Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Kuna kitu cha kutusaidia hapa kiongozi
britanicca instanbul Laki Si Pesa
Chillah,
Kwanza nakushukuru kwa kutuwekea Medali ya Mwenge wa Uhuru ya Mzee Suedi Kagasheki.

Nimefahamiana na mwanae Balozi Abdallah Kagasheki kuanzia miaka ya 1980 alipokuwa Balozi Saudi Arabia na nikimtembelea nyumbani kwake Upanga Dar es Salaam kila alipokuwa likizo na niliwahi mwaka wa 2000 kufika nyumbani kwake Bukoba lakini bahati mbaya alikuwa amesafiri kwa hiyo hatukuonana.

Nimejuana vilevile na wajukuu wa Mzee Suedi Kagasheki yaani watoto wa Balozi Abdallah Suedi.
Nimemtaja Mzee Suedi Kagasheki katika kitabu cha Abdul Sykes na naweka hapo chini sehemu hizo:
1951
''Dr Mutahangarwa alikuwa Mwafrika wa kwanza kufuzu udaktari.​
Baada ya kuelezwa kuhusu ule mkutano wa Arusha, Dr Mutahangarwa alimwonya Dossa kuhusu hatari ya mwenendo aliokuwa akichukua Abdulwahid kama Katibu na Rais wa TAA.​
Dr Mutahangarwa alimweleza Dossa hatari ambazo TAA na uongozi wake ungezikabili pindi serikali ikigundua kwamba TAA ilikuwa ikijaribu kuunganisha mapambano ya TAA na yale ya KAU.​
Hofu hii aliyoonyesha Dr Mutahangarwa ilikuwa bila wasiwasi wowote hofu ya kweli kabisa kwa sababu KAU ilikuwa inaunga mkono harakati za Mau Mau na Waingereza waliamini kuwa uongozi wa mapambano yale ulikuwa ukitoka KAU na Kenyatta wakiwa na Kaggia walishukiwa kuwa kati ya viongozi hao.​
Kutoka Mwanza Dossa alipanda meli hadi Bukoba ambako alipokewa na Chifu Rutinwa pamoja na mwanasiasa mkongwe, Ally Migeyo na Suedi Kagasheki na wanachama wengine wa TAA katika tawi la Bukoba.​
Aliporudi Dar es Salaam, Dossa alikamatwa katika stesheni ya gari moshi na kupelekwa Central Police.''​

1967
''Mwezi Novemba 1967 Tewa Said Tewa alikuwa amefanya ziara ya Mwanza na Bukoba iliyokuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa alifanya majadiliano na viongozi wa Waislam wa huko kama Sheikh Amin Abdallah wa Mwanza, Sheikh Ali Migeyo na Sheikh Suedi Kagasheki wa Bukoba.''​
 
Chillah,
Kwanza nakushukuru kwa kutuwekea Medali ya Mwenge wa Uhuru ya Mzee Suedi Kagasheki.

Nimefahamiana na mwanae Balozi Abdallah Kagasheki kuanzia miaka ya 1980 alipokuwa Balozi Saudi Arabia na nikimtembelea nyumbani kwake Upanga Dar es Salaam kila alipokuwa likizo na niliwahi mwaka wa 2000 kufika nyumbani kwake Bukoba lakini bahati mbaya alikuwa amesafiri kwa hiyo hatukuonana.

Nimejuana vilevile na wajukuu wa Mzee Suedi Kagasheki yaani watoto wa Balozi Abdallah Suedi.
Nimemtaja Mzee Suedi Kagasheki katika kitabu cha Abdul Sykes na naweka hapo chini sehemu hizo:
1951
''Dr Mutahangarwa alikuwa Mwafrika wa kwanza kufuzu udaktari.​
Baada ya kuelezwa kuhusu ule mkutano wa Arusha, Dr Mutahangarwa alimwonya Dossa kuhusu hatari ya mwenendo aliokuwa akichukua Abdulwahid kama Katibu na Rais wa TAA.​
Dr Mutahangarwa alimweleza Dossa hatari ambazo TAA na uongozi wake ungezikabili pindi serikali ikigundua kwamba TAA ilikuwa ikijaribu kuunganisha mapambano ya TAA na yale ya KAU.​
Hofu hii aliyoonyesha Dr Mutahangarwa ilikuwa bila wasiwasi wowote hofu ya kweli kabisa kwa sababu KAU ilikuwa inaunga mkono harakati za Mau Mau na Waingereza waliamini kuwa uongozi wa mapambano yale ulikuwa ukitoka KAU na Kenyatta wakiwa na Kaggia walishukiwa kuwa kati ya viongozi hao.​
Kutoka Mwanza Dossa alipanda meli hadi Bukoba ambako alipokewa na Chifu Rutinwa pamoja na mwanasiasa mkongwe, Ally Migeyo na Suedi Kagasheki na wanachama wengine wa TAA katika tawi la Bukoba.​
Aliporudi Dar es Salaam, Dossa alikamatwa katika stesheni ya gari moshi na kupelekwa Central Police.''​

1967
''Mwezi Novemba 1967 Tewa Said Tewa alikuwa amefanya ziara ya Mwanza na Bukoba iliyokuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa alifanya majadiliano na viongozi wa Waislam wa huko kama Sheikh Amin Abdallah wa Mwanza, Sheikh Ali Migeyo na Sheikh Suedi Kagasheki wa Bukoba.''​
Nashukuru kwa historia hii... Naomba kuja ma swali mengine ambayo yatanisaidia kupata kujua zaidi historia ya nchi yetu
 
Chillah,
Kwanza nakushukuru kwa kutuwekea Medali ya Mwenge wa Uhuru ya Mzee Suedi Kagasheki.

Nimefahamiana na mwanae Balozi Abdallah Kagasheki kuanzia miaka ya 1980 alipokuwa Balozi Saudi Arabia na nikimtembelea nyumbani kwake Upanga Dar es Salaam kila alipokuwa likizo na niliwahi mwaka wa 2000 kufika nyumbani kwake Bukoba lakini bahati mbaya alikuwa amesafiri kwa hiyo hatukuonana.

Nimejuana vilevile na wajukuu wa Mzee Suedi Kagasheki yaani watoto wa Balozi Abdallah Suedi.
Nimemtaja Mzee Suedi Kagasheki katika kitabu cha Abdul Sykes na naweka hapo chini sehemu hizo:
1951
''Dr Mutahangarwa alikuwa Mwafrika wa kwanza kufuzu udaktari.​
Baada ya kuelezwa kuhusu ule mkutano wa Arusha, Dr Mutahangarwa alimwonya Dossa kuhusu hatari ya mwenendo aliokuwa akichukua Abdulwahid kama Katibu na Rais wa TAA.​
Dr Mutahangarwa alimweleza Dossa hatari ambazo TAA na uongozi wake ungezikabili pindi serikali ikigundua kwamba TAA ilikuwa ikijaribu kuunganisha mapambano ya TAA na yale ya KAU.​
Hofu hii aliyoonyesha Dr Mutahangarwa ilikuwa bila wasiwasi wowote hofu ya kweli kabisa kwa sababu KAU ilikuwa inaunga mkono harakati za Mau Mau na Waingereza waliamini kuwa uongozi wa mapambano yale ulikuwa ukitoka KAU na Kenyatta wakiwa na Kaggia walishukiwa kuwa kati ya viongozi hao.​
Kutoka Mwanza Dossa alipanda meli hadi Bukoba ambako alipokewa na Chifu Rutinwa pamoja na mwanasiasa mkongwe, Ally Migeyo na Suedi Kagasheki na wanachama wengine wa TAA katika tawi la Bukoba.​
Aliporudi Dar es Salaam, Dossa alikamatwa katika stesheni ya gari moshi na kupelekwa Central Police.''​

1967
''Mwezi Novemba 1967 Tewa Said Tewa alikuwa amefanya ziara ya Mwanza na Bukoba iliyokuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa alifanya majadiliano na viongozi wa Waislam wa huko kama Sheikh Amin Abdallah wa Mwanza, Sheikh Ali Migeyo na Sheikh Suedi Kagasheki wa Bukoba.''​

Huyu mjukuu wa Dr Mutahangarwa kajaribu kueleza kidogo historia yao...
 
Chilla,
Vitabu hivi utavipata Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Mtoro na Manyema na pia Msikiti wa Mtambani kuna vya Kiingereza na Kiswahili bei elfu kumi tu.
Kwanini vitabu vyako unauza misikitini ?
Uza kwenye maduka ya kawaida pia, au walengwa no waislamu wenzio?
 
Kwanini vitabu vyako unauza misikitini ?
Uza kwenye maduka ya kawaida pia, au walengwa no waislamu wenzio?
Remote,
Ibn Hazm ndiyo waliochapa kitabu hiki na wao wana maduka yao hayo ambayo hayako msikitini kama unavyodhani ni kama mfano wa Cathedral Bookshop pale St. Josephs' kwani duka hili lipo kanisani?

Cathedral Bookshop lipo pembeni ya kanisa na haya maduka yetu pia ni hivyo hivyo unaweza tu kufika Mtaa wa Mafia Msikiti wa Manyema utauona kwa pembeni na hivyo hivyo Mtoro na Mtambani.

Wanapenda kuuza vitabu vyao kwenye maduka mengine ya vitabu lakini hawataki kuchukua vitabu vyetu basi ndiyo tunauza kwenye maduka yetu.

Tanzania Publishing House huwa wanachukua vitabu vyetu, Soma Bookshop na Elite Bookshop lakini biashara ya vitabu ni ngumu sana.
 
Remote,
Ibn Hazm ndiyo waliochapa kitabu hiki na wao wana maduka yao hayo ambayo hayako msikitini kama unavyodhani ni kama mfano wa Cathedral Bookshop pale St. Josephs' kwani duka hili lipo kanisani?

Cathedral Bookshop lipo pembeni ya kanisa na haya maduka yetu pia ni hivyo hivyo unaweza tu kufika Mtaa wa Mafia Msikiti wa Manyema utauona kwa pembeni na hivyo hivyo Mtoro na Mtambani.

Wanapenda kuuza vitabu vyao kwenye maduka mengine ya vitabu lakini hawataki kuchukua vitabu vyetu basi ndiyo tunauza kwenye maduka yetu.

Tanzania Publishing House huwa wanachukua vitabu vyetu, Soma Bookshop na Elite Bookshop lakini biashara ya vitabu ni ngumu sana.
Asante nitapita hapo.
 
Gazeti la Hoja (Ijumaa, 22- 26, Novembe 2019) kuna makala ya Suleiman Kumchaya kuhusu historia ya TAA na TANU ambayo ina makosa sawasawa na makosa katika makala ya Mzee Pius Msekwa iliyochapwa katika gazeti la TAZAMA kiasi cha majuma mawili yaliyopita.

Suleiman Kumchaya anasema kuwa Julius Nyerere alipokuwa Makerere alikuwa anawasiliana na wazee wa Dar es Salaam akiwataka waanzishe chama cha siasa.

Ukisoma makala hizi mbili utazania ni jibu la mtihani la wanafunzi wawili watukutu walioangaliana mtihani jambo amabalo mwalimu hodari ataligundua mara moja katika kusahihisha.

Suleiman Kumchaya karudia maneno ya Mzee Msekwa kuwa TAA kazi yake ilikuwa, ''kutetea maslahi ya wafanyakazi Waafrika,'' na Julius Nyerere ndiye aliyeibadilisha TAA kuwa, ''chama cha siasa cha kudai uhuru,'' kazi ambayo aliifanya kwa kushirikiana na ''wazee wa pwani.''

Maneno haya yote ya Kumchaya hayana ushahidi katika historia ya uhuru wa Tanganyika na nathubutu kusema kuwa Kumchaya haijui historia ya TANU na inashangaza sana katika historia ya TANU kwa kila aizungumzae atataja, ''wazee,' ambao hawana majina kama vile hakuna awajuae.

Nyerere kabla hajafika Dar es Salaam hakuwa anajuana na mzee yeyote katika wazee wa Dar es Salaam ambao walikuwa katika siasa kwa hiyo hakuwa anaandikiana barua na mzee yoyote kuwataka waunde chama cha siasa.

Nyerere alikuja kujuana na wazee wa Dar es Salaam baada ya yeye kujuana na Abdul Sykes mwaka wa 1952 na kugombea nafasi ya urais dhidi ya Abdul Sykes katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 na kushinda.

Kuanzia mwaka huu wa 1953 ndiyo Abdul Sykes akamjulisha Nyerere kwa wazee wa Dar es Salaam kuanzia na Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Jumbe Tambaza, Mshume Kiyate, Sheikh Suleiman Takadir na Said Chamwenyewe kwa kuwataja wachache na hii kazi ya kumtambulisha Nyerere kwa wazee na masheikh maarufu wa Dar es Salaam ilifanywa vilevile na ndugu wawili, Iddi Faiz Mafungo na nduguye Iddi Tosiri kwa kumpeleka Nyerere Bagamoyo kumtambulisha kwa Sheikh Mohamed Ramiya ambae wao alikuwa binamu yao.

Kila anaejisikia kuwataja ''wazee,'' utasikia, ''wazee'' lakini majina yao hayatajwi.
Kwa nini iwe hivi?

Historia ya TANU nimeieleza mara nyingi hapa kiasi naona tabu kuirudia tena.

Katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 Nyerere aliingia katika uongozi na timu ya vijana watupu kama Abdul Sykes, Ally Sykes Tewa Said Tewa, Dossa Aziz, Joseph Kasella Bantu, Dome Budohi kwa kuwataja vijana wachache na mzee katika timu hiyo alikuwa John Rupia.

Wazee wa mwisho katika uongozi awamu yao ilikwisha mwaka wa 1950 baada ya mapinduzi yaliyofanywa na Abdul Sykes na Hamza Mwapachu yaliyowatoa madarakani Thomas Plantan na Clement Mtamila na nafasi zao za urais na katibu kuchukuliwa na Dr. Vedasto Kyaruzi kama Rais na Abdul Sykes Katibu.

Inaelekea Kumchaya kama Mzee Msekwa haijui historia hii na ndiyo sababu ya haya makosa ambayo kwa hakika hayana sababu ya kufanywa.

Hawa wangejitahidi lau kufanya utafiti kidogo katika Maktaba ya CCM wangelikuta pale Dodoma kuna majalada ya Hamza Mwapachu, Abdul Sykes na ya wazalendo wengine ingawa ndani hakuna nyaraka majalada ni matupu.

Mimi katika utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes nimefika hapo.

Wangeanzia hapo wangeweza lau kwa uchache kupata historia ya TANU na wagelijua kuwa historia ya TANU inaanza na historia ya African Association chama kilichoundwa na Kleist Sykes mwaka wa 1929 na katika uasisi wa TANU wanae wawili Abdul na Ally Sykes walishiriki na wana historia ndefu ya chama hicho kushinda Julius Nyerere.

Wangelijua pia kuwa Abdul alifanya mazungumzo na Chief David Kidaha Makwaia kuanzia 1951 wakijadiliana kuhusu kuasisi TANU mazungumzo ambayo Abdul alikuwanayo na Hamza Mwapachu kwa miaka mingi na ilikuwa Hamza ndiye aliyemleta Nyerere katika harakati za TAA Dar es Salaam kuishia na Nyerere kuchaguliwa kuwa kiongozi wa TANU mwaka wa 1954 na kukabidhiwa jukumu la kuongoza mapambano ya kudai uhuru.

Jambo la kuhuzunisha katika magazeti haya ni kuwa baada ya kuandika makosa na mtu akasahihisha na kuwapelekea makala wanakataa kuchapa makala hizo wakitaka wabakie na historia ile rasmi yenye makosa.

Hakika huu ni msiba mkubwa pasi na mfano katika historia ya nchi yetu.
Mohamed usilazimishe kuwa wewe ndiye mwenye hati miliki ya historia ya TAA,TANU nk..
 
Mohamed usilazimishe kuwa wewe ndiye mwenye hati miliki ya historia ya TAA,TANU nk..
Wakuku...
Hapana siwezi kulazimisha ila ukweli na hiki ndicho ninachoringia ni kuwa mimi ndiye wa mwanzo kusema kuwa hii historia inayosomeshwa na watu wakaiamini si historia ya kweli ya TANU na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Nikaandika kitabu kueleza historia yenyewe kama ilivyotakiwa kuandikwa.

Lakini kubwa ndiye mtafiti pekee ukimtoa John Iliffe ambae nimeziona na kusoma Nyaraka za Sykes.

Umuhimu wa hili ni kuwa wao ndiyo waasisi wa African Association na waasisi wa TANU na ndiyo waliompokea Mwalimu Nyerere.
 
Back
Top Bottom