Sasa mbona Kitwanga hajiuzulu kupisha uchunguzi?
Ni rafiki yake Raisi, au shemeji yake, au alimpa posho kidogo wakati wa Kampeni....?! [emoji47]Huyu mtu anajiamini sana, ukumbuke aliposhinda ubunge tu alijiaminisha atapewa wizara nyeti, kwa mdomo wake mwenyewe alitamka kabla baraza halijatangazwa, kumbuka pia ilichuka muda kwa baraza kutangazwa.
Hataweza na hawezi kugusa humo kwani suala hilo limewabeba watu wake wa karibu mno na hata wa familia teule zisizoguswa wala kubugudhiwa. Huyo waziri ni zaidi ya swahiba na yule wa NIDA ni best friend. Ila tusubiri muda utaongea mengi.
Una uhakika hawajawasilisha?Wandugu.
Wengi kwasasa tunaelewa kinachoendelea kati ya uongozi wa jeshi la polisi na kamati ya bunge (PAC) katikati akicheza Saidi Lugumi na timu yake ya vigogo.
Hii Leo jeshi la polisi lilipaswa kua limewasilisha mkataba wao na Lugumi Enterprises ikiwa ni pamoja na payment trends in which 99 % of contract sum ishalipwa kwa lugumi elihal contract execution haijafikia hata 20%.
Katika hili ukiachilia mbali Said mwenyewe pia wanatajwa Riz ,kitwanga na Mwema. Ninaamini kabisa kua wapo wengine wengi wanene.
Kwa jeshi la polis I kushindwa kuwasilisha nyaraka hizo Leo kwa kamati ya Bunge, je ? Polisi wamepuuza amri ya Bunge ? Kuna nini ndani yake? Hapa ndipo tutakapoweza kuupima utumbuaji majipu ya kipenzi rais wetu JPM.
Kuna mpuuzi kama wewe kujiita accused wakati haujui maanake?Ukiwa hujui unachokisema au hulijui jambo linalozungumziwa si lazima na wewe u comment. Huoni aibu kuandika upuuzi?
Swali zuri Sana Mkuu?Sasa mbona Kitwanga hajiuzulu kupisha uchunguzi?
....msema kweli ni mpenzi wa Mungu...Kama Magufuri ni mkweli na ana nia ya dhati tena toka rohoni kama anavyojinadi basi hapa ndipo pa kuonyesha haswa kama kweli anakerwa na uozo,ufisadi na rushwa ndani ya serikali.
Wewe utakuwa Lugumi mwenyewe au KitwangaMpango wenu CHADEMA kuiyumbisha serikali hautafanikiwa
Kila utawala una kashfa yake, pamoja na kwamba kwenye awamu hii natarajia kasfha nyingi zaidi lakini hii ya LUGUMI imekuja sehemu na wakati mbaya. Sehemu mbaya kwa sababu inamuhusisha swahiba wa rais na wakati mbaya kwa sababu serikali ilikuwa imeanza kuaminika kwamba inapambana na vitendo vya ufisadi.
Magufuli hana uchaguzi, hana namna, hana jinsi kama anataka kuaminika lazima amtumbue 'swahiba wake'. Akifanya tofauti atakuwa anaendesha gari la kupambana na ufisadi likiwa kwenye handbreak.
Wananchi wako tayari ahairishe kila kila jipu ili atumbue hili la LUGUMI