Suleiman Kova: Mtu anayekuwa katika msongo wa mawazo anaweza kufanya kama Askofu Gwajima, hajiamini na haamini wengine

Suleiman Kova: Mtu anayekuwa katika msongo wa mawazo anaweza kufanya kama Askofu Gwajima, hajiamini na haamini wengine

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Suleiman Kova, kamanda wa polisi aliyewahi kutamba kwa kuzuia uhalifu akiwa RPC kwenye mikoa mbalimbali ameongelea hoja ya Gwajima kuomba mabadiliko ya mic na kiti. Amesema kwa uzoefu wake ndani ya Jeshi la Polisi na kuhoji watuhumiwa huwa ni suala la saikolojia kwa mtu mwenye msongo wa mawazo na kutojiamini yeye mwenyewe na kutoamini wengine.

Pia, soma=> Bungeni: Askofu Gwajima agoma kukalia kiti na kutumia kipaza sauti alichoandaliwa na Kamati ya Maadili

========

kamishna kova.jpg


Kamanda Mstaafu Kanda Maalum ya Dar es saalaam Kamishna Suleiman Kova leo kwenye Amplifaya ya Clouds FM ameelezea tukio la Mbunge wa Kawe Askofu Josephat Gwajima kuomba kubadilisha kiti na microphone vilivyokuwa vimeandaliwa kwa ajili yake kuvitumia wakati akihojiwa na Kamati ya Bunge Dodoma, Kova ameelezea tukio kama hili kwa kutumia uzoefu wake akiwa Polisi na kuhoji Watu mbalimbali wenye tuhuma.

"Wakati mwingine Mtu akishafanya jambo flani anakuwa na hisia flani ambazo sio za kawaida labda anafikiri nikikaa hapa naweza nikadhurika, ni tatizo la kisaikolojia kwa Mtu ambae ana msongo wa mawazo anakuwa hajiamini na haamini Mtu yeyote yule, kwahiyo anaweza kufanya jambo lolote lile”

"Mfano mimi zamani nilikuwa nahoji Wahalifu, akiletwa kwangu akisikia ni Kova anapoingizwa mule ndani anadondoka chini paap bila kumgusa, yani anaona amekutana na kitu cha hatari sana kutokana na yeye anavyoelewa, kama ni madhambi anayakumbuka yote"

Kamanda Mstaafu Kanda Maalum Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova.
 
Askofu tapeli, yaani haogopi Corona lakini anaogopa kiti na microphone!!! Watu wanaomfuata huyu jamaa na kusikiliza pumba zake ni wajinga zaidi yake yeye mwenyewe, serikali imefanya vyema kumpuuza, ukikimbizana na kichaa nawe utaonekana kichaa
 
Kwani Askofu kuonyesha msimamo wake kwenye chanjo ni dhambi?...

Yeye kaongea ila suala la kuchanja ama la linabaki kwa mtu binafsi. sasa shida ipo wapi?..

Tatizo la Uongozi Tanzania ni kubwa sana kwa sababu watu ni unqualified na hii inatokana na ukweli kwamba mchakato mzima wa kupata viongozi ni mbovu na haungalii merits bali ujanja ujanja na hii ni pande zote nikimaanisha Chama tawala na Opposition...ndio maana tuna viongozi very unpredictable and incompetent.

Nani asiyemjua Kova...? inachekesha sana.
 
Askofu tapeli, yaani haogopi Corona lakini anaogopa kiti na microphone!!! Watu wanaomfuata huyu jamaa na kusikiliza pumba zake ni wajinga zaidi yake yeye mwenyewe, serikali imefanya vyema kumpuuza, ukikimbizana na kichaa nawe utaonekana kichaa
Wewe na yeye nani mjinga!!
 
Si wanasema sumu haiwadhuru? Sasa Gwajima leo hayaamini maneno ya Biblia au mnaoutetea ujinga wake nanyi hamuiamini Biblia?

Marko 16:
15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
 
Kumbe Gwajima aliomba kutumia dawa kabla ya mahojiano kuanza, itakuwa pressure ilipanda, kwanini hakuomba ishuke? kuitwa kule sio kuzuri, ule ujuaji mwisho wake kanisani kwake.

Gwajima ni tapeli asiyemjua Yesu Kristu wala asiefuata mafundisho yake, ni msanii anaecheza na akili za wajinga kupata wafuasi, siwezi kum-support kwa kitu chochote.
 
Kumbe Gwajima aliomba kutumia dawa kabla ya mahojiano kuanza, itakuwa pressure ilipanda, kwanini hakuomba ishuke? kuitwa kule sio kuzuri, ule ujuaji mwisho wake kanisani kwake.

Gwajima ni tapeli asiyemjua Yesu Kristu wala asiefuata mafundisho yake, ni msanii anaecheza na akili za wajinga kupata wafuasi, siwezi kum-support kwa kitu chochote.
huenda ni kinga
 
Kwani Askofu kuonyesha msimamo wake kwenye chanjo ni dhambi?...
Yeye kaongea ila suala la kuchanja ama la linabaki kwa mtu binafsi...sasa shida ipo wapi?..
Tatizo la Uongozi Tanzania ni kubwa sana kwa sababu watu ni unqualified na hii inatokana na ukweli kwamba mchakato mzima wa kupata viongozi ni mbovu na haungalii merits bali ujanja ujanja na hii ni pande zote nikimaanisha Chama tawala na Opposition...ndio maana tuna viongozi very unpredictable and incompetent.
Nani asiyemjua Kova...inachekesha sana.
Hahaa! Hapa swala ni askofu kuogopa kiti na kamera. Haijawahi kutokea duniani.
 
Kumbe Gwajima aliomba kutumia dawa kabla ya mahojiano kuanza, itakuwa pressure ilipanda, kwanini hakuomba ishuke? kuitwa kule sio kuzuri, ule ujuaji mwisho wake kanisani kwake.

Gwajima ni tapeli asiyemjua Yesu Kristu wala asiefuata mafundisho yake, ni msanii anaecheza na akili za wajinga kupata wafuasi, siwezi kum-support kwa kitu chochote.
Wakati anamchambua Bashite mlimunga mkono. Sasa hapo nani mjinga kati yenu na Gwajima?

Wewe unamjua Yesu? Unamfuata? au kwa kuwa uko nyuma ya keyboard basi ni mwendo wa kukashifu tu. Unaweza hata kutaja mstari mmoja wa biblia bila kusoma?
 
Wakati anamchambua Bashite mlimunga mkono. Sasa hapo nani mjinga kati yenu na Gwajima?

Wewe unamjua Yesu? Unamfuata? au kwa kuwa uko nyuma ya keyboard basi ni mwendo wa kukashifu tu. Unaweza hata kutaja mstari mmoja wa biblia bila kusoma?
Inakuwaje ujibu comment yangu kwa kutumia wingi? simuwakilishi yeyote humu ndani.

Ndio namjua Yesu, ndio Namfuata, na ameniambia Gwajima sio Askofu ni tapeli.

Sio mstari mmoja, ninayo ya kutosha, ndio maana nasisitiza Gwajima sio Askofu anawadanganya wajinga kama wewe.
 
Suleiman Kova, kamanda wa polisi aliyewahi kutamba kwa kuzuia uhalifu akiwa na RPC kwenye mikoa mbalimbali ameongelea hoja ya Gwajima kuomba mabadiliko ya mic na kiti. Amesema kwa uzoefu wake ndani ya Jeshi la Polisi na kuhoji watuhumiwa huwa ni suala la saikolojia kwa mtu
Mtu yeyote yule angeweza kupata hisia tofauti na hatimaye kufanya kama vile ambavyo Askofu Gwajima alifanya. Yaani kiti kinaletwa kutoka katika mgahawa kikiwa line rasmi kwa ajili yake huku kikiwa tofauti kabisa na vingine vilivyokuwepo ndani ya kikao!
 
Si wanasema sumu haiwaduru? Sasa Gwajima leo hayaamini maneno ya Biblia au mnaoutetea ujinga wake nanyi hamuiamini Biblia?

Marko 16:
15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
Na maandiko hayo hayo yanasema watu wangu wanateketea kwa kukosa maarifa.

Alichofanya Gwajima ni maarifa ambayo hata kitabu kinashauri.
 
Back
Top Bottom