story zangu za kawaida sana wala sidhani kama zinaboa, lakini pia nisiusemee moyo wa mtu may be zinamboa shida ni kwamba mdomo anao why haniambii? hajawahi sema na bikiona sisikilizwi au nakatishwa njiani nanyamaza baada ya muda utasikia mbona huongei, umeamua kuninunia sasa sielewi sijui ndo hii sitaki nataka au madeko tuu looh kama hapendeki...?
hapa mtoa mada umeonyesha jinsi ambavyo wanawake wako selfish..kwanini wewe uongee kila wakati? kwanini usikilizwe wewe tu kila wakati..mbona hutaki na yeye aongee mbona hutaki na yeye akupe story za kwake why should men always listen to women and not the other way around..sometimes sisi wanaume tunapenda ule ukimya kutafakari mambo mengi kichwani so kila mahali mkiwa mnaongea ni rahisi kupotezea...kwanza bora hata wa kwako anaongeza sauti ya redio..wengine wanaweza kua wanakuitikia we ukajua wanakusikiliza lakini mawazo yao yako mbali
sakapal, On Point, yaani on point kabisa.
Kuna watu kuongea utadhani analipia, achia mbali humlazimishi akusimulie yake hata kusikiliza yako tu taabu.
Mie nilishafanya maamuzi magumu, Ninaongea kila ninachojosikia, achambue yanayomhusu.
Ila tatizo langu huwa nataka nikiongea mtu anitazame usoni "eye contact'
Kama kuna tv iko on redio kuna wakati nazima ili tuongee.
Can you imagine ukaongelee wapi?? Au uanze kwenda nyumba ya tatu kupiga story wakati kwako kuna watu?? lol
oh my God,pole Sakapal,labda nami pia namkera mke wangu kwa tabia kama hiyo,labda hajaniambia tu,ngoja nirudi nikajichunguze kama nami namboa kama wewe unavyoborewa na mmeo nijirekebishe!asante kwa mada yako
Cha mhimu dada yangu jaribu kuona ni aina gani ya story anazopenda. Vilevile as a learned lady you should know WHEN to talk to your husband and HOW to talk to him. You know him better than any one on this forum. All the best in search for harmony and peace and lovely family. Be blessed
Ukisoma kwa nia ya kuelewa utaona huyu mke anamuongelesha mume kwa nia ya kuwa na mazungumzo ya pande mbili kati yao, lakini mume ndo haongei.
Sijui hili umelikosa vipi wakati ndo msingi wa thread nzima.
jamani sio kila wakati muda wa maongezi...mjue wanaume wana mengi kichwani muwapage mda wa kufikiria kidogo...story njia nzima? ndo mana couples zingine kila mtu anakua na gari lake angalau mkirudi nyumbani mnakua mmemissiana...
Sawa,
Lakini kama mtu huko katika mood ya maongezi si unasema?
Halafu huyu mke anakwambia akinyamaza baba anamkoromea kwa nini kawa kimya.
Damned if she does, damned if she doesn't. Hilo unalionaje sasa?
Morning every one!! I salute you all, SALUTE!!!
Ni hivi , leo nina swali kwa wanaume hasa waliooa au walio kwenye mahusiano na mwanamke kwa muda mrefu, tafadhali naomba mueleze ukweli ili kunisaida mimi na hata wadada wengine wenye shida kama hii.
Niko na mahabat wangu, tunatabia ya kuondoka wote home kwenda kazini na kurudi pamoja kwa kutumia kabajaji ketu si unajua bongo usafiriwa shida? Na hii imekuwa ikitupa nafasi ya kuongea mambo mengi njiani na tukifika home ni kuangalia watoto kuoga na kulala. Sasa shida iko hivi, mimi napenda sana kuongea na hili analijua utakuta ile nimeingia tu kwenye gari naanza story sometimes za kuchekesha, sometimes za ofisini yaliyojiri ofisini kwetu siku nzima, leo nani kafanyaje, nani kaambiwa nn na bosi, mkutano leo ulikuwaje, na sometime hata siri za ofisi au mikakati ya ofisi yetu namtaarifu nikijua ni maongezi tu looh. Sijui anakuwa anachoka kusikiliza au hapendi tena sauti yangu yaani utakuta unaongea in btw hata hujamaliza anaongeza sauti ya redio like ninyamaze. Unakaa kimya baada ya muda unaanzisha story ingine heee! unashangaa anakuuliza kitu kingine tofauti labda nilikuwa nasimulia kuhusu habari ya watoto utasikia tuu wale mafundi walimaliza jana uliwalipa hela yao yote looh! nachokaje?
Baada ya kuona shida inazidi na sipati nafasi nzuri ya kusikilizwa nikaona bora nikae kimya na tuwe wote mabubu njia nzima toka mjini hadi home yaani napata shida.
SWALI;- Hivi kwa nini wanaume hampendi kusikiliza masimulizi ya wake zenu? hii hata kijana mmoja hapa ofisini nilishamsikia akiongea kwamba kunarafiki yake ameoa mwaka jana ila ukifika muda wa kwenda kwake hatamani coz anawaza jinsi ya kusikiliza story za mke wake za siku nzima na mkewe huyo anataka mumewe amsikilize hadi amalize. To me huyu kijana anaboreka na hizi story na amechoka kuzisikiliza, sasa kwa nini nyie wanaume msiwaambie wazi wake zenu kwamba usipige story zako za kutwa nzima? au mwambie kwa upole tu pls nimechoka leo naomba tuongee asubuhi au hata ukamwambia nasikia kichwa kinauma reserve the rest for tomorrow huyu mwanamke atakuwa in good place ya kukuelewa that u need a space ila isiwe kila siku. A u hata ukamsikiliza tu then akimaliza yule mwanamke anafurah basi na wewe unaendelea na mambo yako. Naomba niwaibie siri nyie wanaume...,
Sikilizeni wake zenu, hii ni kitu ndogo na ya kijinga but ni kubwa na ya muhimu sana hasa kwa wanawake yaani kama mm hapa naugulia coz sisikilizwi story zangu naishia kujikuta naongea mwenyewe na mbaya zaidi kunawakati anakwambia njoo tuongelee kitandani wakati wa kulala akishapata tunda lake ukirudi kuoga unamkuta anakoroma sometimes unamkuta macho but unaanza story ukijastuka mwenzio alishalala saa nyingi, inaudhi kweli muwe mnatuambia kwamba usiongee baby ninausingizi sana.
Mie napenda sana kuimba hata sometimes unaskia kero kumuimbia coz ukiimba anaona kama unampigia kelele yaani wanaume naomba mnisaidie shida ni nini?
Hampendi story? je ni story za kipuuzi? mbona hamsemi? maudhiiiiiiiiii??
Ever remaining,
Sakapal
na nyie wanawake wengi mmezidi kulalamika mara ohh hatusikizwi mara wanaume this wanaume that...dont u knw maisha ya ndoa ni zaidi ya kusikiza stori zenu andf mostly kwetu wanaume huwa tunaziona "hazina tija na majiungu yasojenga"..am givin you a lil home work mukaifanye kwa nyakati zenu tofauti kila mmoja na mumewe na mutuletee mrejesho.
1- siku 1 jioni mnatoka kazini mcheck mmeo kama anaonyesha dalili za uchovu then mwambie hny lets stop by a nearby joint tukapige mdogomdogo plus story coz kuna deal la kuingiza kiasi flani cha pesa nadhani ushauri wako unahitajika sana, na mkifika agizeni kinywaji then mama anza kumpa hiloo deal la pesa na liwe kama la kifisadi hivi uone jinsi usikivu wa mzee utavyokuwa juu na cooperation ya kutosha to every detail of the deal.
2- another day mnatoka kazini fanya kama hapo juu(1) ila muambie tunaenda kuongelea jinsi shosti yako anavyozinguana na mmewe kiasi wanataka kupeana talaka, au kujadili jinsi mnavyoandaa sendoff ya rafiki yako mpo naye ofcn na wewe ni katibu wa kikao cha kina mama uone na upime usikivu wa mzee.
katika vikao vyote pima yafuatayo
1- attentiveness to your presentation of matters
2- contributions zake kwenye mada nzima
3- idadi yaq bia/soda atazokunywa katika kila kikao
4- muda mutakao tumia kukaa pamoja kujadiliana kwa kila kikao
5- idadi ya simu atazopiga katika kila kikao
6- conclussion yake kwa kila kikao na je kikao kipi kita-amsha au kuendeleza maongezi nyumbani hata usiku wa manane.
majibu utayopata ndio yatakupa picha sahihi ya aina ya story wanaume wanazopenda kusikia toka kwa wapenzi/wake zao.
irizi wari irizi..we r from jupiter you are from marzz.
ha ha ha........................ kama hansadi vile..umenukuu kila kituNa mjaribu saa ingine kuja na story za kuongeza kipato ili familia imee sio mastori ya harusin na maofisini mwenu tu kila siku bana yaaani uje na say mpango wa biashara na jinsi ya operationalization mimi ntakusikiliza kila siku hata wa manane ila ya Mke; Honey nikwambie kitu..........
Mume; Enheee........
Mke; Jana ofisini ile kikao yooote mpaka jioni ile tukatoka secretary na bosi tumewaacha ofisin ana inasemekana wana uhusiano wa kimapenzi
Mume; Bad Habit.........
Mke; Inauma sanaaa
At Home......
Mke; Mume wangu
Mume; Naam......
Mke; Hivi unajua this weekend ndo ile send-off
Mume;Owk....ntakupeleka then ukiwa tayari ntakufuata mke wangu.....
Mke; Sasa utakuta kwenye send-off watu huwa wanajikandika mipoda kama wachawi yaani mi sipendagi...........
Mume; Ngrrrrrrrrrrrrrrr.........................ngrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr kalala zamaaaaani as mistory yako inaboa saaaaanaaaaaaa na ni non-constructive
Tafakari................chukua hatua
Afu kuongea ni kipaji mjue..Kuna wengine wanaongea huku kipaji hawana ni sababu ya stress.
Mwanamme anayejua maongezi anamjibu vizuri mkewe na kuyaongoza hayo maongezi kuelekea kule anakofikiri kunafaa zaidi.
Sasa wewe unaona mkeo anaendekeza gossip, badala ya kuonyesha hufagilii na kuongea habari hizo hizo kwa kina zaidi, unamuacha mamaa anakuwa kama anafanya jitihada za kuwa social wakati wewe ume mute.
Unakosa mvuto.
Unaweza kupinduliwa kwa kitu kidogo tu, katokea kijana mtanashati hana lolote zaidi ya maongezi mazuri, anakufanya mbaya.
Halafu utalalamika wanawake wa siku hizi wasaliti.
Kumbe usaliti umeanza mwenyewe kwa emotional neglect iliyo borderline torture.
Mara nyingine mtu anaweza kuanza kuongelea weather sio kwa maana ya kwamba anataka kuongelea weather, anataka ku crack the ice tu kwa nyepesi nyepesi, sasa kama mwanamme kichwa you take that and run, you build up the convo.
Sasa wewe mtu kaanza na weather tu unasema huyu naye kashaanza story zake za ajabu ajabu.
Utaonyesha humpendi, anakuboa. Mtu kama unampenda kweli hata akikoroma utaona kama muziki.
Na akileta story nyepesi nyepesi unazipeleka kunako, si kumchunia.
nyumba kubwa well said..
Kweli bwana kuna watu kuongea wamejaaliwa yaani wanajua namna ya kupangilia maneno mpaka basi..
Ninaye shemeji yangu kwa kweli ukifika kwake unabaki kucheka tu..she is truly a charming lady..
Bahati mbaya mume wake hapendi vile anavoongea..so, unakuta akianza stori zake broo anaanza kumtuma ili mradi amkate flow ya maongezi..Kingine nilichogundua kupitia huu uzi..wanaume wengi hawapendi kustorishwa na wake zao..
Na wanapenda ile ya one way traffic conversation..yaan mke awage wa kuulizwa na kuitikia tu..lol!!
Hapo ndo mnaambiwa msifakamie, mmeona kijungu kumbe kina dhahma si kijungujiko.
Inabidi kujua haya mambo kabla hujakuwa na mtu.
Pia, mwanamme wa kweli haogopi challenge ya kumuelekeza mwanamke wake.
Na kujidanganya kwamba mtaongea 'story za msingi' muda woye haiyumkiniki.
Anaweza kuleta story ya gossip kama baba kichwa unaipindua gossip ileile inatoa funzo lenye nugget of wisdom kwake, anaweza kutoa story iliyojaa dharau na kijicho baba akaona nafasi ya kueleza umuhimu wa kuheshimu watu na kuondoa husda, anaweza kumcheka kilema akafunzwa kwa methali 'hujafa hujaumbika'.
Sasa ushaona mke wako ana mapungufu, unataka nani ayarekebishe?
Na kumnyamazisha hakutamuelimisha, mwanamme hafukii tatizo kwa muda, analitatua.
Kumnyamazisha kunatengeneza time bomb litakalolipuka siku moja.
...Ni kawaida ya wanaume waongeaji kutokupenda wanawake waongeaji....kwa kuwa wanataka audience, sasa mkiongea wote nani amsikilize nani?..Mimi mwenyewe maishani mwangu sijawahi ku date mwanaume mwenye maneno ka chiriku. Maana najua tutakuwa tunapiga kelele si kuongea...na wala nisingeweza kudumu na mtu anaye ni shut nikiongea.
leo ukiingia tu kwenye bajaji weka headphones masikioni then weka sauti kubwa imba na kufuatia wimbo unaousikiliza ,then mlie chabo anajisikiaje then unipe majibu yangu
pole dada. ninachokiona hapa midundo yenu haiendani, kila mmoja wenu anadunda kivyake. pole sana!Morning every one!! I salute you all, SALUTE!!!
Ni hivi , leo nina swali kwa wanaume hasa waliooa au walio kwenye mahusiano na mwanamke kwa muda mrefu, tafadhali naomba mueleze ukweli ili kunisaida mimi na hata wadada wengine wenye shida kama hii.
Niko na mahabat wangu, tunatabia ya kuondoka wote home kwenda kazini na kurudi pamoja kwa kutumia kabajaji ketu si unajua bongo usafiriwa shida? Na hii imekuwa ikitupa nafasi ya kuongea mambo mengi njiani na tukifika home ni kuangalia watoto kuoga na kulala. Sasa shida iko hivi, mimi napenda sana kuongea na hili analijua utakuta ile nimeingia tu kwenye gari naanza story sometimes za kuchekesha, sometimes za ofisini yaliyojiri ofisini kwetu siku nzima, leo nani kafanyaje, nani kaambiwa nn na bosi, mkutano leo ulikuwaje, na sometime hata siri za ofisi au mikakati ya ofisi yetu namtaarifu nikijua ni maongezi tu looh. Sijui anakuwa anachoka kusikiliza au hapendi tena sauti yangu yaani utakuta unaongea in btw hata hujamaliza anaongeza sauti ya redio like ninyamaze. Unakaa kimya baada ya muda unaanzisha story ingine heee! unashangaa anakuuliza kitu kingine tofauti labda nilikuwa nasimulia kuhusu habari ya watoto utasikia tuu wale mafundi walimaliza jana uliwalipa hela yao yote looh! nachokaje?
Baada ya kuona shida inazidi na sipati nafasi nzuri ya kusikilizwa nikaona bora nikae kimya na tuwe wote mabubu njia nzima toka mjini hadi home yaani napata shida.
SWALI;- Hivi kwa nini wanaume hampendi kusikiliza masimulizi ya wake zenu? hii hata kijana mmoja hapa ofisini nilishamsikia akiongea kwamba kunarafiki yake ameoa mwaka jana ila ukifika muda wa kwenda kwake hatamani coz anawaza jinsi ya kusikiliza story za mke wake za siku nzima na mkewe huyo anataka mumewe amsikilize hadi amalize. To me huyu kijana anaboreka na hizi story na amechoka kuzisikiliza, sasa kwa nini nyie wanaume msiwaambie wazi wake zenu kwamba usipige story zako za kutwa nzima? au mwambie kwa upole tu pls nimechoka leo naomba tuongee asubuhi au hata ukamwambia nasikia kichwa kinauma reserve the rest for tomorrow huyu mwanamke atakuwa in good place ya kukuelewa that u need a space ila isiwe kila siku. A u hata ukamsikiliza tu then akimaliza yule mwanamke anafurah basi na wewe unaendelea na mambo yako. Naomba niwaibie siri nyie wanaume...,
Sikilizeni wake zenu, hii ni kitu ndogo na ya kijinga but ni kubwa na ya muhimu sana hasa kwa wanawake yaani kama mm hapa naugulia coz sisikilizwi story zangu naishia kujikuta naongea mwenyewe na mbaya zaidi kunawakati anakwambia njoo tuongelee kitandani wakati wa kulala akishapata tunda lake ukirudi kuoga unamkuta anakoroma sometimes unamkuta macho but unaanza story ukijastuka mwenzio alishalala saa nyingi, inaudhi kweli muwe mnatuambia kwamba usiongee baby ninausingizi sana.
Mie napenda sana kuimba hata sometimes unaskia kero kumuimbia coz ukiimba anaona kama unampigia kelele yaani wanaume naomba mnisaidie shida ni nini?
Hampendi story? je ni story za kipuuzi? mbona hamsemi? maudhiiiiiiiiii??
Ever remaining,
Sakapal