Suala la kuachiwa Mashehe wa Uamsho ni vema wanasiasa wakaliacha kando

Suala la kuachiwa Mashehe wa Uamsho ni vema wanasiasa wakaliacha kando

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2011
Posts
1,684
Reaction score
2,156
Leo tena jamii ya Watanzania wameshusha pumzi kwa mara nyingine baada ya kusikia Mashehe wa uamsho kuachiliwa huru.

Kuna maoni mengi sana kwa watu. Mengi ya maoni hayo pamoja na kupongeza kitendo hicho wameenda mbali kwamba serikali iwalipe fidia. Hili limekuwa kubwa zaidi.

Wanasiasa na wanaharakati walilipigia kelele kwa muda mrefu Sasa baada ya kuachiliwa wamelipokea tena kwa namna nyingine.

Sio mjuzi wa sheria lakini naamini serikali walikuwa na sababu za msingi kuwashikilia hawa Mashekhe.

Tunapoanza kupiga kelele kuwa wakadai fidia mahakamani nadhani tungewapa muda kwanza. Wale Mashekhe naamini sio watu wa kusemewa na kuelekezwa kila kitu.

Wanao uwezo wa kujisimamia na kuamua kwa busara zao baada ya kusikiliza nafsi zao juu ya tuhuma walizoshutumiwa nazo.

Kuondoa shitaka mahakamani baada ya muda mrefu hivyo Mimi na wewe tunaweza tusijue kwa undani sababu iliyoifanya serikali kufikia uamuzi huo.

Tusije mtaani na kuwatakatifuza wakaonekana kana kwamba walikuwa mahabusu kwa kosa la kusingiziwa au kuonewa

Miaka tisa ni mingi sana kumfanya mtu ajue alipokosea na kujutia makosa yake na akawa tayari kujirudi kabisa.

Moja ya Mashekhe walioachiliwa amekiri kwamba wamejifunza mengi na kifungu kilichotumika kuwaweka huru kinampa mamlaka DPP kuwashitaki tena kwa kosa lilelile la awali endapo watatenda kosa lolote linaloelekeana na kosa walilokuwa wameshitakiwa nalo.

Ni mapema sana kuanza kuona Kama walionewa na kusingiziwa makosa hayo waliyokuwa nayo. Tusitumie muda na nguvu nyingi kutaka jamii iwaone watakatifu.

Si kila shitaka linaloondolewa mahakamani linakuwa limekosa ushahidi, mengine huondolewa kwa manufaa ya umma hasa linapooneka kutokuwa na madhara tena kwa wakati huo.

Lakini pia tufahamu kuwa hawa walishitakiwa kwa kosa la ugaidi. Kwa serikali makini si rahisi sana kufikia hatua ya kutoa hukumu kwa watu wake kwa kosa Kama hilo hasa ukizingatia ugaidi ni tishio la dunia.

Hapa lazima kuna technicalities zimechezwa ili mzani ubalance kati ya serikali na waliokuwa watuhumiwa.

Tumshukuru Mungu hili swala limefika mwisho maana huku nje presha ilishaanza kuwa kubwa pia hivyo hatujui hii presha na kelele ya nje ingetufikisha wapi.

Lakini pia tumuombe Mungu hayo yaliyokuwa yanaendelea kipindi kile wanakamatwa yasitokee tena. Tuishi kwa amani, upendo na utulivu.
 
Shida kubwa ya tz ni ushabiki hats kwenye masuala nyeti.

Kwanza hawauvai muda wa maatukio ya tindikali, kuchomwa nyumba za ibada nk.

Pia kila mtu anaona anajua siri za nchi.

Fidia: Walioumizwa nao wadai fidia kwa hawa waliotoka.

WATZ TUWE TUNAACHIA MAMLAKA MAMBO NYETI KWA KULINDA UMOJA
 
Shida kubwa ya tz ni ushabiki hats kwenye masuala nyeti.

Kwanza hawauvai muda wa maatukio ya tindikali, kuchomwa nyumba za ibada nk
Watanzania hasa wanaharakati na wanasiasa wao wanahisi kila wakati na kwa kila jambo wanataarifa sahihi kuliko serikali na vyombo vyake
 
Hawa ndugu zetu wa mama watoto shida sana,wao huamini Kwamba huwezi kutenganisha Uislam na Siasa, au maisha ya jamii, Awamu ya Mkapa,1995-2005, walimpa Mkapa shida sana.

Kwanza walianza kudai Watoto wa Kiislam wavae hijabu shuleni,Serikali ikaridhia,wakataka Tena,Mwanamke Muislam asitibiwe na Dokta wa kiume,hii ikishindikana,wakataka Tena Hata polisi na wanajeshi wa kike wavae hijabu, Serikali ikagoma, Kipindi fulani,kwenye bunge la Katiba wakataka ofisi ya kadhi mkuu, iwepo kwenye Katiba,Tena Kadhi alipwe mshahara na Serikali.

Sasa hii hukumu ya Mashekhe, kuachiliwa kwao huru,tuombe isije ikawa Uzanzibar na Uislam wa Raisi Samia umechangia,kama ni hivyo,tutakuwa tumefungulia "pandola box"yatatokea Mengi huko mbele.

Nakumbuka miaka ya 93,94,kipindi Cha Mwinyi,hawa ndugu zetu walijichukulia sheria mikononi,kukataa eti bucha za kitimoto zisiwe kwenye maeneo yenye waislam wengi,basi kuanzia Ubungo River side,mpaka ubungo mataa(zamani ubungo minazi)walivamia mabucha na kuanza kuyavunja.

Kipindi Cha Kikwete,wakaja Tena na balaa jingine,wanataka wao ndio waruhusiwe kuchinja,hawataki kabisa "mkristo achinje"kwenye machinjio ya Serikali walitaka waajiriwe wa "Islam tu.

Hii ishu ilimalizwa kwa busara kubwa na Mzee Mwinyi.

Mama Samia Ajipange
 
Mashekhe wakadai FIDIA ili iwe fundisho kwa watendaji wa serikali kuwa makini wanapotuhumu wananchi.

Pia namsihi Mh.Sugu akadai fidia kwani mahakama ilithibitishwa kwamba serikali ilimshitaki kwa hila.

Mwingine ni Mdude Nyagali ambaye suala lake la kuteswa akiwa mikononi mwa Polisi limekuwa likipigwa danadana na Tume ya Haki za Binaadamu. Mdude asikwamishwe kumshtaki IGP na jeshi la Polisi.
 
Hawa ndugu zetu wa mama watoto shida sana,wao huamini Kwamba huwezi kutenganisha Uislam na Siasa, au maisha ya jamii, Awamu ya Mkapa,1995-2005, walimpa Mkapa shida sana.
Wanadai mambo yote hayo kwasababu ccm imekuwa ikiwatumia dhidi ya wapinzani.

Wukitumbukiza udini wakati wa kampeni lazima upate madai ya kidini-kidini utakapounda serikali.
 
Sikiliza bwana! Hawa masheikh inavyoonekana hawana hatia, mahakama ni lazima iwalipe fidia. Miaka yote hiyo familia zao unajua wameishije!

Naimani kabisa na Mama samia atatenda haki kama kawaida yake.

Walioendesha mashitaka hayo dhidi yao na kwendelea kuwasumbua na kuwanyanyasa ilhali hawana kosa, Mungu atawalipa.
 
Kwanza hao kwanini mnawaita mashekh?

Wanaweza kuwa mashekh kweli, lakini katika kesi hii hawakukatwa kwa ushekhe wao,bali kwa tuhuma za ugaidi,

Hivyo watambulike hivyo kwa tuhuma zao au kwa majina yao.kuwaita mashekh mimi sion kama ni sawa
 
Umetumika kibwege sana! hivi wenye makosa ya ugaidi wanaachiliwa huru? nani aliwaweka jela na kwanini, alitumia kanuni ipi, kivipi? na kwanini asihojiwe kwa kuvunja katiba, yeye ni nani hasa?
 
umetumika kibwege sana ! hivi wenye makosa ya ugaidi wanaachiliwa huru ? nani aliwaweka jela na kwanini , alitumia kanuni ipi , kivipi ? na kwanini asihojiwe kwa kuvunja katiba , yeye ni nani hasa ?
Kumbuka kesi haikufikia hatua ya hukumu. Siku zote kilichokuwa kinagombaniwa mahakamani na wanasheria ni makosa yao kusikilizwa na mahakama ya Zanzibar kwasababu makosa yalitendeka huko

Katika hili ni vema kwenda kwa hekima na busara. Si rahisi sana serikali kuwashikilia watu wake tena wanaoitwa viongozi wa dini bila kuwa na sababu za msingi
 
Kwa mi
Shida kubwa ya tz ni ushabiki hats kwenye masuala nyeti.

Kwanza hawauvai muda wa maatukio ya tindikali, kuchomwa nyumba za ibada nk...

Kwa miaka tisa yote, wenye vyombo vya ulinzi na usalama hawajaunganisha hizo dots? Wewe umeweza??
Kama wameweza:

1: Je magaidi wamehurumiwa?
2: Je magaidi wameogopwa?

Ukiulizwa huo ushahidi ukautoe mahakamani unao wa kutosha?

Tuwe tunatumia uhuru wetu vyema na siyo kuzungumza hisia zetu na kuzifanya facts kwa mambo muhimu na mazito.
 
Mashekhe wakadai FIDIA ili iwe fundisho kwa watendaji wa serikali kuwa makini wanapotuhumu wananchi.

Pia namsihi Mh.Sugu akadai fidia kwani mahakama ilithibitishwa kwamba serikali ilimshitaki kwa hila.

Mwingine ni Mdude Nyagali ambaye suala lake la kuteswa akiwa mikononi mwa Polisi limekuwa likipigwa danadana na Tume ya Haki za Binaadamu. Mdude asikwamishwe kumshtaki IGP na jeshi la Polisi.
Hawa siyo mashehe bali ni watuhumiwa wa ugaidi!! Hawakuwa wamekàmatwa kwa ushehe wao bali walikamatwa kwa utuhumiwa wao!!! Vinginevyo mashehe wote wangekuwa wamekamatwa !!!
 
Hawakusingiziwa kwakweli! Labda viongozi wetu walikiwa na hofu kuwa tukiwashtaki yataibuka makundi mengine kama haya.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umetumika kibwege sana ! hivi wenye makosa ya ugaidi wanaachiliwa huru? nani aliwaweka jela na kwanini, alitumia kanuni ipi, kivipi? na kwanini asihojiwe kwa kuvunja katiba, yeye ni nani hasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mi


Kwa miaka tisa yote, wenye vyombo vya ulinzi na usalama hawajaunganisha hizo dots? Wewe umeweza??
Kama wameweza:

1: Je magaidi wamehurumiwa?
2: Je magaidi wameogopwa?

Ukiulizwa huo ushahidi ukautoe mahakamani unao wa kutosha?

Tuwe tunatumia uhuru wetu vyema na siyo kuzungumza hisia zetu na kuzifanya facts kwa mambo muhimu na mazito.
Nafikiri mtoa mada kaliweka vizuri sana! Uenda Serikali iliamua isiwafunge kwa maslahi ya umma kuhofia kuwa yataibuka makundi mengine kwa kasi hivo ikaaamua iwaache tu ila ni kweli hawa jamaa walifanya mambo ya ovyo sana


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawakusingiziwa kwakweli! Labda viongozi wetu walikiwa na hofu kuwa tukiwashtaki yataibuka makundi mengine kama haya.


Sent using Jamii Forums mobile app
Watu wanajisahaulisha tu
 
Back
Top Bottom