Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 4,175
- 2,294
Na bado, zitaharibika kweli kweli. Kwanza mwenzetu zako ziko vipi? Hazijaharibika bado.HUU UPUUZI UNAOITWA DINI UMEHARIBU SANA AKILI ZA WATANZANIA
Kinj...Surah An-Nisa 135,Qur'an inasema;
O you who have believed, be persistently standing firm in justice, witnesses for Allāh, even if it be against yourselves or parents and relatives. Whether one is rich or poor, Allāh is more worthy of both.1 So follow not [personal] inclination, lest you not be just. And if you distort [your testimony] or refuse [to give it], then indeed Allāh is ever, of what you do, Aware.
Mimi ni Muislam typically ila ni ujinga wa hali ya juu kusema kwamba bandari kupewa Mwarabu ni ushindi kwa Waislamu,yani huo ushindi upo vipi mzee wangu mbona me sielewi?? Utajiri watakao pata hapo zitachangia nini kwa Waislamu wa Tanzania zaidi kupelekwa kwao huko UAE
Halafu uache kuijumuisha CHADEMA na mambo yako ya kidini kwa sababu wale walitoa hoja zao kwa kuangalia maslahi ya taifa na ule ulikuwa sio udini,ule unaitwa uzalendo.......ndio maana serikali wakaamua kuurekebisha ule mkataba,unajua ni kwanini?? Ni kwa sababu ya CHADEMA
Kama CHADEMA ingekuwa ni against Islam leo Tundu Lissu asingejitokeza hadharani na kuiunga mkono Palestine na kuikataa Israel
Adui wetu sisi Waislamu ni CCM;Waliingia na mbwa msikitini kwa amri ya mkapa 2000's,wameweka ndani masheikh wetu,wamepora ardhi yetu kwa miaka mingi na mbaya zaidi hawataki kuipa uhuru Zanzibar kwa kisingizio eti wakiachiwa watajiunga na OIC na Kibaya wanachofanya ni kwenye elimu juu ya vijana wetu
Siku nyingine usirudie kuitaja CHADEMA kwenye mambo ya kijinga kama haya ulio andika
said mohamed
Nguruvi3,Mohamed Said
Ningalikushauri ufute hilo bandiko lakini pia natambua haki yako ya kutoa maoni.
Nafasi yako katika Jamii ni kubwa kiasi cha ''kuteka'' uhuru wako wa maoni na kubebeshwa taswira ya jamii.
Cobra....bwana mohamed said maisha yako yote unaishi kwa hofu kubwa na mashaka moyoni dhidi ya kanisa katoliki takatifu la mitume wa kweli, nafurahi sana kuona kanisa katoliki na wakatoliki wanaishi kichwani kwako bila kodi wala gharama yoyote na pale uwaonapo basi unalipuka kwa hasira hofu na chuki kubwa moyoni mwako.
unataabishwa sana na maendeleo ya kanisa pamoja na taasisi zake kongwe katika nyanja za maendeleo na sio hayo tu bali pia mfumo wa maisha, elimu, sekta za afya, mazingira, fedha na kadharika kubwa zaidi uongozi imara na mahiri kuliko serikali yenyewe, hakika kanisa katoliki na nchi huru ndani ya nchi huru. maisha yako sasa 60+ unaendelea kutaabishwa vilivyo na kasi ya maendeleo ya kanisa, taasisi zake na watu wake. nafurahi sana kuona unaendelea kutaabishwa na wivu, chuki, uongo vilivyo ndani ya moyo wako, sishangai wala? ulizaliwa kanisa ukalikuta na najua utaliacha likinawiri na kushamiri kwa kasi.
kwa jicho lako ovu, nia yako ovu na misimamo yako dhaifu, kwa kila ukionacho kwa wakatoliki basi gere hukujaa na kushamiri usoni mwako. Waislamu wote wanajua kasi ya maendeleo ya kanisa katoliki dhidi ya tutaasisi tuchache tulito tudogo twa waislamu. sisi hatutaabishwi na chochote kutoka kwa waislamu au uislam bali wewe na waovu wenzio wachache mnataabishwa sana na ukristo, wakristo na kanisa katoliki kwa ujumla.
chadema wamepigana miaka kwa miaka kurudisha haki za watanzania zilizoporwa, migodi ya bulyanhuru, north mara, gesi ya mtwara, makaa ya mawe huko kiwira mbeya, rushwa, ubadhirifu, wizi na hujuma mbalimbali serikalini, viongozi wa chadema wamepambana dhidi ya dhurma mbalimbali za viongozi wa serikali na makampuni makubwa yanayoiba rasilimali za Tanzania. kamwe hujawahi kaa kitako kuandika chochote kwa hadua hio ya chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) bali hubinua kinywa chako kiapana tena kichafu kulikaripia kanisa, ukristo, wakristo na viongozi wake.
bahati nzuri sana hutokaa kusikia kanisa limekujibu bali waumini wake tutashughurika nawe mpaka mauti, ni miaka na miaka mijadala yako tunaikabili, kukukabili na kukukumbusha kuwa kanisa linanawiri sana. wakatoliki hatutaabishwi nawe wala uislamu wala waislamu tupo tumejitosheleza kwa kila kitu.
Mwalimu Julius Nyerere alipoka mamia ya taasisi za wakristo na mashirika mengine yaliyo na mafungamano na kanisa ili msomeni. usivyo na aibu unazusha uongo, chuki dhidi yake pamoja na ujivuni wako umesoma na kusomeshwa shule za kanisa leo unaona halina maana bali upuuzi. hakika mzee wewe ni mjinga na mpumbavu duniani. amani tuliyonayo utaiacha kama ilivyo si muislamu wala mkristo wala yoyote alie na uwezo wa kuvunja amani hii na kama yupo amwage hata mkojo aone.
Ndio maana nasema uache kuiunganisha Chadema kwenye mambo ya kijinga kama ya UDINI..........Fanya yote ila usiikashifu CHADEMA tafadhali sanaKinj...
Unaandika kwa ukali.
Umeghadhibika.
Ghadhabu humfanya mtu kupoteza umakini wa kufikiri.
Hapakuwa na haja kutumia neno, "ujinga," kwangu.
Ungetulia ungeweza kuwa na ufahamu wa nini nimekusudia na kwa nini nimeunganisha CHADEMA pamoja na TEC na kukumbusha historia mfano wa hili la bandari.
Crapuseless enemy no one is even caring of your narratives, you are here Wrighting rubbish, it's either you stop this unfruitful animosity or you die unprecedented miserable death .
inglorious Bastard.
Mnadanganywa hivi huku huyu akitoka hapa anaenda zake kupokea tende na maziwa ya ngamia anakula ananenepa wewe unabaki kuaminishwa ujinga.Mti wenye matunda ndio utupiwao mawe.
Penye madini ndipo wajaapo wachimbaji.
Uzi imejaa madini
Mohamed, makala yako haijanitaabisha lakini nakiri imenifedhehesha.Nguruvi3,
Unanishauri nifute bandiko langu lakini hujasema lolote kuhusu video iiyonifanya niandike makala hayo ambayo inakutaabisha na umeona salama ni kwa makala hiyo kufutwa.
Ahsante kwa ushauri wako.
Nakuomba turudi wakati wa utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi.
Kinj...Ndio maana nasema uache kuiunganisha Chadema kwenye mambo ya kijinga kama ya UDINI..........Fanya yote ila usiikashifu CHADEMA tafadhali sana
Nguruvi3,Mohamed, makala yako haijanitaabisha lakini nakiri imenifedhehesha.
1. Ansbert Ngurumo amezungumzia pande mbili, ya serikali akisema hakufanikiwa mawasiliano, kama lipo la kuulizwa kuhusu ziara, Serikali Ijibu. Pili, akaeleza mazungumzo na ' Mwanadiplomasia' wa Vatican, hakusema ni kweli au si kweli bali kunukuu. Sina sababu za kumtetea maoni yawe yake na yaheshimiwe kama yako.
Sidhani maoni yenu wawili yanawakilisha taasisi yoyote.
2. Umezungumzia DP kwa kutumia neno '' Waarabu' . Ni kweli ni Waarabu na sidhani kama hilo ni tusi.
Mbona Wazungu wanaitwa hivyo? Kuna ubaya gani kuwaita DP Waarabu kama tunavyoita wale Wazungu waliowekeza bandari ya Zbar!
3. Matatizo ya mikataba ya DP hayakuanzia Tanzania. Kuna nchi nyingi wanayo. '' Reactions' za Watanzania ni kutokana na mafunzo ya DP kwingine. Mkataba uliangaliwa kifungu kimoja hadi kingine na kubaini mapungufu yaliyohitaji ufafanuzi. Kwa mfano, nani anasaini upande wa pili. Ni muda gani wa mkataba, kwanini uhusu maeneo nje ya Bandari ya Dar es Salaam. Kwanini uifunge mikono serikali wakati kunapotokea fursa n.k.
Maoni ya wapinga mkataba yabiwe kwa hoja. Maoni iwe ya kuzua au ya kweli, ukweli ni hoja inajibiwa kwa hoja. Nimefuatilia majibu ya baadhi ya hoja kutoka makundi ya jamii nikasikitika .
Utetezi wa Rais ni Mwislam, wala si kujibu vifungu unatia simanzi. Nilidhani Mohamed Said utakuwa tofauti , sijaiona.
Mohamed, waeleze wanaopinga mkataba, uzuri upo wapi! Upotofu wa vifungu wanavyonukuu upo wapi.
Ni wapi kumefanyiwa hila n.k. Ukijibu hayo kwa kutumia hoja za Wanaopinga kwa kifungu na mantiki utasaidia kuonyesha chuki inayojengwa dhidi ya '' Waarabu'' na DP. Bila hivyo, utakuwa unajenga chuki
Kwa bahati nzuri sana Mohamed Said umefanya kazi Bandari katika nafasi kubwa. Unaelewa abcd zake.
Tueleze kwa kina na vifungu, uzuri wa Mkataba ili tuoene chuki za Wanaopinga mkataba dhidi ya DP
Ukitueleza kwa mtindo rahisi kama uliopo katika bandiko lako, huitendei haki jamii yako na Taifa
4. Umeunganisha Chadema na Wakatoliki kwa ushirika wa hujuma. Sijui kama unajua ACT Wazalendo, CUF ya Lipumba walipinga Mkataba. Ulichokifanya ni 'selective amnesia' ( hukumbuki baadhi ya mambo kwa kuchagua).
Lakini pia Mohamed una ji-contradict. Leo unasema Waislam walikataa wakiunga mkono DP ukiwanasibisha na CCM. Ni hawa CCM iliyokuwa TANU unaowatuhumu kila siku kwa madhila dhidi ya Waislam.
Ni hawa CCM na Serikali yao wasiojibu hoja mlizopeleka 'Bungeni'. Ni hawa waliolea 'mfumo kristo' kwa miaka dahar kwa mujibu wa Mohamed Said . Leo hao wamegeuka wema kwa Waislam!!! Leo Chadema ndio imebeba madhila na yote unayolalamikia! Lini Chadema iliwahi kuongoza nchi kwa sekunde 1.
Kumbuka kwamba Chadema ni Wapinzani , wana mitazamo yao, kuchomeka udini ni kiwango cha chini sana.
Kuna hoja zinaweza kujadiliwa, hili si mojawapo. Wenye Weledi bila kujali itikadi zao wanaiangalia nchi kwanza!
Katika karne hii bado tunatazamana kwa taswira za Wazzungu na Waarabu!
5. Ziara ya Pope Tanzania ilifanyika wakati wa A.H, Mwinyi. Kwanini hili lionekane ni jambo geni.
Huko ulikohamia kwa Mtikila mimi siendi kwasababu hoja ni bandiko lako na hilo ndilo tujadili.
Kwa mtazamo huu, nimeshauri uondoe bandiko lako si kwasababu linakera , la hasha! ni jepesi sana kwa mtu mwenye kalamu kubwa kama yako. Ninahofu sana asijetokea mpuuzi akashawishika kukuomba hiyo kalamu !
JokaKuu Pascal Mayalla Mag3
Mohamed, tulijadili bandiko lako kwa hoja ulizoleta ili tusiwapoteze Wasomaji, ndivyo nilivyojibu hoja kwa bandiko langu #54. Mtikila amefariki kabla ya Waarabu, DP, Muungano wa Chadema na TEC, Waislam na CCM.Nguruvi3,
Nitaanza na aitakae kalamu yangu.
Hata huko kwenu kalamu zipo na ikiwa itaombwa yangu na huku wako na wao wataomba kalamu kutoka kwenu.
Wala usighafilike katika hili.
Ikiwa hutaki kuingia kwa Mtikila hiyo ni khiyari yako.
Lakini mchezo huu ndivyo ulivyochezwa.
Sasa nachukua nilipoishia kwa Mtikila na kusonga mbele.
Utaona sheria za mchezo zilivyobadilika wakati ule kama zinavyobadilika hivi sasa.
Nguruvi3,Mohamed, tulijadili bandiko lako kwa hoja ulizoleta ili tusiwapoteze Wasomaji, ndivyo nilivyojibu hoja kwa bandiko langu #54. Mtikila amefariki kabla ya Waarabu, DP, Muungano wa Chadema na TEC, Waislam na CCM.
Tu focus katika mada tafadhali.
Hapana! tujadili hoja iliyoletwa bandiko #1 na nimeitolea maoni bandiko# 54 ili tuwe na mnkasha nadhifu.Nguruvi3,
Unataka mimi niandike kwa maelekezo yako?
Mohamed, ukisyasoma haya utaona kwamba;Nguruvi3,
Naanza.
Toleo la Rais Mwinyi la Africa Events yuko kwenye meli inayopigwa mabomu ilikuwa ni ''lead story'' yangu na sababu yake ni kuwa Ahmed Saleh Yahya wakati huo akiwa mhariri wa Africa Events alikuja Dar es Salaam na tukawa na mazungumzo kuhusu matatizo aliyokuwa anapata Rais Mwinyi kutoka vyombo vya habari Tanzania pamoja na magazeti ya chama chake akiwa Mwenyekiti na gazeti la serikali akiwa ndiye Rais.
Rais Mwinyi akishambuliwa sana na magazeti na Pastoral Letters.
Ahmed Yahya akaniuliza hii iinawezekana vipi?
Mimi nikamueleza kwa nini inakuwa hivyo.
Siasa za Tanzania ni za aina yake kwa watu fulani.
Hapo tuko katika hoteli moja maarufu inaitwa Chef Pride iko Chagga Street na ndiyo ilikuwa kijiwe changu nikija Dar kutoka Tanga.
Basi niko hapo na Sheikh Ahmed tunashusha chai kababu na sambusa.
Mimi Ahmed Yahya aliponipigia simu kuniambia kuwa yuko mjini na ananiomba tunywe chai pamoja nikajua lipo jambo.
(Nasema liko jambo kwa kuwa AE na jamaa hawa walikubaliana kitu baina yao kuhusu makala zangu lakini hiki ni kisa kingine iko siku In Shaa Allah nitakieleza).
Waamerika wana msemo, ''There is no free lunch in America.''
Ukiona mtu kakualika anakununulia chakula jua utalipa kwa njia nyingine.
Nasema haya kunogesha barza.
Nimekula sana biriani za marehemu Ahmed Yahya London bure na hakunituma kazi.
Sheikh Ahmed akaniomba niandike makala moja kama njia ya kumsaidia mzee wetu.
Ndiyo nikaandika hiyo makala na wakati huo Africa Events walikuwa wameacha kuchapa makala zangu kwa muda mrefu.
Makala hii walichapa kama makala ya ''Special Correspondent.''
Hiki ni kisa kingine Insha Allah iko siku ikipatikana fursa nitakieleza.
Nani anamsaliti nani haya nakuachia msomaji.
Kilichonifurahisha mimi katika toleo hili ni hiyo, ''caricuture'' ya Rais Mwinyi yuko juu ya chombo kinataka kuzama baada ya kupigwa bomu na kushika moto.
Kwa nini hapakuwa na gazeti lolote kumsaidia Rais Mwinyi wakamwacha anashambuliwa na kupigwa kutoka pande zote kama paka mwizi?
Huko ndipo tulipotoka na katika safari hii ''underdog'' kajifunza mengi sana.
Sasa wanajua namna ya kujihami na shari zinazoelekezwa kwao.
Ndiyo maana kwa hili la Waarabu na bandari ukaona mko peke yenu ingawa unasema ACT Wazalendo walipinga.
Kupinga kwao kulikuwa kinamna.
Hawakuwa na ujasiri wa kuonekana wako na waleee!
Nguruvi3,Mohamed, ukisyasoma haya utaona kwamba;
Mosi , hujaweza ku-support hoja yako ya bandiko #1 au japo kuoanisha unachoeleza hapa na kile cha bandiko#1
Pili, kwavile tunajadiliana na nina hoja bandiko #54 zinahusiana na bandiko lako#1 hujazitolea maoni yako.
Tusitoke katika mjadala na kuwapoteza Wasomaji wasijue au kuweza kuoanisha mada na maoni husika.
Sina haki wala sababu yoyote ya kukushwishi uandike kwa namna yoyote ile, lakini ukweli wa kwamba tubaki katika mada haupingiki hasa katika minakasha yenye mitazamo ya mambo mzito.