Suleiman Kova: Mtu anayekuwa katika msongo wa mawazo anaweza kufanya kama Askofu Gwajima, hajiamini na haamini wengine

Suleiman Kova: Mtu anayekuwa katika msongo wa mawazo anaweza kufanya kama Askofu Gwajima, hajiamini na haamini wengine

Suleiman Kova, kamanda wa polisi aliyewahi kutamba kwa kuzuia uhalifu akiwa na RPC kwenye mikoa mbalimbali ameongelea hoja ya Gwajima kuomba mabadiliko ya mic na kiti. Amesema kwa uzoefu wake ndani ya Jeshi la Polisi na kuhoji watuhumiwa huwa ni suala la saikolojia kwa mtu mwenye msongo wa mawazo na kutojiamini yeye mwenyewe na kutoamini wengine.

Pia, soma=> Bungeni: Askofu Gwajima agoma kukalia kiti na kutumia kipaza sauti alichoandaliwa na Kamati ya Maadili

========



Kamanda Mstaafu Kanda Maalum ya Dar es saalaam Kamishna Suleiman Kova leo kwenye Amplifaya ya Clouds FM ameelezea tukio la Mbunge wa Kawe Askofu Josephat Gwajima kuomba kubadilisha kiti na microphone vilivyokuwa vimeandaliwa kwa ajili yake kuvitumia wakati akihojiwa na Kamati ya Bunge Dodoma, Kova ameelezea tukio kama hili kwa kutumia uzoefu wake akiwa Polisi na kuhoji Watu mbalimbali wenye tuhuma.

"Wakati mwingine Mtu akishafanya jambo flani anakuwa na hisia flani ambazo sio za kawaida labda anafikiri nikikaa hapa naweza nikadhurika, ni tatizo la kisaikolojia kwa Mtu ambae ana msongo wa mawazo anakuwa hajiamini na haamini Mtu yeyote yule, kwahiyo anaweza kufanya jambo lolote lile”

"Mfano mimi zamani nilikuwa nahoji Wahalifu, akiletwa kwangu akisikia ni Kova anapoingizwa mule ndani anadondoka chini paap bila kumgusa, yani anaona amekutana na kitu cha hatari sana kutokana na yeye anavyoelewa, kama ni madhambi anayakumbuka yote"

Kamanda Mstaafu Kanda Maalum Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova.
Kova anasaka uteuzi.
 
Wewe umekariri vifungu vya Biblia, huna taaluma ya kuhuisha wala kufafanua hivyo vifungu.
Si wanasema sumu haiwaduru? Sasa Gwajima leo hayaamini maneno ya Biblia au mnaoutetea ujinga wake nanyi hamuiamini Biblia?

Marko 16:
15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
 
Suleiman Kova, kamanda wa polisi aliyewahi kutamba kwa kuzuia uhalifu akiwa na RPC kwenye mikoa mbalimbali ameongelea hoja ya Gwajima kuomba mabadiliko ya mic na kiti. Amesema kwa uzoefu wake ndani ya Jeshi la Polisi na kuhoji watuhumiwa huwa ni suala la saikolojia kwa mtu mwenye msongo wa mawazo na kutojiamini yeye mwenyewe na kutoamini wengine.

Pia, soma=> Bungeni: Askofu Gwajima agoma kukalia kiti na kutumia kipaza sauti alichoandaliwa na Kamati ya Maadili

========



Kamanda Mstaafu Kanda Maalum ya Dar es saalaam Kamishna Suleiman Kova leo kwenye Amplifaya ya Clouds FM ameelezea tukio la Mbunge wa Kawe Askofu Josephat Gwajima kuomba kubadilisha kiti na microphone vilivyokuwa vimeandaliwa kwa ajili yake kuvitumia wakati akihojiwa na Kamati ya Bunge Dodoma, Kova ameelezea tukio kama hili kwa kutumia uzoefu wake akiwa Polisi na kuhoji Watu mbalimbali wenye tuhuma.

"Wakati mwingine Mtu akishafanya jambo flani anakuwa na hisia flani ambazo sio za kawaida labda anafikiri nikikaa hapa naweza nikadhurika, ni tatizo la kisaikolojia kwa Mtu ambae ana msongo wa mawazo anakuwa hajiamini na haamini Mtu yeyote yule, kwahiyo anaweza kufanya jambo lolote lile”

"Mfano mimi zamani nilikuwa nahoji Wahalifu, akiletwa kwangu akisikia ni Kova anapoingizwa mule ndani anadondoka chini paap bila kumgusa, yani anaona amekutana na kitu cha hatari sana kutokana na yeye anavyoelewa, kama ni madhambi anayakumbuka yote"

Kamanda Mstaafu Kanda Maalum Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova.
Shallow explanation, watu wana reference ya CCM kuwadhuru wanaopingana nao. Wanakumbuka yaliyompata Kolimba aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM. Alihojiwa na kufa baada ya mahojiano and it is said alipewa sumu kwenye kikao hicho. Mwenye akili utakataa kiti na mic ambavyo utavigusa katika mahojiano.

Gwajima was right!
 

"Mfano mimi zamani nilikuwa nahoji Wahalifu, akiletwa kwangu akisikia ni Kova anapoingizwa mule ndani anadondoka chini paap bila kumgusa, yani anaona amekutana na kitu cha hatari sana kutokana na yeye anavyoelewa, kama ni madhambi anayakumbuka yote"

Kamanda Mstaafu Kanda Maalum Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova.
Aisee. Alikuwa anawafanya je?
 
Kuna kitu Kova haelewi na wengi wanashindwa kuelewa...

Watu wenye jicho la tatu wanaweza kuelewa kwa nini mtukutu Gwajima aliomba kiti na mic vibadilishwe...tena ingewezekana hata ukumbi angeomba ubadilishwe
 
Inawezekana Kova yuko sahihi kwenye saikolojia ya mtu anapokua anahojiwa lakini suala la kuangalia ni malengo ya vitendo anavyofanya mtu akiwa anahojiwa kwa uzoefu wake yeye anasema kuwa ni kutokujiamini au kumuamini mtu yoyote, vipi kwa wale wenye akili nyingi wanaojua kucheza na saikologia ya mtu mwingine maana mahojiano ni mbinu na maarifa Kama ilivyo kwa paka na panya yaani kuna mmoja anataka kuchomoka mwingine anataka kubana. Mi nadhani kwa upande mwingine Askofu alifanya vile kama mbinu ya kucheza na akili za wanakamati na wale waliohudhuria, inaweza ikawa katika kupunguza tension na kudivert mawazo ya watu kutoka kwenye msingi wa mahojiano maana watu kama wale wanaocheza na akili za watu wengi kila siku sio kuwachukulia polepole ndio maana mpaka Sasa hivi watu hawajadili content ya mahojiano wanajadili aliyofanya Askofu 😄😄 human brain is very complex thing....
 
Si wanasema sumu haiwaduru? Sasa Gwajima leo hayaamini maneno ya Biblia au mnaoutetea ujinga wake nanyi hamuiamini Biblia?

Marko 16:
15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
Karibu tena
 
Si wanasema sumu haiwaduru? Sasa Gwajima leo hayaamini maneno ya Biblia au mnaoutetea ujinga wake nanyi hamuiamini Biblia?

Marko 16:
15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
Alienda kuhuburi injili pale?
 
Wakati anamchambua Bashite mlimunga mkono. Sasa hapo nani mjinga kati yenu na Gwajima?

Wewe unamjua Yesu? Unamfuata? au kwa kuwa uko nyuma ya keyboard basi ni mwendo wa kukashifu tu. Unaweza hata kutaja mstari mmoja wa biblia bila kusoma?
Kwako kukariri vifungu vya biblia ndio kumfuata yesu?
Hizi akili za wapi hizi kwako mtu asiyekariri hata kifungu kimoja hamfuati??
 
kasema kwel lkn Kova kajipangaje, hakika Jumapili siwezi kukosa ibada
 
Askofu tapeli, yaani haogopi Corona lakini anaogopa kiti na microphone!!! Watu wanaomfuata huyu jamaa na kusikiliza pumba zake ni wajinga zaidi yake yeye mwenyewe, serikali imefanya vyema kumpuuza, ukikimbizana na kichaa nawe utaonekana kichaa
Endelea kumuona hana akili kubadilisha kiti na microphone 🎤, Tz na historia yake utakuwa huijui vizuri wewe
 
Si wanasema sumu haiwadhuru? Sasa Gwajima leo hayaamini maneno ya Biblia au mnaoutetea ujinga wake nanyi hamuiamini Biblia?

Marko 16:
15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
Hakuna mtumishi hapo blah bhah tu

Sent from my CPH2185 using JamiiForums mobile app
 
Shallow explanation, watu wana reference ya CCM kuwadhuru wanaopingana nao. Wanakumbuka yaliyompata Kolimba aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM. Alihojiwa na kufa baada ya mahojiano and it is said alipewa sumu kwenye kikao hicho. Mwenye akili utakataa kiti na mic ambavyo utavigusa katika mahojiano.

Gwajima was right!
Vitoto vingi havijui historia yetu, pamoja na mambo yake Gwaji boy.....ila hilo alichanga karata zake vizuri.....sasa Kova anafananisha na wale wezi alikuwa anawatisha hata kwa marungu ili waseme ndiyo hata kama siyo
 
Inakuwaje ujibu comment yangu kwa kutumia wingi? simuwakilishi yeyote humu ndani.

Ndio namjua Yesu, ndio Namfuata, na ameniambia Gwajima sio Askofu ni tapeli.

Sio mstari mmoja, ninayo ya kutosha, ndio maana nasisitiza Gwajima sio Askofu anawadanganya wajinga kama wewe.
Kama unadai Mungu amekuambia hiyo ni uthibitisho kuwa wewe ni zaidi ya tapeli. Bahati mimi ni mkristo tena mfuasi wa kanisa pekee aliloliasisi Kristu mwenyewe sio hayo ya mifukoni au yaliyoanzishwa kutokana na uzinzi au njaa za wanadamu ninauelewa ukristo.
 
Kwako kukariri vifungu vya biblia ndio kumfuata yesu?
Hizi akili za wapi hizi kwako mtu asiyekariri hata kifungu kimoja hamfuati??
Kama hujui hata mstari mmoja wa biblia huo ujasiri wa kumshambulia Gwajima unautoa wapi? Kati yako na yeye nani walau anaijua biblia?

Wewe unao wafuasi wowote kama Gwajima ambaye miongoni mwa wafuasi wake wako kuanzia PhD holders mpaka darasa la saba tena ndani na nje ya nchi ikiwemo huko western countries. Pengina hata wanafamilia yako tu hawakukubali. Wewe sio size ya Gwajima kwa kila hali.
 
Back
Top Bottom