SUA badilikeni, achaneni na Panya imetosha

SUA badilikeni, achaneni na Panya imetosha

Kwani ni lazima SUA wafanye kila kitu? SUA wao wapo na panya, hivyo vingine fanya wewe...

Ani
Katika vyuo vinavyojitahidi kubuni na kuvumbua, SUA inajitahidi sana.
Mleta mada angepeleleza kwanza kabla ya kuja na hizi shutuma.

Sua wameweza hata kubuni mashine (kama tractor ndogo) ya kurahisisha shughuli za mkulima.
 
Ni kweli kabisa, lakini je watakuelewa, maana binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
nakukumbusha kwa sasa lile jina "chuo cha kilimo " ni jina tu ila yaliyo ndani sio kilimo,na kuthibitisha hili tafuta mtu yuko SUA muulize kwanini kuna ualimu,na baadhi ya kozi zisizoeleweka pale kama shahada ya utalii ndio utajua uhalisia nadhani wanataka kuongeza na shahada ya rasilimali watu ambayo wanajua kabisa kuna vyuo vingi vinatoa hadi sasa na ajira hazipo;
hivyo kama mnavyomkosoa mleta mada kuwa hajui alichosema,naona baadhi yenu mmeanza kuchangia msivyovijua pia;
katika uhalisia SUA ni kati ya vyuo ambavyo vina kozi nyingi zisizo na ajira nchi hii,na hakijafanya hata lile lengo lake la kuzalisha wataalamu wa kilimo nchi hii;
Bwana mkubwa ungelikuwa unajua sababu ya hizo kozi kuongezwa usingeandika ulichoandika,nakupa pole kwasababu Jambo usilolijua ni km usiku wa Giza,kwa upeo wako unaona kuwa anayeongeza kozi hizo ni SUA kumbe kiuhalisia sio hivyo,ngoma imeanzia juu kwa Wanasiasa wanaotoa amri kuwa hebu ongezeni kozi ili kuwa na wanafunzi wengi,Nchi hii wanaoiharibu ni Wanasiasa wataalamu wanabebeshwa msalaba usio wa kwao.
 
Ni mwaka jana tu wametengeneza chanjo ya kuku inayokinga magonjwa matatu kwa mpigo. Ni ukombozi mkubwa kwa wafugaji wadogo.
Naam,SUA iko vizuri,sema nchi yetu haisapoti ipasavyo Tafiti za Kisayansi.
 
Mtoa hoja ana hoja. Course ya Education SUA ya nini? Kijishughulishe na lengo la kuanzishwa kwake. Usipindishe hoja nyie Ma-Profesa wetu wa nadharia wakati masuala ya nchi Mhe.Msukuma, Lusinde na wengineo wanapambana nayo.TAFAKARI HOJA KWANZA ACHA NA HAO PANYA WENU[emoji38][emoji38]
Karibu SUA ujifunze.Usisubiri maneno ya kuambiwa.
 
Hizo tafiti zenu zimeinua wakulima? Mnashindwa na wakenya, mbegu na kemikali zimejaa mdukani kutoka kenya, hamuoni aibu?
Kubalini kukosolewa, ili mbadirike nyie ni kujitetea tu.
Kweli Mkuu ukienda mdukani madawa na mbegu nyingi sio kutoka nje ya nchi.

Elimu ya TZ ni utopolo sana basi tu.

Elimu ya Tz ni elimu ya uchuuzi na sio elimu ya kutengeza bidhaa
 
Na Thadei Ole Mushi.

SUA wamekuja na panya wa Kupima Corona... Mimi nshaanza kuchoka na hawa panya wa SUA.

Sayansi hii ya kufundisha wanyama kunusa (Sniffing) kwa wenzetu ilianza muda mrefu sana. Ni mojawapo ya Technolojia ya kizamani kabisa. Huko Cuba Panya wameanza kutumika toka 1954 kunusa maeneo yenye madini, mobomu nk. Kwa sasa haitumiki Sana kwa kuwa njia za kisasa zaidi zimeendelea kugundilika kila kukicha.
Nakuunga mkono, labda ibaki kama maonyesho lakini si kuhesabu kuwa ni mafanikio.
SUA hawataona huu ni ushauri,ni kweli kwa dunia ya leo kufanya utafiti wa panya sijui atambue nini,ni uzembe wa kiwango cha lami;
ningesikia wana-design sensors kwa ajili ya utambuzi wa magonjwa mbalimbali sawa,ila panya hapana;
Nimefanya research kidogo nikajikuta naumia zaidi kwa mambo mawili...

1. Jinsi tunavyodharau huu utafiti, na
2. Jinsi huko duniani utafiti huu ulivyokuwa ume-make headlines mwaka jana lakini bila kutajwa chuo husika!!!

(i) The New York Times- Rat That Sniffs Out Land Mines Receives Award for Bravery.

Wakati Thadei na wenzake mnaona hao ni panya wanaotakiwa kuwekwa makumbusho kwa sababu ni useless na huko ughaibuni wametumika sana na hivi sasa hawana maana yoyote, The New York Times wanasem:-
Not since the fictional Remy of the 2007 Disney-Pixar film “Ratatouille” has a rat done so much to challenge the public’s view of the animals as creatures more commonly seen scuttling through sewers and the subway: Magawa has discovered 39 land mines and 28 pieces of unexploded ordnance, and helped clear more than 1.5 million square feet of land over the past four years.
Kwenye habari hiyo ya NYT, hata Tanzania haikutajwa, na labda unaweza kudhani anazungumziwa panya mwingine kabisa!!!

(ii) USToday:- Meet Magawa, the 'hero rat' awarded a bravery medal for detecting dozens of landmines.
US Today na wenyewe wameshindwa kuitaja hata Tanzania let alone SUA lakini wanafungua habari yao kwa kusema:-
A rat is being honored with one of the highest awards in the animal world after he has potentially saved numerous lives for clearing landmines from fields in Cambodia.
(iii) The Guardian ( UK):- Magawa the landmine detection rat given gold medal for bravery.
Kama kwa hizo media, The Guardian nao hawaitaji SUA wala Tanzania lakini wanaukubali uwezo wa huyo panya ambao unazidi ule wa binadamu kwenye kutegua mabomu ambapo wanasema:-
Magawa, who is now nearing retirement age, can search the area of a tennis court in 30 minutes, something that would take a human with a metal detector up to four days.

(iv) NBC News:- Rat called Magawa awarded prestigious gold medal for Cambodia landmine. detection

Kama hao wengine, NBC News inaonekana hawana ufahamu wowote kuhusu TZ na SUA kwenye uwepo wa hao panya, na matokeo yake wanaishia tu kusema:-
Wet-nosed Magawa was formally presented with his miniature medal in a virtual ceremony from London on Friday, becoming the first rat in the PDSA's 77-year history to receive the honor. Former winners include police dogs, horses, pigeons and a cat.

(v) (i) BBC - Magawa the mine-detecting rat wins PDSA Gold Medal.

Bora hata BBC ambao angalau waliitaja Tanzania ingawaje sio kwa kuipa credit kwamba:-
The seven-year-old rodent was trained by the Belgium-registered charity Apopo, which is based in Tanzania and has been raising the animals - known as HeroRATs - to detect landmines and tuberculosis since the 1990s. The animals are certified after a year of training.

Hiyo ni sehemu ndogo sana ya headlines za Panya ambao Wabongo tunataka wawekwe makumbusho kwa sababu ni "useless"!!

Sasa ikiwa sisi wenyewe tu tuna fikra kama hizi, hivi kuna mtu anaweza kuzishangaa hizo media za nchi za magharibi kutosema chochote kuhusu Tanzania, na hususani SUA ambao ni partner wakubwa wa huo mradi?

Media zote zinatoa credit kwa taasisi ya Kibelgiji inayoitwa Apopo yenye ofisi zake hapo SUA!! Ajabu, hata ukiingia kwenye website ya Apopo, huwezi kuuona ushiriki wa SUA kwa haraka! Binafsi, ilinibidi nitumie keyword tofauti ndipo nikakutana na sehemu ya hii habari:-
APOPO’s innovation in landmine and tuberculosis detection using African giant pouched rats is recognized worldwide as a successful and ground-breaking collaboration with Sokoine University of Agriculture (SUA) in Morogoro.

Ukweli ni kwamba, serikali zetu pays little attention kwenye kazi zinazofanywa na wazawa, no wonder watu kama Ngunichile wanahoji:-
Kama zipo tafiti nyingine mbona hazisikikii ?? Mimi uwa nasikia panya, panya tu
Lakini ukiacha kutumia source za SUA wenyewe ambao nilichelea wasije wakawa wanajimegea, nikalazimia kutafuta credible external source ambayo inasema:-
Sokoine University of Agriculture is a leader and collaborative partner in major international agricultural research and development programs. SUA has a large team or poultry specialists.

Each year, the SUA Faculty of Veterinary Medicine and agricultural departments manage and coordinate numerous animal health and agricultural programs and projects funded by USAID, USAID CRSPs, USAID Feed the Future projects, DFID, Welcome Trust, and numerous other international development funders.
Hayo ni maelezo kutoka tovuti ya University of California, Davis, na ukiingia website ya SUA wenyewe, hapa utakuta mlolongo wa research projects!
 
Mkuu Thadei!

Katika ulimwengu wa Sayansi ni kawaida kwa vyuo fulani kujikita kwenye utafiti wa vitu au kitu fulani. Kwa hili la SUA kupambana na tafiti za panya kila siku nawapa heko.

Hata mimi sipendi tafiti za panya, lakini nadhani zimewapa sifa kubwa duniani. Nadhani jambo muhimu ni kuzifanya hizo tafiti zinapotoa matokeo mazuri basi tuweze zitumia katika maisha yetu ya kawaida na hasa Tanzania.
Sasa shida hizo tafiti hazina tija leo unaulizwa hao panya wanatumika wapi kusaidia wananchi je utakuwa na jibu
 
Mtoa hoja ana hoja. Course ya Education SUA ya nini? Kijishughulishe na lengo la kuanzishwa kwake. Usipindishe hoja nyie Ma-Profesa wetu wa nadharia wakati masuala ya nchi Mhe.Msukuma, Lusinde na wengineo wanapambana nayo.TAFAKARI HOJA KWANZA ACHA NA HAO PANYA WENU[emoji38][emoji38]
Usisahau Tanzania kuna uhaba mkubwa sana, tena sana wa Walimu wa Sayansi!!! Nakumbuka, enzi za JK walitumia njia mbalimbali kutaka kumaliza hilo tatizo, na njia hizo kwa mfuatano zilikuwa:-

1. Kuwapa mikataba wapya wastaafu waliokuwa wanafundisha masomo ya sayansi... waliopatikana hawakufika 100!

2. Wakawaita Form VI leavers waliokuwa wamemaliza masomo ya sayansi, na wapo tu mtaani! Serikali ikawaahidi kuwapa mkopo 100% and guaranteed employment ili kusomea Special Advanced Diploma (Science & Maths) pale DUCE!... Hawakutosha!

3. Offer kama #2 hapo juu ikaja kwa madogo wanaomaliza Form IV na kufaulu masomo ya sayansi ili wakasome 3 years Special Diploma ( Science & Maths) na kuahidiwa ajira moja kwa moja... hawa ndo wale ambao Magu aliwaita vilaza, na akaifuta hiyo special diploma!!

Sasa katika harakati hizo hizo za kupunguza uhaba wa walimu wa sayansi, ndipo SUA napo zikaanzishwa various BSc Educations courses za sayansi kama vile BS Ed ( Chemistry & Physics), Physics & Maths, Chemistry & Biology, Chemistry & Maths, etc!!

Sasa hivi kweli unaweza kuponda hilo suala?!
 
Sasa shida hizo tafiti hazina tija leo unaulizwa hao panya wanatumika wapi kusaidia wananchi je utakuwa na jibu
Kwenye tija hapo ndio shida. Lakini nadhani hii miradi haikuanzishwa na Watanzania, ililetwa na wafadhili ambao yamkini kwao ina tija. Serikali sasa idumishe ufadhili wa tafiti zenye tija kwa watanzania.
 
Nimefanya research kidogo nikajikuta naumia zaidi kwa mambo mawili...

1. Jinsi tunavyodharau huu utafiti, na
2. Jinsi huko duniani utafiti huu ulivyokuwa ume-make headlines mwaka jana lakini bila kutajwa chuo husika!!!

(i) The New York Times- Rat That Sniffs Out Land Mines Receives Award for Bravery.

Wakati Thadei na wenzake mnaona hao ni panya wanaotakiwa kuwekwa makumbusho kwa sababu ni useless na huko ughaibuni wametumika sana na hivi sasa hawana maana yoyote, The New York Times wanasem:-

Kwenye habari hiyo ya NYT, hata Tanzania haikutajwa, na labda unaweza kudhani anazungumziwa panya mwingine kabisa!!!

(ii) USToday:- Meet Magawa, the 'hero rat' awarded a bravery medal for detecting dozens of landmines.
US Today na wenyewe wameshindwa kuitaja hata Tanzania let alone SUA lakini wanafungua habari yao kwa kusema:-

(iii) The Guardian ( UK):- Magawa the landmine detection rat given gold medal for bravery.
Kama kwa hizo media, The Guardian nao hawaitaji SUA wala Tanzania lakini wanaukubali uwezo wa huyo panya ambao unazidi ule wa binadamu kwenye kutegua mabomu ambapo wanasema:-


(iv) NBC News:- Rat called Magawa awarded prestigious gold medal for Cambodia landmine. detection

Kama hao wengine, NBC News inaonekana hawana ufahamu wowote kuhusu TZ na SUA kwenye uwepo wa hao panya, na matokeo yake wanaishia tu kusema:-


(v) (i) BBC - Magawa the mine-detecting rat wins PDSA Gold Medal.

Bora hata BBC ambao angalau waliitaja Tanzania ingawaje sio kwa kuipa credit kwamba:-


Hiyo ni sehemu ndogo sana ya headlines za Panya ambao Wabongo tunataka wawekwe makumbusho kwa sababu ni "useless"!!

Sasa ikiwa sisi wenyewe tu tuna fikra kama hizi, hivi kuna mtu anaweza kuzishangaa hizo media za nchi za magharibi kutosema chochote kuhusu Tanzania, na hususani SUA ambao ni partner wakubwa wa huo mradi?

Media zote zinatoa credit kwa taasisi ya Kibelgiji inayoitwa Apopo yenye ofisi zake hapo SUA!! Ajabu, hata ukiingia kwenye website ya Apopo, huwezi kuuona ushiriki wa SUA kwa haraka! Binafsi, ilinibidi nitumie keyword tofauti ndipo nikakutana na sehemu ya hii habari:-


Ukweli ni kwamba, serikali zetu pays little attention kwenye kazi zinazofanywa na wazawa, no wonder watu kama Ngunichile wanahoji:-

Lakini ukiacha kutumia source za SUA wenyewe ambao nilichelea wasije wakawa wanajimegea, nikalazimia kutafuta credible external source ambayo inasema:-

Hayo ni maelezo kutoka tovuti ya University of California, Davis, na ukiingia website ya SUA wenyewe, hapa utakuta mlolongo wa research projects!
Panya wetu wamefanya nini mpaka sasa
 
Mbona. Kilimo hohe hahe , hizo tafiti zao zinatatua nini ?
Mpaka sasa hakuna mbegu bora za kutosha ,magonjwa mengi tu ya mimea.
Mpaja sasa wakolima wansumia na mipini, hawzna nyenzo.
Sie wengine tunalima na tunakutana na changamoto za ajabu.
Mfano SUA mpaka sasa wameshindwa kugundua njia za kudhibiti barafu mikoa ta nyanda za juu wakulima wanalia kika mwaka mazao yao kukaushwa na barafu.
Wameshindwa kugundua dawa ya homa ya nguruwe.
Wameshindwa kugundua dawa ya mdudu kantangaze wa kwenye nyanya.
Mnyauko kwenye viazi na nyanya .
Ukimwi wa mihoma.
Mnyauko wa mihogo.
Kuna siku nimetafuta mtandaoni tafiti ya chikichi iliofanywa na SUA , hakun,zipi za Wa Asia tu.
Yaani matatizo ni mengi sana.
Watafiti wa SUA wajiuzuru kama mainjinia ya wa maji, wameshindwa kazi.
Kuna mhitimu wa SUA nilimuuliza, hivi zao la kakao linastawi Kigoma, alibaki kuweweseka tu.
Hatujashindwa mkuu hamjaweka hela mezani ndo tatizo. Au unataka professa achukue 4m zake anazo lipwa kwa mwezi ndo afanyie tafiti?

Watu wanafanya tafiti ambazo zinakua funded na donors, na hao donors wako interested na projects ambazo hata bongo hazina tija , ila ndo wana weka hela huko, na ma professa wana fanya hizo research.

Narudia tena, shida haiko SUA, shida iko kwenye serikali na vipaumbele vyake.As long as mtaendelea kupanga mipango ya miaka mitano ya uchaguzi, sahau kuhusu tafiti zenye tija, sahau kabisa.

Mm nakuambia hata kupata chanjo ya korona, inawezekana. Wekeni pesa watu wajifungie maabara, matokeo mtayaona. Lasivyo mtaendelea kupiga makelelw tyu.

[emoji112][emoji112]

Sent from my CPH1819 using JamiiForums mobile app
 
Sasa shida hizo tafiti hazina tija leo unaulizwa hao panya wanatumika wapi kusaidia wananchi je utakuwa na jibu
Ushaambiwa panya wanatumika kutegua mabomu sehemu ambapo kuna mabomu ya ardhini huelewi.

Hao panya wana letewa sampuli kwa ajili ya kupima wagonjwa wa TB kwa haraka zaidi, sampuli zitakazo onyesha positive results zonpelekwa maabara for confirmation. Hii inaongeza speed ya kupima TB.

Pitia kwenye website ya Apopo utaona mpaka sasa, wametegua mabomu mangapi na wame weza ku diagnose sampuli ngapi za TB.



Sent from my CPH1819 using JamiiForums mobile app
 
Usisahau Tanzania kuna uhaba mkubwa sana, tena sana wa Walimu wa Sayansi!!! Nakumbuka, enzi za JK walitumia njia mbalimbali kutaka kumaliza hilo tatizo, na njia hizo kwa mfuatano zilikuwa:-

1. Kuwapa mikataba wapya wastaafu waliokuwa wanafundisha masomo ya sayansi... waliopatikana hawakufika 100!

2. Wakawaita Form VI leavers waliokuwa wamemaliza masomo ya sayansi, na wapo tu mtaani! Serikali ikawaahidi kuwapa mkopo 100% and guaranteed employment ili kusomea Special Advanced Diploma (Science & Maths) pale DUCE!... Hawakutosha!

3. Offer kama #2 hapo juu ikaja kwa madogo wanaomaliza Form IV na kufaulu masomo ya sayansi ili wakasome 3 years Special Diploma ( Science & Maths) na kuahidiwa ajira moja kwa moja... hawa ndo wale ambao Magu aliwaita vilaza, na akaifuta hiyo special diploma!!

Sasa katika harakati hizo hizo za kupunguza uhaba wa walimu wa sayansi, ndipo SUA napo zikaanzishwa various BSc Educations courses za sayansi kama vile BS Ed ( Chemistry & Physics), Physics & Maths, Chemistry & Biology, Chemistry & Maths, etc!!

Sasa hivi kweli unaweza kuponda hilo suala?!
1. Una HOJA lakini haikidhi kujibu hoja ya mtoa hoja.

2. Hizo digrii za ualimu katika masomo ya sayansi kama ulivyotanabaisha zinafundishwa katika Vyuo mbalimbali hapa nchini.

3. Tatizo linaloleta maswali ni lengo/malengo ya chuo kikuu cha kilimo pekee hapa nchini ku-diverge kwenye mambo ya kilimo kuwa na mwelekeo wa kutoa digrii za elimu?

4. Hivi hizo digrii za elimu zinafundishwa na Ma- Profesa Mahoo (ana zaidi ya miaka 30 hapo SUA) Msanya au kuna wengine waliletwa?Wahadhiri wa UDSM, DUCE,TUMAINI,SAUTI,N.K warafundisha nini kwenye vitivo vyao vya Elimu?

5. Hebu wasomi wetu tuwe na mawazo chanya kuendana na dunia ya sasa ili kuiletea nchi yetu maendeleo pamoja na kumsaidia Mhe.Rais wetu Mama SSH ili tupate matokeo chanya.

6. Huoni kuna ukakasi katika malengo ya uanzishwaji wa SUA miaka hiyo na uanzishwaji wa digrii za Elimu SUA miaka ya hivi karibuni?

7. Tutafakari zaidi na hao PANYA WENU. Inaonekana hawana tija kwa Taifa na isiwe kama Chaka la kuomba misaada ya fedha kutoka kwa wafadhili.

KARIBU TUTAFAKARI PAMOJA!!
 
Back
Top Bottom