Suala la Machinga, yafanyike haya

Suala la Machinga, yafanyike haya

Kwani kipindi cha jk, mbona yaliwezekana?meko ndio aliwatia jeuri sana!!walikuwa wakijenga vibanda vinavunjwa, na ukikamtwa ni mahakamani kwani sheria si zipo?serikali ikiamua kwa dhati mbona watakubali tu, mfano kuna masoko yamejengwa yako tupu watu hawaendi huko, eti wanafuata wateja nje!!eti litajitatua lenyewe wakati kila siku ndio linazidi, watu wanajenga mabanda kabisa barabarani, ?!!
Kama suala ni kupata wateja, vp kama wale wenye makampuni ya mabasi nao wakianza kujitafutia maeneo yao binafsi ya maegesho kisa wateja itakuaje??
 
Swala la Machinga ni swala gumu sana kulizungumzia kwa matakwa ya kidola, inaitaji Busara kubwa sana kuli-solve .

Serikali ikitaka kupambana na tatizo hili wafanye yafuatayo.
1.Ajira kwa vijana, watengeneze viwanda vidogovdogo vingi ili vijana wakafanye kazi.
2.Serikali itoe exposure kwenye kilimo kwa vijana . Ili hao vjana wakafanye shughuli za kilimo
Wakifanya haya mbona vijana watapungua mjini tyu.
Mabeberu hawatafurahi wakisikia hayo yakifanikiwa
 
Machinga leo wanaitwa uchafu takataka.

Kama JPM alikuwa anapata feelings nazosikia nikiwatazama wamachinga mitaa ya kariakoo, basi Mungu ampe pumziko jema yule mzee.

Kuna wanangu sijui wataenda kuishije mtu kamaliza chuo miaka 7 hana kazi kaamua kuwa mlengaji anaanza kuona mwanga mara paap anarudishwa kitaa...

Sijui kama watu wanaona kinachoenda kutokea....all in all maisha ni vita ngumu sana mtu asipojua size ya viatu vyako anaweza fanya lolote tu... poleni sana wanangu kwa sasa hamna chenu.
Kama unawapenda wanao wajeengee mazingira maalum na mazuri sio kutulea uchafu barabarani mji umekuwa na vibanda kama tuko porini wacheni ushamba huo hapajulikani mjini wala shambani vujo tu.
 
Ni vizuri kutafuta suluhisho la kufikirisha juu ya hili suala kubwa. Lakini ni muhimu sana kufahamu vizuri "machinga" ni nani hasa.

Kiuhalisia hawa "machinga" ni watu wanaotaka uhuru mkubwa sana wa kufanya biashara nje ya mifumo na taratibu zilizowekwa kisheria. Ni sekta isiyo rasmi kweli kweli. Wahusika wanataka waingie na kutoka katika biashara hiyo bila taratibu wala vibali rasmi, wafanye biashara popote panapopitika na wakati wowote bila udhibiti (kandokando ya barabara, katikati ya magari barbarani, katika njia za waenda kwa miguu, pembeni ya majengo, mbele ya maduka, nje ya masoko rasmi, n.k.). Wengi ni wahamaji hamaji (hawkers). Wanafuata penye wateja wengi kutegemeana na wakati wa siku. Wakizigundua hizo "hot spots", watajazana kama kama nzige hadi kumiminikia pasipostahili (barabarani, kwenye mifereji ya maji machafu na kuziba vituo vya mabasi na njia za waenda kwa miguu).

Sasa hii lugha ya kutafutiwa maeneo ya mazuri ya biashara kwa wamachinga haina maana. Hawawezi kuelewa wala kukubali. Hawako tayari kukalishwa sehemu moja muda mrefu huku wanasikia biashara imechanganya mahali kwingine. Na kwa vile wanaishi kwa kauli ya serikali iliyowaruhusu kufanya biashara bila kubughdhiwa na wameshaambiwa wao ni muhimu sana kama wapiga kura (fallacy), basi hawako tayari kuambiwa wasichotaka. Wako tayari kwa mapambano.
Weweee usicheze na serikali tia vibanda vyote moto mchezo kwisha .Nashauri Serikali iwajengee sehemu rasmi halafu iwahamishe, biashara hizi ndogo ndogo duniani kote zipo lkn si hizi za wamachinga wanavyofanya hawa ni wavamizi wajengewe out of the city maduka au vibanda vidogo vidogo kwa ajili ya biashara zao halafu hamisha kwa nguvu zote
 
Mtaa wa Kongo ulienda kutafuta nini? Nawewe ni mmoja wa waliosababisha idadi kubwa ya watu kariakoo
Mkuu nimesababisha kwa namna ipi?
Mm ni miongoni mwa wanaochukia utaratibu wa biashara za hawa wamachinga na laiti ningekuwa kiongozi ningesafisha majiji yote yenye umachinga.

Jana kuna dada almanusura agongwe na gari kutokana na hawa wanainji.
 
We Acha tu, huyohuyo anayelalamika jioni anapita hapohapo kuhemea nyanya bamia viazi mviringo, eti hamna sehemu za kutembea alijuaje kama hazipo sialipita akitembea alikuwa anatafuta nini kama sio kuhemea

Kukosa utu, roho mbaya na kutowajibika ndio tatizo.
 
Wameharibu nchi kwa sababu wanaotakiwa kuwasimamia wamekaa maofisini bila kufanya mipango yoyote? Kwani kulikua na gharama gani wahusika kuwapangia sehemu zisizotakiwa kufanya biashara kama zile njia za waenda kwa miguu na kwingineko?

Wewe unashauri tuwapeleke wapi watakapoweza kuishi na kutunza familia zao ili nchi unayosema wameiharibu itengamae??

Kabla ya kuwaza juujuu na kuishia kuwaona machinga tatizo tafuteni mzizi wa tatizo
Tufike mahali kama Taifa tufuate taratibu zetu kanuni tulizojiwekea,Machinga hana kodi anayolipa pahali popote, kibaya zaidi wanachagua maeneo yale yenye mirija ya watu wengi wanaweka bidhaa zao mbele ya biashara za wanaolipa mamilion ya shilingi kama kodi, Halafu useme eti nao wana familia zao , Je hawa wanaolipa kodi haki yao iko wapi?
 
TRA na maofisa biashara wa Halmashauri wapitie upya aina za biashara zisizo za kimachinga alafu watoze kodi /leseni kama ambavyo wafanyavyo kwenye viduka vidogo mijini.

Tarura katika miji mikubwa wanayo mamlaka ya kukataza kufanya biashara kwenye kingo za barabara /waweke tozo kama wafanyavyo kwenye parking za magari. mfano wanaweza kutoa leseni za parking /uwazi wa eneo kwa wenye maduka /ofisi ili kuzuia machinga kupanga/kuweka huduma /bidhaa zao.

Maofisa afya/TFDA wanayo mamlaka ya kuzuia biashara holela za vyakula katika maeneo yasiyo rasmi, ubora na viwango.

Wakurugenzi wa halmashauri katika miji mikubwa kwa kushirikiana na watendaji walio chini yao hasa mipango miji wana wajibu wa kutenga maeneo au kubuni njia mbadala za Machinga kufanya shughuli zao. mfano maduka /vibanda vinavyo tembea au kuteua mtaa mmoja kwa ajili ya machinga.

Wakuu wa mikoa /wilaya wana wajibu wa kuratibu maeneo na aina ya biashara ili kuondoa mwingiliano wa bidhaa na huduma kurundikana sehemu moja.

Jeshi la zimamoto linao wajibu wa kutoa elimu juu ya majanga ya moto ambayo yanweza sababishwa na ujenzi holela wa vibanda vya machinga au kuzagaa kwa machinga karibu na maeneo yenye vituo vya mafuta mijini./miundombinu ya Umeme.

Tume ya Ushindani na wakala wa vipimo na TBS nao wana wajibu wa kusimamia /kutoa elimu ya namna ya kuboresha biashara ndogo ndogo ili zikuwe na kuondoa dhana ya Umachinga wa wajasiriamali wadogo wadogo.
Sio kwamba hawajui yote hayo ila siasa ndio inaharibu hi nchi.

Wanasiasa wako juu ya kila kitu
 
Tufike mahali kama Taifa tufuate taratibu zetu kanuni tulizojiwekea,Machinga hana kodi anayolipa pahali popote, kibaya zaidi wanachagua maeneo yale yenye mirija ya watu wengi wanaweka bidhaa zao mbele ya biashara za wanaolipa mamilion ya shilingi kama kodi, Halafu useme eti nao wana familia zao , Je hawa wanaolipa kodi haki yao iko wapi?

Tatizo sio machinga, tatizo ni wenye kutakiwa kuwahudumia na kuwasimamia wamekaa maofisini bila kufanya majukumu yao

Unaposema kibaya zaidi wamekaa kwenye maeneo yenye mirija ya watu wengi wewe ulitaka wakauze kusikokua na watu?

Huu Ubinafsi na roho mbaya vinatufanya tushindwe hata kutoa mawazo yanayoweza kujenga nchi na uchumi wetu zaidi ya kubomoa
 
Takataka ni kitu chochote ambacho kipo mahali kisipostahili kuwepo!
Correct!
Hata benz ikiingizwa sebuleni inageuka kuwa takataka, kila mtu atapiga kelele itolewe.

Machinga hawa wanatakiwa kuwekewa njia sahihi na za kufuata taratibu na sheria katika biashara zao.
 
Tatizo sio machinga, tatizo ni wenye kutakiwa kuwahudumia na kuwasimamia wamekaa maofisini bila kufanya majukumu yao

Unaposema kibaya zaidi wamekaa kwenye maeneo yenye mirija ya watu wengi wewe ulitaka wakauze kusikokua na watu?

Huu Ubinafsi na roho mbaya vinatufanya tushindwe hata kutoa mawazo yanayoweza kujenga nchi na uchumi wetu zaidi ya kubomoa
Turudi nyuma kidogo..kabla utawala wa JPM hawa watu walikua kwenye maeneo rasmi katika minada na masoko, Lakini baada ya J PM kuona wafanyabiashara wengi hawakuupenda muelekeo wake akaruhusu hawa Machinga waingie katikati ya miji ili kupata sapoti ya kisiasa.

Maeneo yao yapo wala hahitajiki hata mjumbe kuwaelejeza wanapajua walipokua hapo kabla.
 
Swala la Machinga ni swala gumu sana kulizungumzia kwa matakwa ya kidola, inaitaji Busara kubwa sana kuli-solve .

Serikali ikitaka kupambana na tatizo hili wafanye yafuatayo.
1.Ajira kwa vijana, watengeneze viwanda vidogovdogo vingi ili vijana wakafanye kazi.
2.Serikali itoe exposure kwenye kilimo kwa vijana . Ili hao vjana wakafanye shughuli za kilimo
Wakifanya haya mbona vijana watapungua mjini tyu.
Huo ndio ukweriii 100% ndugu zangu
 
Mkuu heko sana, umeandika proposal ambayo imekuwepo akilini kwangu...

Huwa nakosa tu mwamko wa kupoteza nguvu zangu kuandika threads za ushauri hapa...

Tatizo ni kwamba hakuna kiongozi/viongozi wanaochukulia serious mitandao kama hii...

Nchi za wenzetu huwa wanatumia sana wanafunzi waliopo vyuo vikuu kwenye ubunifu wa miradi, mifumo, miundombinu n.k...

Mfano hili la vibanda vya kisasa/mimbari za kisasa n.k vya kimachinga lingeweza pelekwa kama sehemu ya assignment au challenge fupi yenye tunzo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kama ardhi, then wanafunzi wanachora na kusanifu na kuikabidhi kamati maalum. Mwisho wa siku kinapatikana chuo na mshindi anapewa tunzo...

Mchoro unapelekwa kwa wahusika wengine kama JKT kwa ajili ya kuufanya kuwa hai juu ya ardhi...
 
Turudi nyuma kidogo..kabla utawala wa JPM hawa watu walikua kwenye maeneo rasmi katika minada na masoko, Lakini baada ya J PM kuona wafanyabiashara wengi hawakuupenda muelekeo wake akaruhusu hawa Machinga waingie katikati ya miji ili kupata sapoti ya kisiasa.

Maeneo yao yapo wala hahitajiki hata mjumbe kuwaelejeza wanapajua walipokua hapo kabla.

Minada inafanyika mara ngapi kwa wiki? Unataka wakauze kusikokua na wateja ili nani anunue?

Hadi waanze kuanua nguo zako ulizofua ukaanika na kukuchomolea sidemirrors ukiwa unaendesha gari yako ndio utaelewa kwamba wao pia wanatafuta chochote waishi na wao pia wana majukumu na familia kama wewe

Nitaendelea kusema Kinachotakiwa ni kuwapangia na kuwasimamia sio kuwafukuza
 
Minada inafanyika mara ngapi kwa wiki? Unataka wakauze kusikokua na wateja ili nani anunue?

Hadi waanze kuanua nguo zako ulizofua ukaanika na kukuchomolea sidemirrors ukiwa unaendesha gari yako ndio utaelewa kwamba wao pia wanatafuta chochote waishi na wao pia wana majukumu na familia kama wewe

Nitaendelea kusema Kinachotakiwa ni kuwapangia na kuwasimamia sio kuwafukuza
Pumbav
 
Turudi nyuma kidogo..kabla utawala wa JPM hawa watu walikua kwenye maeneo rasmi katika minada na masoko, Lakini baada ya J PM kuona wafanyabiashara wengi hawakuupenda muelekeo wake akaruhusu hawa Machinga waingie katikati ya miji ili kupata sapoti ya kisiasa.

Maeneo yao yapo wala hahitajiki hata mjumbe kuwaelejeza wanapajua walipokua hapo kabla.
Utamsingizia jpm, hizi siasa zilianzia Zambia, maiko satta alipata support kubwa ya machinga, yule mgombea mwenza yule mzungu alikula sahani moja na machinga tena akitumia bodaboda, baada ya hapo mtizamo wa machinga kisiasa ibadilika.

Pia tukumbuke Lau Masha alipigwa chini na hawahawa machinga baada ya kuwatamkia kuwa akishinda ubunge atawafutilia mbali wakati huo akiwa waziri wa mambo ya ndani sirro akiwa rpc mwanza. Anaijua vizuri nguvu ya machinga.
 
Minada inafanyika mara ngapi kwa wiki? Unataka wakauze kusikokua na wateja ili nani anunue?

Hadi waanze kuanua nguo zako ulizofua ukaanika na kukuchomolea sidemirrors ukiwa unaendesha gari yako ndio utaelewa kwamba wao pia wanatafuta chochote waishi na wao pia wana majukumu na familia kama wewe

Nitaendelea kusema Kinachotakiwa ni kuwapangia na kuwasimamia sio kuwafukuza

Umeandika kwa kutumia akili za mtafuta kura uchaguzi ukija...

Lakini ungeandika kama mtu wa mipango miji sidhani hata kama ungeandika hivi...

Mpangilio wa mji ni kitu kizuri na faida hata kwa hao wafanyabiashara ndogondogo...

Nitakupa mfano, mji sijui jiji la Mbeya eneo la Kabwe hapo awali lilikuwa eneo wafanyabiashara ndogondogo wanapanga vitu vyao shagalabagala...lakini baadaye kuna kiongozi meenye akili alikuja na utaratibu wa kuwatengenezea meza zilizopangwa vizuri...
 
Umeandika kwa kutumia akili za mtafuta kura uchaguzi ukija...

Lakini ungeandika kama mtu wa mipango miji sidhani hata kama ungeandika hivi...

Mpangilio wa mji ni kitu kizuri na faida hata kwa hao wafanyabiashara ndogondogo...

Nitakupa mfano, mji sijui jiji la Mbeya eneo la Kabwe hapo awali lilikuwa eneo wafanyabiashara ndogondogo wanapanga vitu vyao shagalabagala...lakini baadaye kuna kiongozi meenye akili alikuja na utaratibu wa kuwatengenezea meza zilizopangwa vizuri...

Sasa wewe unafikiri hao wamachinga wakifa njaa au kuchomwa moto kwa kuwa vibaka kura zitatoshaje😂😂😂

Utaratibu ndio kitu cha msingi, sio kuwadharau wala kuwafukuza. Wao pia wana familia na mahitaji kama wewe
 
Back
Top Bottom