Hot bird
Member
- Jan 18, 2021
- 82
- 169
SUA hao wanafunzi wanaoenda field bila kuwapa pesa za kujikimu mnatuwazia nini?Hili ni swali ninalojiuliza ila hadi sasa hakuna majibu.
Watanzania kazi iendelee.
Katika mambo yanayoonekana kuwa na matatizo ni jinsi baadhi ya vyuo vikuu vinavyotekeleza mambo yake,leo nitaandika mambo yanayoendelea pale chuo kikuu cha sokoine (SUA) Morogoro.
1. Semester ya pili imefupishwa eti kisa kupisha zoezi la sensa,muda wa kufundisha ulipunguzwa kutoka mwezi wa 6 hadi mwezi wa 5 mwishoni, na yafuatayo ndio matokeo yake;
(a) Waalimu wengi hawajamaliza kozi walizopangiwa kufundisha,na wengine hata test hawajatoa.Hii imesababisha wanafunzi waende field bila kufanya baadhi ya tests na wakirudi wanatakiwa kufanya UE tu sio test tena. Chuo hakina mpango wowote na hili kabisa,na matokeo ya mwaka huu mengi yatakua ni ya kupika tu sio uhalisia.
(b) Wanafunzi tunajikuta tumebanwa sana kwa msururu wa waalimu wa kozi mbalimbali kutaka kumaliza baada ya kujua muda wa semester ni mfupi,hii inasababisha wanafunzi wengi kukariri (japo kwa SUA vitu vingi ni kukariri hakuna kuelewa) na hata wengine kuona chuo hakina mfumo uliopangiliwa vizuri na kuchukia masomo.
(c) Sasa hili la mwisho ndio tatizo lililoibuka ambalo linazidi kutuumiza wanafunzi.
Kuanzia leo tarehe moja Juni 2022 wanafunzi wote tunaosoma ualimu tunaanza field,sasa tunatakiwa kwenda field ila hatujapewa pesa za kujikimu huko field tuendako,tumejaribu kuuliza tukaambiwa tutumie bumu tulilonalo,kwa akili ya kawaida,maisha ya mauki au maziwa na ukinipeleka field unadhani gharama za maisha zitakua zilezile?,halafu kwanini mtupangie muda wa field mkiwa mnajua hakuna hela za field wakati huo?
Mnakumbuka mwaka jana wenzetu wa ESM mlipobadili field kupeleka mwezi wa pili nae mkashindwa kuwapa pesa za kujikimu, je mbona wao mlihairisha baada ya kuona mmekurupuka?
Sasa gharama za maisha huko tunakoenda field ni tofauti na hapa morogoro,kwanini msitulipe pesa yetu tuishi vizuri kwa kuwa hata field yenyewe inatuumiza tu,haiwezekani unaenda field huku ukitoka unakuja kukutana na UE na ufanye vizuri,NEVER!sijui nani aliwaza vile tu,mambo mengi kwa sasa tunaona mnakurupuka.
Hili la kutupeleka field bila stipends mnatuumiza sana sidhani mpaka raisi asikie ndio mjue mmekosea,lile mlilofanya wale ESM 2021 wakahairisha kwenda field mwezi mzima wakakaa mauki na maziwa wanafanya ngono tu haikutosha? Je, kukurupuka kule si kumejirudia? Ni nani anatoa mawazo haya kuendesha elimu yetu?
SUA, badilikeni, namaliza mwaka wangu niondoke, sirudi Morogoro tena, hii sio elimu ni kukomeshana sasa.
Watanzania kazi iendelee.
Katika mambo yanayoonekana kuwa na matatizo ni jinsi baadhi ya vyuo vikuu vinavyotekeleza mambo yake,leo nitaandika mambo yanayoendelea pale chuo kikuu cha sokoine (SUA) Morogoro.
1. Semester ya pili imefupishwa eti kisa kupisha zoezi la sensa,muda wa kufundisha ulipunguzwa kutoka mwezi wa 6 hadi mwezi wa 5 mwishoni, na yafuatayo ndio matokeo yake;
(a) Waalimu wengi hawajamaliza kozi walizopangiwa kufundisha,na wengine hata test hawajatoa.Hii imesababisha wanafunzi waende field bila kufanya baadhi ya tests na wakirudi wanatakiwa kufanya UE tu sio test tena. Chuo hakina mpango wowote na hili kabisa,na matokeo ya mwaka huu mengi yatakua ni ya kupika tu sio uhalisia.
(b) Wanafunzi tunajikuta tumebanwa sana kwa msururu wa waalimu wa kozi mbalimbali kutaka kumaliza baada ya kujua muda wa semester ni mfupi,hii inasababisha wanafunzi wengi kukariri (japo kwa SUA vitu vingi ni kukariri hakuna kuelewa) na hata wengine kuona chuo hakina mfumo uliopangiliwa vizuri na kuchukia masomo.
(c) Sasa hili la mwisho ndio tatizo lililoibuka ambalo linazidi kutuumiza wanafunzi.
Kuanzia leo tarehe moja Juni 2022 wanafunzi wote tunaosoma ualimu tunaanza field,sasa tunatakiwa kwenda field ila hatujapewa pesa za kujikimu huko field tuendako,tumejaribu kuuliza tukaambiwa tutumie bumu tulilonalo,kwa akili ya kawaida,maisha ya mauki au maziwa na ukinipeleka field unadhani gharama za maisha zitakua zilezile?,halafu kwanini mtupangie muda wa field mkiwa mnajua hakuna hela za field wakati huo?
Mnakumbuka mwaka jana wenzetu wa ESM mlipobadili field kupeleka mwezi wa pili nae mkashindwa kuwapa pesa za kujikimu, je mbona wao mlihairisha baada ya kuona mmekurupuka?
Sasa gharama za maisha huko tunakoenda field ni tofauti na hapa morogoro,kwanini msitulipe pesa yetu tuishi vizuri kwa kuwa hata field yenyewe inatuumiza tu,haiwezekani unaenda field huku ukitoka unakuja kukutana na UE na ufanye vizuri,NEVER!sijui nani aliwaza vile tu,mambo mengi kwa sasa tunaona mnakurupuka.
Hili la kutupeleka field bila stipends mnatuumiza sana sidhani mpaka raisi asikie ndio mjue mmekosea,lile mlilofanya wale ESM 2021 wakahairisha kwenda field mwezi mzima wakakaa mauki na maziwa wanafanya ngono tu haikutosha? Je, kukurupuka kule si kumejirudia? Ni nani anatoa mawazo haya kuendesha elimu yetu?
SUA, badilikeni, namaliza mwaka wangu niondoke, sirudi Morogoro tena, hii sio elimu ni kukomeshana sasa.