Suala la abiria kwenye mabasi makubwa ya mikoani kujaa hadi wengine kusimama limehalalishwa?

Suala la abiria kwenye mabasi makubwa ya mikoani kujaa hadi wengine kusimama limehalalishwa?

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Nakumbuka kulikuwa na utaratibu barabarani kwenye mabasi makubwa ya masafa marefu yanayotoka mkoa mmoja hadi mwingine, askari wanaingia kukagua mabasi na moja ya mambo waliyokuwa wanaangalia ni kama basi limezidisha idadi ya abiria.

Kutokana na hulka ya Watanzania tulivyo, tulikuwa tunakaushia pale mabasi yalipokuwa yanazidisha watu wawili watatu, ambao wengi walikuwa wanakaa kwenye vigoda au hata chini katikati ya siti. Sasa hivi hili tatizo tulipofikia na tunapoelekea ni kubaya sana.

Juzijuzi nimepanda basi kulikuwa na abiria zaidi ya 10 waliokuwa wamesimama safari nzima. Kwa kuwa ni kama tumehalalisha hili suala, tunapoelekea unaweza kukata tiketi kwa bei halali ukiingia kwenye basi hauna uhakika wa siti kama ilivyo kwenye daladala na litaonekana kama jambo la kawaida na tutakuwa tumeshachelewa kulitatua.

Muundo na matarajio ya huduma katika usafiri wa mabasi makubwa ya masafa marefu hauna tofauti kubwa na usafiri wa ndege. Suala la "comfort" kwa abiria limezingatiwa sana. Inapofika hatua unasafiri umbali mrefu ila unajihisi kama uko ndani ya daladala ya Gongolamboto, hili ni tatizo kubwa.

Niliwahi kusema itafika kipindi hata kwenye safari za ndani za ndege, idadi ya abiria wanaopanda itaanza kuongezeka kuzidi inayotakiwa na huko pia abiria watakuwa wanasimama. Kipindi ndege inaruka au kutua, abiria mlio na siti zenu mtaambiwa msogee mshee siti na wenzenu na jinsi Watanzania tulivyo wakarimu tutafanya hivyo. Kama mtu anaweza kusimama masaa 4 katika basi atashindwa kusimama lisaa katika ndege?
 
Ni kampuni zisizoeleweka tu ndio wanafanya hivyo, tena dereva na konda wanafanya hivyo ili wapate maokoto bila boss kujua.

Kampuni zinazojielewa hazifanyi hivyo
Nini kifanyike kulitatua maana abiria wengine ni kama hawaoni hili ni tatizo au wanaogopa kusema lolote ili wasionekane wana roho mbaya
 
Nini kifanyike kulitatua maana abiria wengine ni kama hawaoni hili ni tatizo au wanaogopa kusema lolote ili wasionekane wana roho mbaya
Udhibiti uimarishwe ingawa ni ngumu maana basi itatoka stand ipo level ila itaokota abiria njiani na kujaza halafu njia ndefu itatembea bila kukutana na trafiki.

Bado udhibiti utakuwa mgumu maana huwezi kuweka trafiki njia nzima.
 
Inakera sana MTU umekaa kwenye siti mwingine anakuja kukusimamia na kukupa shida!
 
Niliwahi kusema itafika kipindi hata kwenye safari za ndani za ndege, idadi ya abiria wanaopanda itaanza kuongezeka kuzidi inayotakiwa na huko pia abiria watakuwa wanasimama. Kipindi ndege inaruka au kutua, abiria mlio na siti zenu mtaambiwa msogee mshee siti na wenzenu na jinsi Watanzania tulivyo wakarimu tutafanya hivyo. Kama mtu anaweza kusimama masaa 4 katika basi atashindwa kusimama lisaa katika ndege?
Nigeria abiria wanasimama kwenye ndege nahisi ndiyo maana hutasikia wanapata hasara, na uingiaji wao kwenye ndege ni kama wa Mbagala kwenye daladala.
 
Nini kifanyike kulitatua maana abiria wengine ni kama hawaoni hili ni tatizo au wanaogopa kusema lolote ili wasionekane wana roho mbaya
Sio nini kifanyike, hapa naona tatizo linaanza kwa abiria mwenyewe....
Yani kwanini mtu upande gari ambalo tayari limejaa na hakuna seat??
Abiria wa hivi inapaswa sasa waanze kutandikwa bakora ili akili iwakae mujarabu.
 
Sio nini kifanyike, hapa naona tatizo linaanza kwa abiria mwenyewe....
Yani kwanini mtu upande gari ambalo tayari limejaa na hakuna seat??
Abiria wa hivi inapaswa sasa waanze kutandikwa bakora ili akili iwakae mujarabu.
Unaongea hivyo kwa sababu hujawahi kupakatwa na shida kubwa inayokufanya uwahi sehemu chap na mahali ulipo usafiri ni wa shida wewe. Aliyeshiba hamjui mwenye njaa!
 
Udhibiti uimarishwe ingawa ni ngumu maana basi itatoka stand ipo level ila itaokota abiria njiani na kujaza halafu njia ndefu itatembea bila kukutana na trafiki.

Bado udhibiti utakuwa mgumu maana huwezi kuweka trafiki njia nzima
Hapo hata hao trafiki wenyewe hata wakikutana na hayo mabasi hawana msaada sana maana inawezekana wanapewa mlungula wanafumba macho. Nilichoona juzi ndiyo kimenishtua zaidi.

Kuna umuhimu wa kuwa na kampeni ya kuongeza ushirikiano kati ya mamlaka husika na abiria. Moja ni sheria iwepo itakayolazimisha kuweka stika nyuma ya siti ya kuripoti matukio yoyote ya uvunjifu wa sheria, kuanzia uendeshaji mbovu hadi kuzidisha abiria.
 
Nigeria abiria wanasimama kwenye ndege nahisi ndiyo maana hutasikia wanapata hasara, na uingiaji wao kwenye ndege ni kama wa Mbagala kwenye daladala
Hivi hili kumbe limeshaanza kufanyika huko Nigeria? Basi ni suala la muda tu kabla hatujaliona kwenye ndege za ATCL
 
Unaongea hivyo kwa sababu hujawahi kupakatwa na shida kubwa inayokufanya uwahi sehemu chap na mahali ulipo usafiri ni wa shida wewe. Aliyeshiba hamjui mwenye njaa!
Mkuu, kama inatokea una haraka... basi jiandae mapema uweze kusafiri kabla ya leo.
Na inapo tokea dharura kwamba mtu anakata roho basi pale hua lazima pawe na namna ya kufanya wepesi tofauti na public transport
 
Hivi hili kumbe limeshaanza kufanyika huko Nigeria? Basi ni suala la muda tu kabla hatujaliona kwenye ndege za ATCL
Kitambo nilikwenda huko 2006 nikayashuhudia, tena usishangae baadhi ya route mkapanda na kuku
 
Unaongea hivyo kwa sababu hujawahi kupakatwa na shida kubwa inayokufanya uwahi sehemu chap na mahali ulipo usafiri ni wa shida wewe. Aliyeshiba hamjui mwenye njaa!
Nilichoona mimi siyo kwamba hizo ruti zina uhaba wa mabasi ni kwamba wanaofanya hivyo wanapata unafuu wa nauli na wengine wanapakiwa katika stand kubwa kabisa huku mabasi mengine yakiwepo. Sasa jiulize, wewe unaweza kukodi bajaji au hata bodaboda ulipe nauli kamili ya kukubeba peke yako halafu njiani dereva abebe abiria wengine achukue nauli bila wewe kupata punguzo lolote na uwe tayari kwa kadhia ya kubanana?
 
Mods Cookie Mhariri mnaweza kuiweka hii mada katika kipengele cha KERO? Sijui kama itasaidia kuwafikia wahusika kwa haraka ila nimeona mna hiyo option
 
Kitambo nilikwenda huko 2006 nikayashuhudia, tena usishangae baadhi ya route mkapanda na kuku
Yaani imefanya ni gugo kama kuna ndege ambazo abiria wanasimama, kumbe mabepari walishawahi kulifikiria hili wazo na kudesign kabisa ndege za namna hiyo ingawa inaonyesha hili wazo halijawahi kukubaliwa. Wazilete tu huku hizo ndege maana mahitaji ni mengi.
 
Unaongea hivyo kwa sababu hujawahi kupakatwa na shida kubwa inayokufanya uwahi sehemu chap na mahali ulipo usafiri ni wa shida wewe. Aliyeshiba hamjui mwenye njaa!
Tembea " ukutwe na shida" mm siku moja nilisafiri toka Manyoni mpaka stand kuu Dodoma.

Lengo na madhumuni nifike Gairo, pale nikapokelewa na wahudumu ambao walinitaarifu kuwa ntapata gari wakanitajia nauli .

Shida inaanzia kwenye tiketi wanayokupa ni zile za vitabu lkn zikiwa zimetaja bus husika.

Nikapelekwa sehemu nikaambiwa kaa hapa bus likija tutakuita. Nikawauliza ntapata SITI, wakanijibu utapata na hakuna gari inayotoka pale getini bila KUKAGULIWA

Kweli bus likafika nikaitwa na kuingia ndani ya bus nikihimizwa kusogea nyuma HAKUKUWA HATA NA SITI 1 ILIYOWAZI.

Nikajipa imani pale getini bus litakaguliwa tutapigwa chini , HAKUNA CHA KUKAGULIWA wala nini, nikasimama mpaka GAIRO.

KUNA ulegevu mahala fulani.
 
Mkuu, kama inatokea una haraka... basi jiandae mapema uweze kusafiri kabla ya leo.
Unapata taarifa ya msiba na ujuavyo baadhi yetu mtu akifa saa 8 usiku mchana wa siku hiyohiyo lazima azikwe
 
Unapata taarifa ya msiba na ujuavyo baadhi yetu mtu akifa saa 8 usiku mchana wa siku hiyohiyo lazima azikwe
Jibu ni kwamba, usijilazimishe kuwahi msibani wakati wewe inajiweka kwenye higher risk.
Tena kwahili naona kama sisi watanzania tuna.......
Anyways...🙌
 
Back
Top Bottom