Suala la Academic International School kudai ada ya muhula wakati huu halikubaliki, Serikali tunaomba muingilie kati

Suala la Academic International School kudai ada ya muhula wakati huu halikubaliki, Serikali tunaomba muingilie kati

Hapo ni kweli wanawaumiza lakini kwa upande wa pili pia na wao wanaumia maana wafanyakazi wao wana mikataba ambayo wanawalipa mishahara ambayo ni full hata kama wapo nyumbani kipindi hichi.

Na chanzo cha mapato ya shule ili iweze kuwalipa hao wafanyakazi ambao wana mikataba ni ada za wanafunzi.

Sema kinachotakiwa ni kupunguza hizo ada ili wao wasiumie sana na nyinyi msiumie sana.

Kwenye janga hili la corona kuna watu wengi wataumia.




Sent from my iPhone using JamiiForums
Ni kweli ila kwa wafanyakazi wao nao wapunguziwe mishahara? Nadhani wazazi walipe full ada tu.
 
Sidhani kama ni sahihi kulipa ada kipindi hiki ambacho wanafunzi hawasomi,shule itafute namna ya kujiendesha,unalipaje ada wakati huna uhakika watoto wanarudi lini shuleni
itafute namna?namna ipi,hembu weka hiyo namna hapa
 
Sidhani kama ni sahihi kulipa ada kipindi hiki ambacho wanafunzi hawasomi,shule itafute namna ya kujiendesha,unalipaje ada wakati huna uhakika watoto wanarudi lini shuleni
Hii si sahihi, ni wazi kuwa ipo siku shule zitafunguliwa tu. Wazazi walipe ada ili mambo mengine kwa watumishi wa hizo shule yaendelee. Uongozi wa shule utafidia tu!!
 
Mtoto ulimpeleka mwenyewe wala hukushauriana na serikali, sasa hivi unataka serikali iingilie kwenye maamuzi ulofanya mwenyewe!!!
Shule zina utaratibu wa kujiendesha, kama mna malalamiko kama wazazi basi shaurianeni na bodi ya shule muone cha kufanya.
 
itafute namna?namna ipi,hembu weka hiyo namna hapa
Hio ni kazi ya shule kuumiza kichwa,labda kwa ushauri ;kama wana mikopo waombe benki zisitishe makato kwa muda,watumie akiba ya shule kujiendesha,kama ni kodi waiombe serikali isitishe kwa muda,kama shule ina miradi mbadala ndio muda wa kuitumia nk nk
 
Kinachotakiwa kwa Sasa ni kulipia ada kidogo ambazo zitasaidia kuendesha shule na sio kulipa full. Logic ni simple kipindi hiki wanafunzi hawafundishwi kwa hiyo walipe kidogo kwa ajili ya assignment wanazotuma online. Tuchukulie mfano huu ugonjwa ukaenda kwa miaka miwili je tutaendelea kulipa ada?

Na je ukiisha kesho na shule zikarudi na kuna wanafunzi mfano form six walishamaliza ada je watalipa tena?

Kikubwa hapa Wizara husika itoe mwongozo ambao utafuatwa na shule zote.

Halafu wana JF mna balaa. Humu humu ndio wote tunamiliki vogue, tunaishi USA, tunamijengo Masaki nk. Leo kaja mtu anasomesha mtoto international mnamshauri ampeleke shule ya kata. Mmeshasahau majivuno yenu yote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mh Waziri wa Elimu na Serikali tunaomba muingilie kati hili linaloendelea katika hii shule ya Academic International School ya hapo Dsm kwani wanawalazimisha Wazazi kulipa Ada ya term nzima wakati huu ambao tupo kwenye janga la Corona, shule zote zimefungwa na haijulikani ni lini hali itarudi kuwa ya kawaida pale shule zitakapofunguliwa rasmi.

Ipo hivi, mara baada ya Serikali kuzifunga shule zote kutokana na janga la corona, shule hii kama zilivyo nyingine nyingi, imekuwa ikiwatumia wanafunzi wake assignments/maswali mbalimbali kupitia walimu wa masomo kama sehemu ya kuwa keep watoto busy hasa kipindi hiki ambacho wapo nyumbani.

Hili ni jambo jema na Wazazi hawakatai kwamba kwenye hili kuna gharama za hapa na pale ambazo Shule na walimu wamekuwa wakiingia ili kulifanikisha hili la kuwasaidia watoto kipindi hiki wakiwa nyumbani. Lakini hili la kuwaambia Wazazi walipe ADA/TUITION FEES ya muhula mzima HALIKUBALIKI kwani watoto wapo nyumbani na hawapati zile class sessions za masomo yote kama wanapokuwa shuleni full time. Hakuna chochote kipya cha kwenye masomo ambacho wanakipata hivi sasa zaidi ya Walimu kuwatumia assignments/maswali ili kuwa keep busy kipindi hiki ambacho wapo nyumbani.

Shule walau ingesema Wazazi wanapaswa kulipa kiasi fulani cha Ada/percent fulani ya Ada ili kusaidia hili ambalo linafanywa na walimu hivi sasa la kuwasaidia wanafunzi wakiwa nyumbani lakini sio kulipa Ada kamili.

Tunaomba sana Serikali kupitia Waziri wa Elimu Prof Joyce Ndalichako kulimulika hili.Vyombo vya kiuchunguzi vya serikali viliangalie hili linalofanywa na hii Academic Internationl School la kudai Ada kwa Wazazi wenye watoto kwani hii sio HAKI kabisa.

View attachment 1420400
View attachment 1420395View attachment 1420396

Hiyo shule ina walimu je unataka hao walimu walipwe na nini?

Kama huwezi kulipa peleka mtoto shule za kata.
 
Mh Waziri wa Elimu na Serikali tunaomba muingilie kati hili linaloendelea katika hii shule ya Academic International School ya hapo Dsm kwani wanawalazimisha Wazazi kulipa Ada ya term nzima wakati huu ambao tupo kwenye janga la Corona, shule zote zimefungwa na haijulikani ni lini hali itarudi kuwa ya kawaida pale shule zitakapofunguliwa rasmi.

Ipo hivi, mara baada ya Serikali kuzifunga shule zote kutokana na janga la corona, shule hii kama zilivyo nyingine nyingi, imekuwa ikiwatumia wanafunzi wake assignments/maswali mbalimbali kupitia walimu wa masomo kama sehemu ya kuwa keep watoto busy hasa kipindi hiki ambacho wapo nyumbani.

Hili ni jambo jema na Wazazi hawakatai kwamba kwenye hili kuna gharama za hapa na pale ambazo Shule na walimu wamekuwa wakiingia ili kulifanikisha hili la kuwasaidia watoto kipindi hiki wakiwa nyumbani. Lakini hili la kuwaambia Wazazi walipe ADA/TUITION FEES ya muhula mzima HALIKUBALIKI kwani watoto wapo nyumbani na hawapati zile class sessions za masomo yote kama wanapokuwa shuleni full time. Hakuna chochote kipya cha kwenye masomo ambacho wanakipata hivi sasa zaidi ya Walimu kuwatumia assignments/maswali ili kuwa keep busy kipindi hiki ambacho wapo nyumbani.

Shule walau ingesema Wazazi wanapaswa kulipa kiasi fulani cha Ada/percent fulani ya Ada ili kusaidia hili ambalo linafanywa na walimu hivi sasa la kuwasaidia wanafunzi wakiwa nyumbani lakini sio kulipa Ada kamili.

Tunaomba sana Serikali kupitia Waziri wa Elimu Prof Joyce Ndalichako kulimulika hili.Vyombo vya kiuchunguzi vya serikali viliangalie hili linalofanywa na hii Academic Internationl School la kudai Ada kwa Wazazi wenye watoto kwani hii sio HAKI kabisa.

View attachment 1420400
View attachment 1420395View attachment 1420396
Kwa nini ya vyumbani unayaleta sebuleni?
 
Hii si sahihi, ni wazi kuwa ipo siku shule zitafunguliwa tu. Wazazi walipe ada ili mambo mengine kwa watumishi wa hizo shule yaendelee. Uongozi wa shule utafidia tu!!
Serikali imefunga shule kwa muda usiojulikana,sasa utaendelea kulipa ada mpaka chanjo ipatikane?
 
Back
Top Bottom