Suala la Academic International School kudai ada ya muhula wakati huu halikubaliki, Serikali tunaomba muingilie kati

Suala la Academic International School kudai ada ya muhula wakati huu halikubaliki, Serikali tunaomba muingilie kati

Kuna wanaoponda sana mara ni upumbavu kupeleka mtoto shule za binafsi hili mara lile unaweza ukawa uwezo wako wa kifikiri na kupambanua mambo ndo umefikia ukomo hapo. Hebu tujiulize wenye kuwaza hivyo je shule binafsi zinachukua idadi ya wanafunzi kiasi gani kwa nchi nzima ndo tuone kama bado serikali inaweza kuwaaccomodate hao wanafunzi wote. Hivi tumeshajiuliza kwanini hata serikali inaweka mwongozo kwa kima cha chini kwa sekta binafsi?
Mzazi anapoamua na kumpeleka mtoto shule binafsi haimaanishi kuwa ana pesa za kumwaga wengi humu tunajfahamu matokeo ya shule nyingi hasa hizi za kata kwa mantiki kwamba mzazi ambaye ameona umuhimu wa kujinyima ampeleke mwanae shule za binafsi anakubaliana na sharti la kuumizwa na wenye hizi shule.
Kwa baadhi ya members wamemuwakia mtoa mada kama vile sijui kajimwambafai vile.
Humu ndani kuna zaidi ya threads mbili zinazungumzia baadhi ya watamzania kufurahia amguko au mtu mwimgine hasa mwenye mafanikio haijalishi ni makubwa kiasi gani ila mzazi katoa lalamiko just from no where unaanza kumwita mpumbavu. Unafaidika nini ikiwa wanao wanasoma shule za kata tulia tu hiko ni jambo la kawaida . Hakuna jamii isiyo na watu wa daraja la juu kati na chini. Kubaliane tu na hali yako haisaidii kumtolea mwenzio pofu mtu hata kumfahamu humfahamu. Nawaza nimewakwaza ila ndo hivyo. Social stratification haikosekani ktk jamii yoyote ulimwenguni ila haimaanishi uadui.
 
Mimi nadhani ingependeza jiwe angesema tufunge na tuombe ili watu wasiojulikana wajulikane ili tuwaulize ni nani alim shoot Kamanda Tundu lisu

Kwaio Haya maombi ya covid 19 hayana maana kwangu kama hatutaanza na maombi ya kuwasakama watu wasiojulikana.

Mmenipata hapo lumumba? Over.

son of almighty God.
 
Capitalist system, unanipa huduma nakulipa. Hunipi huduma nasitisha malipo. Ningekuwa mzazi nisingetoa mia, it's give n take.
 
Swali linabaki pale pale kwamba hao wanafunzi usajili wao ni wa kusona online au ni wa kuingia darasani physically!
Kwa hiyo wale watakaoshindwa kusoma online hawataenda darasa linalofuata? Shule zisijitafutie kesi watakazoshindwa kizembe mahakamani. Wasubiri utaratibu na maelekezo ya serikali.
Tena hapo vocha juu yako mzazi....na bado unawalipa !! Kuna wazazi wengine ni mama lishe wanapenda watoto wao wasome shule nzuri na wao hali ngumu sasa hivi. Kingine ni wazazi wote wana smartphone?
 
Hizo ni mbwembwe zako! Hiyo hela ungeweka bank ningezaa kbs. Mtoto akipata ugonjwa ghafla akishindwa kusoma kwa mwaka au miaka 2,utajilaumu na kujuta kimoyo moyo au kwenda kbs shule kulalanika.....punguza sifa za kwenye keyboard.
Mimi nimelipa ada ya miaka miwili mbele.

Wewe ya mwaka mmoja tu unalialia hapa wakati shule za Magufuli zipo
 
Hahahaa...ndo maana mmewaambia siye tunaosomesha katani tuache wivu jamani
Kinachotakiwa kwa Sasa ni kulipia ada kidogo ambazo zitasaidia kuendesha shule na sio kulipa full. Logic ni simple kipindi hiki wanafunzi hawafundishwi kwa hiyo walipe kidogo kwa ajili ya assignment wanazotuma online. Tuchukulie mfano huu ugonjwa ukaenda kwa miaka miwili je tutaendelea kulipa ada?

Na je ukiisha kesho na shule zikarudi na kuna wanafunzi mfano form six walishamaliza ada je watalipa tena?

Kikubwa hapa Wizara husika itoe mwongozo ambao utafuatwa na shule zote.

Halafu wana JF mna balaa. Humu humu ndio wote tunamiliki vogue, tunaishi USA, tunamijengo Masaki nk. Leo kaja mtu anasomesha mtoto international mnamshauri ampeleke shule ya kata. Mmeshasahau majivuno yenu yote

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walipe tu hakuna namna kama bado mwafundisha sisi huku mpk shule zifunguliwe kwa kweli tukutane mwisho wa agizo full burdaan
Mim ni mwalimu shule ya international x hapa Arusha, hivi ninavoandka reply hii ni nimetoka mapumzko baada ya kuwa na vipind darasan (online classroom), ni video meeting via google classroom, yan ni normal classroom session . Tunafanya kazi kama kawaida na shule inaoperate kama kawaida, so wazaz wasipolipa ada mambo yataendaje? Swali kwako....Online courses hazilipiwi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hujatumia busara mkuu, kumbuka hiyo shule ni biashara ya mtu. Na biashara kipindi hiki zimepata pigo kubwa, na ukumbuke pia wanahitaji nao kulipa mishahara.

Kumbuka, IF YOU ASK THE PRICE, YOU CAN NOT AFFORD IT

Wewe hizo shule sio class yako
Tatizo sio class tatizo ni value for money, hali ngumu sio kwao tu ni kwetu sote kuna watu wamefunga biashara, watu wamepoteza ajira hiki ni kipindi cha kufunga mkanda kwelikweli hili janga bado tunalo vya kutosha tu ukiwachekea mabepari unakufa na njaa quarantine
 
Unataka serikali ifanyaje? Suspend mikataba? Sheria hazijaenda quarantine ndugu yangu, au mliambiwa incase shule zimefungwa kwa emergency hamtalipa ada?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi naona ni haki yao kudai ada, maana hata ukipangishwa nyumba miezi sita alafu ukasafiri miezi minne ukiwa ndani ya mkataba huwezi kusema hulipi kisa hujakaa kwa kuwa ulikua upo safari
ASA si kwa sababu vyombo vyako viko ndani na umefunga chumba,we leo aje kondakta akwambie lipa nauli ili hali gari hujapanda utakubali?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoto ulimpeleka mwenyewe wala hukushauriana na serikali, sasa hivi unataka serikali iingilie kwenye maamuzi ulofanya mwenyewe!!!
Shule zina utaratibu wa kujiendesha, kama mna malalamiko kama wazazi basi shaurianeni na bodi ya shule muone cha kufanya.
Hakukua na utaratibu kwenye corona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni vema kulipa kwa kadri ya mkataba kuwa utalipa kiasi hiki January, March, July na August 2020!
Je kama kwa bahata mbaya Mtoto amekufa je? Maana hakuna tofauti ya Mtoto aliyekufa na ambae hayupo shuleni kwa mda huo, wote hawafundishwi kwa na wote hawatumii maji na wote hawali chakula cha hapo,na wote hawachafui mazingira ya shule,so why should I pay for

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mh Waziri wa Elimu na Serikali tunaomba muingilie kati hili linaloendelea katika hii shule ya Academic International School ya hapo Dsm kwani wanawalazimisha Wazazi kulipa Ada ya term nzima wakati huu ambao tupo kwenye janga la Corona, shule zote zimefungwa na haijulikani ni lini hali itarudi kuwa ya kawaida pale shule zitakapofunguliwa rasmi.

Ipo hivi, mara baada ya Serikali kuzifunga shule zote kutokana na janga la corona, shule hii kama zilivyo nyingine nyingi, imekuwa ikiwatumia wanafunzi wake assignments/maswali mbalimbali kupitia walimu wa masomo kama sehemu ya kuwa keep watoto busy hasa kipindi hiki ambacho wapo nyumbani.

Hili ni jambo jema na Wazazi hawakatai kwamba kwenye hili kuna gharama za hapa na pale ambazo Shule na walimu wamekuwa wakiingia ili kulifanikisha hili la kuwasaidia watoto kipindi hiki wakiwa nyumbani. Lakini hili la kuwaambia Wazazi walipe ADA/TUITION FEES ya muhula mzima HALIKUBALIKI kwani watoto wapo nyumbani na hawapati zile class sessions za masomo yote kama wanapokuwa shuleni full time. Hakuna chochote kipya cha kwenye masomo ambacho wanakipata hivi sasa zaidi ya Walimu kuwatumia assignments/maswali ili kuwa keep busy kipindi hiki ambacho wapo nyumbani.

Shule walau ingesema Wazazi wanapaswa kulipa kiasi fulani cha Ada/percent fulani ya Ada ili kusaidia hili ambalo linafanywa na walimu hivi sasa la kuwasaidia wanafunzi wakiwa nyumbani lakini sio kulipa Ada kamili.

Tunaomba sana Serikali kupitia Waziri wa Elimu Prof Joyce Ndalichako kulimulika hili.Vyombo vya kiuchunguzi vya serikali viliangalie hili linalofanywa na hii Academic Internationl School la kudai Ada kwa Wazazi wenye watoto kwani hii sio HAKI kabisa.

View attachment 1420400
View attachment 1420395View attachment 1420396
Kazi kwelikwei
 
Hapo ni kweli wanawaumiza lakini kwa upande wa pili pia na wao wanaumia maana wafanyakazi wao wana mikataba ambayo wanawalipa mishahara ambayo ni full hata kama wapo nyumbani kipindi hichi.

Na chanzo cha mapato ya shule ili iweze kuwalipa hao wafanyakazi ambao wana mikataba ni ada za wanafunzi.

Sema kinachotakiwa ni kupunguza hizo ada ili wao wasiumie sana na nyinyi msiumie sana.

Kwenye janga hili la corona kuna watu wengi wataumia.




Sent from my iPhone using JamiiForums
Kwani mzazi analipa ada kwa sababu gani? Basi kama ni hivyo ufanyike utaratibu shule zipewe reimbursement toka serikalini. Mzazi analipia huduma anayopata mwanaye na si kulipia mshahara wa mfanyakazi huku mtoto akiwa hapati huduma yoyote. Kumbuka wazazi nao wanahangaika kutafuta pesa na kujinyima ili watoto wapate huduma kusudiwa. Ni heri kama hizi zingekuwa shule za wazazi na sio biashara binafsi.
 
Back
Top Bottom