SUA badilikeni, achaneni na Panya imetosha

SUA badilikeni, achaneni na Panya imetosha

CHUO KIBOVU,MIUNDOMBINU MIBOVU,WAALIMU WABOVU,KOZI MBOVU,TAFITI MBOVU.
 
Kwa taarifa yako:
1. Sua wanafanya tafiti nyingi sana, hiyo ya panya ni ndogo tu.

2. Hujui sua wametengeneza chanjo za magonjwa mengi ya wanyama ikiwemo kuku? Wiraza zenu izinaendelea kuabudu chanjo kutoka nje. Sio kosa la sua

3. Vipi vipaumbele vya taifa kuhusu maendeleo? Je wametenga bajeti kiasi gani na sua wakashindwa kuomba na kutekeleza? Umeelewa?

4. Training kubwa ya MSC na PhD sehemu kubwa tumeachia wafadhili, wakija na ajenda za panya wasiombe fund?

Yako mengi nadhani mleta mada anaufinyu mkubwa wa uelewa kuhusu hali za vyuo vyetu. Afanye tafiti kabla ya kukurupuka kuandika

Naishia hapo
Hizo kila nchi inavumbua, chanjo za kuku sio ishu tena kwa Dunia ya sasa,
 
Hizo kila nchi inavumbua, chanjo za kuku sio ishu tena kwa Dunia ya sasa,
Kwa mfugaji yoyote. Au aliyejaribu kufuga na kuishia kuokota vibudu vya mizoga lazima ataishangaa hii comment.
Chanjo 3, za magonjwa hataree katika ufugaji kuku, huchomi sindano unawawekea matone kwenye macho.
Kwangu mkulima na mfugaji ni kitu kikubwa mno, halafu siisubiri ije na ndege tokea uholanzi.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Naunga mkono hoja yako kwa asilimia 100, ulichokiongea kina mantiki kubwa sana sisi hapa vitu tunavyoona ni ugunduzi vilifanywa ni zaidi ya miaka 60 iliyopita sisi hapa ndio tunaona ni ugunduzi baadala ya kuendana na kasi ya sayansi na teknolojia ya wenzetu duniani, tafiti zetu nyingine zinazofanyika haziendani na hali halisi ya sasa na hazina mashiko,
 
mimi nijuavyo kwa zama zetu kufanya tafiti za panya tena kwa kiwango kile ni uelewa mdogo wa mambo au kutaka kutafuta funds tu kujipa miradi,tuache uongo chuo kikuu kufanya utafiti wa aina ile kwenye wanyama ni kukwepa majukumu yake;
Muwe mnatafuta habari! Kwani umesikia wanafanya tafiti za panya peke yake?! Halafu nyie watu mnashindwa hata kutumia common sense... SUA ni multi-displinary university! Pale kuna wataalamu wa mimea, misitu, wanyama. n.k!

Sasa unamtarajia mtu aliysema Veterinary Medicine kwa mfano afanye utafiti wa mbegu bora ya mahindi?! Unamtarajia mtu aliyesomea Forestry aje kufanya utafiti kuhusu wadudu wanashambulia mtama?!

Sasa kama kuna watu waliosomea jambo linaloendana na utafiti wa panya, shida ipo wapi wakitumia elimu yao kufanya hilo jambo?!

Au kwa akili yenu mnadhani watu wa BVM or Animal Science kwa mfano, wakiwa wanafanya tafiti kuhusu panya basi watu wa Crop Science hawafanyi utafiti zinazoendana na taaluma yao?

kuna mtu amesema waliwahi kumfunza panya kutambua makohozi yenye kifua kikuu,sasa application yake iko wapi?,kumbuka hapo SUA kuna hospitali mbili moja main campus moja kule kijijini (mazimbu) ,kwahiyo ningetegemea kuona maabara ya kupima kifua kikuu ikiwa SUA maana tayari tuna panya ila kila kitu ni kulaumu serikali;
Kwa mujibu wa taasisi ya Apopo ambao wanafanya kazi na SUA wanasema kwamba:-
Impact - TB Detection
A HeroRAT can check 100 sputum samples for tuberculosis just 20 minutes, a job that would take a lab technician using conventional microscopy up to 4 days
Sasa angalia hiyo tofauti kisha linganisha na hayo mavifaa mnayoyasifia! Je, wanatumika hao panya? Again, Apopo hawa hapa:-
Rat.png


Pia soma kipande hiki cha habari kutoka Gazeti la Mwananchi:-
Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Abel Makubi akiwa amembeba panyabuku aitwae Justin ambaye alitumia dakika tano kubaini sampuli 6 za vimelea vya kifua kikuu kutoka katika makohozi 60. Profesa Makubi ametembelea mradi wa Apopo unaofundisha panya hao kubaini vimelea vya Kifua kikuu katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) kilichopo Morogoro.
Just imagine, within 5 minutes, panya wameweza kupima 60 samples from which 6 samples zikagundulika kuwa na ugonjwa, na nyie bado mnakejeli?!

Mwananchi wanaendelea:-
Profesa Makubi amesema Panya hao wana uwezo mkubwa wa kugundua vimelea vya Kifua Kikuu hata kwa mtu ambaye alifanya vipimo Hospitalini kama vile vya hadubuni (microscope) na mashine za kupima vinasaba mfano GeneXpert na vipimo vingine na vikatoa majibu kuwa hana TB, lakini panya hao wana uwezo wa kubaini vimelea ambavyo mashine za hospitalini zinaweza zisibaini.
Kisha gazeti linamnukuhu Professor Makubi kwamba:-
Panya mmoja ana uwezo wa kugundua kama sampuli ina vimelea vya kifua kikuu kwa muda wa sekunde moja, na hupima sampuli za makohozi 100 kwa dakika 20 hivyo teknolojia hii inaweza kutumika hata kwenye upimaji wa sampuli nyingi kutoka kwenye kundi kubwa la watu (mass Screening) kwa muda mfupi.”
Are you guys serious?!

Thadei Ole Mushi anaponda lengo la sasa la kutaka kutumia hao panya kupima COVID-19, na hapo Professor Makubi anasema teknolojia hii inaweza kutumika kwenye mass screening!

Hivi mlishapata kujiuliza hilo la COVID-19 likifanikiwa litakuwa na impact kiasi gani kutokana na huo uwezo wa kufanya mass screening?
 
Sikutarajia hao mabeberu wangeipa credit sua, in fact hiyo project ime fadhiliwa na hao mabeberu.

Hivi serikali yetu sijui ina kwama wapi?? Kwann wasiwe wanatenga fungu kwa ajili ya tafiti?
Upo sahihi kwa 1000%... wakati serikali imelala, credit zinaenda kwa Apopo ambao nao wanatumia hiyo research kuombea pesa ughaibuni!

Na hiyo ya corona kama itafanikiwa, jamaa itawapa mileage kubwa sana kwa sababu hata huko kwenye TB, hawa panya wameonekana wapo efficient na wana uwezo wa kufanya mass screening kuliko vifaa ya wazungu!!
 
Naunga mkono hoja yako kwa asilimia 100, ulichokiongea kina mantiki kubwa sana sisi hapa vitu tunavyoona ni ugunduzi vilifanywa ni zaidi ya miaka 60 iliyopita sisi hapa ndio tunaona ni ugunduzi baadala ya kuendana na kasi ya sayansi na teknolojia ya wenzetu duniani, tafiti zetu nyingine zinazofanyika haziendani na hali halisi ya sasa na hazina mashiko,
Umefanya utafiti kuangalia impact ya hao panya, au unaunga mkono tu?!
 
[emoji38][emoji38],wasalimie Ma-Profesa Mahoo na Msanya. Pia Dr. Raymond Salanga.

Bado nipo hapa baa ya Kambarage nazimenya Balimi kwa kwenda mbele.

Karibu tusongeshe maisha,au Mugroo wamefyonza fedha zako?

Upo Main Campus au Solomon Mahlanga/Mazimbu?

Hivi Chini ya Mti bado ipo au ilishapoteaga?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Khaaa!!! Unadhani nina interests na hayo yanayoendelea?! Sipo SUA mzee, hapa ninajaribu kuweka rekodi sawa kama ambavyo nimekuwa nikifanya kwa mambo mbalimbali!!!
 
Tunakwama wapi? Leo Tarehe 15/5/2021 asubuhi hii China imefanikiwa kurusha kifaa kwenda Sayari ya Mars na kimetua vizuri na kitakaa huko Miezi 3 kutafiti kama Kuna uwezekano wa maisha kwenye Sayari hiyo. Huko Sua Profesa anaamka na Box la Panya anaenda kuwachungulia na anatokea hadharani anasema amevumbua kitu
WEWE NI MSHENZI MZOEFU
 
Umefanya utafiti kuangalia impact ya hao panya, au unaunga mkono tu?!
Jamaa umetokwa povu sio la nchi hii au ndio unawalisha hao panya hapo SUA unaona kama tunakusagia kunguni.. 😂😂😂😂... tuambie wewe unaowalisha hiyo impact maana tunapokwenda kutest COVID 19 hatuwaoni hao panya wako tunatumia testing kits kutoka abroad
 
Jamaa umetokwa povu sio la nchi hii au ndio unawalisha hao panya hapo SUA unaona kama tunakusagia kunguni.. 😂😂😂😂... tuambie wewe unaowalisha hiyo impact maana tunapokwenda kutest COVID 19 hatuwaoni hao panya wako tunatumia testing kits kutoka abroad
TOO LOW to argue with.
 
Kama sniffing dogs wanatumika kwanini iwe ajabu panya kutumika?
Tunaona ni ajabu kwa sababu hata kama tafiti itaonyesha kweli panya hao wanaweza kugundua kitu fulani hawana Msaada mwishoni. Kwa mfano walisema wanao panya wanaogundua makohozi yenye vimelea vya TB, ok niambie Sasa ni hospitali gan Tanzania hii wanatumia hao panya kwenye maabara zao kupima TB? Fanyia tafiti Jambo ambalo litakuwa applicable iwapo utafiti huo utakamilika ili kuwa Msaada kwa Watanzania lkn sio utafiti ambao ukifanikiwa unakuwa hauna faida kwa taifa. Ndio mtoa mada anasema tuachane na tafiti za Aina hiyo na wawekeze nguvu kwenye tafiti nyigine ambazo najua zipo wanazifanya na zinafaida km ilivyo chanjo ya mifugo
 
Kwa kweli hata mimi wamenichosha,wanaacha kutafiti mbegu bora za Mazao ya kilimo na ufugaji,na teknolojia rahisi wanakomaa na vitu vya kijinga miaka na miaka
 
Back
Top Bottom