sawa, chetu?”

“Ninazo...naona niwalipe nusu kwanza, kazi ikikamilika nitawamalizia. Chukua hii...” akasema Levina akimkabidhi bahasha iliyovimba!
“Ahsante sana, hatuna muda wa kusubiri zaidi, kila kitu umeshatuelekeza kwenye simu, namba yake ya simu tunayo, anapofanyia kazi tunapajua, kazi iliyobaki ni ndogo sana, ni kumfuatilia baasi!”

“Sawa, nawatakieni kazi njema yenye mafanikio!”
“Itakuwa hivyo, usijali!”
“Ok! Poa.”
Wale vijana wakasimama na kumuacha Levina akiwa amekaa kimya sehemu ile. Moyoni mwake alitamani sana zoezi lile likamilike, hakutaka kabisa Cleopatra afunge ndoa na Deo, mwanaume wa maisha yake.

“Tutaona sasa, mimi si katili, lakini wakati mwingine inabidi ili niweze kutetea penzi langu, naamini sasa nitafanikiwa,” akawaza Levina akisimama na kutoka katika baa hiyo.

***
Deo aligandisha macho yake usoni mwa Levina akiwa haamini kabisa anachosimuliwa, hakutegemea kama Levina angefanya tukio kubwa kiasi kile.
“Lakini levina hukuwa na njia nyingine zaidi ya hiyo?” Deo akamwuliza akiwa ameyatoa macho yake.

“Unadhani ningetumia njia gani hapo? Hata kama ni wewe ungetumia njia gani?”
“Kwanini usingenitafuta tukaongea?”
“Deo ulikuwa unatafutika wewe? Hata simu yangu ulikuwa unaiona kama kinyaa, sikuwa na njia nyingine Deo, naomba unisamehe lakini nitakusamehe kama na wewe utanisamehe na kutimiza ahadi zako zote!”

Deo akatulia kwa muda akatafakari, aliyaona makosa yake lakini pia aligundua kwamba Levina hakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya tukio alilolifanya ambalo liliweza kuwarudisha tena pamoja.

Alipata maumivu makali sana, aliteseka sana hospitalini, lakini mwisho wa siku aligundua wakulaumiwa ni yeye mwenyewe. “Nimekusamehe Levina!”
“Nimekusamehe pia Deo!”
“Sasa?” Deo akauliza akiwa anamwangalia Levina machoni.
“Nini tena mpenzi wangu?”

“Kuhusu ndoa, itawezekana kweli kuoana?”
“Nini kinachoshindikana chini ya jua?”
“Wazazi wako baby, hawanitaki kabisa hilo ndiyo tatizo.”
“Kuna kitu nilikuwa sijakuambia sweetie!”
“Kitu gani?”

“Nilishaongea na mama kila kitu...hakuna tatizo tena, mzee Massamu huwa haongei kwa mkewe Diana. Lazima kieleweke, kwa hiyo ondoa shaka mpenzi wangu. Tutapanda madhabahuni na kufunga ndoa yetu!”
“Kweli dear?” Deo akauliza akiwa ametoa macho.
“Niamini mimi mpenzi wangu!”

Deo na Levina wakasimama, kisha wakakumbatiana. Hawakuogopa macho ya watu. Walichojua wao ni kitu kimoja tu, kuwa wanapendana!
Kama Levina alivyosema, haikuwa kazi ngumu mama yake kumshawishi baba yake mzee Massamu kuhusu Deo kumuoa Levina hasa kwa kuwa tayari alikuwa na sifa walizokuwa wanazihitaji.

Deo akasafiri hadi nyumbani kwao Singida, akawaeleza wazazi wake juu ya kupata mchumba, hakuna aliyepingana naye. Taratibu zote zikafanyika, ndoa ya kifahari ikafungwa jijini Dar es Salaam.

Watu wengi sana walihudhuria, akiwemo Cleopatra ambaye tayari walishaweka mambo sawa. Mama yake Cleopatra ndiye aliyewakutanisha na kuwapatanisha. Jambo la kushangaza zaidi, Cleopatra ndiye alikuwa Mweka Hazina wa kamati ya sherehe ya Deo na Levina.

Ukawa mwisho wa machozi kwa Levina na mwanzo wa maisha ya furaha, akiwa na mwanaume aliyeota kuwa naye, mwanaume aliyemuhangaikia kwa muda; aliyekuwa tayari kufanya chochote kwa ajili yake.
Mwanaume wa maisha yake!

UNLIMITED SWAGGAZZ:.

Nawashukuru sana wasomaji wangu wapenzi kwa kufuatilia simulizi hii kuanzia mwanzo hadi mwisho, naamini haijakuacha kama ulivyokuwa, kuna kitu umejifunza.
Ila kama story itakuwa Imekukela wala Hukuifraiya

Samahan

*********MWISHO************
 
[emoji109] [emoji109] [emoji109] [emoji109] [emoji109] [emoji109] [emoji109] [emoji120]
 
Back
Top Bottom