Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Mkuu, Nguruvi 3, kwanza asante kuni tag hapa, Mkuu Maalim Mohammed Said kila anapoleta urongo humu, ukishutukiwa, hukwepa ama kwa kutoka baru, kwa kunyamaza, ama kwa kuzunguka zunguka, yuko vizuri sana kwenye kupiga chenga. Mfano mzuri ni hilo swali lako la kwenye bandiko No. 31 kumhusu Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, kamwe hatalijibu maana litamuumbua urongo wake kuwa Mwalimu katambulishwa mjini na babu zake tuu. Babu zake pekee ndio walimtambulisha Mwalimu kwa Wazee wa Dar es Salaam in 1950s, hivyo data zozote kuwa Mwalimu Nyerere alifika Dar 1948 na kuhudhuria mkutano Mkuu wa TAA, is not a good news!.

Kuna siku humu yule Bidada wake alileta bandiko humu la urongo mtupu wa mchana kweupe akidai

ndani ya bandiko hilo akaweka voice clip ya Mkuu Maalim Mohammed Said akitema urongo fulani kwa kudai ndani ya Bunge la JMT, wabunge asilimia 76% ni Wakristu Wakatoliki, Asilimia 18% ni Wakristu wa madhehebu mengine, na Waislamu ni asilimia 6% tuu!.

Nilipokosoa bandiko hilo, na kuanzisha bandiko hili,

Kwanza ile sound clip ya maurongo ya Mkuu Maalim Mohammed Said, ilifutwa from the source, pili Mkuu Maalim Mohammed Said mwenyewe akaingia front with an excuse kuwa hizo data za urongo na yeye alizisoma tuu kutoka sources fulani.

Hivyo Mkuu Maalim Mohammed Said akileta urongo humu, akishtukiwa, kamwe hawezi kukiri urongo wake, atazuga kwa kuzunguka zunguka hadi watu wasahau kama lilivyo bandiko lako No. 31, Mkuu Maalim Mohammed Said hawezi jibu hilo ataumbuka.

P
Umesahau ulichoahidi kwenye huo uzi?

Tunasubiri.
 
"Dini" mpya inaebdelea kutungwa kama ileee!
Badili kilichopita kwa kuchanganya hila, uongo, ukweli, umaamuma n.k!.. Unapata "dini" mpya ya kweli sio kama ile ambayo historia yake imepotoshwa!

Ni muendelezo wa upuuzi tu!
 
Lakini mbn huyu mzee huwa anapenda sana hizi habari ni madai ya kutaka wazee wake watambulike tu au kuna jambo liko nyuma ya pazia.

Huenda kuna jambo maana kuna wengine humu jf wameomba ikulu irejeshwe kwa waislam. Madai ambayo ni ya ajabu kabisa kama kila aliyefanya jambo fulani arejeshewe kutakuwa na kubakia na nini, taifa litagawanyika.
hii ni hoja ya msingi sana
P
 
Ni dhahiri yaonyesha unakerwa na baadhi ya mambo, ila hilo halimaanishi kwamba kile usemacho wewe ndicho kilicho sahihi kwa 100%.

Suleiman Kumchaya anasema kuwa Julius Nyerere alipokuwa Makerere alikuwa anawasiliana na wazee wa Dar es Salaam akiwataka waanzishe chama cha siasa.
Ni kweli hapo juu sio kwamba Mwalimu aliwasiliana na "Wazee wa Dar" waanzishe chama, ila ni kweli alipokuwa Makerere alikuwa na mawasiliano na Dar, na nijuavyo mimi Mwalimu alitaka kuanzisha Chama ila kwa kuwasiliana na walio Dar ndipo aliposhawishiwa kuachana na huo mpango na ajiunge na Chama/harakati zilizopo tayari Dar. kwa hiyo hapo upo sahihi usemapo hakukuwa na mawasiliano ya kwamba wao Wazee waanzishe chama.

Wangelijua pia kuwa Abdul alifanya mazungumzo na Chief David Kidaha Makwaia kuanzia 1951 wakijadiliana kuhusu kuasisi TANU
Nakubaliana na wewe kina Sykes ndio walibuni (jina)TANU, na jina hilo ndio lilipitishwa wakati wa kuiua TAA...ingawa naona unasisitiza sana KUASISI kuliko KU transform TAA.

Katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 Nyerere aliingia katika uongozi na timu ya vijana watupu kama Abdul Sykes, Ally Sykes Tewa Said Tewa, Dossa Aziz, Joseph Kasella Bantu, Dome Budohi
Ni sahihi kabisa na hata Mwalimu anapowataja Wazee hawahusishi akina Sykes kwani wao hawakuwa Wazee wakati huo, sioni ni kipi kinachanganya hapa, inaonyesha kana kwamba Mzee said hutaki kukubali kwamba walikuwepo Wazee wengine wengi tu kwenye harakati zile.

Kila anaejisikia kuwataja ''wazee,'' utasikia, ''wazee'' lakini majina yao hayatajwi.
Kwa nini iwe hivi?

Na hii ndio sababu ya kuwataja Wazee bila kujali majina maana yaweza kuwa ukawataja wachache na kuonekana hukuwajali wengine wengi tu

Nyerere kabla hajafika Dar es Salaam hakuwa anajuana na mzee yeyote katika wazee wa Dar es Salaam ambao walikuwa katika siasa kwa hiyo hakuwa anaandikiana barua na mzee yoyote kuwataka waunde chama cha siasa.
Huu ni urongo wa mchana, na ndio maana unapishana na wengine wengi mimi nikiwa mmoja wao. Mwalimu alikuwa na mawasiliano na baadhi ya Watu/Wanaharakati waliokuwepo Dar, na miongoni mwao aliitwa Mzee Mwangosi...ingawa ni kweli alitambulishwa kwa kina Syke baada ya kufika Dar.

Historia zako Mzee Saidi zinapungukiwa baadhi ya mambo, umeegemea sana kwenye taarifa za kina Sykes na wengine wachache tu.
Mkuu huyu mzee ana kitu kingine kabisa anachokipigania, sio historia!
 
Mkuu huyu mzee ana kitu kingine kabisa anachokipigania, sio historia!
Naunga mkono hoja
P
 
Pascal,
Hapana neno.
Ni yale yale ya simba wa Agip ana miguu mingapi?
Sasa mbona historia ya Kivukoni haikuandika haya usemayo?
Mkuu Maalim Mohammed Said, hapo ndipo ninapokupendea, kukwepa mishale kama nyani Mzee ni kwasababu uko very smart upstairs, tena ungekuwa wakili, usinge shindwa kesi hata lile jengo la Makao Makuu ya Uislaam la Darusulum, ungelikomboa.

Kama kuna mahali umeeleza Mwalimu Nyerere na Hamza Mwapachu walikuwa viongozi wa TAA, mwaka 1945, Hamza Katibu, Mwalimu Katibu Msaidizi, Mwaka 1956, Hamza akahamishwa, Mwalimu akapokea mikoba, hivyo Mwalimu Nyerere ndiye alikuwa Katibu wa TAA, Tabora; mwaka 1956. Ukadai Wazee wako ndio waliomuingiza mjini Mwalimu Nyerere na kumtambulisha kwa wazee wa Dar es Salaam, miaka ya early 1950s na kabla ya hapo Mwalimu alikuwa hajulikani na hawajui wazee wowote wa Dar es Salaam hadi aliposhikwa mkono na wazee wako kutambulishwa ndipo akajulikana na kulijua jiji.

Mkuu Nguruvi3 katika bandiko No. 31 kamaliza kwa kukuuliza kajiswali kadogo tuu, "Katika mkutano Mkuu wa TAA wa mwaka 1948, uliofanyika jijini Dar es Salaam, juu ujumbe kutoka Tawi la TAA Tabora, uliwakilishwa na nani?",
4. Mkutano mkuu wa mwaka 1948 Dar es Salaam nani alihudhuria kutoka tawi jipya Tabora(3/3/1945) miongoni mwa Waanzilishi uliowataka hapo juu.

Tuanzie hapa halafu tutaendelea kuteta jamvini.
Kwanini hili unalikwepa kulijibu, naomba tuanzie hapo ili tuweze kupembua zipi ni pumba na upi mchele, ndipo tuendelee kupindua jiwe moja baada ya jingine la urongo wa Mkuu Maalim Mohammed Said, and no stone will be left unturned!.
P
 
Hizi ngano zako sasa zinachosha…! Najua wazee wa Dar es Salaam walikuwa wazee wako na ungependa sana uwainue. Najua unavyohangaika na ngano zile zile kila mara lakini utake usitake kwa ufupi sana ni hivi...

Ni uongo uliopitiliza kudai kwamba AA iliyoanzishwa mwaka 1929 na Gavana wa wakati huo Cameroun kama klabu ya starehe kwa wasomi weusi ilikuwa na malengo ya kudai uhuru.

Hilo la kwanza na pili ni ukweli kuwa wakati Nyerere anahudhuria mkutano mkuu wa AA akiwakilisha jimbo la Tabora wewe ulikuwa hujazaliwa. Na kwamba viongozi wa AA walikuwa hawamjui Mwalimu Nyerere kabla ya mwaka 1953 alipohamia Dar es Salaam pia ni uongo.

Mtu ambaye yawezekana hakumjua Mwalimu Nyerere labda ni Abdul Sykes peke yake kwa sababu nyakati hizo hakuwepo...tunaanza kumsikia tu pale alipoongoza uvamizi wa ofisi za AA kuwatoa wazee wake!

Mwalimu Nyerere tayari alikuwa kiongozi wa AA mwaka 1945 akiwa Tabora na mwaka huo huo alifika Dar es Salaam na kukutana na viongozi na wanachama wa AA mojawapo akiwa Dossa Aziz.

Sasa, kama Mwalimu Nyerere na Abdul hawakukutana ni wazi kumbe Abdul Sykes hakuwa kati ya vinara wa AA mjini Dar es Salaam...swali la kujiuliza ni je, Abdul alikuwa nani ndani ya AA kabla ya kuvamia ofisi za TAA mwaka 1948 kwa ngumi na mateke?

cc: Nguruvi3, Yericko Nyerere, JokaKuu
Mkuu Mag 3, asante kwa hii.
P
 
4. Mkutano mkuu wa mwaka 1948 Dar es Salaam nani alihudhuria kutoka tawi jipya Tabora(3/3/1945) miongoni mwa Waanzilishi uliowataka hapo juu.

Tuanzie hapa halafu tutaendelea kuteta jamvini.
Swali hili halijajibiwa mpaka sasa.
Lijibiwe!.
P
 
Pascal usikatae Historia isiyo rasmi inasema kwamba Mwalimu alishirikiana na wazee wa pwani ktk harakati za kudai uhuru.

Kuna moja inasema kwamba wazee walimteua nyerere kuwa msitari wa mbele ktk harakati za kudai uhuru kwa sababu wao walikua hawajui Kiingereza. Na wakati wa kwenda kudai uhuru Mwalimu aliongozana na hao wazee na Waingereza wakamuuliza baada ya kuingia Ofisini wenyewe Waswahili wako wapi wanaotaka Uhuru akawaambia nimekuja nao.

Kwahiyo Pasal hili jambo ni kweli kwamba Wazee wa pwani ndio waliongoza harakati za kudai Uhuru wakishirikiana na mwalimu
 
Mohamed Said, huu ni mchango wangu wa mwisho katika santuri hii yako ambayo imechuja lakini bado wapo watu wanaomeza tu ngano zako bila takafuri yoyote.

Wakati wote unapodai unaandika historia ya Waislaam ukweli ni kuwa unaandika historia ya wazee wako, Wazulu na Wamanyema.

Unapodai unaandika historia ya Watanganyika ukweli ni kuwa unaandika historia ya wazazi wako na babu zako,Wamanyema na Wazulu.

Kwa kukufahamisha Watanganyika walikuwepo sana tu ingawa huwapi kipaumbele stahiki katika hizi ngano zako.

Huwezi kuongelea AA bila kumtaja muasisi na Kiongozi wake Mkuu wakati inaanzishwa mwaka 1929 na huyo si mwingine bali Mtanganyika Myao na Msomi Hayati Mwalimu Cecil Matola.

Baada ya Matola kufariki, AA ilikosa uongozi madhubuti hali iliyoifanya AA kuwa kama chombo kilichokosa dira hadi Zanzibar ilipojitoa mwaka 1948 na kuzaliwa TAA.

Lakini hata ilipozaliwa TAA, uongozi thabiti ulikuja kupatikana mwaka 1950, Mtanganyika Mhaya Dr. Vedasto Kyaruzi alipochaguliwa kuwa Raisi wake wa kwanza.

Baada ya Wakoloni kumpa uhamisho wa nguvu Raisi wa TAA, shughuli za TAA zilizorota kwa sababu kiongozi mkuu hakuwepo.

Kumbuka kwamba Dr. Kyaruzi alipopewa uhamisho wa kwanza hakupelekwa mbali na hivyo aliweza kuendelea kuwasiliana na wasaidizi wake mojawapo akiwa Abduwahid Sykes.

Wakoloni walipogundua hilo ilibidi wamhamishe tena wampeleke mbali zaidi ili mawasiliano na wasaidizi wake yawe magumu zaidi na hivyo kupelekea TAA kuzorota hadi ujio wa Mwalimu Nyerere mwaka 1952.

Hivyo nafasi ya Abdulwahid Sykes ndani ya TAA wakati Mwalimu Nyerere yuko Makerere ni kwamba wakati huo TAA haikuwapo, ilikuwepo AA iliyoasisiwa na Cecil Matola mwaka 1929.

Huyu Abdulwahid Sykes unamtajataja sana na bila shaka kwa sababu unazozijua wewe mwenyewe lakini ukweli ni kwamba hakuwahi kuwa kiongozi Mkuu wa TAA wala TANU wakati wowote ule.

Dai la kuwa ndiye alipendekeza jina la TANU ni kweli kwa kiasi Fulani kwani alichofanya ni kwamba jina alilopendekeza awali Mwalimu Nyerere lilikuwa gumu kidogo kutamkwa kwa haraka ingawa maneno yalikuwa yale yale.

Mwalimu Nyerere alitaka maneno manne yasikosekane nayo ni AFRICAN, TANGANYIKA, NATIONAL na UNION yawepo na iliyobakia ni namna tu ya kuyapanga na ndipo Abdulwahid Sykes kupendekeza Tanganyika African National Union (TANU)
Mag3,
Cecil Matola alifariki mwaka wa 1933 miaka minne baada ya kuasisiwa kwa African Association na akiishi Mission Quarter.

Nyumbani kwake ndiko mkutano wa kuasisi African Association ulipofanyika.

Waliohudhuria mkutano huu walikuwa yeye Cecil Matola, Kleist Sykes, Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Ali Said Mpima, Zibe Kidasi, Rawson Watts na Raikes Kusi.

Haya majina kayaandika Kleist katika mswada wa kitabu cha maisha yake ambao ndiyo rejea kuu ya historia ya African Association.

Kleist katika mswada wake anaeleza sababu kwa nini waliokuwa wamejitokeza katika siasa walikuwa wengi Waislam na akaeleza kuwa kabla ya African Association, mwakilishi wa Waafrika Alikuwa Father Gibbons kutoka Pugu Mission.

Katika mswada huu yapo mengi yaliyoelezwa pamoja na msuguano uliokuwa unatokea mara kwa mara kati ya wenyeji na hiki kizazi cha kwanza cha watoto wa wahamiaji kutoka Sudan, Belgian Congo na hawa Wazulu kutoka Mozambique waliopewa jina la "Wakuja" yaani Wanubi kama Ibrahim Hamisi, Wamanyema kama Mzee bin Sudi na Wazulu kama Kleist Sykes.

Walikuwa wakilaumiwa kwa kujitia kimbelembele katika mambo ya Dar es Salaam ilhali wao ni ''wageni.''

African Association wao viongozi wapo, Maulid Committee wao viongozi wapo, ilmradi hawapungui.

Umesema kweli kuwa naandika historia ya wazee wangu Wamanyema na Wazulu lakini na wengine pia kama Ali Said Mpima, Mwinjuma Mwinyikambi, Max Mbwana, Said Chamwenyewe kuwataja wachache ambao ni Wamashomvi, Warufiji na Wazaramo pia nimeandika historia zao.

Nimeandika hadi historia za Waafrika ambao hawakuwa Watanganyika lakini walishiriki katika kupigania uhuru wa Tanganika kama Dome Budohi Mkenya na Denis Phombeah Mnyasa,

Hawa wamesahauliwa na historia mimi nimekuelezeni kuwa walikuwapo na picha zao nimekuonyesheni.

Watafute kwenye kitabu changu utawakuta.
Kuwa siwapi kipaumbele hii si kweli kila mmoja nimemweleza kwa stahili yake.

Kuwa Cecil Matola ni muasisi wa African Association mswada wa Kleist haukumueleza kwa sifa hiyo.

Kleist ameeleza jinsi yeye alivyokutana na Dr. Aggrey mwaka wa 1924 na akamshauri kuasisi chama hicho.

Si kweli kuwa alipofariki Cecil Matola chama kilikosa uongozi madhubuti.

Mzee bin Sudi alichaguliwa kuwa Rais na huu ndiyo mwaka Kleist na Mzee bin Sudi waliunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Nafasi walizoshika katika Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ni hizo hizo walizoshika katika African Association.

Maendeleo haya si dalili ya viongozi waliochoka.
Umemtaja Dr. Vedasto Kyaruzi na TAA kuzaliwa 1950.

Hakika huijui historia ya TAA.

TAA ilibadili jina 1948 wala haikuwa kuwa chama kipya kimeanzishwa na sababu ni kujitofautisha na African Association ya Zanzibar.

Lakini umeshindwa kueleza Dr. Kyaruzi kaingia vipi katika uongozi wa African Association mwaka wa 1950.

Nina mswada wa Dr. Kyaruzi, "Mhaya Doctor," kuna sura kaipa jina, "Action Group," humo kaeleza mchango wa Dr. Tsere na yeye katika African Association na kamtaja Abdul Sykes na "uncle," wake Schneider Abdillah Plantan katika mabadiliko haya.

Unaweza kusema Schneider, Hamza Mwapachu ndiyo waliofanya mabadiliko haya ya uongozi.

Ati Abdul Sykes "msaidizi," wa Dr. Kyaruzi.
Hii wewe umeitoa wapi nimeipenda sana kama una ''citation.'' nipatie.

Hayo yote ya Dr. Kyaruzi hayapo popote katika historia za TANU zilizoandikwa isipokuwa katika kitabu cha Abdul Sykes halafu unanirudishia mimi historia uliyoisoma kutoka kitabu changu.

Umenifurahisha sana
Kumtajataja Abdul Sykes.

Mimi si "nimemtajataja," nimemwandikia kitabu kizima na humo ndimo ulipotoa mengi uliyoandika hapa.

Kivukoni wamejaribu kuandika historia ya TANU bila kumataja Abdul Sykes.
Sina haja ya kukueleza balaa lake.

Tuko hapa mwaka wa 10 tunamjadili Abdul Sykes.

Abdul Sykes hakushika nafasi ya kuongoza TANU lakini mikutano yote ya siri ya kuunda TANU na "retreat" zote baada ya kuunda TANU walizokuwa wanafanya viongozi wa TANU wakiwa na jambo zito, mikutano hii ikifanyika nyumbani kwake Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Ushajiuliza kwa nini?

Ushajiuliza kwa nini Nyerere alipofika Dar es Salaam mwaka wa 1952 alikwenda nyumbani kwa Abdul na alipojiuzulu kazi mwaka wa 1955 alikwenda kukaa kwa Abdul?

Jina la TANU wala si kitu mimi na wewe tuvutane hapa.
Mimi nakuuliza kitu kimoja.

Haikushangazi kuwa historia ya TANU haimtaji Abdul Sykes au mdogo wake Ally au baba yao Kleist kama waasisi na wafadhili wa harakati hizi?
 

Attachments

  • DOME OKOCHI BUDOHI 1.jpg
    DOME OKOCHI BUDOHI 1.jpg
    646.3 KB · Views: 1
  • DENIS PHOMBEAH 1.jpeg
    DENIS PHOMBEAH 1.jpeg
    33.4 KB · Views: 1
Mkuu mag3 asante kwa historia nzuri .nafatilia kwa karibu huu mnakasha
Mosebelbay,
Ikiwa umependezewa na historia ya Mag3 nakushauri usome kitabu alichohariri John Iliffe, ''Modern Tanzanians,'' Nairobi, 1973, ndani kuna sura kaandika Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, uk.. 95-114.

Pia kuna ''seminar paper'' ya Daisy aliyoandika mwaka wa 1968 ambayo ndiyo chanzo cha sura hiyo ipo Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, East Africana.

Daisy aliandika hiyo semina paper wakati akiwa mwanafunzi wa historia chini ya John Iliffe enzi hizo, University of East Africa.

Hayo yote ya Cecil Matola kayapata kutoka kwangu na mimi nimeyatoa kutoka kwa dada yangu Daisy.

Baada ya Abdul Sykes kusahauliwa na historia mwaka wa 2011 katika kuadhimisha uhuru wa Tanganyika, Abdul na Ally Sykes walitunukiwa Medali ya Mwenge wa Uhuru.

Picha hiyo nakuwekea hapo chini nimeshika medali hiyo watoto wa Abdul Sykes wanasema ati nimefanya juhudi kubwa kueleza historia ya baba yao na ndiyo maana ikafahamika na serikali kuamua kumuadhimisha marehemu baba yao:

1574739476548.png

Kushoto Kleist Abdulwahid Sykes, Miski Abdulwahid Sykes, Mwandishi na Medali ya Mwenge wa Uhuru, Aisha ''Daisy'' Sykes, llyas Abdulwahid Sykes
 
Lakini mbn huyu mzee huwa anapenda sana hizi habari ni madai ya kutaka wazee wake watambulike tu au kuna jambo liko nyuma ya pazia.

Huenda kuna jambo maana kuna wengine humu jf wameomba ikulu irejeshwe kwa waislam. Madai ambayo ni ya ajabu kabisa kama kila aliyefanya jambo fulani arejeshewe kutakuwa na kubakia na nini, taifa litagawanyika.

Huyu mzee anadai kila siku watambuliwe watambuliwe kivipi sasa hao walishapita wakajenga kwa sehemu yao imepita wakumbukweje basi. Kila mmoja wetu hufanya kwa sehemu yao na yote waliyofanya watalipwa na MUNGU huko mbele ya haki.

Tukianza kutafuta nani alihusika na nini tutafika wapi haya mpewe Ikulu ya Dar mkakae hapo sijui mnaitaka mukaishi pale sijui Mhimbili nayo watoto wa Mwaisela sijui wauze majengo wagawane. Kumbukeni hao wazee wenu walianzisha wengine wakaendeleza. Kumbukeni hata hao walioendeleza ndiyo wa maana zaidi. Maana hao ndiyo waliofanya yaliyopo leo na tunajivunia kilichopo kwa faida ya sisi sote.
Jengo la ikulu halikuwa hivyo jengo la mhimbili halikuwa vile chama chenu cha TAA hakikuwa hivyo waliojenga juu yake ndiyo wa maana zaidi.

Huyu mzee kila kukicha ya nyuma tuuu ndiyo kukua huko haya basi eee tumekusikia tuwafanyie nini hao wazee wako.
Hao wazee wako hawawezi kukumbukwa kwa kupewa sijui majengo au madaraka kwa vitukuu wao ambao hawakuweza kuendeleza chochote juu yake na wakaishia kukimbilia ubaharia na kuterekeza harakati za wazazi wao, au hawakuweza kuonesha vipaji sawa na wazazi wao katika nyazifa mbalimbali na kwa uhitaji wa nyakati hizo wakawepo wengine kuendeleza kazi zao hao wazee.
Domsel,
Hii ''Huyo Mzee,'' nimeipenda sana.

Hapa nyumbani kwangu nikiwaambia wanangu mimi mzee wanakataa wanasema, ''Ah baba wewe bado kijana.''

Basi hii asubuhi nimewaonyesha hili bandiko lako la ''Huyu Mzee.''
Wanasema ati unaniita mzee kwa kuwa umehamaki.

Hakika miaka 67 mimi ni mzee sana.
 
"Pascal Mayalla, post: 33576077, member: 17813"]
Mkuu, Nguruvi 3, kwanza asante kuni tag hapa, Mkuu Maalim Mohammed Said kila anapoleta urongo humu, ukishutukiwa, hukwepa ama kwa kutoka baru, kwa kunyamaza, ama kwa kuzunguka zunguka, yuko vizuri sana kwenye kupiga chenga.
Mkuu ukiriejea bandiko #31 mwanzo kabisa niliweka wazi kuwa twende kwa hoja na si hadithi.

Moja ya mbinu za Mohamed kukwepa hoja ni kulundika habari irrelevant na hoja.

Utamsikia akijigamba, au kuleta picha na habari zisizohusiana na hoja.

Sijui kama ni ujanja wake au ni mapungufu ya kibinadamu.
Mohamed ni orator mzuri sana lakini hawezi ku articulate hoja au ku defend
Mfano mzuri ni hilo swali lako la kwenye bandiko No. 31 kumhusu Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, kamwe hatalijibu maana litamuumbua urongo wake kuwa Mwalimu katambulishwa mjini na babu zake tuu. Babu zake pekee ndio walimtambulisha Mwalimu kwa Wazee wa Dar es Salaam in 1950s, hivyo data zozote kuwa Mwalimu Nyerere alifika Dar 1948 na kuhudhuria mkutano Mkuu wa TAA, is not a good news!.
Swali hilo halitajibiwa kwasababu mwisho ni kuua hoja ya Nyerere kupokewa na wazee wake na kuingizwa katika siasa na Abdul

Anajua, Tabora ilikuwa tawi jipya na ameeleza kufunguliwa kwake 3/3/1945

Kawataja waliohusika, asichokieleza ni lini Nyerere alichukua madaraka na kwa utaratibu gani.

Haelezi ni akina nani waliohudhuria mkutano wa 1948 akijua Nyerere alikwenda.

Maana yake, Nyerere alikutana na Wazee akina Dosa na Abdul Sykes, kwasababu kuu mbili.

Kwanza, ni katibu wa Tawi kubwa sana baada ya Dar es Salaam, obvious walijulikana.

Pili, Nyerere alikuwa msomi na enzi hizo walihesabiwa kwa vidole vya mkono

Ni uongo kwamba Abdul hakumjua hadi alipotambulishwa kwake miaka hiyo ya 50

Hoja yake ni kuonyesha Nyerere si lolote si chochote, alikuja na kuingizwa katika siasa na Abdul Sykes. Kupitia hilo Abdul atakuwa ''king maker''

Katika mabandiko yaliyofuata nimemuomba kupitia kavazi la Nyerere na kavazi la Klesit Sykes hadi Abdul atuonyeshe karatasi moja iliyoitwa katiba. Hakujibu

Mohamed huyo huyo anasema Abdul ndiye alibuni jina la TANU akiwa Burma. Fair enough

Haipaswi kuishia hapo, Mohamed haelezi kuwa TANU ilikuwa na katiba baada ya Mwalimu

Kwanini hajibu hoja kama hizo?
Jibu ni rahisi kwamba, ataondoa mantiki ya vyama vya siasa kuwa kama klabu tu.

Hapa haina maana vilabu vya pombe, hapana!

Vilikuwa vilabu vya siasa kwa nyakati hizo vikikosa vionjo vya kusonga mbele.
Ujio wa Mwalimu uliongeza nguvu palipokuwa na mapungufu kama uwepo wa katiba.

Hili nalo linatupeleka katika hoja ya AMNUT.
Mohamed anasema Abdul hakuwa mwanzilishi, haelezi kuwa Abdul alikuwa mwanachama?

Utaona details zinakosekana kwasababu ukileta AMNUT utafungua mapungufu ya kushindwa kwa AMNUT na katika hilo Abdul hatakosekana.

Katika kufunika mapungufu ya AMNUT au kiungo hicho na akina Abdul, Mohamed atakueleza kuhusu EAMWS na Kuundwa kwa Bakwata kwa undani sana. Hilo sina tatizo nalo hata kidogo.

Asichokueleza ni kuwa wakati huo Nyerere alikuwa na asilimia takribani 98 ya Wazee wetu wa Dar ndani ya halmashauri kuu ya TANU.

Ilikuwaje mtu mmoja akawa na nguvu kiasi hicho bila usaidizi kutoka ndani ya TANU iliyokuwa na wazee wake kwa asilimia kubwa? Hatakueleza

Katika kukwepa hoja Mzee Said atakueleza kisa cha kufukuzwa kwa Mufti Ameir
Hapo hatukueleza wakati huo sheikh alikuwa TANU au AMNUT?

Siku za karibuni baada ya kuona hoja zake dhidi ya Nyerere zinafifisha nguvu ya hoja zake, Mohamed anasema Nyerere na Abdul walikuwa ndugu wa Familia.

Hilo sioni kama lina tatizo,akina Abdul walikuwa wenyeji na walimuhifadhi Mwalimu.

Mo hatakueleza nini kiliwafarakanisha kama ambavyo hatakueleza AMNUT ilifia wapi au Sheikh Ameir alifukuzwa kwanini na wakati huo alikuwa upande gani, TANU au AMNUT

Reading between the lines the whole history is disjointed. Hii haina maana ya kuwa anachoeleza hakikuwepo, la hasha. Matukio na wahusika walikuwepo na wapo bado.

Kinachoifanya historia isomeke kama ngano ni ''embellishment to skew the facts so as to fit his narratives hence to demean Mwalimu Nyerere''

Rekodi iwekwe kwa sahihi, Mo mapungufu ni sehemu ya ubainadamu, kukwepa au kukimbia kimbia hoja hakusaidii
Hivyo Mkuu Maalim Mohammed Said akileta urongo humu, akishtukiwa, kamwe hawezi kukiri urongo wake, atazuga kwa kuzunguka zunguka hadi watu wasahau kama lilivyo bandiko lako No. 31, Mkuu Maalim Mohammed Said hawezi jibu hilo ataumbuka.
 
Pascal usikatae Historia isiyo rasmi inasema kwamba Mwalimu alishirikiana na wazee wa pwani ktk harakati za kudai uhuru.

Kuna moja inasema kwamba wazee walimteua nyerere kuwa msitari wa mbele ktk harakati za kudai uhuru kwa sababu wao walikua hawajui Kiingereza. Na wakati wa kwenda kudai uhuru Mwalimu aliongozana na hao wazee na Waingereza wakamuuliza baada ya kuingia Ofisini wenyewe Waswahili wako wapi wanaotaka Uhuru akawaambia nimekuja nao.

Kwahiyo Pasal hili jambo ni kweli kwamba Wazee wa pwani ndio waliongoza harakati za kudai Uhuru wakishirikiana na mwalimu
Mkuu Nyambiza jr, kwanza hakuna mtu yoyote mkweli anayeukataa ukweli, hivyo hakuna mtu yoyote anayepinga mchango wa wazee wa Dar es Salaam katika harakati za kudai uhuru, tunachopinga ni juhudi kubwa za kumdogosha Mwalimu Nyerere, na kuwakuza wazee wa mtu fulani kuwa wao ndio kila kitu!.

Katika kumdogosha Mwalimu Nyerere, tukalishwa urongo humu kuwa Mwalimu hukuwajua wazee wa Dar es Salaam hadi alipotambulishwa na wazee wa fulani ile miaka ya 1950s.

Mkuu Nguruvi3, akauliza swali la msingi sana ili kuupinga urongo tunaolishwa humu kumhusu Mwalimu Nyerere, kwa kuuliza ujumbe wa mkutano Mkuu wa TAA wa mwaka 1948 ulihudhuriwa na nani kutoka tawi la Tabora?. Jibu la swali hilo ni kigugumizi mpaka sasa!. Njia ya mwongo ni fupi, mtu akileta urongo humu, the best way to counter urongo huo ni kumpa facts mrongo huyu kwa kumuuliza maswali ya datas ambapo akiyajibu tuu ni kamba ya kujinyonga mwenyewe.

Kama umeelezwa humu kuwa Mwalimu aliletwa mjini mwaka 1950, kabla ya hapo alikuwa bush, hakumjua Mzee yoyote wa mujini, halafu ukapata taarifa ya uhakika kuwa mwaka 1946 Mwalimu Nyerere ndiye alikuwa Katibu wa chama cha TAA, tawi la Tabora, na ukatibu wenyewe kaupokea kutoka kwa mtoto wa mujini, tena alwatan kabisa!.
Kisha ukaelezwa Mwalimu Nyerere ndiye aliyehudhuria mkutano Mkuu wa TAA wa mwaka 1948 jijini Dar es Salaam, akiwawakilisha mkoa wa Tabora, hivyo kama Nyerere hakuwajua wazee wa Dar es Salaam kabla ya kutambulishwa ile 1950s, huo mkutano Mkuu wa TAA wa mwaka 1948, inamaana Mwalimu alihudhuria na mawe na sio na wazee wa mujini hadi miaka ya 1950s alipotambulishwa na wazee wa fulani, ndipo Mwalimu Nyerere akafahamika mujini!.

Siku zote, ukweli utabaki kuwa ukweli daima na kwenye ukweli uongo hujitenga, hakuna kabisa ubishi kuhusu mchango wa wazee wa Darisalama, katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika lakini pia sio haki kutaka kumdogosha Mwalimu Nyerere na kuwakweza wazee wa fulani, kwenye harakati za uhuru wa Tanganyika, Mwalimu ana very special role, ataendelea kuwa alfa na omega wa mashujaa wa uhuru wa Tanganyika na kustahili title ya Baba wa Taifa.

P
 
Mkuu Nyambiza jr, kwanza hakuna mtu yoyote mkweli anayeukataa ukweli, hivyo hakuna mtu yoyote anayepinga mchango wa wazee wa Dar es Salaam katika harakati za kudai uhuru, tunachopinga ni juhudi kubwa za kumdogosha Mwalimu Nyerere, na kuwakuza wazee wa mtu fulani kuwa wao ndio kila kitu!.

Katika kumdogosha Mwalimu Nyerere, tukalishwa urongo humu kuwa Mwalimu hukuwajua wazee wa Dar es Salaam hadi alipotambulishwa na wazee wa fulani ile miaka ya 1950s.

Mkuu Nguruvi3, akauliza swali la msingi sana ili kuupinga urongo tunaolishwa humu kumhusu Mwalimu Nyerere, kwa kuuliza ujumbe wa mkutano Mkuu wa TAA wa mwaka 1948 ulihudhuriwa na nani kutoka tawi la Tabora?. Jibu la swali hilo ni kigugumizi mpaka sasa!. Njia ya mwongo ni fupi, mtu akileta urongo humu, the best way to counter urongo huo ni kumpa facts mrongo huyu kwa kumuuliza maswali ya datas ambapo akiyajibu tuu ni kamba ya kujinyonga mwenyewe.

Kama umeelezwa humu kuwa Mwalimu aliletwa mjini mwaka 1950, kabla ya hapo alikuwa bush, hakumjua Mzee yoyote wa mujini, halafu ukapata taarifa ya uhakika kuwa mwaka 1946 Mwalimu Nyerere ndiye alikuwa Katibu wa chama cha TAA, tawi la Tabora, na ukatibu wenyewe kaupokea kutoka kwa mtoto wa mujini, tena alwatan kabisa!.
Kisha ukaelezwa Mwalimu Nyerere ndiye aliyehudhuria mkutano Mkuu wa TAA wa mwaka 1948 jijini Dar es Salaam, akiwawakilisha mkoa wa Tabora, hivyo kama Nyerere hakuwajua wazee wa Dar es Salaam kabla ya kutambulishwa ile 1950s, huo mkutano Mkuu wa TAA wa mwaka 1948, inamaana Mwalimu alihudhuria na mawe na sio na wazee wa mujini hadi miaka ya 1950s alipotambulishwa na wazee wa fulani, ndipo Mwalimu Nyerere akafahamika mujini!.

Siku zote, ukweli utabaki kuwa ukweli daima na kwenye ukweli uongo hujitenga, hakuna kabisa ubishi kuhusu mchango wa wazee wa Darisalama, katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika lakini pia sio haki kutaka kumdogosha Mwalimu Nyerere na kuwakweza wazee wa fulani, kwenye harakati za uhuru wa Tanganyika, Mwalimu ana very special role, ataendelea kuwa alfa na omega wa mashujaa wa uhuru wa Tanganyika na kustahili title ya Baba wa Taifa.

P
Mkuu unafahamu historia ya wachagga?
Walimtangulia sana Nyerere.
Mfumo wao wa Uongozi hadi mwaka 1954 ulikuwa mbali sana.

Ulishasikia kitu kuhusu Mangi Thomas Marialle?
 
Mkuu ukiriejea bandiko #31 mwanzo kabisa niliweka wazi kuwa twende kwa hoja na si hadithi.

Moja ya mbinu za Mohamed kukwepa hoja ni kulundika habari irrelevant na hoja.

Utamsikia akijigamba, au kuleta picha na habari zisizohusiana na hoja.

Sijui kama ni ujanja wake au ni mapungufu ya kibinadamu.
Mohamed ni orator mzuri sana lakini hawezi ku articulate hoja au ku defend Swali hilo halitajibiwa kwasababu mwisho ni kuua hoja ya Nyerere kupokewa na wazee wake na kuingizwa katika siasa na Abdul

Anajua, Tabora ilikuwa tawi jipya na ameeleza kufunguliwa kwake 3/3/1945

Kawataja waliohusika, asichokieleza ni lini Nyerere alichukua madaraka na kwa utaratibu gani.

Haelezi ni akina nani waliohudhuria mkutano wa 1948 akijua Nyerere alikwenda.

Maana yake, Nyerere alikutana na Wazee akina Dosa na Abdul Sykes, kwasababu kuu mbili.

Kwanza, ni katibu wa Tawi kubwa sana baada ya Dar es Salaam, obvious walijulikana.

Pili, Nyerere alikuwa msomi na enzi hizo walihesabiwa kwa vidole vya mkono

Ni uongo kwamba Abdul hakumjua hadi alipotambulishwa kwake miaka hiyo ya 50

Hoja yake ni kuonyesha Nyerere si lolote si chochote, alikuja na kuingizwa katika siasa na Abdul Sykes. Kupitia hilo Abdul atakuwa ''king maker''

Katika mabandiko yaliyofuata nimemuomba kupitia kavazi la Nyerere na kavazi la Klesit Sykes hadi Abdul atuonyeshe karatasi moja iliyoitwa katiba. Hakujibu

Mohamed huyo huyo anasema Abdul ndiye alibuni jina la TANU akiwa Burma. Fair enough

Haipaswi kuishia hapo, Mohamed haelezi kuwa TANU ilikuwa na katiba baada ya Mwalimu

Kwanini hajibu hoja kama hizo?
Jibu ni rahisi kwamba, ataondoa mantiki ya vyama vya siasa kuwa kama klabu tu.

Hapa haina maana vilabu vya pombe, hapana!

Vilikuwa vilabu vya siasa kwa nyakati hizo vikikosa vionjo vya kusonga mbele.
Ujio wa Mwalimu uliongeza nguvu palipokuwa na mapungufu kama uwepo wa katiba.

Hili nalo linatupeleka katika hoja ya AMNUT.
Mohamed anasema Abdul hakuwa mwanzilishi, haelezi kuwa Abdul alikuwa mwanachama?

Utaona details zinakosekana kwasababu ukileta AMNUT utafungua mapungufu ya kushindwa kwa AMNUT na katika hilo Abdul hatakosekana.

Katika kufunika mapungufu ya AMNUT au kiungo hicho na akina Abdul, Mohamed atakueleza kuhusu EAMWS na Kuundwa kwa Bakwata kwa undani sana. Hilo sina tatizo nalo hata kidogo.

Asichokueleza ni kuwa wakati huo Nyerere alikuwa na asilimia takribani 98 ya Wazee wetu wa Dar ndani ya halmashauri kuu ya TANU.

Ilikuwaje mtu mmoja akawa na nguvu kiasi hicho bila usaidizi kutoka ndani ya TANU iliyokuwa na wazee wake kwa asilimia kubwa? Hatakueleza

Katika kukwepa hoja Mzee Said atakueleza kisa cha kufukuzwa kwa Mufti Ameir
Hapo hatukueleza wakati huo sheikh alikuwa TANU au AMNUT?

Siku za karibuni baada ya kuona hoja zake dhidi ya Nyerere zinafifisha nguvu ya hoja zake, Mohamed anasema Nyerere na Abdul walikuwa ndugu wa Familia.

Hilo sioni kama lina tatizo,akina Abdul walikuwa wenyeji na walimuhifadhi Mwalimu.

Mo hatakueleza nini kiliwafarakanisha kama ambavyo hatakueleza AMNUT ilifia wapi au Sheikh Ameir alifukuzwa kwanini na wakati huo alikuwa upande gani, TANU au AMNUT

Reading between the lines the whole history is disjointed. Hii haina maana ya kuwa anachoeleza hakikuwepo, la hasha. Matukio na wahusika walikuwepo na wapo bado.

Kinachoifanya historia isomeke kama ngano ni ''embellishment to skew the facts so as to fit his narratives hence to demean Mwalimu Nyerere''

Rekodi iwekwe kwa sahihi, Mo mapungufu ni sehemu ya ubainadamu, kukwepa au kukimbia kimbia hoja hakusaidii
Nguruvi3,
Abdul Sykes alikuwa mwanachama wa AMNUT...

Dunia haishi maajabu.
Hii nzuri sana na uzuri wake ni huu.

Unamtoa Abdul mwanachama muasisi wa TANU kadi no. 3 katika TANU na kati ya wafadhili wake wakuu toka TAA.

Unakata mnyororo wao wote katika TANU na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Vipi wadogo zake Ally na Abbas nao walitoka TANU na kujiunga na AMNUT?

Zipo taarifa?

Sheikh Hassan bin Ameir je na yeye pia alitoka TANU na kujiunga na AMNUT?

Ala! Sikujua kama katika historia ya TANU kuna mambo "relevant," yanatakiwa yafahamike na kinyume chake hayatakiwi kuelezwa.

Yawezekana hii ndiyo iliyosababisha historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kuwa na upungufu mkubwa usio kifani.

Hayo mengine wala sina haja ya kuyasemea.

Ila moja.

Kama hayo yote mnayosema ya AMNUT na wazee wangu na mengine mengi ambayo mnaamini na mna ushahidi mnashindwaje kuandika kitabu kujibu kitabu changu?

Andikeni kwani mtakuwa mmeisahihisha historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika na kufuta chembelecho Paschal "maurongo,"yangu.
 
Back
Top Bottom