Suala la Mishahara kwa watumishi wa Umma liangaliwe upya, tena kwa macho manne

Suala la Mishahara kwa watumishi wa Umma liangaliwe upya, tena kwa macho manne

Man Mvua

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2016
Posts
2,183
Reaction score
3,521
Amani iwe juu yenu.

Jambo la mishahara ni kitu muhimu sana kwa mtu ndio maisha yake na ndio uhai wake. Kuna mtumishi namba moja aliyepita alipata kusema "Asiyefanya kazi na asile na maana yake afe" hivyo kila mtu hufanya kazi ili aishi yeye na familia yake.

Unyeti wa mshahara ndio umefanya mimi leo niandike hii mada, Nchi yetu bado ina unyonyaji ambao tunafanyiana sisi kwa sisi. Tumejitengenezea matabaka kwenye ofisi na taasisi zote za umma. Tumefanya aina fulani za kazi zikimbiliwe na watu wengi (ubunge) na zingine zikimbiwe (na matajiri) zikimbiliwe na maskini mfano UALIMU.

Ili Nchi yoyote iendelee kwanza jambo la usawa ni muhimu sana na kada za kuendeleza Nchi ndio hupewa kipaumbele Mf: Elimu, viwanda na technology. Nchi hii wanaozalisha hulipwa kiduchu na wafanyamaamuzi hulipwa pesa mlima its contrary the opposite.

Hivi ni kwa nini wanaofanya kazi TRA, BOT, TPA, TASAC na n.k hulipwa zaidi kuliko Walimu na Manesi na Polisi na Majeshi yetu? Bado wana posho, marupurupu na per diem? Hivi kwa nini Mwalimu wa Degree anachukua mshahara laki tano au sita kwa mwezi na hana posho wala per diem mwaka mzima. Halafu mtu mwingine mwenye kiwango sawa cha Elimu anayefanya kazi BOT analipwa 1.8M kwa mwezi? Aiseee!

Mtumishi namba moja aliyepita awamu ya tano alipata kujiuliza kitu ambacho hata mimi najiuliza, "KWANI WALISOMAJE HAWA" mpaka mtu alipwe 25M au 30M kwa mwezi? Mwisho wa kunukuu.

Nchi hii kuna kazi za watoto wa maskini mfano UALIMU, UNESI, UDAKTARI, UFUNDI na n.k pia kuna kazi za watoto wa vigogo (wazee wa kujipangia mishahara yao) na huu mfupa ni mgumu sana kwa sababu hata watoto wa maskini wanaofanikiwa kufika juu kama Magufuli na Samia hushindwa kuuondoa na kuweka usawa ili nchi Iendelee.

Maendeleo ya Nchi tutayasikia kwenye bomba tu kwa aina hii ya unyonyaji isipokuwa mwenye nacho ataongezewa (be rich to get rich)

Kazi njema wajameni nilikuwa na frustrations zangu tu baada ya kupata report ya BOT.

"TUSIDANGANYWE TENA NCHI HII HAKUNA MZALENDO HATA MMOJA LABLA MIAKA 100 IJAYO NDIO WATAZALIWA."
 
Naunga mkono hoja, mishahara itolewe kwa kuangalia vigezo vya elimu, umri kazini na uadilifu wa mtu. Mchezo wa kubagua sekta kwa sekta Sio mzuri. Kama ni degree holder wote walipwe sawa idara zote sio udaktari, mwalimu, mhasibu engineer n.k
 
Hehehe, yaani mtu anayelipwa, say, 3m ndo huyo huyo mwenye marupurupu, posho na nyumba anapewa.

Na huyu anayelipwa 500k ndo hana cha marupurupu, posho na nyumba apange kwa kumega hiyo hiyo 500k yake kwa kiwango cha elimu kile kile.

Hii mifumo sijui imerithiwa kutoka wapi.

SUKAH
 
Mkuu wewe umezungumzia habar ya 'usawa katika mishahara' ukitamani wanaolipwa Kidogo waongezewe ili wawe sawa na wa sector nyinginezo kwa kulinganisha kiwango cha elimu zao.

Nadhani ungejikita kwa kupaza sauti juu ya usawa wa Mshahara kwa kulipa wafanyakazi kiwango Cha wastani ili kuokoa vijana ambao wanatamani kuingia kwenye system ya mshahara japo walipwe kiduchu tu, lakini imeshindikana toka 2012 mpaka 2021 Leo wapo mitaani wakijikita na mambo yasiyo chaguo lao walau tu mkono uende kinywani.
 
Siku zote maskini ndiyo wengi kuliko matajiri. Ndiyo maana kazi za maskini mfano :- udaktari, ualimu, unesi na upolisi zina watu wengi Sana.

Haiwezekani na hautatokea kamwe kuwapa watu hawa mishahara mikubwa. Kwani kufanya hivyo kuna madhara 2 makubwa:-

1.--maskini akipata matako hulia mbwaa, hivyo nchi haitatawalika.
2.--kwa wingi wao fedha za mishahara hazitatosha

Maskini fanyeni kazi za kimaskini mbakie maskini ili mtawaliwe vizuri
 
Siku zote maskini ndiyo wengi kuliko matajiri. Ndiyo maana kazi za maskini mfano :- udaktari, ualimu, unesi na upolisi zina watu wengi Sana.

Haiwezekani na hautatokea kamwe kuwapa watu hawa mishahara mikubwa. Kwani kufanya hivyo kuna madhara 2 makubwa:-

1.--maskini akipata matako hulia mbwaa, hivyo nchi haitatawalika.
2--kwa wingi wao fedha za mishahara hazitatosha

Maskini fanyeni kazi za kimaskini mbakie maskini ili mtawaliwe vizuri
Point kabisa
 
Hehehe, yaani mtu anayelipwa, say, 3m ndo huyo huyo mwenye marupurupu, posho na nyumba anapewa.
Na huyu anayelipwa 500k ndo hana cha marupurupu, posho na nyumba apange kwa kumega hiyo hiyo 500k yake kwa kiwango cha elimu kile kile.
Hii mifumo sijui imerithiwa kutoka wapi.

SUKAH
Wanaofanyakaz ni watu wengine. Haya Mambo ya hovyo kabisa. Kila Jema au baya mtunga Sheria ndio chanzo.

Warekebishe Sheria.
 
Bila kuiondoa CCM haitawezekana. Maskini na Wajinga ndio mtaji wa CCM kutawala.
 
Amani iwe juu yenu.

Jambo la mishahara ni kitu muhimu sana kwa mtu ndio maisha yake na ndio uhai wake. Kuna mtumishi namba moja aliyepita alipata kusema "Asiyefanya kazi na asile na maana yake afe" hivyo kila mtu hufanya kazi ili aishi yeye na familia yake.

Unyeti wa mshahara ndio umefanya mimi leo niandike hii mada, Nchi yetu bado ina unyonyaji ambao tunafanyiana sisi kwa sisi. Tumejitengenezea matabaka kwenye ofisi na taasisi zote za umma. Tumefanya aina fulani za kazi zikimbiliwe na watu wengi (ubunge) na zingine zikimbiwe (na matajiri) zikimbiliwe na maskini mfano UALIMU.

Ili Nchi yoyote iendelee kwanza jambo la usawa ni muhimu sana na kada za kuendeleza Nchi ndio hupewa kipaumbele Mf: Elimu, viwanda na technology. Nchi hii wanaozalisha hulipwa kiduchu na wafanyamaamuzi hulipwa pesa mlima its contrary the opposite.

Hivi ni kwa nini wanaofanya kazi TRA, BOT, TPA, TASAC na n.k hulipwa zaidi kuliko Walimu na Manesi na Polisi na Majeshi yetu? Bado wana posho, marupurupu na per diem? Hivi kwa nini Mwalimu wa Degree anachukua mshahara laki tano au sita kwa mwezi na hana posho wala per diem mwaka mzima. Halafu mtu mwingine mwenye kiwango sawa cha Elimu anayefanya kazi BOT analipwa 1.8M kwa mwezi? Aiseee!

Mtumishi namba moja aliyepita awamu ya tano alipata kujiuliza kitu ambacho hata mimi najiuliza, "KWANI WALISOMAJE HAWA" mpaka mtu alipwe 25M au 30M kwa mwezi? Mwisho wa kunukuu.

Nchi hii kuna kazi za watoto wa maskini mfano UALIMU, UNESI, UDAKTARI, UFUNDI na n.k pia kuna kazi za watoto wa vigogo (wazee wa kujipangia mishahara yao) na huu mfupa ni mgumu sana kwa sababu hata watoto wa maskini wanaofanikiwa kufika juu kama Magufuli na Samia hushindwa kuuondoa na kuweka usawa ili nchi Iendelee.

Maendeleo ya Nchi tutayasikia kwenye bomba tu kwa aina hii ya unyonyaji isipokuwa mwenye nacho ataongezewa (be rich to get rich)

Kazi njema wajameni nilikuwa na frustrations zangu tu baada ya kupata report ya BOT.

"TUSIDANGANYWE TENA NCHI HII HAKUNA MZALENDO HATA MMOJA LABLA MIAKA 100 IJAYO NDIO WATAZALIWA."
Pale walipofuta pesa ya nyumba,likizo na malupulupu na kuzuia seminar,nikajua kazi ipo
 
MH. Raisi mwakani siku ya mei mosi tunaomba skeli ya mishahara ya watumishi ivunjwe ipangwe upya watumishi asilimia kubwa wanastaafu katika hali ya ufukara sana kwa kuwa kuna watumishi wameshaonekana wao ni wa mishahara ya chini wakiwemo walimu, sekta ya afya na kwengineko lakini kwa elimu hiyo hiyo aliyekuwa nayo huyo mtumishi anayeishi kwa shida kuna watumishi shida hawazijui kabisa kama waliopo kwenye mashirika ya selikari na viongozi yaani mtu anachukua 20ml kwa mwezi halafu kuna mtumishi anasuburi mshahara wa laki tatu kweli ina make sense tuwe wakweli jamani.
 
MH. Raisi mwakani siku ya mei mosi tunaomba skeli ya mishahara ya watumishi ivunjwe ipangwe upya watumishi asilimia kubwa wanastaafu katika hali ya ufukara sana kwa kuwa kuna watumishi wameshaonekana wao ni wa mishahara ya chini wakiwemo walimu, sekta ya afya na kwengineko lakini kwa elimu hiyo hiyo aliyekuwa nayo huyo mtumishi anayeishi kwa shida kuna watumishi shida hawazijui kabisa kama waliopo kwenye mashirika ya selikari na viongozi yaani mtu anachukua 20ml kwa mwezi halafu kuna mtumishi anasuburi mshahara wa laki tatu kweli ina make sense tuwe wakweli jamani.
Unadhani pale BOT au TRA kuba BAED tumia akili kingine izo kada hata mm nilitishwa ntakosa mkopo soma ualimu sijaenda nikakosa kweli japo sina ajira

Sasa mtu anasoma akibahatisha kweny izo sekta katusua waambie watoto wenu waache kukimbilia ualimu
 
Back
Top Bottom