Ambiele Kiviele
JF-Expert Member
- Dec 29, 2014
- 15,267
- 29,917
- Thread starter
- #141
usife kwanza mpenzi wangu....episode.36
Deo ameamua kutua mzigo mzito moyoni mwake, amemwambia Cleopatra kwa uwazi kabisa kwamba hawezi kumuoa tena kwa kuhofia kumuudhi Levina ambaye alimsaidia sana hadi kupata elimu na baadaye kazi, jambo hilo linaungwa mkono na mama yake Cleopatra. Deo anaondoka zake.
Akiwa ndiyo kwanza anaingia nyumbani kwake, Deo anapokea ujumbe mfupi kutoka kwa Levina ambaye anamshukuru kwa kusikia sauti yake. Kwa Deo inakuwa maajabu, maana hakumweleza chochote kuhusu uamuzi wake. Jambo hilo linamchanganya sana Deo.
SASA ENDELEA…
ALIRUDIA kusoma ule ujumbe mara mbili zaidi, lakini maneno yaliendelea kuwa yale yale, kutoka kwa mtu yule yule, yakiwa ndani ya simu yake yeye mwenyewe! Deo akapigwa na butwaa.
“Amejuaje haya?” Akajiuliza, lakini hakupata majibu.
Akajivuta hadi mlangoni, akafungua mlango na kuingia ndani, akaenda kujitupa kwenye sofa kubwa akihema kwa kasi. Hapo akaanza kumkumbuka kwa upya kabisa Levina. Kuna kitu kilianza kumwingia akilini mwake.
Hakuwaza tena juu ya meseji ile iliyoingia kwenye simu yake kimaajabu, alimuwaza Levina, mwanamke ambaye alimpenda kwa mapenzi yake yote, pasipo shinikizo kutoka kwa mtu yeyote. Pasipo matarajio ya kupata kitu chochote! Alimpenda yeye tu!
Mapenzi tu!
Penzi la dhati!
“Kuna kitu natakiwa kufanya,” akawaza akiangalia simu yake.
Wazo la kumpigia Levina likamwingia akilini mwake.
Ilikuwa lazima azungumze naye. Wakati huo hakuwaza tena kuhusu kazi, suala la kazi halikuwa na maana sana kwake. Kwa kutumia vyeti vyake alikuwa na uhakika mkubwa sana wa kupata kazi sehemu nyingine, kuliko kuendelea kukaa na mateso moyoni kwa kuishi na mwanamke ambaye mapenzi yake yalikuwa ya wasiwasi.
Akabonyeza namba za Levina na kumpigia, kiasi cha sekunde nane tu, Levina alikuwa hewani akizungumza na Deo…
“Haloo Levina!”
“Yes Deo, mambo vipi?”
“Poa, lakini sipo sawa sana!”
“Nini tatizo?”
“Kuna kitu nahisi kinaniumiza sana moyoni mwangu, Levina naomba unisamehe kwa yote yaliyotokea, tafadhali sana, nakuomba kwa moyo wangu wote. Mimi ni binadamu na nilipitiwa, siku zote kwenye maisha ni vyema kukosea ili kupata nafasi pia ya kujifunza.
“Waswahili wanasema, watu wanajifunza kutokana na kukosea. Nakuomba unisamahe ili niweze kuishi kwa amani moyoni mwangu!” Deo akasema kwa sauti ya chini sana akionekana kujutia sana yaliyotokea.
“Deo!” Levina akaita.
“Nakusikia mama…”
“Ni kweli unaomba msamaha kwa moyo wako wote?”
“Kweli kabisa, naweza kuapa kwa namna yoyote unayotaka!”
“Hakuna sababu ya kuapa, ni wewe mwenyewe na nafsi yako, kama ni kweli unajua umekosea ni vizuri na ni rahisi kusamehewa.”
“Kweli Levina najuta kukukosea, nimetambua kosa langu, nisamehe tafadhali!”
“Nilishakusamehe Deo, lakini ukweli ni kwamba sijakusamehe kikamilifu!”
“Unamaanisha nini?”
“Namaanisha kwamba nilishakusamehe tangu siku nyingi, lakini si kwa moyo wangu!”
“Sawa, naomba basi kuanzia leo uwe umenisamehe kwa moyo wako Levina!”
“Inawezekana Deo, lakini kuna masharti mawili!”
“Masharti?” Deo akauliza kwa mshangao mkubwa.
“Ndiyo kuna masharti mawili, kama ukiweza kuyatimiza, basi nitakusamehe moja kwa moja na nyongo iliyokuwa ndani ya moyo wangu itaondoka.”
“Ni masharti gani hayo? Niambie tafadhali!”
“Si kwa haraka kiasi hicho, lakini nitakuambia.”
“Lini?”
“Nipe muda, lazima nikutane na wewe, nahitaji kuzungumza na wewe, tena uso kwa uso.”
“Itakuwa lini?”
“Nitakujulisha, kwa sasa pumzika kwanza.”
“Sawa Levina, lakini nina ombi moja kwako!”
“Nakusikia!”
“Isiwe muda mrefu sana, siwezi kukaa na hili jambo muda mrefu, nahisi moyo wangu unaungua!”
“Usijali najua ni kiasi unateseka, najua pia ni kiasi gani unataka kuishi huru. Yote hayo nayajua na nitayachukulia kwa uzito mkubwa, muda ukifika nitambia!”
“Nimekuelewa vizuri, lakini nilikuwa na lingine!”
“Nini tena?”
“Nimepata meseji yako muda si mrefu!”
“Ndiyo!”
“Umejuaje hayo?”
“Siku zote kama kitu unakipenda, ni rahisi kujua kinavyoendea hata kama hutapewa taarifa. Nimejua kwa sababu nakupenda Deo!”
“Lakini haraka sana!”
“Ni kwa sababu nakupenda sana!”
“Haya bwana.”
“Siku njema Deo!”
“Kwako pia.”
Deo hakutoa simu haraka sikioni pamoja na kwamba alikuwa ameshaagana na Levina ambaye alishakata simu. Ni kama alikuwa amepigwa bumbuwazi au hajui kinachoendelea. Moyo uliendelea kuteswa na mapenzi, alimtaka sana Levina kwa wakati huu.
Aligundua kwamba penzi lake kwa Levina lilikuwa zito na lenye thamani zaidi ya Cleopatra ambaye alijilazimisha kutokana na mali zake.
“Nitampata Levina wangu, lazima arudi tena kwangu, lazima...” akawaza akisimama na kujivuta chumbani mwake.
***
Mama Cleopatra baada ya kutoka chumbani na kuwaacha Deo na Cleopatra aliifuata simu yake chumbani kwake na kumpigia Levina ili kutafuta ukweli.
“Hujambo mwanangu?”
“Sijambo mama shikamoo...” Levina akasalimia.
“Marhaba...haya mbona mwenzio anafanya mambo ya ajabu unashindwa kuniambia binti yangu?”
“Nani mama? Patra?”
“Ndiyo!”
“Amefanya nini tena?”
“Unamjua Deo?”
“Ndiyo!”
“Unamjuaje?”
“Mama Deo alikuwa mpenzi wangu, lakini Patra kwa sababu ya pesa zake ak....” Levina alishindwa kumalizia sentesi yake na kuanza kulia
Deo ameamua kutua mzigo mzito moyoni mwake, amemwambia Cleopatra kwa uwazi kabisa kwamba hawezi kumuoa tena kwa kuhofia kumuudhi Levina ambaye alimsaidia sana hadi kupata elimu na baadaye kazi, jambo hilo linaungwa mkono na mama yake Cleopatra. Deo anaondoka zake.
Akiwa ndiyo kwanza anaingia nyumbani kwake, Deo anapokea ujumbe mfupi kutoka kwa Levina ambaye anamshukuru kwa kusikia sauti yake. Kwa Deo inakuwa maajabu, maana hakumweleza chochote kuhusu uamuzi wake. Jambo hilo linamchanganya sana Deo.
SASA ENDELEA…
ALIRUDIA kusoma ule ujumbe mara mbili zaidi, lakini maneno yaliendelea kuwa yale yale, kutoka kwa mtu yule yule, yakiwa ndani ya simu yake yeye mwenyewe! Deo akapigwa na butwaa.
“Amejuaje haya?” Akajiuliza, lakini hakupata majibu.
Akajivuta hadi mlangoni, akafungua mlango na kuingia ndani, akaenda kujitupa kwenye sofa kubwa akihema kwa kasi. Hapo akaanza kumkumbuka kwa upya kabisa Levina. Kuna kitu kilianza kumwingia akilini mwake.
Hakuwaza tena juu ya meseji ile iliyoingia kwenye simu yake kimaajabu, alimuwaza Levina, mwanamke ambaye alimpenda kwa mapenzi yake yote, pasipo shinikizo kutoka kwa mtu yeyote. Pasipo matarajio ya kupata kitu chochote! Alimpenda yeye tu!
Mapenzi tu!
Penzi la dhati!
“Kuna kitu natakiwa kufanya,” akawaza akiangalia simu yake.
Wazo la kumpigia Levina likamwingia akilini mwake.
Ilikuwa lazima azungumze naye. Wakati huo hakuwaza tena kuhusu kazi, suala la kazi halikuwa na maana sana kwake. Kwa kutumia vyeti vyake alikuwa na uhakika mkubwa sana wa kupata kazi sehemu nyingine, kuliko kuendelea kukaa na mateso moyoni kwa kuishi na mwanamke ambaye mapenzi yake yalikuwa ya wasiwasi.
Akabonyeza namba za Levina na kumpigia, kiasi cha sekunde nane tu, Levina alikuwa hewani akizungumza na Deo…
“Haloo Levina!”
“Yes Deo, mambo vipi?”
“Poa, lakini sipo sawa sana!”
“Nini tatizo?”
“Kuna kitu nahisi kinaniumiza sana moyoni mwangu, Levina naomba unisamehe kwa yote yaliyotokea, tafadhali sana, nakuomba kwa moyo wangu wote. Mimi ni binadamu na nilipitiwa, siku zote kwenye maisha ni vyema kukosea ili kupata nafasi pia ya kujifunza.
“Waswahili wanasema, watu wanajifunza kutokana na kukosea. Nakuomba unisamahe ili niweze kuishi kwa amani moyoni mwangu!” Deo akasema kwa sauti ya chini sana akionekana kujutia sana yaliyotokea.
“Deo!” Levina akaita.
“Nakusikia mama…”
“Ni kweli unaomba msamaha kwa moyo wako wote?”
“Kweli kabisa, naweza kuapa kwa namna yoyote unayotaka!”
“Hakuna sababu ya kuapa, ni wewe mwenyewe na nafsi yako, kama ni kweli unajua umekosea ni vizuri na ni rahisi kusamehewa.”
“Kweli Levina najuta kukukosea, nimetambua kosa langu, nisamehe tafadhali!”
“Nilishakusamehe Deo, lakini ukweli ni kwamba sijakusamehe kikamilifu!”
“Unamaanisha nini?”
“Namaanisha kwamba nilishakusamehe tangu siku nyingi, lakini si kwa moyo wangu!”
“Sawa, naomba basi kuanzia leo uwe umenisamehe kwa moyo wako Levina!”
“Inawezekana Deo, lakini kuna masharti mawili!”
“Masharti?” Deo akauliza kwa mshangao mkubwa.
“Ndiyo kuna masharti mawili, kama ukiweza kuyatimiza, basi nitakusamehe moja kwa moja na nyongo iliyokuwa ndani ya moyo wangu itaondoka.”
“Ni masharti gani hayo? Niambie tafadhali!”
“Si kwa haraka kiasi hicho, lakini nitakuambia.”
“Lini?”
“Nipe muda, lazima nikutane na wewe, nahitaji kuzungumza na wewe, tena uso kwa uso.”
“Itakuwa lini?”
“Nitakujulisha, kwa sasa pumzika kwanza.”
“Sawa Levina, lakini nina ombi moja kwako!”
“Nakusikia!”
“Isiwe muda mrefu sana, siwezi kukaa na hili jambo muda mrefu, nahisi moyo wangu unaungua!”
“Usijali najua ni kiasi unateseka, najua pia ni kiasi gani unataka kuishi huru. Yote hayo nayajua na nitayachukulia kwa uzito mkubwa, muda ukifika nitambia!”
“Nimekuelewa vizuri, lakini nilikuwa na lingine!”
“Nini tena?”
“Nimepata meseji yako muda si mrefu!”
“Ndiyo!”
“Umejuaje hayo?”
“Siku zote kama kitu unakipenda, ni rahisi kujua kinavyoendea hata kama hutapewa taarifa. Nimejua kwa sababu nakupenda Deo!”
“Lakini haraka sana!”
“Ni kwa sababu nakupenda sana!”
“Haya bwana.”
“Siku njema Deo!”
“Kwako pia.”
Deo hakutoa simu haraka sikioni pamoja na kwamba alikuwa ameshaagana na Levina ambaye alishakata simu. Ni kama alikuwa amepigwa bumbuwazi au hajui kinachoendelea. Moyo uliendelea kuteswa na mapenzi, alimtaka sana Levina kwa wakati huu.
Aligundua kwamba penzi lake kwa Levina lilikuwa zito na lenye thamani zaidi ya Cleopatra ambaye alijilazimisha kutokana na mali zake.
“Nitampata Levina wangu, lazima arudi tena kwangu, lazima...” akawaza akisimama na kujivuta chumbani mwake.
***
Mama Cleopatra baada ya kutoka chumbani na kuwaacha Deo na Cleopatra aliifuata simu yake chumbani kwake na kumpigia Levina ili kutafuta ukweli.
“Hujambo mwanangu?”
“Sijambo mama shikamoo...” Levina akasalimia.
“Marhaba...haya mbona mwenzio anafanya mambo ya ajabu unashindwa kuniambia binti yangu?”
“Nani mama? Patra?”
“Ndiyo!”
“Amefanya nini tena?”
“Unamjua Deo?”
“Ndiyo!”
“Unamjuaje?”
“Mama Deo alikuwa mpenzi wangu, lakini Patra kwa sababu ya pesa zake ak....” Levina alishindwa kumalizia sentesi yake na kuanza kulia