Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Nyerere ndio alie itransform TAA kutoka chama kisichoeleweka mpaka kuwa chama "serious" cha kupigania uhuru na mpaka katiba ya TAA kaiandika Nyerere. TAA ya Abdul Sykes haikuwa na katiba
 
Nyerere ndio alie itransform TAA kutoka chama kisichoeleweka mpaka kuwa chama "serious" cha kupigania uhuru na mpaka katiba ya TAA kaiandika Nyerere. TAA ya Abdul Sykes haikuwa na katiba[/QUOTE]Laki...
Unakusudia katiba ya TAA au ya TANU?
Ungesema hivi ingekuwa vizuri zaidi ungesema, "TAA ya baba yake Abdul," kwa kuwa African Association aliasisi baba yake Kleist Sykes 1929.

Ingekuwa baba kamuachia mwana chama kisichoeleweka na kisichokuwa na katiba.
Hivi ungefikisha ujumbe vizuri zaidi.
 
Laki...
Unakusudia katiba ya TAA au ya TANU?
Ungesema hivi ingekuwa vizuri zaidi ungesema, "TAA ya baba yake Abdul," kwa kuwa African Association aliasisi baba yake Kleist Sykes 1929.

Ingekuwa baba kamuachia mwana chama kisichoeleweka na kisichokuwa na katiba.

Hivi ungefikisha ujumbe vizuri zaidi.
Lakini Abdul Sykes wakati alipokuwa kiongozi wa TAA hakuona umuhimu wa kuandika katiba, mpaka alipochaguliwa Nyerere kuwa kiongoz wa TAA ndipo akaandika katiba, hapo ndipo utakapojua Nyerere ndio alikuwa "king maker" wa TAA, ndio alioamsha ari ya kudai uhuru. bila Nyerere TAA isingefika popote
 
Lakini Abdul Sykes wakati alipokuwa kiongozi wa TAA hakuona umuhimu wa kuandika katiba, mpaka alipochaguliwa Nyerere kuwa kiongoz wa TAA ndipo akaandika katiba, hapo ndipo utakapojua Nyerere ndio alikuwa "king maker" wa TAA, ndio alioamsha ari ya kudai uhuru. bila Nyerere TAA isingefika popote
Laki...
Hii ya kuwa TAA haikuwa na katiba na katiba kaja kuiandika Nyerere wewe hii umeipata wapi?
Ikiwa umesoma mahali tafadhali hebu tupe rejea yake.

Baada ya hayo ndiyo In Shaa Allah tuje kwenye, ''king maker.''
Tusitangulize kwama punda akaja nyuma.
 
Hotuba hii ya Nyerere inajibu vipi tuhuma dhidi yake kwamba amepindisha na kuficha historia ya ukombozi Tanzania?
Kiranga,
Nataabika sana nafsi yangu kupitia maneno hayo hapo chini:

"Mimi nimeanza siasa na Wazee wa Dar es Salaam. Nimeanza nao mapema sana; mapema kweli. Nilirudi kutoka masomoni, Uingereza Oktoba 1952 – miaka 33 nyuma. Wakati huo nikiwa kijana mdogo wa miaka thelathini na kidogo hivi.''

Swali litakuwa aliwajuaje hawa wazee?
Kafika Pugu kawatafuta katika mitaa ya Dar es Salaam?

Wazee wa Dar es Salaam waliokuwa katika siasa wanafahamika na nitawataja wachache.

Kulikuwa na Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Said Chaurembo na John Rupia ambao walikuwa katika TAA Political Subcommittee toka mwaka wa 1950.

Nitawataja wengine ambao hawa walikuwa wanachama shupavu wa TAA na baadhi walihudhuria katika mkutano wa kwanza wa TANU August 1954 - Iddi Faiz Mafungo na ndugu yake Iddi Tosiri na kulikuwa na Sheikh Suleiman Takadir, Mshume Kiyate, Iddi Tulio, Issa Nasir, Abdallah Shomari, Jumbe Tambaza, Rajab Simba, Boi Singizi, Said Chamwenyewe na wengineo wengi.

Hawa wazee aliwajua vipi hadi akawaamini na wao wakamuamini katika jambo kubwa kama lile la kuunda chama cha siasa na kudai uhuru?

Haiyumkiniki hata kidogo kuwa hakupelekwa na mtu kwenda kujulishwa na kuwa ati alikwenda mwenyewe kama mwanasiasa.

Mambo hayakuwa yanaendeshwa hivyo.

Dar es Salaam ya miaka ile bila wasta hufiki popote na wala huna atakaekupokea.

Sina haja ya kueleza nafasi ya Hamza Mwapachu kwa Mwalimu katika siasa hizi bandiko litakuwa refu sana.

Hao wazee hapo chini wote walikuwa wanachama wa TAA wengine toka enzi za African Association wakati ikiongozwa na Kleist Sykes na wakaja pia kuwa chini ya uongozi wa Abdul Sykes baada ya kifo cha baba yake 1949 na walikuwanae katika Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na katika mambo mengi ya mjini achilia mbali kuwa wengine walikuwa na biashara zao Kariakoo Market ambako Abdul ndiye alikuwa Market Master.

Baadhi ya wazee hawa Mwalimu Nyerere aliwajua pale Kariakoo Market alipokuwa akienda mara kwa mara kumuona Abdul Sykes na mmoja katika hawa ambao wakajakuwa karibu sana ni Mzee Mshume Kiyate na Shariff Abdallah Attas.

Historia hii inafahamika vyema sana na watu wa Dar es Salaam wa miaka ile.


1574787001269.png
 
Kiranga,
Nataabika sana nafsi yangu kupitia maneno hayo hapo chini:

"Mimi nimeanza siasa na Wazee wa Dar es Salaam. Nimeanza nao mapema sana; mapema kweli. Nilirudi kutoka masomoni, Uingereza Oktoba 1952 – miaka 33 nyuma. Wakati huo nikiwa kijana mdogo wa miaka thelathini na kidogo hivi.''

Swali litakuwa aliwajuaje hawa wazee?
Kafika Pugu kawatafuta katika mitaa ya Dar es Salaam?

Wazee wa Dar es Salaam waliokuwa katika siasa wanafahamika na nitawataja wachache.

Kulikuwa na Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Said Chaurembo na John Rupia ambao walikuwa katika TAA Political Subcommittee toka mwaka wa 1950.

Nitawataja wengine ambao hawa walikuwa wanachama shupavu wa TAA na baadhi walihudhuria katika mkutano wa kwanza wa TANU August 1954 - Iddi Faiz Mafungo na ndugu yake Iddi Tosiri na kulikuwa na Sheikh Suleiman Takadir, Mshume Kiyate, Iddi Tulio, Issa Nasir, Abdallah Shomari, Jumbe Tambaza, Rajab Simba, Boi Singizi, Said Chamwenyewe na wengineo wengi.

Hawa wazee aliwajua vipi hadi akawaamini na wao wakamuamini katika jambo kubwa kama lile la kuunda chama cha siasa na kudai uhuru?

Haiyumkiniki hata kidogo kuwa hakupelekwa na mtu kwenda kujulishwa na kuwa ati alikwenda mwenyewe kama mwanasiasa.

Mambo hayakuwa yanaendeshwa hivyo.
Dar es Salaam ya miaka ile bila wasta hufiki popote na wala huna atakaekupokea.

Sina haja ya kueleza nafasi ya Hamza Mwapachu kwa Mwalimu katika siasa hizi bandiko litakuwa refu sana.

Hao wazee hapo chini wote walikuwa wanachama wa TAA wengine toka enzi za African Association wakati ikiongozwa na Kleist Sykes na wakaja pia kuwa chini ya uongozi wa Abdul Sykes baada ya kifo cha baba yake 1950 na walikuwanae katika Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na katika mambo mengi ya mjini achilia mbali kuwa wengine walikuwa na biashara zao Kariakoo Market ambako Abdul ndiye alikuwa Market Master.

Baadhi ya wazee hawa Mwalimu Nyerere aliwajua pale Kariakoo Market alipokuwa akienda mara kwa mara kumuona Abdul Sykes na mmoja katika hawa ambao wakajakuwa karibu sana ni Mzee Mshume Kiyate na Shariff Abdallah Attas.

Historia hii inafahamika vyema sana na watu wa Dar es Salaam wa miaka ile.


Sasa hujaona hapo amesema Kasela Bantu ndiye aliyempeleka kwa Sykes, na hapo ndipo akapata kujuana na wazee?

Nashangaa unaandika kama Nyerere anaficha historia hii, wakati mwenyewe kasema haya kwenye hotuba hii?

Kataja mpaka machimbo aliyokuwa akifukizwa na wazee, kwa kisomo cha Quran na cha njia za jadi!
 
Sasa hujaona hapo amesema Kasela Bantu ndiye aliyempeleka kwa Sykes, na hapo ndipo akapata kujuana na wazee?

Nashangaa unaandika kama Nyerere anaficha historia hii, wakati mwenyewe kasema haya kwenye hotuba hii?

Kataja mpaka machimbo aliyokuwa akifukizwa na wazee, kwa kisomo cha Quran na cha njia za jadi!
Kiranga,
Hajasema kitu hapo.

Kusema angesema kuwa kamsikia Abdul kutoka kwa Hamza Mwapachu.

Kusema angesema aligombea nafasi ya urais wa TAA dhidi ya Abdul Ukumbi wa Arnautoglo na akashinda Abdul akawa makamo wa Rais.

Kusema angesema kiongozi wa wazee wote wa Dar es Salaam alikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na waliompeleka kwake ni Abdul Sykes na Dossa Aziz.

Kusema angesema kwa kuwatambua wazee kwa majina yao.

Hizi dua nadhani Mwalimu anadhani yeye wa kwanza kufanyiwa na wazee.

In Shaa Allah ikitokea fursa nitazieleza dua zote kuanzia ile ya Abdul alipovamiwa ofisini na Town Clerk Mzungu anauza kadi za TANU.

Sakata hili wazee wakuamua kutawaswil kwa Allah Abdul anusurike asifukuzwe kazi.
Kuna kisoma cha Rashid Ali Meli.

Kuna mambo mengi sana sikutaka kuyaandika katika kitabu cha Abdul Sykes.
 
Mi nadhani kitendo cha Abdul Sykes kuchukua madaraka ya TAA kwa kutumia ubabe na vurugu, hakikuwafurahisha wazee wengi wa TAA, ndio maana kwenye uchaguzi alishindwa kirahisi na Nyerere, Hata huo umakamo wa rais itakuwa alipewa kwa shingo upande ili asimletee vurugu Nyerere, Haiwezekan ushindwe uchaguz halaf upewe cheo kikubwa hivyo
 
Kiranga,
Hajasema kitu hapo.

Kusema angesema kuwa kamsikia Abdul kutoka kwa Hamza Mwapachu.

Kusema angesema aligombea nafasi ya urais wa TAA dhidi ya Abdul Ukumbi wa Arnautoglo na akashinda Abdul akawa makamo wa Rais.

Kusema angesema kiongozi wa wazee wote wa Dar es Salaam alikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na waliompeleka kwake ni Abdul Sykes na Dossa Aziz.

Kusema angesema kwa kuwatambua wazee kwa majina yao.

Hizi dua nadhani Mwalimu anadhani yeye wa kwanza kufanyiwa na wazee.

In Shaa Allah ikitokea fursa nitazieleza dua zote kuanzia ile ya Abdul alipovamiwa ofisini na Town Clerk Mzungu anauza kadi za TANU.

Sakata hili wazee wakuamua kutawaswil kwa Allah Abdul anusurike asifukuzwe kazi.
Kuna kisoma cha Rashid Ali Meli.

Kuna mambo mengi sana sikutaka kuyaandika katika kitabu cha Abdul Sykes.
Unategemea Mjamaa mwenye faksafa za collectivism, baada ya kusema "wazee" in a collective fashion, akutajie majina ya mmoja baada ya mwingine?

Hivyo itakuwa ni kinyume na kanuni za Ujamaa zinazoiangalia jamii collectively.

Kashakutajia wawiki watatu hao, jashasema wazee, kwa mujibu wa wajamaa kamaliza hapo.

Mengine mjazie nyie wanahistoria.

Sasa angeandika kitabu cha kuelezea yote uliyoelezea wewe, wewe ungekuwa na justificatiin gani ya kuandika kitabu?

Yani unataka Nyerere aanze kukumbuka majina ya watu wote aliokutana nao mwaka 1952?

Hoja ya kwamba Nyerere amepindisha historia kwa kutotaka watu wajue alikoanzia imezimwa kwa hotuba hii.

Angetaja majina ya wazee mia, ungeweza kuja na majina mengine ya wazee mia ambayo hakuyataja, alijuana na wazee wengi sana, hawezi kumaliza kuwataja wote.

Kitu cha msingi ni kwamba, kakubali kwamba alileleea na wazee wa Dar.

Sasa hapo utasemaje anataka kuficha historia hii?
 
Laki...
Hii ya kuwa TAA haikuwa na katiba na katiba kaja kuiandika Nyerere wewe hii umeipata wapi?
Ikiwa umesoma mahali tafadhali hebu tupe rejea yake.

Baada ya hayo ndiyo In Shaa Allah tuje kwenye, ''king maker.''
Tusitangulize kwama punda akaja nyuma.
sina rejea ya katiba ya TAA , nilikuwa naunganisha dots tu, ingawa nina uhakika niko sahihi
 
Mi nadhani kitendo cha Abdul Sykes kuchukua madaraka ya TAA kwa kutumia ubabe na vurugu, hakikuwafurahisha wazee wengi wa TAA, ndio maana kwenye uchaguzi alishindwa kirahisi na Nyerere, Hata huo umakamo wa rais itakuwa alipewa kwa shingo upande ili asimletee vurugu Nyerere, Haiwezekan ushindwe uchaguz halaf upewe cheo kikubwa hivyo
Laki...
Shida kubwa unayoipata wewe ni kuwa unataka kufanya mjadala ukiwa hata kitabu cha Abdul Sykes hujasoma.

Mapinduzi dhidi ya Thomas Plantan na Clement Mtamila yalifurahiwa na iliundwa TAA Political Subcommittee ambayo ilimuingiza Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na Sheikh Said Chaurembo katika nafasi za uongozi ndani ya TAA.

Nyerere ilipangwa Nansio nyumbani kwa Hamza Mwapachu asaidiwe kuingia katika uongozi wa juu wa TAA na walioshiriki katika mazungumzo haya alikuwa Mwapachu, Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Historia hii nimeieleza hapa mara kadhaa.

Ilihofiwa kuwa ikiwa Abdul atagombea kwa nia ya kushinda Nyerere hatafua dafu na Hamza alimwambia Abdul kuwa akishapita Nyerere katika uchaguzi ule wa 1953 mwaka unaofuata wanaunda TANU na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.

Nakuona umempenda sana Abdul Sykes.
Hakika ana historia ya pekee katika waasisi wale 17 wa TANU.
 
Unategemea Mjamaa mwenye faksafa za collectivism, baada ya kusema "wazee" in a collective fashion, akutajie majina ya mmoja baada ya mwingine?

Hivyo itakuwa ni kinyume na kanuni za Ujamaa zinazoiangalia jamii collectively.

Kashakutajia wawiki watatu hao, jashasema wazee, kwa mujibu wa wajamaa kamaliza hapo.

Mengine mjazie nyie wanahistoria.

Sasa angeandika kitabu cha kuelezea yote uliyoelezea wewe, wewe ungekuwa na justificatiin gani ya kuandika kitabu?

Yani unataka Nyerere aanze kukumbuka majina ya watu wote aliokutana nao mwaka 1952?

Hoja ya kwamba Nyerere amepindisha historia kwa kutotaka watu wajue alikoanzia imezimwa kwa hotuba hii.

Angetaja majina ya wazee mia, ungeweza kuja na majina mengine ya wazee mia ambayo hakuyataja, alijuana na wazee wengi sana, hawezi kumaliza kuwataja wote.

Kitu cha msingi ni kwamba, kakubali kwamba alileleea na wazee wa Dar.

Sasa hapo utasemaje anataka kuficha historia hii?
Kiranga,
"Disadvantage," niliyonayo mimi ni kuwa nimeishi ndani ya historia hii kama mtoto wa watu hawa kwa hiyo nayajua mengi ambayo kwa staha sikuweza kuyaandika.

Uhuru ulikuja na changamoto nyingi sana na hasad hazikukosekana.

Hivi hujiulizi mimi nani hadi niaminike kiasi cha kukabidhiwa nyaraka zote za TAA na TANU walizokuwanazo akina Sykes na kuruhusiwa kuandika maisha ya marehemu Abdul Sykes.

Hakuna mtafiti yeyote aliyepata kuziona hizi nyaraka isipokuwa mimi na kuna mengi.
Uhuru ulikuja na fitna na husda.

Hakuna anaetaka Mwalimu akumbuke majina 100.
Aĺitakiwa akumbuke jina moja tu la Mshume Kiyate lingetosha:


Hiyo picha hapo chini tumepiga mwaka wa 1968 mimi nilikuwa na umri wa miaka 16 na Kleist miaka 18.

Picha hii niko mimi, Kleist Sykes, Abdallah Tambaza, Abdul Mtemvu na Wendo Mwapachu sisi watano familia zetu zote zimehusika kwa karibu sana na historia ya TANU.

Naamini umenielewa.

1574801922182.png
 
sina rejea ya katiba ya TAA , nilikuwa naunganisha dots tu, ingawa nina uhakika niko sahihi
Laki...
Waingereza wasingeliweza kusajili taasisi bila ya kuwa na katiba.
Suala la katiba kwa hiyo halikuwa katika agenda ya TAA toka mwaka wa 1929 ilipoasisiwa.

Katiba ilikuja kushughulikiwa mwaka wa 1954 wakati wa kuunda TANU na TANU hawakuandika katiba mpya walinakili neno kwa neno katiba ya Convention People's Party (CPP) chama cha Kwame Nkrumah wa Ghana.

Badala ya CPP waliweka TANU.

Katiba hii ilikuwa ishapitishwa Ghana kwa hiyo Waingereza hawakuwa na ujanja wa kuikataa katiba ya TANU.

Unamkumbuka Earle Seaton rafiki yake Abdul Sykes yule wakili kutoka Bermuda aliyekuwa Moshi?
 
Kiranga,
"Disadvantage," niliyonayo mimi ni kuwa nimeishi ndani ya historia hii kama mtoto wa watu hawa kwa hiyo nayajua mengi ambayo kwa staha sikuweza kuyaandika.

Uhuru ulikuja na changamoto nyingi sana na hasad hazikukosekana.

Hivi hujiulizi mimi nani hadi niaminike kiasi cha kukabidhiwa nyaraka zote za TAA na TANU walizokuwanazo akina Sykes na kuruhusiwa kuandika maisha ya marehemu Abdul Sykes.

Hakuna mtafiti yeyote aliyepata kuziona hizi nyaraka isipokuwa mimi na kuna mengi.
Uhuru ulikuja na fitna na husda.

Hakuna anaetaka Mwalimu akumbuke majina 100.
Aĺitakiwa akumbuke jina moja tu la Mshume Kiyate lingetosha:


Hiyo picha hapo chini tumepiga mwaka wa 1968 mimi nilikuwa na umri wa miaka 16 na Kleist miaka 18.

Picha hii niko mimi, Kleist Sykes, Abdallah Tambaza, Abdul Mtemvu na Wendo Mwapachu sisi watano familia zetu zote zimeusika kwa karibu sana na historia ya TANU.

Naamini umenielewa.


Mtu akikwambia:-

1. Nyerere ni mjamaa.
2. Wajama ni collectivists, ndiyo maana ya Ujamaa.
3.Alitaka kujenga nchi isiyo na matabaka ya "Hawa wazee wa TANU walioleta Uhuru pamoja na familia zao", na "Hawa vifaranga wengine tumewapa hadhi tu ya uraia wa Tanzania". Alitaka kujenga jamii ya watu sawa.Ndiyo maana hata uchifu aliupiga marufuku. Licha ya yeye kutoka ukoo wa kichifu. Kama alifanikiwa au alishindwa ni suala jingine, hii ndiyo nia yake.
4 Alitaka kwa upande mmoja kuwapa wazee heshima zao, na kutunza historia, ndiyo maana katoa hiyo hotuba, na ndiyo maana shule niliyosoma mimi inaitwa Tambaza.
5. Lakini pia, hakutaka kuwafanya wazee hawa na familia zao wajione wana hadhi ya kipekee nchini Tanzania, kwani, Tanzania ni nchi ya watu sawa.
6. Kawataja wachache, wengine kawataja "wazee" in a collective way, typical of a Mjamaa.

Utapingaje hoja hiyo?
 
Mtu akikwambia:-

1. Nyerere ni mjamaa.
2. Wajama ni collectivists, ndiyo maana ya Ujamaa.
3.Alitaka kujenga nchi isiyo na matabaka ya "Hawa wazee wa TANU walioleta Uhuru pamoja na familia zao", na "Hawa vifaranga wengine tumewapa hadhi tu ya uraia wa Tanzania". Alitaka kujenga jamii ya watu sawa.Ndiyo maana hata uchifu aliupiga marufuku. Licha ya yeye kutoka ukoo wa kichifu. Kama alifanikiwa au alishindwa ni suala jingine, hii ndiyo nia yake.
4 Alitaka kwa upande mmoja kuwapa wazee heshima zao, na kutunza historia, ndiyo maana katoa hiyo hotuba, na ndiyo maana shule niliyosoma mimi inaitwa Tambaza.
5. Lakini pia, hakutaka kuwafanya wazee hawa na familia zao wajione wana hadhi ya kipekee nchini Tanzania, kwani, Tanzania ni nchi ya watu sawa.
6. Kawataja wachache, wengine kawataja "wazee" in a collective way, typical of a Mjamaa.

Utapingaje hoja hiyo?
Kiranga,
Ndugu yangu nataka nikuulize swali umekisoma kitabu cha Abdul Sykes?

1574805058348.png
 
Kiranga,
Ndugu yangu nataka nikuulize swali umekisoma kitabu cha Abdul Sykes?

Sijakisoma kitabu, kinapatikana wapi? Kuna wadogo zangu wanakuja kunisalimia mapumziko yao ya Christmas naweza kuwaagizia waninunulie.

Maadam sijakisoma, nimekusoma na kukupata wewe muandishi, tujadili mantiki ya hoja nilizoweka hapo juu.

Hujanijibu, japo kwa dondoo tu, wakati nasubiri wadogo zangu waniletee kitabu.
 
Sijakisoma kitabu, kinapatikana wapi? Kuna wadogo zangu wanakuja kunisalimia mapumziko yao ya Christmas naweza kuwaagizia waninunulie.

Maadam sijakisoma, nimekusoma na kukupata wewe muandishi, tujadili mantiki ya hoja nilizoweka hapo juu.

Hujanijibu, japo kwa dondoo tu, wakati nasubiri wadogo zangu waniletee kitabu.

Kiranga,
Maana yangu ya kukuuliza ni kuwa katika kitabu cha Abdul Sykes, sehemu ya mwisho nimeeleza yaliyotokea baada ya uhuru.

Elewa nimeandika kitabu hiki nikiwa na umri wa miaka 30 bado kijana na ujana ni wazimu.

Yale niliyoandika ni kweli lakini sasa mimi ni mtu mzima sana na utu uzima unakwenda na staha.

Kurudia maneno yale sasa siwezi lakini hii sehemu ya mwisho ndiyo iliyovuruga wengi akili zao.

Kwa ajili ya hitimisho hili langu ndipo Mwalimu akaombwa na Prof. Haroub Othman na yeye aandike maisha yake ili kitabu cha Mohamed Said kisibaki kuwa ndiyo ukweli wa historia ya maisha yake na uhusiano wake na Waislam ambao wamemsaidia pakubwa wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika.

Mwalimu alikubali lakini aliomuomba Prof. Haroub atengeneza kamati yeye atawaeleza maisha yake na kamati itaandika.

Bahati mbaya Mwalimu hakuweza kufanya hayo kwa ajili ya maradhi.

Hata hivyo kamati hiyo inayoongozwa na Prof. Issa Shivji wa Kavazi la Mwalimu Nyerere hivi tuzungumzavyo inaandika kitabu hicho na wamefanya mahojiano na mimi katika utafiti wao na nimewapa baadhi ya nyaraka za Sykes na picha.

Nakusihi subiri kitabu.

Kitabu kinapatikana Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Mtoro, Manyema na Mtambani, Tanzania Publishing House, Elite Bookshop na Soma Bookshop.

Bei ni elfu kumi kipo kwa Kiingereza na Kiswahili.
Kitabu kimependwa sana tunakwenda toleo la nne.

1574822473872.png

Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Othman wakimuhoji Mwandishi 2013
(Dr. Kamata out of sight)
 
Nyerere ndio alie itransform TAA kutoka chama kisichoeleweka mpaka kuwa chama "serious" cha kupigania uhuru na mpaka katiba ya TAA kaiandika Nyerere. TAA ya Abdul Sykes haikuwa na katiba
KUSAJILIWA KWA TANU ABDUL NA ALLY SYKES WALIMSUBIRI NYERERE MTAA WA KIPATA

Wakati ujumbe wa umoja wa mataifa ulipofika Tanganyika, TANU ilikuwa bado haijasajiliwa na serikali.

TANU ilipata tasjila yake tarehe 30 Desemba, 1954 baada ya kuzishinda hila nyingi na vizingiti vilivyowekwa na serikali za kupinga usajili wake.

Bi Zainabu, mke wa Ally Sykes anakumbuka siku moja adhuhuri, jua lilikuwa kali, wakati Nyerere alipokwenda nyumbani kwao Mtaa wa Kipata (Siku hizi Mtaa wa Kleist) ambako Ally na kaka yake Abdulwahid walikuwa wakimsubiri atoke mjini alikokwenda kushughulikia tasjila ya TANU.

Alipofika Nyerere alionekana amechoka taabani na mwenye wasiwasi.

Alizama ndani ya sofa akaufunika uso wake kwa mikono yake na akakaa kimya kwa muda.

Abdulwahid na Ally walikuwa wakimsubiri azungumze.

Nyerere alikuwa na habari mbaya.
Serikali ilikuwa imekataa kuisajili TANU.

Nyerere aliwaambia kuwa serikali ilikataa kutoa usajili kwa sababu za kiufundi.

Serikali ilidai kuwa TANU haikuwa na wanachama.

Baada ya kufahamu kuwa serikali imekataa maombi ya TANU kwa kuwa ati haikuwa na wanachama wa kutosha, mithili ya onyesho la mchezo wa kuigiza unaokwenda haraka, Abdulwahid alitumia hekima na mara moja akamuomba Said Chamwenyewe aende nyumbani kwao Rufiji kusajili wanachama kwa ajili ya TANU.

Rufiji ni sehemu ya Waislam watupu.

Kwa ajili hii TANU haikuwa na tatizo la kuwapata wanachama.

Kwa hakika wanachama wa mwanzo wa TANU walikuwa kutoka Gerezani na Rufiji. Illife ameandika kuwa:

"Mwelekeo wa kuungwa mkono kwa TANU mjini Dar es Salaam unahitaji uchunguzi, lakini mapato ya fedha kwa mwaka 1958 yanaonyesha sehemu iliyo kubwa ya kuungwa mkono chama ilikuwa kutoka makazi ya Waafrika - Kariakoo, Ilala, Gerezani... kufikia Septemba, 1955 Dar es Salaam ikiwa na watu kama 110,000 - ilichukua kiasi cha 25,000 kati ya 40,000 za kadi za uanachama wa TANU zilitolewa kote nchini.

Huu ulikuwa ndiyo msingi ambao TANU iliteka Tanganyika."

Abdulwahid sasa akiwa na umri wa miaka 30, alikuwa amekamilisha lile lengo lake kubwa katika maisha yake, lengo ambalo lilianza kwa marehemu baba yake ambaye miaka ishirini na moja iliyopita alitabiri kuendelea kwa mapambano kati ya Waafrika wa Tanganyika na serikali ya kikoloni.

Kleist Sykes alikuwa halikadhalika ametabiri jukumu la kizazi kijacho.

Katika barua aliyomwandikia Mzee bin Sudi, Rais wa African Association, mwaka wa1933, Kleist katika umri mdogo wa miaka ishirini na tisa, akiwa kijana mdogo sana aliandika maneno haya:

"Tupambane kwa nguvu zetu zote kuelekea njia ya ustaarabu kama vile watu wa makabila mengine wanavyofanya.

Haidhuru kitu ikiwa hatukamilishi kila kitu.

Wale watakaokuja baada yetu watakamilisha yatakayobakia."

Kwa hakika Kleist alikuwa mtu wa fikra.

Alizungumzia kuhusu "ustaarabu," ambao hivi leo ungemaanisha ''kujitawala'' na kuhusu makabila ambayo TANU imeyageuza kuwa ''taifa.''

Katika mwaka wa 1954 robo karne baadaye katika jengo lilo hilo, 25 New Street ambalo Kleist alisaidia kulijenga kwa njia ya kujitolea, kizazi kipya nchini Tanganyika kilikuwa kikiigeuza African Association aliyoiunda katika mwaka 1929 kuwa chama cha siasa.

Lengo lake lilikuwa kuwatayarisha Watanganyika kujitawala.

Miongoni mwa waliokuwa wakiongoza harakati za kudai uhuru zilizokuwa zikiibuka walikuwa watoto wake watatu, Abdulwahid, Ally na Abbas."

 
IMG_20191130_124033.jpg

Screenshot_20191130-124822.png


FaizaFoxy


Mkuu... Mimi naomba kufahamishwa kama una historia ya huyo Mzee kagasheki... Na kama waliwahi kuwa na mahusiano ya kudai Uhuru na Dr Kyaruzi na viongozi wengine wa kipindi hicho toka hapo kanda ya ziwa...
 
Back
Top Bottom